Posts

Showing posts with the label Matukio

BOSI WA CRYPTO NCHINI SINGAPORE ASHIKILIWA KWA KUJARIBU KUTOROKA BAADA YA KAMPUNI KUFIRISIKA

Image
Picha kwa hisani ya The Verge  Su Zhu, mwanzilishi mwenza wa kampuni ya crypto iliyofilisika ya Three Arrows Capital (3AC) ya nchini Singapore, alikamatwa nchini nchini humo siku ya Ijumaa akijaribu kutoroka. Zhu aliwekwa kizuizini alipokuwa akijaribu kuondoka nchini humo kupitia Uwanja wa Ndege wa Changi wa Singapore, kama ilivyoripotiwa awali na Bloomberg. Teneo, kampuni ya kufilisi inayohusika na kufilisi mali za 3AC, inasema ilipokea amri ya kumzuia Zhu kushiriki kwa namna yoyote katika mali za kampuni baada ya kushindwa kutii amri ya mahakama iliyomlazimu kushirikiana na Teneo katika mchakato wa kufilisi. Amri hiyo ililielekeza jeshi la polisi la Singapore kumkamata Zhu na kumweka gerezani kwa miezi minne. Teneo inasema ilipata agizo sawa na hilo kwa mwanzilishi mwenza wa 3AC, Kyle Davies. Wakati akiwa gerezani, Teneo anasema wafilisi watashirikiana na Zhu kuhusu maswala yanayohusiana na 3AC, yakilenga urejeshaji wa mali ambayo ni mali ya 3AC au ambayo imepatikana kwa

PICHA ZA NDOA YA KIFALME PRINCE HARRY & MEGHAN MARKLE

Image
Umati wa watu uliofurika kushuhudia harusi hiyo. Maua yaliyopambwa kwenye kanisa la Kasri ya Windsor katika kanisa la Mt. George. Usharika wa Mt. George uliokusanyika kanisani hapo. Princess Eugine, Prince Andrew na Princess Beatrice walipowasili harusini. Meghan Markle wakiwa kwenye gari kutoka Clevedon kulekea kasri ya Windsor. Prince Haary akiwa na msaidizi wake harusini jana Duke wa Cambridge. Prince Harry akipunga mkono kusalimia umati uliohudhuria harusi hiyo. Jeshi pia lilikuwepo katika harusi hiyo. Gari la bibi Harusi lilipowasili kanisania kwa ajili ya kufunga ndoa. Bibi harusi na mama yake wakiwapungia mkono umati ukiokusanyika harusini hapo. Prince Harry na Prince William wakisalimiana na watu waliofika harusini Malkia Elizabeti akishuka kwenye gari alipowasili harusini. Malkia Elizabeti katika vazi lake la kiutamaduni wa Uingereza akielekea kanisani kushuhudia harusi. Meghan Marke ndani ya shela iliyobuniwa na mwanam

MSHAMBULIAJI WA MANCITY SERGIO AGUERO AJERUHIWA KATIKA AJALI

Image
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amejeruhiwa katika ajali ya barabarani mjini Amsterdam, saa chache baada ya kuhudhuria tamasha. Raia huyo wa Argentina, mweny e umri wa miaka 29, anaarifiwa kuwa ndani ya taxi akielekea katika uwanja wa ndege baada ya kuhudhuria tamasha la muimbaji Maluma. City imesema "alikuwa Uholanzi katika siku yake ya mapumziko na amepata majeraha". Image caption Sergio Aguero Aguero anatarajiwa kurudi Manchester Ijumaa na atakaguliwa na kikosi cha madaktari wa City kabla ya kuelekea kwa mchuano wa Premier League watakapokaribishwa na Chelsea Jumamosi. Polisi Amsterdam wameithibitishia BBC kwamba watu wawili walikuwa ndaniya taxi iliyohusika katika ajali katika eneo la De Boelelaan mjini humo. Chanzo: BBC

WALIOKUFA KATIKA TETEMEKO WAFIKIA 16

Image
Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kuaga miili ya waliokufa katika tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Maafa zaidi yameripotiwa katika janga la tetemeko la ardhi, lililotokea juzi mkoani Kagera, ambapo imeripotiwa idadi ya vifo kuongezeka na kufikia watu 16, huku wengine 253 wakijeruhiwa na kusababisha simanzi na masikitiko kwa familia nyingi. Katika tukio hilo, pia nyumba 840 za makazi zimeanguka, nyumba 1,264 zimepata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule yameanguka. Tukio hilo limemfanya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kulazimika kufanya ziara ya ghafla ya kuwatembelea waathirika wa tetemeko hilo, ambalo limedaiwa kusababisha tafrani pia katika nchi jirani za ukanda wa Afrika Mashariki za Kenya na Rwanda. Katika hatua nyingine, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimeeleza mpango wa kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga ha