Skip to main content

MWILI WA NELSON MANDELA KUZIKWA LEO KIJIJINI KWAKE QUNU

NDEGE ya kijeshi aina ya C-130 Hercules iliyobeba mwili wa Rais wa Kwanza Mzalendo wa Afrika Kusini, ilitua Uwanja wa Ndege wa Mthatha jana majira ya saa 6.37.Ikisindikizwa na ndege nyingine mbili za kijeshi, iliruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kijeshi wa Waterkloof, Pretoria saa 4:58, tayari kwa safari ya mwisho ya kuuhifadhi mwili wa Mandela kwa maziko kijijini kwake Qunu katika Jimbo la Eastern Cape.Mwili wa mwanamapinduzi huyo kipenzi cha dunia, unatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya familia ya Mandela, shughuli inayotarajiwa kuanza saa 3 asubuhi.Shujaa huyo wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi, alifariki dunia Alhamisi ya Desemba 5, 2013 saa 2:50 usiku nyumbani kwake, Mtaa wa Laa Namba 12, Houghton jijini Johannesburg akiwa amezungukwa na wanafamilia wote, wakiwemo mkewe Graca Machel na mtalaka wake, Winnie Medikizela –Mandela na mtoto wake mkubwa, Makaziwe Mandela.Tayari Serikali imetangaza leo kuwa siku ya mapumziko, ili kuwawezesha wananchi kufuatilia maziko ya kiongozi huyo ambaye tangu kufa kwake siku kumi zilizopita, amekuwa gumzo kubwa kutokana na heshima aliyojiwekea kote duniani.Kama ilivyokuwa katika miji ya Soweto na Pretoria ulikoagwa mwili wa shujaa huyo aliyeaga dunia akiwa na umri wa miaka 95, Mji wa Mthatha nao ulifurika umati wa wananchi ambao bila kutarajia, walijikuta wakitengeneza mstari mrefu kutoka katikati ya mji hadi uwanja wa ndege kuulaki mwili wa shujaa wao.Na baada ya kutua, mwili huo ulizunguka katika mitaa ya Mthatha na baadaye kusafirishwa kwa msafara mkubwa wa magari na pikipiki za kijeshi hadi Qunu, umbali wa kilomita 31 kutoka Mthatha, huku anga lote la barabara iliyotumika kusafirisha mwili huo ikilindwa kwa helikopta za kijeshi.Akizungumza kutoka Qunu mapema, mmoja wa watu walioteuliwa na familia kusimamia maandalizi ya mazishi, Phathekile Holomisa kabla na kupaa kwa ndege na wakati wote wa safari angani, wazee wa familia walizungumza na mwili wa marehemu mithili ya mtu anayesikia, wakiutaarifu juu ya safari nzima kuelekea Qunu.“Wanazungumza na Mandela kama mtu aliye hai,” alisema Holomisa na kuongeza;” Hii ni kwa sababu tunaamini kiroho bado yu hai.” Mwili wa Mandela uliwasili kijijini Qunu saa 9:26 alasiri, huku mji wote ukiwa na umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza kumlaki shujaa wao. Mara baada ya ujio wa mwili huo, helikopta nne za kijeshi zilionekana zikizunguka anga la Qunu.Tutu kutomzika `swahiba’ wakeLicha ya kuwa rafiki wa siku nyingi wa Mzee Mandela, taarifa za kushangaza zinasema kuwa, Askofu mashuhuri mstaafu wa Kanisa la Anglikana Afrika Kusini, Desmond Tutu ambaye pia ni Mshindi wa Nishani ya Amani ya Nobel, hatashiriki katika shughuli ya kuupumzisha kaburini mwili wa Mandela leo kijijini Qunu.“Hakuna taarifa zaidi zitakazotolewa kuhusiana na Askofu Tutu kutomzika Mandela,” anasema Mpho Tutu, binti wa Askofu Tutu ambaye ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa taasisi ya Desmond Tutu na mkewe Leah. “Askofu hakualikwa, hivyo hatakwenda,” alikaririwa na kusisitiza kutozama katika kuelezea suala hilo.Taarifa za baadaye kutoka Ikulu ya Afrika Kusini zinasema, Askofu Tutu amealikwa kwenda Qunu. “Askofu Tutu si mtu wa kawaida, ana nguvu na ushawishi ndani na nje. Ni mtu muhimu nchini mwetu, yupo katika orodha yetu,” anasema Mac Maharaj wa Ikulu ya Afrika Kusini.Hata hivyo, vyombo vya habari vimedokeza kuwa, huenda hakualikwa kutokana na misimamo yake `migumu’ dhidi ya serikali ya sasa inayoongozwa na Jacob Zuma.Vyombo hivyo vimeongeza kuwa, Tutu hakuwamo katika orodha ya wasemaji siku ya mazishi ya kitaifa ya Mzee Mandela kwenye Uwanja wa Soka wa FNB, Soweto Jumanne wiki hii.Hata hivyo, katika dakika za mwisho aliombwa kutoa `neno’ baada ya umati wa waombolezaji kumzomea Rais Zuma. Askofu Tutu aliweza kupoza hasira za wananchi hao wa Afrika Kusini, baada ya kuzungumza kwa ukali akisema; “Tuioneshe dunia tumekuja hapa kumuaga shujaa wetu.Lazima tuoneshe kuwa sisi ni watu wenye nidhamu, tutulie na ikiwezekana kwa ukimya wenu nisikie sauti ya pini ikidondoka.”Alimmwagia sifa Mandela kuwa alikuwa mtu wa maajabu na alionesha maajabu akiwa hai kutokana na matendo yake yanayopaswa kuigwa na hata baada ya kuaga dunia, kwani licha ya kuiliza dunia nzima, amefanikiwa pia kuwakutanisha viongozi mahasimu wa kisiasa duniani katika uwanja mmoja wakimuaga.Miongoni mwa viongozi mahasimu waliokutana ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe aliyekutana na Rais Barack Obama na Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron.Obama na Cameron waliweka vikwazo vya kiuchumi kwa Zimbabwe wakipinga matokeo ya uchaguzi uliompa Mugabe ushindi wa asilimia 61 dhidi ya wapinzani wake, wakidai kuwa kiongozi huyo alichakachua kura.Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Natanyahu ambaye awali aliripotiwa kutokwenda, alifika na kukaa katika uwanja mmoja na Rais wa Mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, licha ya kuwa na ugomvi wa muda mrefu na unaoendelea baina yao.Pia Rais Obama, alikutana na hasimu wa nchi yake wa siku nyingi, Rais Raul Castrol wa Cuba, ambao uhusiano wao umekuwa ukidorora tangu Mapinduzi ya Cuba ya mwaka 1959.Kutokana na uhusiano mbovu kati ya nchi hizo, mpaka leo Marekani haina uhusiano wa kibalozi na Cuba, huku nchi hiyo ikiweka katika sheria zake vizuizi kwa kampuni za Marekani kufanya biashara na Cuba.Nchini Marekani, wachambuzi wa kisiasa walishangazwa na uamuzi wa familia za kisiasa za Obama, George W. Bush na Bill Clinton, kupanda ndege moja kwenda Afrika Kusini kumuaga Mandela.

Comments

Popular posts from this blog

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MOVIE: X-MEN APOCALYPSE RELEASED TODAY

  Release date: May 27, 2016 Director: Bryan Singer Starring: James McAvoy Jennifer Lawrence Oscar Isaac Michael Fassbender Rose Byrne Sophie Turner Synopsis: In this comic-book adventure set in the 1980s, the X-Men are forced to confront an ancient mutant called Apocalypse (Oscar Isaac). After the resurrected beast recruits a super-team to take over the world and destroy hunmanity, Professor X (James McAvoy) and his charges must come to the rescue for the fate of the planet. The film co-stars Michael Fassbender, Jennifer Lawrence and Olivia Munn.

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD