Jana usiku shujaa wa Afrika Mzee Nelson Mandela alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 95. Amefariki kwa ugonjwa wa maambukizi ya pafu, ugonjwa uliomsumbua kwa muda mrefu. Pia katikati ya mwaka huu alikaa hospitali kwa muda wa miezi 3 na baadaye mwezi wa tisa alitolewa hospitali na kwenda kutibiwa nyumbani kwake Johanesburg mpaka mauti yalipomfika. Rais wa nchi hiyo, Jackob Zuma amesema taifa limempoteza shujaa wao na kwamba mwili wake utasifirishwa kwenda kuhifadhiwa katika mochwari ya mji mkuu Pretoria na kwa taratibu za mazishi zitafanywa Jumamosi ijayo pia atazikwa kwa heshima kubwa ya kitaifa na pia bendera zote zitapepea nusu mlingoti nchini humo kama maombolezo ya shujaa huyo...
MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI..
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...
Comments
Post a Comment