Venance Blog inawatakieni HERI YA KRISMAS. Mpendwa msomaji wa blog hii, leo Wakristu duniani kote wanaadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwokozi wao, Yesu Kristu aliyezaliwa takribani miaka 2000 iliyopita. Venance Blog inakukumbusha katika sikukuu hii kama ni mnywaji usilewe sana na pia ukumbuke ugonjwa hatari wa UKIMWI hasa siku kama hii ya leo kuwa makini sana, pia tuwasaidie watoto wetu au wadogo zetu kuvuka mabarabara salama huko mitaani kwetu. Krismasi ni siku ya furaha na kuoneshana upendo, hivyo tupendane wote kwa pamoja.
HERI YA KRISMAS NA KRISMAS YENYE FURAHA SHEREHEKEA KWA AMANI NA UPENDO!!!
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

Comments
Post a Comment