Akihojiwa katika kipindi cha ng'ari ng'ari, Shaa alisema," mimi sikuwa sababu ya kuachana kwa wao wawili (Master Jay na mama watoto wake), kwani ugomvi au kuachana kwa watu wawili huwa inahusu wao wenyewe wawili ila sio mtu watatu, na kwakuwa mimi nilikuwa nimetoka kutendwa ilichukua muda kidogo hadi kuja kuwa na mahusiano na Master Jay hata yeye pia aliniambia alikuwa na maumivu yake ndio mana ilichukua muda hadi kuwa na mahusiano. Hivyo kwanini niachie bahati yangu, Nampenda sana Master"
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

Comments
Post a Comment