Majeshi ya Ufaransa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, yanaongeza kasi ya juhudi zao dhidi ya vurugu na kuzieneza katika sehemu nyengine za taifa hilo ili kurejesha utulivu baada ya mapigano ya kidini.Wanajeshi zaidi wa Ufaransa walishika doria katika mji mkuu Bangui huku wengine wakiingia nchini humo kupitia Cameroon.Msemaji wa jeshi hilo amesema kuna wanajeshi zaidi watahitajika kwenda maeneo ya Kaskazini na Magharibi, Ufaransa, inaongeza idadi ya wanajeshi wake nchini humo hadi 1,600, kuisaidia wanajeshi wanaolinda Amani kukabiliana na vurugu kati ya waisilamu na wakristo.Afrika ya Kati imekuwa ikikumbwa na vurugu tangu Michel Djotodia kumng’oa mamlakani aliyekuwa Rais Francis Bozize.Djotodia amejitangaza kuwa kiongozi wa kwanza wa waisilamu katika taifa hilo lenye idadi kubwa ya wakristo.Kundi la waasi la Seleka ambalo lilimuingiza mamlakani Djotodia, linatuhumiwa kwa kuwaua wakristo .Duru zinasema kuwa mamia ya watu waliuawa wiki jana katika vita vinavyochochewa na waasi wa Seleka.Rais wa Ufaransa, Francis Hollande amesema viongozi wa Afrika lazima wahakikishe kuwa wanadhibiti ulinzi na usalama katika mataifa yao.
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment