Showing posts with label Matukio. Show all posts
Showing posts with label Matukio. Show all posts

BOSI WA CRYPTO NCHINI SINGAPORE ASHIKILIWA KWA KUJARIBU KUTOROKA BAADA YA KAMPUNI KUFIRISIKA

Picha kwa hisani ya The Verge 
Su Zhu, mwanzilishi mwenza wa kampuni ya crypto iliyofilisika ya Three Arrows Capital (3AC) ya nchini Singapore, alikamatwa nchini nchini humo siku ya Ijumaa akijaribu kutoroka. Zhu aliwekwa kizuizini alipokuwa akijaribu kuondoka nchini humo kupitia Uwanja wa Ndege wa Changi wa Singapore, kama ilivyoripotiwa awali na Bloomberg.

Teneo, kampuni ya kufilisi inayohusika na kufilisi mali za 3AC, inasema ilipokea amri ya kumzuia Zhu kushiriki kwa namna yoyote katika mali za kampuni baada ya kushindwa kutii amri ya mahakama iliyomlazimu kushirikiana na Teneo katika mchakato wa kufilisi. Amri hiyo ililielekeza jeshi la polisi la Singapore kumkamata Zhu na kumweka gerezani kwa miezi minne. Teneo inasema ilipata agizo sawa na hilo kwa mwanzilishi mwenza wa 3AC, Kyle Davies.

Wakati akiwa gerezani, Teneo anasema wafilisi watashirikiana na Zhu kuhusu maswala yanayohusiana na 3AC, yakilenga urejeshaji wa mali ambayo ni mali ya 3AC au ambayo imepatikana kwa kutumia pesa za 3AC. Kampuni hiyo inaongeza kuwa wafilisi watafuata hatua zote kuhakikisha Bwana Zhu anatii amri kamili ya mahakama.

3AC iliwasilisha kesi ya kufilisika mwezi Julai wakati soko la crypto lilipoanza kudorora. Muda mfupi baada ya kuanguka, Teneo iliripoti kwamba haikuweza kumpata Zhu au Davies. Mapema mwezi huu, benki kuu ya Singapore iliwapiga marufuku Zhu na Davies kusimamia, kuongoza, au kuwa wanahisa wa kampuni yoyote ya huduma za soko la mitaji kwa miaka tisa ijayo.

MAKALA HII IMEANDIKWA NA EMMA ROTH NA KUSIMULIWA KWA KISWAHILI NA VENANCE GILBERT.

PICHA ZA NDOA YA KIFALME PRINCE HARRY & MEGHAN MARKLE


Umati wa watu uliofurika kushuhudia harusi hiyo.


Maua yaliyopambwa kwenye kanisa la Kasri ya Windsor katika kanisa la Mt. George.
Usharika wa Mt. George uliokusanyika kanisani hapo.
Princess Eugine, Prince Andrew na Princess Beatrice walipowasili harusini.
Meghan Markle wakiwa kwenye gari kutoka Clevedon kulekea kasri ya Windsor.
Prince Haary akiwa na msaidizi wake harusini jana Duke wa Cambridge.
Prince Harry akipunga mkono kusalimia umati uliohudhuria harusi hiyo.
Jeshi pia lilikuwepo katika harusi hiyo.
Gari la bibi Harusi lilipowasili kanisania kwa ajili ya kufunga ndoa.
Bibi harusi na mama yake wakiwapungia mkono umati ukiokusanyika harusini hapo.
Prince Harry na Prince William wakisalimiana na watu waliofika harusini
Malkia Elizabeti akishuka kwenye gari alipowasili harusini.
Malkia Elizabeti katika vazi lake la kiutamaduni wa Uingereza akielekea kanisani kushuhudia harusi.
Meghan Marke ndani ya shela iliyobuniwa na mwanamitindo Clare Waight Keller.
Kibongo tunasema bibi harusi na bwana harusi mdogo wakiwasili na wazai wao harusini.
Bibi harusi akiingia kanisani huku akisindikizwa na wasaidizi wake.
Muonekano wa karibu wa shela.
Baadhi ya wanafamilia wa familia ya kifalme wakifuatilia tukio hilola harusi.
Malkia Elizabet na Duke wa Edinburgh
Bibi Harusi Meghan ndani ya kanisa.
Ndani ya kanisa.
Princess Charles akimsindikiza Meghan mahala pa kukaa.
Prince Harry na mkewe Meghan wakiwa Altare tayari kwa kufunga ndoa.
Tabasamu la ndoa hili bila shaka.
Prince Harry akimvua shela mkewe.
Maharusi wakifurahi pamoja.
Maharusi wakisikiliza wimbo ulioimbwa na Karen Gibson na kwaya ya The Kingdom. Wimbo unaitwa 'Stand by me' ukimaanisha "Baki na Mimi"
Maharusi wakibadilishana pete.
Tabsamau la Ndoa hili bila shaka.
Askofu akisoma maneno ya kubariki ndoa.
Ndani ya kanisa.
Baada ya kubadilishana pete.
Maharusi wakiondoka kanisani baada ya kufunga ndoa.
Tabasamu wakati wakiondoka kanisani. Baada ya ndoa sasa wanakua ni Duke & Duchess wa Sussex kwa mujibu wa taratibu za Uingereza.
Wakibusiana wakati wakiondoka kanisani.
Princess Meghan mwenyewe.
Nje ya kanisa.
Kenye gari ya kijeshi tayari kwa maandamano ya hsrusi.
Malkia Elizabet na Duke wa Edinburgh.

Prince Harry akiwapungia mkono walioshirki harusi.

Princess Meghan akiwapungia mkono walioshirkik harusi.

Baada ya harusi ikafuatia sherehe na hivi ndivyo walivaa wakenlekea ukumbini.
Prince Harry akimfungulia mkewe Princess Meghan mlango wa gari.
Wkianga sasa kuelekea ukumbini.
Pincess Meghan akiwa amevaa pete ya marehemu mama mkwe wake Princess Wales kwa pamoja wakiwapungia watu mkono wakati wakielekea ukumbini .



NIMEKUANDALIA PICHA HIZI KWA HISANI YA JARIDA LA MITINDO LA UINGEREZA, THE VOGUE.

MSHAMBULIAJI WA MANCITY SERGIO AGUERO AJERUHIWA KATIKA AJALI

Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amejeruhiwa katika ajali ya barabarani mjini Amsterdam, saa chache baada ya kuhudhuria tamasha.
Raia huyo wa Argentina, mwenye umri wa miaka 29, anaarifiwa kuwa ndani ya taxi akielekea katika uwanja wa ndege baada ya kuhudhuria tamasha la muimbaji Maluma.
City imesema "alikuwa Uholanzi katika siku yake ya mapumziko na amepata majeraha".
Sergio Aguero
Image captionSergio Aguero
Aguero anatarajiwa kurudi Manchester Ijumaa na atakaguliwa na kikosi cha madaktari wa City kabla ya kuelekea kwa mchuano wa Premier League watakapokaribishwa na Chelsea Jumamosi.
Polisi Amsterdam wameithibitishia BBC kwamba watu wawili walikuwa ndaniya taxi iliyohusika katika ajali katika eneo la De Boelelaan mjini humo.

Chanzo: BBC

WALIOKUFA KATIKA TETEMEKO WAFIKIA 16

Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kuaga miili ya waliokufa katika tetemeko la ardhi mkoani Kagera.


Maafa zaidi yameripotiwa katika janga la tetemeko la ardhi, lililotokea juzi mkoani Kagera, ambapo imeripotiwa idadi ya vifo kuongezeka na kufikia watu 16, huku wengine 253 wakijeruhiwa na kusababisha simanzi na masikitiko kwa familia nyingi. Katika tukio hilo, pia nyumba 840 za makazi zimeanguka, nyumba 1,264 zimepata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule yameanguka.

Tukio hilo limemfanya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kulazimika kufanya ziara ya ghafla ya kuwatembelea waathirika wa tetemeko hilo, ambalo limedaiwa kusababisha tafrani pia katika nchi jirani za ukanda wa Afrika Mashariki za Kenya na Rwanda.

Katika hatua nyingine, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimeeleza mpango wa kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga hayo kutokea.

Katika mradi huo maalumu chini ya Kitengo cha Utafiti wa Miamba na Volcano, chuo hicho kitashirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo Ulaya na Marekani, hasa Chuo Kikuu cha Glasgow kilichopo Scotland, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Burton Mwamila. Ziara ya Waziri Mkuu

Akitoa taarifa kwa Waziri Mkuu jana katika Uwanja wa Kaitaba ulioko mjini Bukoba ambapo umeandaliwa maalumu kwa ajili ya kuaga miili ya watu waliopoteza maisha katika tukio hilo la kusikitisha, Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu alisema tukio hilo ni la kwanza kutokea mkoani humo na kwamba limeleta madhara makubwa kwa wananchi na kuacha majonzi makubwa.

Kijuu alisema mpaka taarifa inaandaliwa watu 16 waliripotiwa kupoteza maisha na kusababisha majeruhi 253, huku 170 wakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo na 83 wakitibiwa na kuruhusiwa.

Alisema pia tetemeko hilo limesababisha nyumba 840 za makazi kuanguka, nyumba 1,264 kupata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule kuanguka.

Alisema tetemeko hilo lenye ukubwa wa alama 5.7 uliopimwa kwa kipimo cha Ritcher cha kisayansi cha kupima matetemeko, limeleta madhara makubwa ambapo Serikali ya Mkoa inaendelea kutathmini kwa kina athari zaidi zilizosababishwa na tetemeko hilo na pia uharibifu uliojitokeza kisha kupeleka katika Ofisi ya Waziri Mkuu waone jinsi ya kusaidia.

Alisema hatua zilizochukuliwa na mkoa mpaka sasa ni kuwaokoa na kuwapeleka watu hospitali kwa ajili ya matibabu na kuwapatia makazi ya muda baadhi ya wananchi wenye nyumba zilizoathirika, wakati mipango mingine ikiandaliwa.

Taarifa hiyo ya Mkuu wa Mkoa, ilimfanya Waziri Mkuu kueleza masikitiko yake na serikali kutokana na janga hilo na kutoa salamu za pole kwa wananchi waliopatwa na madhara na kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa na pia maeneo yote yaliyoathirika.

"Leo si siku nzuri kwetu, nimekuja kumwakilisha Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye anawapa pole sana wana Kagera wote na Watanzania kwa ujumla. Pia Makamu wa Rais anawapa pole kwa msiba huu mkubwa, lengo la safari yangu ni kuja kuwapa pole, tukio hili ni kubwa na halijawahi kutokea Tanzania, tumekuwa tukisikia kutoka mataifa ya nje lakini leo limetupata nchini kwetu," alisema Majaliwa.

Aliwasihi na kuwataka wananchi kuwa wavumilivu, kuonesha umoja na ushirikiano, lakini pia kujitokeza kuwafariji wenzao wakati wote wa majonzi, huku akisema Watanzania kwa miaka mingi wamekuwa wakishuhudia mitikisiko midogo, lakini juzi tumeshuhudia mtikisiko mkubwa kabisa ambao umeleta madhara makubwa kwetu.

"Mpaka sasa hatuna uhakika mtikisiko huu utakuwa endelevu kwa kiasi gani, nataka niwahakikishie Watanzania wote, Serikali tunafanya mawasiliano na taasisi zenye uwezo wa kubaini mtikisiko huu ili tuweze kujua jambo hili litakuwa endelevu kwa kiasi gani na kuona dalili na ukubwa wake utakuwaje ili tujipange katika kutoa elimu lakini pia tahadhari pindi jambo kama hili linapoweza kutokea au tunapoona viashiria au dalili za jambo hili," alisema Waziri Mkuu.

Alisema kuwa Mkuu wa Mkoa katika taarifa yake alimweleza kwamba tathmini inaendelea na kwamba ameiagiza Kamati ya Maafa ya Ofisi ya Waziri Mkuu kufika mkoani Kagera mara moja na kuzunguka mkoa mzima kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa kwa lengo la kufanya tathmini ya jumla.

Alisema baada ya tathmini hiyo, utaratibu utafuatwa kwani serikali haiwezi kuwatupa mkono wananchi hao, pia alitumia fursa hiyo kuwaambia wafiwa kuwa Watanzania nchini kote wako pamoja nao katika janga hilo.

Akielezea mkasa huo, majeruhi Happines Apolinary ambaye ni mkazi wa kata ya Buyekera aliyelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera kwa kuumia kichwani na mgongoni, alisema alishtuka kusikia mtikisiko mkubwa wakati akiwa ndani ya nyumba yake na ghafla aliangukiwa na kuta na kumsababishia majeraha. Pamoja na kueleza kuumia vibaya kutokana na tukio hilo, Happines aliwashukuru wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Kagera kwa huduma nzuri waliyompatia tangu juzi alipofikishwa hospitalini hapo.

Majeruhi mwingine, Paulina Spilian aliyelazwa hospitalini hapo akiwa amejeruhiwa miguu alisema akiwa ndani ya nyumba yake ghafla alisikia mtikisiko mkubwa ulioambatana na kishindo cha kuanguka kwa kuta za nyumba na akiwa katika harakati za kutaka kukimbia nje aliangukiwa na ukuta miguuni.

Majeruhi huyo aliiomba Serikali kuwasaidia kwa kuwajengea nyumba na pia kuwapa elimu kuhusiana na matukio kama hayo ili waweze kujiokoa baada ya kuona dalili au viashiria tofauti na ilivyotokea juzi.

Advela Respicius ambaye ni mama wa marehemu, Verdiana Respicius aliyekufa baada ya kufunikwa na kifusi cha nyumba, akizungumza kwa niaba ya familia za wafiwa wa tukio hilo, alitoa shukrani kwa serikali kwa kutoa majeneza, sanda na usafiri wa kuwapeleka marehemu hao mpaka vijijini kwa ajili ya maziko.

Vifaa vya kutabiri kufungwa Wakati hofu ikiwa bado imetawala kutokana na tukio hilo hasa kutokana na wananchi wa Kagera kueleza kutofahamu lolote kabla ya kutokea kwa tetemeko kutokana na kutopewa taarifa zozote na mamlaka za serikali, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimesema kinatarajia kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga hayo kutokea.

Katika mradi huo maalumu chini ya Kitengo cha Utafiti wa Miamba na Volcano, chuo hicho kitashirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo Ulaya na Marekani, lakini hasa Chuo Kikuu cha Glasgow kilichopo Scotland, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Burton Mwamila.

Katika mradi huo wa kwanza nchini unaolenga kutoa utabiri wa matukio ya matetemeko na ulipukaji wa volcano nchini, vifaa maalumu vitakavyokuwa vinapima uwezekano wa kutokea majanga hayo, vitafungwa katika maeneo nyeti kama milima, vilima na sehemu ambazo huwa na volcano hai.

Mtaalamu wa miamba ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya 'Eco Science' inayoshughulika na utafiti wa miamba pamoja na milipuko ya volcano, Dk Ben Beeckmans amefafanua kuwa 'Mlima wa Mungu' (Oldonyo Lengai) uliopo eneo la Ngaresero, wilayani Ngorongoro ndio chanzo kikubwa cha matetemeko ya ardhi katika eneo lote la Afrika Mashariki. Mlima huo wenye volkano hai pia umekuwa ukilipuka mara kwa mara na tukio la mwisho lilirekodiwa mwaka 2007.

Vifaa hivyo vya kutabiri matetemeko ya ardhi vitafungwa kuzunguka eneo la mlima huo, Ziwa Natron, Mlima Meru na hata Mlima Kilimanjaro pamoja na maeneo mengine nchini.

Lakini hatua hiyo si kwamba imetokana na matukio ya tetemeko yaliyoyakumba maeneo mengi ya nchi juzi bali ni mpango uliobuniwa na wataalamu mapema mwaka huu na kwamba kilichobaki ni utekelezaji tu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), Karimu Meshaki alisema atatoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya mpango huo wiki hii.

Hivi karibuni Serikali ilijenga maabara kubwa kabisa ya utafiti wa kisayansi katika Chuo cha Nelson Mandela, Arusha ambayo ilizinduliwa miezi miwili iliyopita.

Serikali ya India pia ilitoa mchango wake kwa kukipatia chuo hicho kompyuta kubwa na yenye uwezo mkubwa zaidi nchini ijulikanayo kama 'Param Kilimanjaro,' ambayo pamoja na shughuli nyingine pia inatarajiwa kutumika katika tafiti za miamba, gesi asilia na pia kwenye huu mradi mpya wa kufuatilia matukio ya tetemeko la ardhi na milipuko ya volkano.



Chanzo: Habarileo