MAANDAMANO YAKITHIRI BANGKOK, THAILAND

Maelfu ya waandamanaji wanaopinga serikali wamefurika katika barabara za mji mkuu wa Thailand ,Bangkok licha ya serikali kutangaza uchaguzi wa mapema nchini humo.Waziri mkuu Yingluck Shinawatra alitoa taarifa katika Runinga kabla ya maandamano hayo kuanza na kusema kuwa analivunja bunge ili kuitisha uchaguzi mpya nchini humo hivi karibuni.Kiongozi wa maandamano hayo Suthep Thauksuban amesema kuwa ataendelea na vita hivyo na akawaambia waandamanaji kuwa wameshinda vita vikubwa dhidi ya serikali.Kiongozi huyo alikuwa amekataa kufanyika kwa uchaguzi mpya na badala yake anataka kubadilishwa kwa serikali hiyo na kile alichokitaja kama baraza la raia.Wabunge wote wa chama cha upinzani cha Demokrat walijiuzulu bungeni hapo jana.

Comments

Popular Posts

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

VAN VICKER AKUMBWA NA MAFURIKO AKIELEKEA KWAKE

ACTION MUVI MPYA INATOKA AGUST 2, SNIPER: GHOST SHOOTER

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

QUOTES BY BOB MARLEY