Showing posts with label Anga. Show all posts
Showing posts with label Anga. Show all posts

WANASAYANSI WAGUNDUA UHAI KATIKA SAYARI YA SATURN

Sayari ya Saturn
Sayari ya Sarateni "Saturn"

Mwezi wa Enceladus ambao uko kwenye sayari ya Saturn huenda ukawa mahali bora zaidi pa kwenda kutafuta maisha nje ya dunia.

Tathmini hii inatokea kufuatia uchunguzi katika sayari hiyo yenye kilomita 500 uliofanywa na Cassini.

Uchambuzi wa kemia wa Cassini unaonyesha matundu ya maji moto kwenye sakafu ya bahari ya Enceladus, maeneo ambayo yanahusishwa na kuwepo kwa maisha, hapa duniani.

Kuwepo kwa maji haya sio thibitisho kamili kwamba vitu vilivyo na uhai vinaishi katika mwezi huo mdogo lakini teknolojia zinaweza kutumika kupima maji hayo na kutoa ushahidi zaidi.

"Tuna uhakika kuwa kitu chenye uhai kinaweza kuishi kwenye bahari ya Enceladus lakini lazima tufanye utafiti zaidi," alisema mwanasayansi wa Cassini kutoka Taasisi ya Utafiti ya Southwest, San Antonio, Dkt. Hunter Waite.

"Iwapo hakuna maisha huko, ni sawa, lakini ikiwa maisha yapo itakuwa bora zaidi," alieleza BBC.
Bahari iliyopo kwenye Enceladus inakisiwa kuwa na kina kirefusana sana na yapo majimaji kwa sababu ya joto linalotokana na mvuto wa mara kwa mara kutoka kwenye sayari ya Saturn.

Cassini tayari amedhibitisha kwamba maji hayo yanashikana na sakafu ya bahari kutokana na aina ya chumvi na silika ambayo pia imeonekana katika mashimo.
 
Lakini wanachotaka kujua sana wanasayansi ni ikiwa maswala fulani yanayotendeka duniani pia yanaweza kufanyika katika Enceladus - kitu kinachoitwa serpentinisation, ambayo hutengeneza gesi ya hidrojeni.

"Kwa viumbe hai, hidrojeni huwa ni kama kama pipi - ni chakula wanachokienzi," alieleza Dkt Chris McKay, mwanabiolojia wa maswala ya anga wa shirika la Nasa.

"Ni nzuri sana kwa kuvipa nguvu, na inaweza kusaidia viumbe vidogo sana. Kupata hidrojeni itakuwa vizuri sana na itakuwa moja ya ushahidi utakaoonyesha uwezekano wa kuwepo na uhai."

Viumbe hai anavyozungumzia Dkt McKay vinaitwa methanojeni kwa sababu vinatengeneza gesi ya metheni vinapogusana na hidrojeni na gesi ya kaboni .

Nasa, ambayo inaongoza ujumbe wa Cassini , ilitakikana kufanya tangazo la hidrojeni miezi michache baada ya uchunguzi wa mwisho waroketi ya mwezini, Oktoba mwaka wa 2015.

Ziara ya Cassini sasa inakamilika . Baada ya kuizunguka Saturn kwa muda wa miaka 12, inaendelea kuishiwa na mafuta na sasa itawachiliwa kuingia kwenye anga ya dunia hiyo ya Saturn mwezi Septemba, kuhakikisha kuwa haiwezi kugongana na Enceladus na kusababisha kuchafuka kwake.


Chanzo: BBC

SATELITE YA JUNO YAFIKA KATIKA SAYARI YA JUPITA

juno crop for ICYMI 160701
Satelite ya Juno ikiwa imewasili katika sayari ya Jupita.

Satelite ya Juno inayokuwa inayoongozwa taasisi ya Utafiti wa Anga NASA iliyoko nchini Marekani imefanikiwa kufika katika sayari ya Jupita ambayo ni sayari ya tano katika mfumo wa jua kutoka kwenye jua.

Satelite hiyo ya Juno iliondoka duniani miaka mitano iliyopita ambayo ilikuwa na rocket engine kuiongoza satelite hiyo mpaka kuifika satelite hiyo..

Wattafiti wanapanga kuitumia satelite hiyo kuichunguza sayari hiyo kwa jina. Wanadai kuwa muonekano wa sayari hiyo na kemia yake unaweza kuichunguza zaidi sayari hii ambayo ni kubwa kuliko zote katika mfumo wa jua toka ilipotengenezwa zaidi ys miaka bilioni 4 na nusu iliyopita.

Hakuna chombo kilichofanikiwa kupita au kuisogelea sayari hiyo ya Jupita kutokana na mionzi iliyopo katika sayari hii kama chombo hicho hakijalindwa na vifaa maalumu vya kieletroniki ambavyo vinazuia mionzi hiyo kupenya.

Mahesabu ya haraka yanaonesha kuwa satelite hiyo imeundwa kwa miyonzi zenye X Ray zinazokadiriwa kuwa zaidi ya milioni. Kabla chombo hicho hakijafikia mwisho wa electron za kujilinda, chombo hiyo inatakwa ianze kuichunguza sayari hiyo mapema baada ya kuwasili katika sayar hyo.

Satelite ya Juno kama inavyoonekana angani.



Rocket ya pili ambayo inatarajiwa kuanza kuungua katikati ya mwezi wa kumi mwaka huu itaungua hasa kwa muda wa siku 14 na ndipo hapo sasa utafiti utanza rasmi.

Juno iitataumia vifaa vyake 8 vya kuhisi pamoja na kamera kuelekea katika ukanda wa gesi chini ya sayari hiyo ili kupima vlivyounda sayari hiyo, joto na mambo mengne. Utafiti huo utsisitizwa zaidi katika ugunduzi wa uwepo wa hewa ya Oksijeni pamoja na maji.

"Ni kwa kiasi gani sayari hii itakuwa na maji kitatuekeza ni lini sayari hii iliundwa katka mfumo wa jua" alieleza Candy Hansen mmoja wa timu ya Juno.

MAMBO 8 UNAYOTAKIWA KUYAFAHAMU

  • Sayari hii ina ukubwa mara 11 ya ukubwa wa Dunia yetu tunayoishi.
  • Inaichukua dunia mara 12 kulizunguka jua katika mhimili wake; siku inakuwa na masaa 10.
  • Katika kuundwa kwake inafanana na nyota; imeundwa sana kwa gesi ya Oksijeni na Haidrojeni.
  • Katika mgandamizo wa hewa wa kawaida Haidrojeni inakadiriwa kuwa gesi ya ambayo inaconduct umeme.
  • Hii metallic haidrojeni ni chanzo kikuu cha utepe wa kimagnetic.
  • Mawingu mengi yanaonekana kuwa yameundwa na gesi ya Amonia na Haidrojeni Salfaidi.
  • Sayari ya Jupita ina upepo mkali unaotoka mashariki kwenda magharibi.
  • The Great Red Spot is a giant storm vortex twice as wide as Earth.


NASA wamepanga kukiongoza chombo hicho hadi mwezi wa pili mwaka 2018 (Februari) ambapo bado mionzi hiyo itakuwa haijakiharibu chombo hicho. Kamera yake inakadiriwa kupungua uwezo miezi michache ijayo.


Kama ilivyo katika tafiti kwenye sayari zilizopita, utafiti katika sayari hii utaishia katika kuchunguza tabaka la hewa lilipo katika sayari hiyo.



Chanzo: BBC