Maelfu ya waandamanaji wanaopinga serikali wamefurika katika barabara za mji mkuu wa Thailand ,Bangkok licha ya serikali kutangaza uchaguzi wa mapema nchini humo.Waziri mkuu Yingluck Shinawatra alitoa taarifa katika Runinga kabla ya maandamano hayo kuanza na kusema kuwa analivunja bunge ili kuitisha uchaguzi mpya nchini humo hivi karibuni.Kiongozi wa maandamano hayo Suthep Thauksuban amesema kuwa ataendelea na vita hivyo na akawaambia waandamanaji kuwa wameshinda vita vikubwa dhidi ya serikali.Kiongozi huyo alikuwa amekataa kufanyika kwa uchaguzi mpya na badala yake anataka kubadilishwa kwa serikali hiyo na kile alichokitaja kama baraza la raia.Wabunge wote wa chama cha upinzani cha Demokrat walijiuzulu bungeni hapo jana.
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment