Majeshi ya Ufaransa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, yanaongeza kasi ya juhudi zao dhidi ya vurugu na kuzieneza katika sehemu nyengine za taifa hilo ili kurejesha utulivu baada ya mapigano ya kidini.Wanajeshi zaidi wa Ufaransa walishika doria katika mji mkuu Bangui huku wengine wakiingia nchini humo kupitia Cameroon.Msemaji wa jeshi hilo amesema kuna wanajeshi zaidi watahitajika kwenda maeneo ya Kaskazini na Magharibi, Ufaransa, inaongeza idadi ya wanajeshi wake nchini humo hadi 1,600, kuisaidia wanajeshi wanaolinda Amani kukabiliana na vurugu kati ya waisilamu na wakristo.Afrika ya Kati imekuwa ikikumbwa na vurugu tangu Michel Djotodia kumng’oa mamlakani aliyekuwa Rais Francis Bozize.Djotodia amejitangaza kuwa kiongozi wa kwanza wa waisilamu katika taifa hilo lenye idadi kubwa ya wakristo.Kundi la waasi la Seleka ambalo lilimuingiza mamlakani Djotodia, linatuhumiwa kwa kuwaua wakristo .Duru zinasema kuwa mamia ya watu waliuawa wiki jana katika vita vinavyochochewa na waasi wa Seleka.Rais wa Ufaransa, Francis Hollande amesema viongozi wa Afrika lazima wahakikishe kuwa wanadhibiti ulinzi na usalama katika mataifa yao.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment