Serikali ya Somalia imesema haiwezi kuhusishwa na kesi ya mwananamke ambaye amehukumiwa kifungo jela baada ya kusema kwamba alibakwa, ikisema hili ni suala la kisheria.Msemaji waserikali Ridwaan Haji amesema polisi na mahakama walifanya uchunguzi wa kina, ambao matokeo yake ni kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka kumi na tisa kuhukumiwa kifungo jela na waandishi wawili wa habari walioripoti habari hiyo nao pia wakahukumiwa.Mwananamke huyo ambaye amehukumiwa miezi sita kifungo cha nyumbani, atabakia nyumbani kwake kipindi chote hicho. Amesema alibakwa akiwa ameelekezewa bunduki na wanaume wawili.Sio mara ya kwanza kwa mwanamke Somalia kudai kuwa amebakwa.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment