Jana usiku shujaa wa Afrika Mzee Nelson Mandela alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 95. Amefariki kwa ugonjwa wa maambukizi ya pafu, ugonjwa uliomsumbua kwa muda mrefu. Pia katikati ya mwaka huu alikaa hospitali kwa muda wa miezi 3 na baadaye mwezi wa tisa alitolewa hospitali na kwenda kutibiwa nyumbani kwake Johanesburg mpaka mauti yalipomfika. Rais wa nchi hiyo, Jackob Zuma amesema taifa limempoteza shujaa wao na kwamba mwili wake utasifirishwa kwenda kuhifadhiwa katika mochwari ya mji mkuu Pretoria na kwa taratibu za mazishi zitafanywa Jumamosi ijayo pia atazikwa kwa heshima kubwa ya kitaifa na pia bendera zote zitapepea nusu mlingoti nchini humo kama maombolezo ya shujaa huyo...
MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI..
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment