Posts

Showing posts with the label Kimataifa

GOODALL MWANASAYANSI WA AUSTRALIA (104) AMEJITOA UHAI WAKE NCHINI USWISI

Image
  Mwanasayansi David Goodall, 104, aliyesafiri kutoka Australia hadi Uswisi ili kujitoa uhai amefariki katika kliniki moja nchini Uswisi, shirika linalotetea haki za watu wanaotaka kufa limetangaza. Mwanaikolojia huyo ambaye pia alikuwa mtaalamu wa mimea hakuwa anaugua lakini alisema aliamua kujitoa uhai kutokana na kudhoofika kwa 'ubora wa maisha yake'. Goodall mwaka 1984 enzi za ujana. Bw Goodall alikuwa amezua mjadala kutokana na safari yake ya kutoka Australia kwenda kujitoa uhai. Muda mfupi kabla ya kifo chake, alisema alikuwa na "furaha kuhitimisha" maisha yake. "Maisha yangu yamekuwa dhaifu sana kwa mwaka mmoja hivi uliopita na hivyo basi nina furaha kuyahitimisha," alisema akiwa amezingirwa na jamaa wake kadhaa. "Nafikiria, kuangaziwa kwa kisa changu kutachangia kutetea haki za wazee kuruhusiwa kujitoa uhai, jambo ambalo nimekuwa nikitaka." Mtazame Goodall katika video hii hapa chini: Alifari

IRAN IMEFANYA JARIBIO LA KOMBORA LA NYUKLIA

Image
Iran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr. Kombora hilo lilionyeshwa hadharani katika maonyesha ya kijeshi jana Ijumaa. Iran imesema kuwa kombora hilo linaweza kusafiri mwendo wa kilomita 2,000. Kituo cha runinga cha taifa hilo kilionyesha picha za sherehe hizo. Kombora la kwanza la Khorram-Shahr lilirushwa angani Januari lakini likalipuka katikati ya mwendo. Jaribio hilo lilifanywa siku chache baada ya Rais Trump wa Marekani kushambulia Iran katika hotuba yake katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Rais wa Iran, Hassan Rouhani, ametetea hatua ya taifa lake kuimarisha zana zake kwa lengo la kujitetea. Chanzo

RAIS PUTIN AMEAGIZA WANADIPLOMASIA 755 WA MAREKANI KUONDOKA URUSI

Image
Rais wa Urusi Vladimir Putin ameagiza wafanyakazi 755 wa ubalozi wa Marekani nchini Urusi kusitisha shughuli zao kufikia Septemba mosi mwaka huu. Urusi imeidhinisha hatua hiyo kwa ghadhabu kufuatia vikwazo vipya vilivyopitishwa na bunge la Marekani dhidi yake, kwa tuhuma za kuingilia uchaguzi wa taifa hilo mwaka jana. Marekani kwa upande wake, inasema imesikitishwa na uamuzi huo, na inapima athari na kutafakari namna ya kujibu hatua hiyo. Hatua hii ya Urusi imekuja baada ya vikwazo vipya dhidi ya Urusi kuidhinishwa kwa wingi wa kura na mabunge yote ya congress nchini Marekani Jumanne, licha ya kwamba Ikulu ya White house ilipinga kura hiyo. Rais huyo wa Urusi ameapa kuwa upo uwezekano wa kuongeza vikwazo zaidi dhidi ya serikali ya Marekani. Akizungumza kwenye televisheni ya taifa ya Urusi, rais Putin alisema kuwa alitarajia uhusiano baina ya Moscow na Washington ungebadilika na kuwa mzuri, lakini hilo haliwezekani kwa sasa. Akizungumza wakati wa ziara yake nchini Estonia,

TRUMP AWASILI SAUDI ARABIA

Image
Rais Donald Trump  akikaribishwa  kwa bashasha  kubwa  na  ukoo  wa  kifalme  wa  Saudi Arabia  jana , wakati  akiweka  kando, japokuwa  kwa  muda  tu , utata mkubwa  unaoukumba utawala  wake  mjini  Washington. Rais Trump akilakiwa mjini Riyadh Trump  amewazawadia  wenyeji wake  mpango  wa mauzo  ya  bilioni 110  wa  silaha  wenye  lengo  la  kuimarisha  usalama  wa  Saudi  Arabia pamoja  na  makubaliano  kadhaa  ya  kibishara. "Hii  ni  siku  muhimu  sana, uwekezaji  mkubwa  katika  Marekani ," Trump  alisema wakati wa  mkutano  na  mwanamfalme Mohammed bin Nayef. Rais Trump (Kushoto) akisalimiana na mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz(kulia) Ziara  katika  mji  mkuu  wa  Saudi Arabia  ilikuwa  ni ziara  ya  kwanza  ya  Trump  nje  ya nchi  akiwa  rais, ikiwa  ni  ziara  itakayokuwa  na vituo  vitano ambayo  itamchukua  katika mataifa  ya  mashariki  ya  kati  hadi  Ulaya. Ni  rais  pekee  wa  Marekani kuifanya  Saudi Arabia , ama  taifa  lolote  le

KOREA KASKAZINI IMEFANYA JARIBIO LINGINE LA KOMBORA

Image
Jeshi la Korea Kusini linasema kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio kombora lingine. Ofisi ya kijeshi nchini Korea Kusini inasema kuwa kombora hilo lilirushwa siku ya Jumapili jioni saa za Korea. Jaribio hilo linafanyika wiki moja baada ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora lingine ambalo inadai kuwa ni jipya na ambalo lina uwezo wa kubeba silaha kubwa ya nyuklia. W achambuzi wanasema kwamba huko mbeleni linaweza kuifikia Alaska. Jumatatu iliyopita baraza la usalama la Umoja wa Mataifa liliitaka Korea K askazini kusitisha majaribio kama hayo. Baraza hilo la UN lilisisitiza umuhimu wa nchi hiyo kuachana na hatua hizo. Korea Kaskazini inafahamika kwa kuunda zana za nyuklia na imefanya jumla ya jaribio matano ya nyuklia na ya makombora yenye uwezo wa kusafirisha zana hizo hadi maeneo inayolenga. Korea Kusini inasema kuwa jaribio la hivi punde lilifanyiwa eneo la Pukchang magharibi mwa nchi. Chanzo: BBC & DW

MGAHAWA WAKUMBWA NA KASHFA YA KUUZA NYAMA YA BINADAMU

Image
Mgahawa mmoja mjini London umekumbwa na habari bandia za kuuza nyama ya mtu. Wafanyikazi katika mkahawa wa Karri Twist katika eneo la New Cross nchini Uingereza wamehangaishwa kwa kupigiwa simu kutoka kwa wateja wanaosema ''Kwa nini hamujafunga''?. Mkahawa huo wa chakula cha jioni ni mwathiriwa wa habari za mzaha zilizodai kwamba mmiliki wake alikamatwa kwa kuweka nyama ya binadamu katika chakula na kwamba miili 9 ilipatikana katika jokovu la mkahawa huo. Na watu wengine waliamini mzaha huo. Habari hiyo ilichapishwa katika chombo cha habari cha channel23news.com, mtandao ambao wateja wake wanaweza kuchapisha habari za uwongo ili kuwafanyia mzaha rafiki zao kwa kuchapisha moja kwa moja katika mtandao wa fecbook. Shinra Begum ambaye ndio mmiliki wake aliambia Newsbeat kwamba biashara hiyo ya familia imekumbwa na wakati mgumu tangu habari hiyo ilipochapishwa siku ya Alhamisi. ''Wakati watu walipoanza kunipigia simu na kuuliza iwapo tulikuw

NDEGE YA MAREKANI YAZUILIWA NA NDEGE ZA CHINA

Image
Ndege mbili za kijeshi za China zimeizuia 'vibaya' ndege ya Marekani kulingana na jeshi la Marekani. Ndege hiyo inayohusika na kufanya uchunguzi, ilikuwa katika safari yake ya kutaka kugundua mionzi katika anga ya kimataifa iliopo mashariki mwa bahari ya China. Ndege hiyo ilikuwa imetumiwa kugundua ushahidi kuhusu majaribio ya kinyuklia ya Korea Kaskazini.  China imekuwa ikituhumu vitendo vya Marekani karibu na maji hayo yenye utajiri mkubwa yaliopo katika pwani yake ,hatua ambayo imesababisha wasiwasi kati ya mataifa hayo mawili. ''Swala hilo linaangaziwa na China kupitia njia mwafaka ya kidiplomasia mbali na zile za kijeshi'', msemaji wa jeshi la angani la Marekani Luteni kanali Lori Hodge amesema. ''Uzuizi huo haukufanywa kwa njia ya ''utaalamu'' kutokana na hali ya rubani wa ndege hiyo ya China ikiwemo kasi ya ndege zote mbili'', aliongezea akisema uchungzi wa kijeshi unaendelea.

MABOMU YASABABISHA WATU ZAIDI YA ELFU 50 KUHAMA UJERUMANI

Image
Operesheni kubwa ya kuwaondoa wakaazi wengi wa mji wa Hanover ulioko kaskazini mwa Ujerumani, inaendelea, ya kuwahamisha zaidi ya watu elfu 50 baada ya mabomu makubwa ya wakati wa vita vya dunia, kupatikana kama hayajalipuka. Wakaazi hao wanatarajiwa kuondoka majumbani mwao baadaye leo, ili kuwapa nafasi wataalamu wa kutegua mabomu, kuhamishia mahala salama mabomu hayo ambayo yanakisiwa kuwa matano. Operesheni hiyo itachukua siku nzima, na hata zaidi ikiwa mabomu mengineyatapatikana. Washambuliaji walivamia mji wa Hanover mara 125 kwa mabomu, wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Haki miliki ya picha Getty Images.     Wataalamu wanaamini kuwa mabomu ambayo hayakulipuka huenda yako chini ya jengo hili                 Zaidi ya asilimia 20 ya mabomu yaliyoangushwa mjini humo hayakulipuka. Baadhi ya mabomu mengine yalikuwa na vifaa vinavyochukua muda mrefu kulipuka, na ambayo kwa sasa yameanza kuoza, na kusababisha hatari kubwa. C

WAPIGANAJI WA HAMAS WAPATA KIONGOZI MPYA

Image
Ismael Haniyeh ndio kiongozi mpya wa kundi la Hamas Wapiganaji wa Palestina Hamas wamepata kiongozi mpya. Kiongozi huyo ni Ismail Haniyeh ambaye hadi hivi karibuni alikuwa ndio kiongozi wa kundi hilo katika ukanda wa Gaza. Akijulikana kama kiongozi anayetumia akili nyingi wakati wa kutatua maswala, anachukua mahala pake Khaled Meshaal ambaye ameliongoza kundi hilo akiwa ughaibuni kwa miongo miwili. Uchaguzi wa kiongozi mpya ulifanyika kupitia njia ya Video Link kati ya wajumbe waliopo katika ukanda wa Gaza na wale waliopo nchini Qatar ambako Meshaal ana makao yake. Mwandishi wa BBC anasema kuwa bwana Meshaal anaachia ngazi wakati ambapo Hamas limeanza kulegeza msimamo wa kisiasa. Kwa mara ya kwanza wiki iliopita katika sera mpya kundi hilo liliwachilia wito wake wa kuiharibu Israel. Hamas bado lina wapiganaji wake katika eneo la Gaza na bado linaaminika kuwa kundi la kigaidi na Israel Marekani na mataifa ya bara Ulaya. Chanzo: BBC

WAHAMIAJI 239 WAHOFIWA KUZAMA KATIKA AJALI YA MELI WAKITOKEA LIBYA

Image
Wahamiaji 239 wamehofiwa kuzama katika ajali ya meli wakitokea nchini Libya. Hii ni kwa mujibu wa habari kutoka shirika la Wakimbizi UNHCR. Msemaji wa UNHCR mjini Roma Italia amesema kuwa taarifa hizo zimethibitishwa na manusura wa ajali walipofikishwa katika ukingo wa bahari katika kisiwa cha Lampedusa. Mpaka sasa hakuna ambaye amekwishapatikana katika hao 239. Sami alisema kuwa watu 31 wamenusurika katika ajali za meli mbili zilizopata ajali baharini kufuatia dhoruba kali. Walisema kuwa watu 29 walinusurika katika meli ya kwanza huku wengine 120 hawajulikani walipo. Katika jitihada za kuokoa watu, wanawake 2 waliokuwa wakiogelea kujinusuru waliwambia waokoaji kuwa watu hao 120 walikufa katika meli hiyo. Katika matukio yote mawili, wengi wa wahamiaji hao wanaonekana kuwa ni raia kutoka eneo la Jangwa la Sahara. Leonard Doyle, msemaji mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) amesema kuwa watu 4,220 wamepoteza maisha katika mwaka huu 2016 kwenye ajali za meli katik

OBAMA AWATAHADHARISHA WAPIGA KURA KUHUSU TRUMP

Image
Rais Barrack Obama amewahimiza wafuasi wa chama cha Democratic kumpigia kura Hillary Clinton na kuonya kwamba Donald Trump ni tishio kwa haki za kijamii, taifa la Marekani na dunia nzima kwa ujumla. Rais wa Marekani Barrack Obama amewahimiza wafuasi wote wa chama cha Democratic kumpigia kura kwa wingi Hillary Clinton siku ya uchaguzi wiki ijayo na kuonya kwamba Donald Trump mgombea urais wa chama cha Republican ni tishio kwa haki za kijamii ambazo ziliafikiwa kupitia hali ngumu , taifa la Marekani na dunia nzima kwa ujumla. Akigusia chaguo la rais siku ya Jumanne wiki ijayo, rais Barrack Obama alimpuuzilia mbali Trump kuwa mtu asiyestahili kabisa kuwa rais. Kufikia sasa Clinton bado anaonyesha uwezekano wa kuwa rais wa 45 wa Marekani lakini huku zikiwa zimesalia siku sita kabla ya uchaguzi huo mkuu, wafuasi wa chama cha Demokratic bado wako chonjo hasa kutokana na mienendo ya Trump isiyotabirika. Obama aliwaambia wapiga kura katika mji wa Chapel Hill kuwa hatima ya taifa h

VIDEO: TRUMP AKATAA KUJIBU SWALI KUHUSU KUKUBALI MATOKEO KAMA ATASHINDA KWENYE UCHAGUZI

Image
Ni katika Mdahalo wa tatu na wa mwisho ukiofanyika Nevada, Las Vegas. Swali liliulizwa kwa Bwana Trump "utakubali matokeo ya Urais baada ya kushindwa na mpinzania wako Hillary Clinton?" Trump hakujibu moja kwa moja, alisema "nitaliangalia hilo kwa wakati huo". Awali ya hapo Rais Obama alishangazwa na kutokujiamini kwa Trump kuhusu kuwa na mashaka na Uchaguzi hata kabla ya Uchaguzi wenyewe kufanyika. Nitakuandalia makala kamili kutoka kwenye Mdahalo huo. Hii hapa video ikimuonesha Trump alivyokataa kujibu swali aliloulizwa: Video kwa hisani ya France24.

HILLARY CLINTON AMEREJEA KATIKA KAMPENI NA KUMSHAMBULIA TRUMP

Image
Mgombea wa chama cha Democratic katika kinyan'ganyiro cha urais nchini Marekani Hillary Clinton amerejea tena katika kampeni na kutoa kauli ya tahadhari dhidi ya mpinzani wake Donald Trump. Mgombea wa chama cha Democrats Hillary Clinton akiwahutubia wafuasi wake North Carolina Akizungumza katika mikutano miwili tofauti ya kampeni kwenye majimbo mawili, North Carolina na Washington, Hillary Clinton alisema amefurahi kurejea katika kampeni hizo baada ya hapo awali kushauriwa na madaktari kubakia nyumbani hadi atakapopata nafuu kutokana na maradhi ya homa ya mapafu yaliyokuwa yakimkabili. Hali ya afya ya Hillary Clinton ilidhoofika wakati wa kumbukumbu ya mika 15 tangu yalipofanyika mashambulizi ya kigaidi nchini Marekani tarehe 11/9/ 2001. "Ni jambo jema kuwa nimerejea katika kampeni" alisema mgombea huyo wa chama cha Democratic huku akishangiliwa na wafuasi wake alipohutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika eneo la Greensboro, North Carolina

MTU MMOJA AMEJITOA MUHANGA NA KUUA WATU 16 KATIKA MSIKITI WA MOHMAND PAKISTAN

Image
Takribani watu 16 wameuawa na wengine 35 kujeruhiwa katika swala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Mohmand huko Pakistan. Duru za habari zinasema kuwa mtu huyo aliyejitoa muhanga ameua watu 16 na wengine 35 kujeruhiwa walipokuwa wakihudhuria swala ya Ijumaa kaskazini mashariki mwa  Pakistan. Shambulio hilo limetokea katika kijiji cha Anbar Tehsil katika wilaya inayokaliwa na kabila la Mohmand ambapo jeshi la Pakistan limekuwa likipambana na kundi la Taliban. "Swala ya Ijumaa ilikuwa ikiendelea msikitini hapo wakati ambapo mshambuliaji huyo wa kujitoa muhanga alijilipua na kuua waumini 16 na kujeruhi wengine 35" kiongozi mmoja wa Mohmand aliliambia shirika la habari la AFP. Hakujatokea taarifa zozote kuhusu shambulio hilo, lakini kundi la Taliban linashutumiwa kuhusika na shambulio hilo kwa kuwa limekuwa likifanya mashambulio katika maeneo ya mahakama, shule na misikiti. Jeshi la Pakistan limekuwa likifanya operesheni toka Juni 2014 kuangamiza makundi yote ya kigaidi yal

MAPIGANO YAPAMBA MOTO SYRIA KUELEKEA SULUHU YA MGOGORO

Image
Saa chache baada ya Marekani na Urusi kutangaza makubaliano ya kumaliza mgogoro wa kivita uliyodumu kwa miaka mitano nchini Syria, mapigano yemepamba moto upya. Karibu raia 100 wameuawa katika mashambulizi ya angani. Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London,Uingereza, limeripoti siku ya Jumamosi kwamba raia wasiopungua 58 wameuawa katika mkoa unaodhibitiwa na waasi wa Idlib baada ya ndege za kivita kuliripua kwa mabomu soko kaskazini-magahribi mwa mji huo, saa kadhaa baada ya kutangazwa kwa masharti ya makubaliano ya kusitishwa mapigano nchini kote. Mjini Aleppo, jeshi la Syria lilifanya mashambulizi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi katika jitihada za kuimarisha nafasi yake kuelekea usitishaji wa uhasama, unaoanza siku ya Jumatatu wakati wa siku kuu ya Eid al-Adha. "Mapigano yamepamba moto katika maeneo yote ya Aleppo," alisema kapteni Abdul Salam Abdul Razak, msemaji wa kundi la waasi la Brigedi za Nour al-Dine al Zi

MAREKANI NA URUSI ZAKUBALIANA KUSITISHA MAPIGANO SYRIA

Image
Marekani na Urusi zimefikia makubalinao kuhusu mchakato wa kupatikana amani nchini Syria ikiwemo kusitishwa kwa mapigano kote nchini Syria kuanzia Jumatatu wiki ijayo. Makubaliano hayo pia yanajumuisha kuimarisha shughuli za kutolewa kwa misaada na opereshenzi za pamoja za kijeshi kupambana dhidi ya makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali. Makubaliano hayo yaliyofikiwa mapema Jumamosi (10.09.2016) kati ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov yanafuatia mazungumzo ya kina yaliyokuwa yakifanyika mjini Geneva, Uswisi. Lavrov amesema licha ya kuendelea kutoaminiana kati ya pande hizo mbili, wamefanikiwa kuafikiana kuhusu jinsi ya kushirikiana kupambana dhidi ya ugaidi na kuyafufua mazungumzo ya kisiasa ya kupatikana amani nchini Syria kwa njia bora zaidi. Je mzozo wa Syria utakoma sasa? Kerry ambaye alichelewesha kwa siku moja safari yake kutoka Geneva na kurejea Marekani ili kuhakikisha wamefikia makubaliano na mwenzake wa Urusi a

WATU 10 WAMEKUFA KATIKA AJALI YA MOTO KIWANDANI HUKO BANGLADESH

Image
Takribani watu 10 wamekufa katika mlipuko mkubwa wa moto huko Bangladesh kufuatia kulipuka kwa kontena la kuchemshia maji ya moto.  Polisi wamesema kuwa takribani watu 100 walikuwa ndani ya kiwanda hicho chenye jengo la ghorofa 4 ambapo mlipuko ulisikika katika mji wa Tongi. Takribani watu 30 wamejeruhiwa  kutokana na moto huo kusambaa kwa haraka katika jengo hilo. Huduma za dharura zinadai kuwa moto bado unaendelea kuwaka na inasemekana idadi ya watu kufariki katika ajali hiyo inaweza kuongezeka. "Mpaka sasa tumepata uhakika wa watu 10 kufariki. Lakini bado idadi inaweza kuongezeka kwa sababu moto bado ni mkali kushindwa kuzimwa." Inspekta wa Polisi Sirajul Islam aliiambia AFP. Kumekuwa na majanga mengi ya moto viwandani nchini Bangladesh kufuatia kutokuwa na usalama wa kuzuia majanga hayo katika nchi hiyo. Canzo: BBC

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI

Image
Kansela Angela Merkel akihutubia bungeni siku ya Jumatano (7 Septemba 2016). Licha ya chama cha CDU kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi la kwao la Mecklenburg-Vorpommern kutokana na sera yake ya wahamiaji, Kansela Angela Merkel anasema sera yake ni sahihi na kamwe hatarudi nyuma. Vichwa vya habari katika magazeti na ripoti za televisheni na redio mara tu baada ya CDU kushindwa uchaguzi huo wa Jumapili, zilitazamiwa kumrejesha Kansela Merkel nyuma, na hotuba ya leo ilidhaniwa kuwa ingekuwa nyepesi na laini. Lakini hivyo sivyo ilivyokuwa, kwani kwenye hotuba ya bungeni ya leo Jumatano (7 Septemba 2016), ambapo alionekana kusimama imara. "Hali yetu leo ni bora zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka mmoja uliopita kwetu sote. Hapana shaka, bado kuna mambo ya kufanywa. Changamoto kubwa ikiwa kuwarejesha nyumbani wahamiaji ambao hawawezi kubakia hapa na sisi. Na kwa uadilifu kuwahudumia raia wetu, huku tukiwafahamisha kuwa tunapaswa kuwasiaidia wale wenye haki ya kusaidiwa," aliwaambi

RAIS WA UZBEKISTAN AZIKWA KWA HESHIMA YA DINI YA KIISLAMU

Image
Rais wa Uzbekistan, Islam Karimov amezikwa leo kwenye mji wa nyumbani kwake wa Samarkand, ulioko katikati ya nchi hiyo, wakati ambapo taifa hilo limeanza siku tatu za maombolezo ya nchi nzima. Karimov, mwenye umri wa miaka 78 na ambaye ameiongoza Uzbekistan kwa muda mrefu, alifariki dunia jana Ijumaa baada ya kuugua kiharusi mwishoni mwa wiki iliyopita. Waziri Mkuu wa Urusi, Dmitry Medvedev anatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo yatakayofanyika kwa heshima ya dini ya Kiislamu. Mazishi hayo pia yatahudhuriwa na viongozi wengine wa mataifa ya iliyokuwa Umoja wa Kisovieti, akiwemo Rais wa Tajikistan, Emmomali Rakhmon, Rais wa Turkmenistan, Gurbanguly Berdymukhamedov na Waziri Mkuu wa Kyrgyzstan, Belarus na Kazakhstan. Rais wa Marekani, Barack Obama ameelezea kusikitishwa na kifo hicho na amethibitisha kwamba nchi yake iko tayari kuwasaidia wananchi wa Uzbekistan katika kipindi hiki. Waombolezaji wajipanga barabarani Uvumi ulianza kuzagaa siku chache zilizopita kuwa kiongozi h

WAZIRI MKUU WA NEPAL KHADGA PRASAD OLI AMEJIUZURU

Image
Waziri Mkuu wa Nepal Khadga Prasad Oli amejiuziru wadhifa wake ikiwa ni muda mchache kabla ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye katika Bunge la nchi hiyo. Inadaiwa katika kura hiyo Oli angeshindwa. Oli mwenye umri wa miaka 64 alishinikizwa kujiuzuru na wapinzani wa chama chake kufuatia kutoheshimu mgawanyo wa madaraka ambao ndiyo uliompa Uwaziri mkuu miezi 9 iliyopita. "Nimekwisha wasilisha barua yangu ya kujiuzuru kwa Rais nilipokutana naye kabla hata ya Bunge" amesikika akisema Oli aliponukuliwa na The Reuters katika Bunge la Nepal. Oli aliyezaliwa kaskazini mwa Nepal Fenruari 22 mwaka 1952 alikuwa mwanachawa wa Nepal Communist Party mwaka 1970 baada ya kuvutiwa na viongozi wa kikomunisti alipokuwa kijana. Amewahi kutumikia kifungo cha miaka 14 jela. Oli aliingia madarakani Oktoba mwaka jana huku akikosolewa sana na kuwepo kwa maandamano kufuatia kushindwa kuchukua hatua katika tetemeko lililowaacha wananchi katika umaskini mkubwa. Zaidi ya watu 50 wali