“Tutawatumia mawaziri vivuli kuhakikisha mawaziri mizigo wanang’oka nafasi zao kwa masilahi na mustakabali wa maendeleo ya nchi yetu” – John Mnyika. Kuna kila dalili kuwa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na zile za Kamati za Bunge zinazosimamia fedha za umma, huenda zikawang’oa baadhi ya mawaziri.Hofu kuu inaonekana kuwakumba baadhi ya mawaziri huku waziri mmoja mwandamizi alisema; “Wengi wetu tumeshikwa na kihoro, hatujui nini kitatokea.”Ni ripoti za aina hiyo zilizowasilishwa bungeni Aprili 2012, zilisababisha kuwapo shinikizo kwa Rais Jakaya Kikwete kupangua baraza lake la mawaziri, Mei 4, 2012 na kuwatupa nje mawaziri hao.Katika panguapangua hiyo, Rais Kikwete aliwatosa mawaziri sita akiwemo Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko na Mbunge wa Moshi Vijijini,Dk Cyril Chami.Wengine waliotoswa kwa shinikizo hilo la wabunge ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu.Pia Naibu Waziri wa Uchukuzi wa wakati huo, Athuman Mfutakamba alitoswa sanjari na Waziri wa Afya, Dk Haji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya.Katika mkutano huu wa 14 unaoendelea, zipo tetesi kuwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamejipanga kuwang’oa mawaziri kamili sita na manaibu mawaziri saba kwa kushindwa kuwajibika.“Hizi siku nne za taarifa za kamati, inawatia kiwewe baadhi ya mawaziri na hakuna ubishi ripoti hizi zinaweza kuchochea kuwapo uamuzi mgumu,” alidokeza mmoja wa mawaziri waandamizi.Mbunge wa Ubungo na Mkurugenzi wa Habari wa Chadema, John Mnyika, alisema pia kila waziri kivuli wa wizara ambayo imeonekana kuongozwa na waziri mzigo, amepewa maelekezo maalumu.
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

Comments
Post a Comment