Skip to main content

TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA


Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya.

Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili.

Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz.

Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika.

Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya HAPA ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya HAPA ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa:

1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye
Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno kutoka Vyuo Vikuu/Vyuo
vinavyotambuliwa na Serikali waliomaliza mafunzo ya kazi“Internship” ya muda
usiopungua miezi kumi na miwili na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari
Tanganyika (Medical Council of Tanganyika).

Kazi na majukumu:
i. Kufanya kazi zote za matibabu hospitalini zinazohusiana na magonjwa ya
kinywa na meno.
ii. Kushiriki katika kutengeneza na kusimamia utekelezaji wa Sera ya Serikali
juu ya afya ya kinywa na meno.
iii. Kusimamia utekelezaji wa mipango ya kitaifa inayohusu afya ya kinywa na
meno.
iv. Kutayarisha elimu ya kujiendeleza ya watumishi wa afya ya kinywa na
meno.
v. Kuchunguza, kufuatilia na kuzuia milipuko ya magonjwa .
vi. Kubuni na kutayarisha mikakati ya kuinua ubora wa huduma ya fani yake.
vii. Kuandaa upatikanaji wa vifaa na mahitaji mengine ya tiba ya meno katika
ngazi ya taifa.
viii. Kushauri wizara kuhusu uendeshaji wa shughuli za afya ya kinywa na
meno nchini.
ix. Kubuni, kusimamia na kuendesha utafiti katika maeneo mbalimbali ya afya.
x. Kufundisha wanafunzi katika vyuo vya afya vilivyo katika eneo lake la kazi.


2 Afisa Mteknolojia Daraja la II TGHS E – (NAFASI 7)

Afisa Mteknolojia - Daraja la II - Viungo Bandia – (Nafasi 5)
Afisa Mteknolojia - Daraja la II - Radiografia – (Nafasi 2)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada ya Sayansi kutoka chuo kinachotambuliwa na
Serikali na kusajiliwa na Mabaraza ya Taaluma husika.

Kazi na majukumu:
Afisa Mteknolojia Daraja la II - Viungo Bandia
i. Kusimamia kliniki ya wanaohitaji viungo bandia
ii. Kukagua mlemavu ili kuelewa matatizo yatakayohitaji viungo bandia
iii. Kupanga taratibu za uundaji sahihi wa viungo bandia.
iv. Kuchukua vipimo vinavyohusika na utengenezaji viungo bandia.
v. Kutengeneza Viungo bandia kutokana na ulemavu uliothibitika
vi. Kumvalisha mlemavu viungo bandia na kufanya marekebisho ya
lazima inapobidi
vii. Kuwafundisha walio chini yake.
viii. Kufundisha wanafunzi katika vyuo vya viungo bandia
ix. Kutoa ushauri nasaha kwa wanohitaji viungo bandia
x. Kusimamia shughuli zote zinazohusu ubunifu, utengenezaji, uangalizi
na utunzaji wa malighafi ya vitimwendo.
xi. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake

Kazi na majukumu:
Afisa Mteknolijia - Daraja la II - Radiografia
i. Kufanya vipimo vya aina mbalimbali vya radiolojia.
ii. Kutunza mitambo na vifaa vya Radiolojia katika eneo lake
 la kazi. 
iii. Kuhakikisha ubora wa picha za X-Ray.
iv. iv. Kutunza picha za wagonjwa hadi majibu yanapowafikia madaktari
waliowatuma wagonjwa
v. Kusimamia watumishi walio chini yake
vi. Kuandaa vifaa vya tiba/uchunguzi na kusimamia utakasaji vifaa
vii. katika eneo lake la kazi (sterilization)
viii. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
ix. zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake


3 Mteknolojia Daraja la II – TGHS B (NAFASI 28)
i. Mteknolojia Daraja II –Viungo Bandia (Nafasi 11)
ii. Mteknolojia Daraja II – Macho (Nafasi 15)
iii. Mteknolojia Daraja II – Radiolojia (Nafasi 2)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne/sita wenye Stashahada katika fani ya
Uteknolojia Viungo Bandia ya muda wa miaka mitatu kutoka Chuo
kinachotambuliwa na Serikali na ambao wamesajiliwa na Baraza la Kitaaluma.

Kazi na majukumu:
Mteknolojia Daraja II –Viungo Bandia
i. Kutoa ushauri katika kliniki ya viungo bandia
ii. Kutunza takwimu za walemavu
iii. Kubuni vifaa vitakavyotumika kwa mlemavu (Prosthesis/Orthosis).
iv. Kufanya marekebisho/matengenezo ya vifaa vya walemavu
(Prosthesis/Orthosis)
v. Kukagua mlemavu ili kuelewa aina ya kiungo bandia kinachohitajika.
vi. Kupanga taratibu za uundaji sahihi wa viungo bandia.
vii. Kuchukuwa vipimo (cast) vinavyohusika na utengeneji viungo bandia
viii. Kutengeneza Viungo bandia kutokana na ulemavu uliyothibitika
(Prosthesis/Orthosis)
ix. Kumvalisha mlemavu viungo bandia na kufanya marekebisho ya
lazima inapobidi (Prosthesis/Orthosis)
x. Kumfundisha mlemavu matumizi na usafi wa viungo bandia
(osthesis/Orthosis)
xi. Kupanga kazi na kuwafundisha walio chini yake.
xii. Kutoa ushauri kuhusu matumizi bora ya viatu.
xiii. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake

4. Mteknolojia Daraja II – Macho
i. Kufanya uchunguzi wa upeo wa kuona na kutibu
ii. Kurufaa wagonjwa kwenye ngazi za juu, zinazohitaji utaalamu zaidi
iii. Kutoa ushauri nasaha
iv. Kutunza na kurekebisha uharibifu wa vifaa vya macho
v. Kutengeneza miwani na kurekebisha miwani aina zote
vi. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake.
 
Mteknolojia Daraja II – Radiolojia
(i) Kuwapima wagonjwa wanaolekezwa kwenye eneo lake la kazi
(ii) Kutunza mitambo na vifaa vya Radiolojia katika eneo lake la
kazi
(iii) Kukagua picha za X-Ray zilizopimwa kwa ubora na
kutosheleza (diagnostic quality)
(iv) Kutunza picha za wagonjwa hadi majibu yanapowafikia
madaktari waliowatuma wagonjwa
(v) Kusimamia watumishi walio chini yake
(vi) Kutoa Ushauri kuhusu masuala ya na kazi za Radiolojia na
Mionzi katika eneo lake la kazi.
(vii) Kuandaa vifaa vya tiba/uchunguzi na kusimamia utakasaji vifaa
katika eneo lake la kazi (sterilization)
(viii) Kutoa mafunzo ya awali kwa watumishi wanaopangiwa kazi
katika eneo lake la kazi.
(ix) Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake


4 Afisa Lishe Daraja – TGS D (NAFASI 10)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza ya lishe, Sayansi Kimu na Lishe, au
Sayansi ya Chakula na teknolojia ya Chakula (BSc - Nutrition, Home
Economics and Nutrition, Food Science and Technology, Food Science) au
Stashahada ya Juu ya Lishe (Higher Diploma in Nutrition) kutoka Chuo cha
elimu ya Juu kinachotambuliwa na Serikali.
Kazi na Majukumu
i. Kukusanya taarifa na takwimu za lishe kutoka kwa wadau na
makundi mbalimbali na kutoa ushauri kuhusu lishe bora katika 5
ngazi ya wilaya
ii. Kuchambua takwimu za lishe na kuandaa taarifa ya watoto na
makundi mengine yenye lishe duni.
iii. Kushiriki katika kuandaa mipango na bajeti ya lishe katika ngazi
ya wilaya
iv. Kutoa taarifa za mara kwa mara za hali ya lishe katika ngazi ya
wilaya
(i) Kusimamia kazi za lishe katika wilaya.
v. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake


5 Msaidizi wa Afya – TGHOS A (NAFASI 174)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha Nne waliofuzu mafunzo ya mwaka mmoja
katika fani ya Afya, Afya Ngazi ya Jamii (NTA level 4) au mafunzo yoyote
yanayofanana na hayo kutoka Vyuo vya Afya vinavyotambuliwa na Serikali.
Kazi na Majukumu
i. Kufanya usafi wa vifaa vya kazi, maeneo ya kutolea huduma za afya
pamoja na mazingira yanayozunguka kituo.
ii. Kusaidia mgonjwa asiyejiweza kwa mfano, kumlisha, kwenda haja, usafi
wa mwili, nk.
iii. Kukusanya nguo chafu na kuzipeleka kufuliwa (Laundry).
iv. Kupeleka sampuli za mgonjwa kwa ajili ya vipimo vya maabara na
kufuatilia majibu.
v. Kuwasafirisha wagonjwa kati ya ldara moja na nyingine ndani ya kituo cha
kutolea huduma za afya.
vi. Kutunza vifaa vya usafi.
vii. Kupokea, kupeleka chumba cha kuhifadhi, kuosha na kutunza maiti.
viii. Kufanya shughuli nyingine atakazopangiwa na kiongozi wake wa kazi.
ix. Kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa usafi wa mazingira na mwili ili
kujikinga na milipuko ya magonjwa.
x. Kufanya shughuli nyingine atakazopangiwa na kiongozi wake wa kazi.


6 Muuguzi II – TGHS A (NAFASI 20)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne au Sita wenye cheti cha
Uuguzi cha miaka miwili kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali na
kuandikishwa (Enrolled) na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania.

Kazi na Majukumu
i. Kufanya kazi za kiuguzi za kuhudumia wateja katika jamii, hospitali na
sehemu zote zinapotolewa huduma za afya.
ii. Kusimamia na kuratibu kazi zote za wahudumu wa afya katika sehemu
yake ya kazi.
iii. Kukusanya takwimu na kutayarisha taarifa za utendaji wake wa
kazi.
iv. Kutoa huduma kwa wagonjwa majumbani.
v. Kutoa ushauri nasaha.
vi. Kutoa huduma za kinga na uzazi wa mpango.
vii. Kutoa huduma za uzazi na afya ya mtoto.
viii. Kuelimisha wagonjwa na jamii kuhusu matatizo yao ya kiafya.
ix. Kufuatilia utunzaji wa vitendea kazi katika maeneo yake ya kazi.
x. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi
zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake.


7 Afisa Fiziotherapia Daraja la II -TGHS C (NAFASI 9)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye
Shahada ya Fiziotherapia (BSc in Physiotherapy) kutoka Vyuo Vikuu
vinavyotambuliwa na Serikali waliomaliza “Internship” na kupata usajili
(Full Registration) kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical
Council of Tanganyika).

Kazi na Majukumu
i. Kufanya kazi zote za Mfiziotherapia hospitalini zinazohusiana na
magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa ya watoto, wazee, na wote
waliolazwa.
ii. Kuchunguza mgonjwa, kupanga matibabu kulingana na tatizo la
mgonjwa na kufuatilia hali ya mgonjwa husika.
iii. Kutoa ushauri wa tiba na rufaa ya mgonjwa kwa kada nyingine za afya
kulingana na tatizo la mgonjwa.
iv. Kutoa na kusimamia elimu ya Fiziotherapia, Utengamao na tiba na
kuboresha afya ya mwili na viungo katika Wilaya na Mikoa au eneo lake la
kazi.
v. Kutoa ushauri nasaha wa utengamao kwa wagonjwa katika jamii (CBR).
vi. Kutunza takwimu za wagonjwa wa Fiziotherapia na watu wenye ulemavu
na kuzitumia kama inavyoelekezwa katika misingi ya MTUHA.
vii. Kutathimini huduma za Fiziotherapia na Utengamao katika eneo lake la
kazi.
viii. Kusimamia na kuelekeza watumishi walio chini yake.
ix. Kuandaa mipango na makisio ya bajeti ya huduma za Fiziotherapia katika
eneo lake la kazi.


8 Tabibu Meno Daraja la II – TGHS B (NAFASI 2)
7
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne au Sita wenye Stashahada
ya Tabibu Meno ya muda wa miaka mitatu kutoka Chuo kinachotambuliwa
na Serikali.

Kazi na Majukumu
i. Kutambua na kutibu magonjwa ya kawaida.
ii. Kusimamia utendaji wa watumishi walio chini yake na kufanya upasuaji
mdogo.
iii. Kushiriki katika kupanga na kutekeleza Huduma za Afya Msingi.
iv. Kushauri na kuhamasisha wananchi kuchangia huduma za Afya za Mfuko
wa Afya ya Jamii.
v. Kuweka kumbukumbu za vifaa na zana za kutolea huduma.
vi. Kuweka kumbukumbu, kuandaa na kutoa taarifa za utekelezaji.
vii. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.


9 Tabibu Daraja la II – TGHS B (Nafasi 23)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne au Sita wenye Stashahada
ya Utabibu ya muda wa miaka mitatu kutoka Chuo kinachotambuliwa na
Serikali na ambao wamesajiliwa na Baraza la Kitaaluma.

Kazi na Majukumu
viii. Kutambua na kutibu magonjwa ya kawaida.
ix. Kusimamia utendaji wa watumishi walio chini yake na kufanya upasuaji
mdogo.
x. Kushiriki katika kupanga na kutekeleza Huduma za Afya Msingi.
xi. Kushauri na kuhamasisha wananchi kuchangia huduma za Afya za Mfuko
wa Afya ya Jamii.
xii. Kuweka kumbukumbu za vifaa na zana za kutolea huduma.
xiii. Kuweka kumbukumbu, kuandaa na kutoa taarifa za utekelezaji.
xiv. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.


10 Katibu wa Afya Daraja la II – TGHS C (NAFASI 2)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne au Sita wenye Shahada ya
Uongozi wa Huduma za Afya (Health Services Administration) kutoka Chuo
Kikuu kinachotambuliwa na Serikali.
Kazi na Majukumu
i. Kutoa ushauri wa kiutawala na uendeshaji katika masuala ya kila siku
kuhusu utekelezaji wa shughuli za afya kwa viongozi na wadau mbalimbali.
ii. Kusimamia rasilimali na nyenzo za kuendeshea huduma za afya.
iii. Kuratibu utayarishaji wa mipango ya afya katika sehemu yake ya kazi.
iv. Kuratibu maandalizi ya makisio ya fedha ya shughuli zinazohusiana na
afya.
v. Kutayarisha taarifa za shughuli za uendeshaji na utekelezaji wa mwezi,
robo mwaka na mwaka mzima.
vi. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.


11 Daktari Msaidizi Daraja la II – TGHS C (NAFASI 4)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne au Sita wenye Stashahada
ya juu ya Tiba kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali walio na leseni ya
kufanya kazi kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika pamoja na uzoefu wa
kazi kwa muda usiopungua miaka mitatu.

Kazi na Majukumu
i. Kutambua matatizo ya wagonjwa na kutoa huduma za tiba, kinga na
huduma kwa kina mama na watoto.
ii. Kufanya upasuaji wa dharura na wa kawaida.
iii. Kupanga, kutekeleza na kutathmini huduma za afya sehemu za kazi.
iv. Kupanga utekelezaji wa mipango ya kukabili majanga na dharura
mbalimbali.
v. Kufanya utafiti katika maeneo mbalimbali ya afya ili kuboresha utoaji wa
huduma.
vi. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.


12 Mteknolojia Msaidizi Daraja la II - Maabara – TGHS A (NAFASI 7)
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne au Sita wenye cheti katika
fani ya Maabara kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali na ambao
wamesajiliwa na Baraza la kitaaluma.

Kazi na Majukumu
i. Kuandaa vitendanishi (reagents) vya kufanyia vipimo vya maabara.
ii. Kufanya kazi za awali sampuli zinazotolewa maabara.
iii. Kukusanya damu kutoka kwa wagonjwa na watu wanaojitolea.
iv. Kurekodi matokeo ya vipimo kwenye regista.
v. Kutayarisha vifaa vya kazi.
vi. Kuhifadhi kwa mujibu wa taratibu sampuli zote zinazohitaji kuhifadhiwa
baada ya uchunguzi.
vii. Kufanya kazi nyinge atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.


A. Maelekezo ya Kuzingatiwa kwa waombaji
i. Waombaji watakaochaguliwa watapangiwa kazi kwenye maeneo yenye
upungufu mkubwa wa wataalam wa Kada za Afya, na hakutakuwa na
kubadilisha kituo pindi watakapopata nafasi hiyo. Maeneo hayo ni kama
ifuatavyo; Hospitali za Rufaa za Mikoa; (1) Kigoma; (2) Katavi; (3) Sumbawanga;
(4) Songwe; (5) Njombe; (6) Ruvuma; (7) Mtwara; (8) Lindi; (9) Simiyu; (10)
Geita; (11) Shinyanga; (12) Tabora; (13) Singida; (14) Manyara; na (15) Mara;
Hospitali za Kanda, Chato na Mtwara, Hospitali ya Magonjwa Ambukizi
Kibong’oto pamoja na Vyuo vya Afya. Hivyo, waombaji wawe tayari kupangiwa
katika maeneo yaliyoainishwa hapo juu.
ii. Waombaji ambao hawatakuwa tayari kwenda kwenye maeneo tajwa hapo juu
inashauriwa kutotuma maombi.
iii. Waliopo masomoni hawaruhusiwi kuomba nafasi hizi za ajira.
iv. Mwombaji atapaswa kuchagua maeneo matatu ambayo angependa kupangiwa
kazi endapo atachaguliwa.
v. Mwombaji mwenye nia ya kwenda kufundisha katika Vyuo vya Afya aainishe
wakati wa kutuma maombi kwenye mfumo pamoja na barua ya maombi.
vi. Nakala za vyeti vyote vithibitishwe na Mahakama au Wakili.

B. Sifa za ujumla kwa Mwombaji:
i. Awe raia wa Tanzania.
ii. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 45.
iii. Asiwe Mwajiriwa wa Serikali au Mwajiriwa wa Hospitali za Mashirika ya Dini
ambaye mshahara wake unalipwa na Serikali.
iv. Mwombaji aliyewahi kuajiriwa Serikalini na kupata cheki namba, atatakiwa
kuzingatia Utaratibu wa kuomba Kibali cha kurejea katika Utumishi wa Umma na
kuendelea kutumia Cheki Namba baada ya kuacha kazi kama ilivyobainishwa
kwenye Waraka Na. CCB.228/271/01 wa tarehe 7 Agosti, 2012.
v. Mwombaji awe na sifa na weledi kwa Mujibu wa Waraka wa Maendeleo ya
Utumishi Namba. 1 wa mwaka 2009 kuhusu kada zilizo chini ya Wizara ya Afya
kama zilivyoainishwa hapo juu.

C. Maombi yote yaambatishwe na;-
i. Nakala ya cheti cha kuzaliwa.
ii. Nakala ya cheti cha Kidato cha Nne au/na cha Sita au Stashahada kulingana na
Kada ya Mwombaji. Kwa aliyesoma nje ya nchi au mitaala ya nje waambatishe
cheti cha Ithibati kutoka Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).
iii. Nakala ya Vyeti vya Taaluma (Cheti na Transcripts). Aidha, waliosoma vyuo vya
nje ya Nchi, waambatishe cheti cha Ithibati kutoka TCU.
iv. Wasifu (C.V).
v. Nakala ya cheti cha Usajili na Leseni hai ya taaluma husika (Full Registration &
Valid Licence).
vi. Nakala ya cheti cha Mafunzo kwa Vitendo (Internship)
vii. Picha ndogo (passport size) moja na iwekwe kwenye mfumo.
viii. Nakala ya kitambulisho cha uraia (NIDA)/Namba ya Utambulisho ya NIDA.
ix. Iwapo majina yako yanatofautiana katika vyeti vyako pamoja na cheti cha
kuzaliwa na NIDA hakikisha unawasilisha kiapo cha majina (Deed Pool) kutoka
kwa Msajili wa Viapo na kusajiliwa na Msajili wa Hati, Wizara ya Ardhi na
Maendeleo ya Makazi.

D. Namna ya kuwasilisha maombi:
Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa
Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika
kupitia tovuti ajira.moh.go.tz.

Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika.

Imetolewa na:
KATIBU MKUU
WIZARA YA AFYA
S.L.P 743, DODOMA
20/10/2023

Comments

Popular posts from this blog

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MOVIE: X-MEN APOCALYPSE RELEASED TODAY

  Release date: May 27, 2016 Director: Bryan Singer Starring: James McAvoy Jennifer Lawrence Oscar Isaac Michael Fassbender Rose Byrne Sophie Turner Synopsis: In this comic-book adventure set in the 1980s, the X-Men are forced to confront an ancient mutant called Apocalypse (Oscar Isaac). After the resurrected beast recruits a super-team to take over the world and destroy hunmanity, Professor X (James McAvoy) and his charges must come to the rescue for the fate of the planet. The film co-stars Michael Fassbender, Jennifer Lawrence and Olivia Munn.

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD