Posts

Showing posts with the label Fahamu

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

Image
10. YUSUF MANJI Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini. 9. FIDA RASHID Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine. 8. GHALIB SAID MOHAMMED Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Image
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba

ZIJUE FAIDA NA HASARA ZA KUWA NA AKAUNTI BINAFSI "PRIVATE" KATIKA MTANDAO WA INSTAGRAM

Image
Uhali gani mpenzi msomaji wa segment yetu ya Fahamu? Nakukaribisha katika segment yetu ya kila siku ya Fahamu, kama ilivyo kawaida, hapa nakufahamisha mambo kadhaaa ambayo labda hukuyafahamu ama uliyafahamu ila si kwa kina basi huwa nakufahamisha hapa. Kumekuwepo na akaunti nyingi binafsi hasa hasa zile za watoto wa kike kwenye mtandao wa Instagram. Kuna faida na hasara za kuweka akaunti yako kuwa binafsi na hasara zake pia. Leo nakuletea mada kuhusu faida na hasara za kuwa na akaunti binafsi ambazo hizi ndizo zinazotofautisha kua na akaunti huru na binafsi: Huu ni mfano wa akaunti binafsi ya Instagram ukiitembelea FAIDA ZAKE 1. KUA NA MAMLAKA YA KURUHUSU AMA KUTORUHUSU NANI AKUFUATE Unapaokuwa na akaunti private ya instagram basi unakua na uwezo wa kuamua mwenyewe kwamba nani akufuate (following) na nani asikufuate kwa mfano unaweza kuzuia watu ambao ni wanafamilia ikiwa akaunti yako ina mambo yako ya siri lakini hii haizuii wao kuangalia kwa maana bado wanaweza kutum

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Image
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

Image
Leo nakufahamisha baadhi ya mambo ambayo huenda hukuyafahamu ama ulichukulia kawaida tu. Mambo hayo ni hapahapa Tanzania.  Tanzania ina eneo la kilomita za mraba 945,087. Ina jumla mikoa 31 kote bara na visiwani. Mpaka kufikia mwaka 2017 idadi ya watu nchini ilikadiriwa kuwa milioni 52.554 kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya takwimu. Twende sasa tuanze kuhesabu moja baada ya jingine #1 . Wimbo wa taifa "Mungu Ibariki Tanzania"  ni wimbo unaofanana na nyimbo za mataifa ya Afrika Kusini na Zambia. Wimbo huu ulitungwa na Enock Sontonga kwa lugha ya Xhosa "Nkosi Sikelel iAfrika" . Wimbo huu pia uliwahi kutumiwa na nchi za Zimbabwe na Namibia. Enock Sontonga mtunzi wa wimbo Mungu Ibariki Afrika #2. Ni Tanzania pakee ambako kunapatikana Simba wenye uwezo wa kupanda juu ya miti. Simba hawa wanapatikana katika hifadhi ya taifa ya Ziwa Manyara. Simba wenye uwezo wa kupanda miti hifadhi ya Ziwa Manyara. #3. Tanzania ni nchi ambako fuvu la mtu wa kale z

FAHAMU MAKALA BORA ZA KISAYANSI ZILIZOSAIDIA JAMII 2017

Image
Karibu ndugu msomaji wa VENANCE BLOG. Leo nimekuletea makala fupi zakisayansi ambazo zilipata umaarufu kwa mwaka huu kwa ufupi sana, na tuanze sasa Biashara ya siri kuuzwa sokwe Afrika Magharibi David Shukman na Sam Piranty walifanya utafiti mrefu Afrika Magharibi na BBC kugundua mipango ya siri inayohusiana na uuzwaji wa wanyamapori hasa sokwe. Hii ilisaidia kunusurika kwa sokwe aitwaye Nemley Jr ambaye alikuwa na umri wa mwaka mmoja. Mtambo wa Kupunguza Kabonidayoksaidi angani Katika mwaka 2017, riport zilionesha kwamba kuna mrundikano mwingi wa gesi ya kabonidayoksaidi angani mpaka kufikia wingi huo kuvunja rekodi huku juhudi za kimataifa zikishindwa kutatua changamoto hiyo ili kuepuka hatari ya kuongezeka kwa joto duniani. Je teknolojia hiyo inaweza kuondoa gesi hiyo ya kabonidayoksaidi ili kujibu maswali mengi ambayo juhudi za kimataifa zimekua zikishinwa kujibu? Hii iliandikwa na Matt McGrath. Misheni ya Anga ya Cassini kuitafiti sayari ya Sarateni ili