Kiongozi wa vuguvugu la Muslim Brotherhood, amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tangu kukamatwa kwake.Hata hivyo mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi Februari 11 mwaka 2014,Wadadisi wanasema ni sehemu ya kampeini ya serikali dhidi ya vuguvugu hilo baada ya jeshi kumuondoa mamlakani aliyekuwa rais Mohamed Morsi.Mohamed Badie -- aliyefikishwa mahakamani na viongozi wengine wa kundi hilo, alikanusha madai kua alitumia kundi hilo kuchochea ghasia.Miongoni mwa washitakiwa wenza wa Badie ni pamoja na Isam al-Iryan, Muhammad al-Biltaji, Basim Udah na Safwat Hijazi. Makosa mengine wanayokabiliwa nayo ni pamoja na kuunda genge la kuwahangaisha watu, uharibifu wa mali ya watu binafsi na kumiliki silaha kinyune na sheria.Makosa wanayokabiliwa nayo yanatokana na ghasia za mwezi Julai ambapo makabiliano yalizuka kati ya wafuasi elfu tano wa Mohammed Morsi pamoja na majeshi katika eneo la Giza na katika msikiti wa Al-Istiqamah baada ya kungo'olewa mamlakani kwa Mohammed Morsi.Hata hivyo Badie Alihoji kwa nini uchunguzi haukufanyika kuhusu kifo cha mwanawe pamoja na kuteketezwa kwa makao makuu ya Brotherhood.Wanafunzi katika chuo kikuu cha Al Azhar wameendelea kuandamana na kulazimisha polisi kuingia chuoni humo ili kusitisha vurugu zao.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment