JUMLA ya shilingi bilioni 64.8 zinatarajiwa kukusanywa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya katika mwaka wa fedha 2014/2015.Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Musa Zungiza alipotoa taarifa ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka huo wa fedha kwenye kikao cha baraza la madiwani cha kujadili bajeti hiyo.Zungiza alisema kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 11.3 sawa na asilimia 17.5 zitakusanywa kutoka katika vyanzo vya ndani vya halmashauri wakati michango ya nguvu ya wananchi itakuwa bilioni moja sawa na asilimia 1.5.Kutoka serikali kuu, halmashauri inatararajia kupokea Sh bilioni 37.7 sawa na asilimia 58 kwa ajili ya mishahara ya watumishi, Sh bilioni 3.4 sawa na asilimia tano kwa ajili ya matumizi mengineyo na Sh bilioni 11.4 sawa na asilimia 18 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.Zungiza alisema pia halmashauri inatarajia kutumia jumla ya Sh bilioni 64.8 katika mwaka huo wa fedha kwa ajili ya mishahara ya watumishi, utekelezaji wa miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida.Hata hivyo, baadhi ya madiwani akiwemo Meya, Athanas Kapunga na Diwani wa Kata ya Sinde, Fanuel Kyanula walihoji hatua ya miradi ambayo ujenzi wake haujakamilika ya Soko la Mwanjelwa na Hosteli iliyopo Sokomatola, kuingizwa katika matarajio ya kuwa sehemu ya vyanzo vya ndani vya mapato.Diwani Kyanula alisema ni kwa takriban miaka mitatu sasa, miradi hiyo imekuwa ikiingizwa katika bajeti kwa matarajio kuwa itakamilika kwa wakati na kuanza kuliingizia jiji fedha, lakini matokeo yake imekuwa ni kuzua hoja za ukaguzi.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment