JESHI la Polisi wilayani Igunga mkoani Tabora limefanikiwa kukamata bastola katika nyumba ya kulala wageni ambayo inadhaniwa imesahaulika na majambazi.Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Tabora, Peter Ouma alisema silaha hiyo imekamatwa juzi katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Sophia Lodge iliyopo mtaa wa Bank, Igunga mjini.Alisema kuwa bastola hiyo yenye namba za usajili 224335 aina ya Browing Court ilidakwa na risasi 38 pamoja na magazini 4.
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...
Comments
Post a Comment