Kiongozi wa vuguvugu la Muslim Brotherhood, amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tangu kukamatwa kwake.Hata hivyo mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi Februari 11 mwaka 2014,Wadadisi wanasema ni sehemu ya kampeini ya serikali dhidi ya vuguvugu hilo baada ya jeshi kumuondoa mamlakani aliyekuwa rais Mohamed Morsi.Mohamed Badie -- aliyefikishwa mahakamani na viongozi wengine wa kundi hilo, alikanusha madai kua alitumia kundi hilo kuchochea ghasia.Miongoni mwa washitakiwa wenza wa Badie ni pamoja na Isam al-Iryan, Muhammad al-Biltaji, Basim Udah na Safwat Hijazi. Makosa mengine wanayokabiliwa nayo ni pamoja na kuunda genge la kuwahangaisha watu, uharibifu wa mali ya watu binafsi na kumiliki silaha kinyune na sheria.Makosa wanayokabiliwa nayo yanatokana na ghasia za mwezi Julai ambapo makabiliano yalizuka kati ya wafuasi elfu tano wa Mohammed Morsi pamoja na majeshi katika eneo la Giza na katika msikiti wa Al-Istiqamah baada ya kungo'olewa mamlakani kwa Mohammed Morsi.Hata hivyo Badie Alihoji kwa nini uchunguzi haukufanyika kuhusu kifo cha mwanawe pamoja na kuteketezwa kwa makao makuu ya Brotherhood.Wanafunzi katika chuo kikuu cha Al Azhar wameendelea kuandamana na kulazimisha polisi kuingia chuoni humo ili kusitisha vurugu zao.
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment