MKAZI wa Kijiji cha Ikola katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi , Richard Clavery ( 34 ) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma ya kufukua kaburi la mwanamke, aliyekufa na kuzikwa kaburini humo. Mtu huyo anatuhumiwa kukutwa na waombolezaji, akiwa amevua nguo zake zote na kuzitundika juu ya msalaba, uliosimikwa kaburini hapo. Mwendesha Mashitaka, Godfrey Luzabila alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Ntengwa, Februari 25 mwaka huu kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Februari 18 mwaka huu saa nne usiku nyumbani kwa dada wa marehemu, Lenada Sakafu katika kijiji cha Ikola . Luzabila alidai usiku wa tukio hilo, mtuhumiwa alifika nyumbani kwa Lenada Sakafu na kufukua maiti ya mdogo wa Lenada, Tabu Omera aliyekuwa amezikwa kaburini siku tatu kabla ya tukio hilo. Kaburi alimozikwa marehemu, lilikuwa katika eneo la nyumba ya Lenada. Alidai usiku huo, Lenada akiwa nyumbani hapo pamoja na waombolezaji, wakiwemo majirani na ndugu, ghaf...
Comments
Post a Comment