Posts

Showing posts from September, 2016

WALIOCHAGULIWA TEKU MAJINA YAPO HAPA

Image
Chuo Kikuu Theofilo Kisanji (TEKU) kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho ktk mwaka wa masomo 2016/2017. BOFYA HAPA KUANAGALIA MAJINA VENANCE BLOG ITAENDELEA KUSOGEZA SELECTION HIZO ZA VYUO MBALIMBALI KADIRI ZINAVYOTOKA.

SELECTION ZA TUMAINI MAKUMIRA NA UNIVERSITY OF IRINGA ZIPO HAPA

Image
Tumaini Makumira University of Iringa Chuo Kikuu cha Iringa na Chuo Kikuu Tumaini Makumira vimetoa majina ya waliochaguliwa katika vyuo hivyo. KWA TUMAINI MAKUMIRA BOFYA HAPA KWA UNIVERSITY OF IRINGA BOFYA HAPA Uangaliaji wa majina ktk vyuo hivi ni tofauti kwani wao hawatumii Index ya form 4 wala 6 ni majina tu, hivyo kama uliapply na unataka kuona jina tuma jina lako kwenda namba 0753400208. Huduma hii ni bure kabisa.

WALIOCHAGULIWA BUGANDO (CUHAS) MAJINA HAYA HAPA

Image
Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Kikatoliki (Bugando) (CUHAS) kimetoa majina ya wanafunzi mbalimbali waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA Aidha unaweza kutuma jina lako na index ya form four au six bila kusahau kozi uliyoomba chuoni hapo kwenda namba 0753400208 na utaangaliziwa jina bure kabisa.

WALIOCHAGULIWA UDSM, DUCE NA MKWAWA BATCH 1 MAJINA HAYA HAPA

Image
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na matawi yake DUCE na MKWAWA (MUCE) kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kozi mbalimbali za shahada chuoni hapo kwa mwaka wa masomo 2016/2017. BOFYA HAPA KUANGALIA Unaweza kutuma jina lako, pamoja na namba ya kidato ya cha 4 au 6 kwenda namba 0753400208 na utaangaliziwa jina BURE . Kumbuka kutuma jina lako, index ya 4 au 6 na chuo unachotaka kuangalia hata kama ni zaidi ya kimoja. Mfano: Venance Gilbert s2509/0575/2012 (iv) au s0494/0141/2015 (vi) Mzumbe, MUHAS, SUA, UDSM, UDOM, SAUT n.k. kwenda 0753400208. Huduma hii ni BURE .

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA UDOM BACHELOR DEGREE YAPO HAPA

Image
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2016/2017. Ili kuona matokeo haya kwa njia ya  simu hakikisha simu yako ina WPS Office, Polaris Office n.k. kisha  BONYEZA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO VENANCE BLOG IKO NA WEWE, UKISHINDWA KUANGALIA MAJINA HAYO TUMA UJUMBE MFUPI (SMS) UKIANDIKA JINA LAKO NA INDEX YA KIDATO CHA 4 AU 6 KWENDA NAMBA 0753400208 UTAANGALIZIWA JINA LAKO BURE KABISA KUPEWA MAJIBU.

WALIOCHAGULIWA KOZI ZA SHAHADA CBE KAMPASI YA DAR ES SALAAM

Image
Chuo cha Elimu ya Biashara kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa kwanza wa masomo 2016/2017. Majina yapo hapa. Kumbuka hili ni toleo la kwanza (First Batch).  BOFYA HAPA KUANGALIA

WALIOCHAGULIWA KOZI MBALIMBALI ZA SHAHADA IFM

Image
  Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM) imetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kusoma kozi mbalimbali za Shahada katika fani mbali mbali chuoni hapo. Majina hayo yako hapa.  BOFYA HAPA KUONA MAJINA HAYO

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU TUMAINI MAKUMIRA KAMPAS YA MBEYA HAYA HAPA

Image
Chuo Kikuu Tumaini Makumira kampus ya Mbeya kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Chuo hicho kwa kozi za Shahada ya Elimu na Sanaa (Bachelor of Arts with Education BA.Ed) na Shahada ya Elimu katika Sanaa (Bachelor of Education in Arts BED). Majina hayo yapo kwenye tovuti ya Chuo toka juzi Septemba 15. KUANGALIA BA.Ed BOFYA HAPA KUANGALIA BEd BOFYA HAPA Aidha taarifa zote za Chuo hiko unaweza kuzipata kwa  KUBOFYA HAPA VENANCE BLOG IKO NA WEWE KWA TAARIFA ZOTE ZA VYUO MBALIMBALI NCHINI. ENDELEA KUWA NAMI.

HILLARY CLINTON AMEREJEA KATIKA KAMPENI NA KUMSHAMBULIA TRUMP

Image
Mgombea wa chama cha Democratic katika kinyan'ganyiro cha urais nchini Marekani Hillary Clinton amerejea tena katika kampeni na kutoa kauli ya tahadhari dhidi ya mpinzani wake Donald Trump. Mgombea wa chama cha Democrats Hillary Clinton akiwahutubia wafuasi wake North Carolina Akizungumza katika mikutano miwili tofauti ya kampeni kwenye majimbo mawili, North Carolina na Washington, Hillary Clinton alisema amefurahi kurejea katika kampeni hizo baada ya hapo awali kushauriwa na madaktari kubakia nyumbani hadi atakapopata nafuu kutokana na maradhi ya homa ya mapafu yaliyokuwa yakimkabili. Hali ya afya ya Hillary Clinton ilidhoofika wakati wa kumbukumbu ya mika 15 tangu yalipofanyika mashambulizi ya kigaidi nchini Marekani tarehe 11/9/ 2001. "Ni jambo jema kuwa nimerejea katika kampeni" alisema mgombea huyo wa chama cha Democratic huku akishangiliwa na wafuasi wake alipohutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika eneo la Greensboro, North Carolina

MTU MMOJA AMEJITOA MUHANGA NA KUUA WATU 16 KATIKA MSIKITI WA MOHMAND PAKISTAN

Image
Takribani watu 16 wameuawa na wengine 35 kujeruhiwa katika swala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Mohmand huko Pakistan. Duru za habari zinasema kuwa mtu huyo aliyejitoa muhanga ameua watu 16 na wengine 35 kujeruhiwa walipokuwa wakihudhuria swala ya Ijumaa kaskazini mashariki mwa  Pakistan. Shambulio hilo limetokea katika kijiji cha Anbar Tehsil katika wilaya inayokaliwa na kabila la Mohmand ambapo jeshi la Pakistan limekuwa likipambana na kundi la Taliban. "Swala ya Ijumaa ilikuwa ikiendelea msikitini hapo wakati ambapo mshambuliaji huyo wa kujitoa muhanga alijilipua na kuua waumini 16 na kujeruhi wengine 35" kiongozi mmoja wa Mohmand aliliambia shirika la habari la AFP. Hakujatokea taarifa zozote kuhusu shambulio hilo, lakini kundi la Taliban linashutumiwa kuhusika na shambulio hilo kwa kuwa limekuwa likifanya mashambulio katika maeneo ya mahakama, shule na misikiti. Jeshi la Pakistan limekuwa likifanya operesheni toka Juni 2014 kuangamiza makundi yote ya kigaidi yal

LEO SEPTEMBA 14 KATIKA HISTORIA

Image
Rapa Nas Escobar alizaliwa September 13, 1973. Leo ni Jumatano Septemba 14, 2016. Ni siku ya 258 katika mwaka 2016. Zimesalia siku 108 kuukamilisha mwaka 2016. MATUKIO 1960 - Iraq, Iran, Kuwait na Saudi Arabia ziliunda jumuiya ya OPEC. 1979 - Nur Muhammad Tarak, Rais na na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Afghanistan aliuawa katika mapinduzi ambapo Waziri Mkuu Hafizullah Amin alishika madaraka. KUZALIWA 1849 - Mwanasaikolojia wa Urusi, Ivan Pavlov. 1864 - Robert Cecil,  miongoni mwa waanzilishi wa Jumuiya ya Mataifa alizaliwa. 1879 - Margaret Sanger, wakili na muanzilishi wa Uzazi wa mpango. 1973 - Rapa Nas Escobar alizaliwa. 

NEW AUDIO: DOWNLOAD BARAKA DA PRINCE FT ALI KIBA-NISAMEHE MP3

Image
Baraka Da Prince akishirikiana na Ali Kiba wanakusikilizisha kitu hiki hapa kipya, wimbo unaitwa Nisamehe umefanyikwa kwa Imma the Boy. DOWNLOAD HAPA

TCU IMERUHUSU UDAHILI VYUO VIKUU AWAMU YA PILI

Image
Tume ya Vyuo Vikuu nchini Tanzania (TCU) imeruhusu awamu ya pili ya udahili kwa wanafunzi waliokosa vyuo kwa kukosa sifa katika udahili wa awamu ya kwanza na wale ambao hawakuomba kudahiliwa kabisa. Aidha TCU inakumbusha kwamba wale waliokwisha omba na hawakupangiwa kwa kukosa sifa stahiki za vyuo walivyopangiwa hawatatakiwa kulipia tena. Pia wadahiliwa wapya wanatakiwa kulipia kiasi cha fedha za kitanzania Tsh. Elfu Hamsini (50,000/=) kama gharama za udahili. Fedha hii huwa hairudishwi. Vilevile TCU inakumbusha kwamba kozi ambazo zimejaa tayari hazitaonekana kwenye mfumo wa Udahili (CAS). Aidha TCU inawakumbusha waombaji kuwa mwisho wa kutuma maombi ya udahili ni Septemba 23 na hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza kwa wale watakaoshindw kuomba vyuo katika muda huo ulioongezwa. MAELEZO ZAIDI  BOFYA HAPA

IGGY AZALEA ASISITIZA YEYE NA FRENCH MONTANA NI MARAFIKI TU

Image
Iggy Azalea amekataa kuwa na uhusiano na French Montana japo wameonekana mara kadhaa wakiwa sehemu za starehe pamoja. Rapper huyo wa kike ameuambia mtandao wa TMZ kuwa hana mpenzi kwa sasa hivyo yeye na French Montana ni marafiki tu. “We are Single, I’m single,” amesema Iggy. “just friends.” Wiki kadhaa zilizopita Iggy alidai kuwa yeye na French Montana kuna wimbo wamefanya ila hawana mahusiano yoyote lakini baada ya wiki moja wawili hao walionekana wakiwa wanakula bata pamoja huko Cabo San Lucas, Mexico. Walionekana pia wakibusiana.

LEO SEPTEMBA 13 KATIKA HISTORIA

Image
Tarehe kama ya leo Septemba 13' Tupac Shakur alifariki. Leo Septemba 13 siku ya 257 katika mwaka 2016, zimesalia siku 109 kuukamilisha mwaka 2016. MATUKIO 1759 - Vikosi vya majeshi ya Uingerza viliyashinda majeshi ya Ufaransa katija mapigano kwenye nyanda za Abraham huko Quebec. 1914 - Wanaharakati wa Ireland waliomba msaada kwa wajerumani. 1940 - Italia iliivamia Misri. 1945 - Vikosi vya majeshi ya Uingereza viliingia Japan kupunguza uwezo wa jeshi la Japan. 1993 - Mkataba wa amani kusitisha mapigano Israel na Palestina ulisainiwa. VIFO 1996 - Mwanamuziki 2Pac Shakur alifariki. KWA MSAADA WA MTANDAO.

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Image
Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha

LEO SEPTEMBA 12 KATIKA HISTORIA

Image
Tarehe kama ya leo Septemba 12, 1973 muigizaji wa Marekani, Paul Walker alizaliwa huko Glendale, Califonia.Alifariki Novemba 30, 2013. Leo ni tarehe 12 Septemba, siku ya 256 katika mwaka 2016, zimesalia siku 110 kuukamilisha mwaka 2016. MATUKIO Leo kuna matukio mengi sana hata hivyo tuyaangalie kama ifuatavyo: 1217 - Mfalme wa Ufaransa Prince Louis na Mfalme wa Uingerza Henry III walisaini mkataba wa amani. 1624 - Meli ya kwanza kupita chini ya maji ilijaribiwa katika Mto Thames kwa ajili ya kutumiwa na Mfalme James I huko Uingereza. 1662 - John Flamsteed aliona nusu ya kupatwa kwa jua na ikampelekea kuvutiwa na elimu ya anga (unajimu) 1703 - Jeshi la Uingereza chini ya Archiduke Charles wa Austria waliwasili nchini Ureno. 1722 - Vikosi vya Urusi viliteka Baku na Derbent huko Persia ambayo kwa sasa ni Iran. 1751 - Amsterdam ilikataa kuanzisha makazi ya Wayahudi. 1753 - Mnajimu wa Ufaransa Charles Messier bila kutarajia aligundua gesi ya miamba (crab

ALI KIBA KUTUMBUIZA TUZO ZA MTV MAMA OKTOBA 22

Image
Mwanamzuki mwenye vionjo vya kipekee Ali Kiba a.k.a. King Kiba amethibitisha katika ukurasa wake wa Facebook kuwa ataperform katika tuzo za MTV MAMA zitakazofanyika Johanesburg Afrika Kusini Octoba 22 mwaka huu.

KATY PERRY AMESEMA ATAFANYA COLLABO NA TAYLOR SWIFT KAMA ATAOMBA MSAMAHA

Image
Katy Perry na Taylor Swift wakiwa Berley Hilton Hotel Januari 30, 2010 Katy Perry na Taylor Swift kufanya  collabo?  Collabo hiyo inaweza kutokea lakini kwa sharti moja tu kutoka kwa Katy Perry, kama Taylor Swift atakubali kumuomba msamaha. Hili linakuja baada ya shabiki mmoja wa Katy Perry kuuliza katika mtandao wa Twitter kama Katy Perry anaweza kufanya collabo na Swift, Perry akajibu kwa kifupi "hakika, kama ataomba msamaha" Mgogoro kati ya mastaa hawa wawili wa Pop ulianza mwaka 2014 kufuatia Swift kumteta Katy katika Mtandao wa The Rolling Stone kuwa wimbo wake "Bad blood" ulikuwa unamhusu Swift. "Alifanya kitu kibaya sana" alisema Swift. "Ilikuwa kama hivyo. Tumekuwa maadui. Na sababu haikuwa mwanaume. Ni kazi tu. Alijaribu hata kuvuruga tamasha langu. Alijaribu hata kuwapa hela vijana waje kunitoa jukwaani" JE, KATY PERRY AMETHIBITISHA KUWA WIMBO WA 'BAD BLOOD' UNAMHUSU SWIFT? Mtandao wa The Internet ulisema kwamba

WALIOKUFA KATIKA TETEMEKO WAFIKIA 16

Image
Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kuaga miili ya waliokufa katika tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Maafa zaidi yameripotiwa katika janga la tetemeko la ardhi, lililotokea juzi mkoani Kagera, ambapo imeripotiwa idadi ya vifo kuongezeka na kufikia watu 16, huku wengine 253 wakijeruhiwa na kusababisha simanzi na masikitiko kwa familia nyingi. Katika tukio hilo, pia nyumba 840 za makazi zimeanguka, nyumba 1,264 zimepata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule yameanguka. Tukio hilo limemfanya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kulazimika kufanya ziara ya ghafla ya kuwatembelea waathirika wa tetemeko hilo, ambalo limedaiwa kusababisha tafrani pia katika nchi jirani za ukanda wa Afrika Mashariki za Kenya na Rwanda. Katika hatua nyingine, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimeeleza mpango wa kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga ha

VIDEO: HII NDIYO MAANA HALISI YA SEPTEMBA 11 HUKO MAREKANI

Image
Mnamo mwaka 2001 ndege mbili za abiria za chini Marekani zilitekwa angani na magaidi wanaodhaniwa kuwa ni Al-Qaeda. Ndege hizo mbili aina ya Boeing 767 ziligonga katika majengo pacha ya Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililoko katika jiji la New York nchini Marekani. Hili lilikuwa ni shambulio kubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na magaidi wa Al-Qaeda ambao kwa kipindi hicho kundi hilo lilikuwa likiongozwa na Osama bin Laden ambaye aliuawa miaka ya hivi karibuni na wanajeshi wa jeshi la Marekani (wanavyodai wao Marekani).  Pia kundi la Al Qaeda lilikuwa limelenga kuteketeza jengo la Idara ya Ulinzi ya Marekani, The Pentagon ambako ndiyo makao makuu ya Idara ya Ulinzi ya nci ya Marekani. Lakini pia ililengwa Ikulu ya Marekani 'The White House'. Watu wapatao 2,996 pamoja na watekelezaji wa tukio hilo wakiwa 19 waliuawa. Watu zaidi ya 6,000 walijeruhiwa katika tukio hilo. Pia tukio hilo lilisababisha uharibifu wa mali hasa majengo na miundo mbinu uliofikia dola bilioni 10

LEO SEPTEMBA 11 KATIKA HISTORIA

Image
Leo ni tarehe 11 Septemba, siku ya 255 katika mwaka 2016, zimesalia siku 111 kumaliza mwaka huu 2016. MATUKIO 1740 - Daktari mweusi aliyetibu meno alitajwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la The Pennsylvania  1777 - Mapigano ya vita ya Brandywine yalianza huko Pennsylvania ambapo General George Washington na vikosi vyake walishindwa na General Sir William Howe wa Uingereza 1915 - Mkutano wa Zimmerwald uliitishwa kurejesha amani wakati wa vita ya kwanza ya Dunia. 1940 - Adof Hitler alituma vikosi vyake Mashariki mwa Romania katika vita ya pili ya dunia. 1944 - Vikosi vya Marekani viliingia Luxembourg. 1974 - Haile Selassie I aliondolewa madarakani huko Ethiopia. 1997 - Scotland ilipiga kura ya kuwa na Bunge lake kamili baada ya miaka 290 ya Muungano na England. Jengo la Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililolipuliwa Septemba 11, 2001 na kundi la Al-Qaeda. 2001 - Mnamo majira ya saa 2 na  dakika 45 asubuhi ikiwa siku ya Jumanne, ndege mbili za abiri

MAPIGANO YAPAMBA MOTO SYRIA KUELEKEA SULUHU YA MGOGORO

Image
Saa chache baada ya Marekani na Urusi kutangaza makubaliano ya kumaliza mgogoro wa kivita uliyodumu kwa miaka mitano nchini Syria, mapigano yemepamba moto upya. Karibu raia 100 wameuawa katika mashambulizi ya angani. Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London,Uingereza, limeripoti siku ya Jumamosi kwamba raia wasiopungua 58 wameuawa katika mkoa unaodhibitiwa na waasi wa Idlib baada ya ndege za kivita kuliripua kwa mabomu soko kaskazini-magahribi mwa mji huo, saa kadhaa baada ya kutangazwa kwa masharti ya makubaliano ya kusitishwa mapigano nchini kote. Mjini Aleppo, jeshi la Syria lilifanya mashambulizi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi katika jitihada za kuimarisha nafasi yake kuelekea usitishaji wa uhasama, unaoanza siku ya Jumatatu wakati wa siku kuu ya Eid al-Adha. "Mapigano yamepamba moto katika maeneo yote ya Aleppo," alisema kapteni Abdul Salam Abdul Razak, msemaji wa kundi la waasi la Brigedi za Nour al-Dine al Zi

TETEMEKO LA ARDHI LIMEPITA MIKOA YA MWANZA NA KAGERA NA KUFANYA UHARIBIFU

Image
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.7 limetikisa mkoa wa Mwanza likitokea mkoa wa Kagera umbali wa kilomita 44 karibu na ukingo wa magharibi wa Ziwa Victoria huku likijirudia kwa ukubwa zaidi ya ule wa awali. Tetemeko hilo lilipita umbali wa kilomita 10 kwenda chini limefanya uharibifu mkoani Kagera kama picha zinavyoonesha hapa chini. Pia kumeripotiwa vifo vya watu. PICHA KWA HISANI YA JAMII FORUMS.