Jana usiku shujaa wa Afrika Mzee Nelson Mandela alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 95. Amefariki kwa ugonjwa wa maambukizi ya pafu, ugonjwa uliomsumbua kwa muda mrefu. Pia katikati ya mwaka huu alikaa hospitali kwa muda wa miezi 3 na baadaye mwezi wa tisa alitolewa hospitali na kwenda kutibiwa nyumbani kwake Johanesburg mpaka mauti yalipomfika. Rais wa nchi hiyo, Jackob Zuma amesema taifa limempoteza shujaa wao na kwamba mwili wake utasifirishwa kwenda kuhifadhiwa katika mochwari ya mji mkuu Pretoria na kwa taratibu za mazishi zitafanywa Jumamosi ijayo pia atazikwa kwa heshima kubwa ya kitaifa na pia bendera zote zitapepea nusu mlingoti nchini humo kama maombolezo ya shujaa huyo...
MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI..
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment