“Tutawatumia mawaziri vivuli kuhakikisha mawaziri mizigo wanang’oka nafasi zao kwa masilahi na mustakabali wa maendeleo ya nchi yetu” – John Mnyika. Kuna kila dalili kuwa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na zile za Kamati za Bunge zinazosimamia fedha za umma, huenda zikawang’oa baadhi ya mawaziri.Hofu kuu inaonekana kuwakumba baadhi ya mawaziri huku waziri mmoja mwandamizi alisema; “Wengi wetu tumeshikwa na kihoro, hatujui nini kitatokea.”Ni ripoti za aina hiyo zilizowasilishwa bungeni Aprili 2012, zilisababisha kuwapo shinikizo kwa Rais Jakaya Kikwete kupangua baraza lake la mawaziri, Mei 4, 2012 na kuwatupa nje mawaziri hao.Katika panguapangua hiyo, Rais Kikwete aliwatosa mawaziri sita akiwemo Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko na Mbunge wa Moshi Vijijini,Dk Cyril Chami.Wengine waliotoswa kwa shinikizo hilo la wabunge ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu.Pia Naibu Waziri wa Uchukuzi wa wakati huo, Athuman Mfutakamba alitoswa sanjari na Waziri wa Afya, Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya.Katika mkutano huu wa 14 unaoendelea, zipo tetesi kuwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamejipanga kuwang’oa mawaziri kamili sita na manaibu mawaziri saba kwa kushindwa kuwajibika.“Hizi siku nne za taarifa za kamati, inawatia kiwewe baadhi ya mawaziri na hakuna ubishi ripoti hizi zinaweza kuchochea kuwapo uamuzi mgumu,” alidokeza mmoja wa mawaziri waandamizi.Mbunge wa Ubungo na Mkurugenzi wa Habari wa Chadema, John Mnyika, alisema pia kila waziri kivuli wa wizara ambayo imeonekana kuongozwa na waziri mzigo, amepewa maelekezo maalumu.
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

Comments
Post a Comment