Posts

Showing posts with the label Michezo

UCL: FAHAMU MACHACHE MECHI YA MAN CITY VS LYON

Image
Mechi itachezwa saa 4:00 usiku saa za Afrika Mashariki katika dimba la Man City Etihad. Mwamuzi wa mechi hii ni Muitalia Daniele Orsato.  Hii ni mechi ya kwanza baina ya timu hizi. Mpaka sasa hakuna klabu ya Ufaransa iliyowahi kushinda ugenini dhidi ya Man City zaidi ya kuambulia suluhu 1 na kupoteza michezo 2. Lyon imeshinda mechi 1 tu kati ya 8 ilizocheza na timu za Uingereza. Hii ilikua ni dhidi ya Liverpool katika dimba la Anfield Oktoba 2009. Hii ni mara ya 8 mfululizo kwa Man City kushiriki katika ligi ya mabingwa Ulaya. Hii ni rekodi ya juu kwa sasa katika timu za Uingereza kushiriki idadi hii ya Man City ambayo mara nyingi imekua ikiondolewa katika mechi ya 5 ya michuano hii hatua ya makundi. Katika mechi zao zote 42 walizocheza Man City hakuna mechi hata moja ambayo hawakufunga katika ligi hii. Hii ni mara ya 15 kwa Lyon kushiriki michuano hii. Hii inaifanya kuwa timu pekee kutoka nchini Ufaransa kushiriki mara nyingi zaidi. Wamekuwa wakiondolewa katika

TAZAMA HAPA MAGOLI 10 BORA YA KOMBE LA DUNIA 2018

Image
Michuano ya Kombe la Dunia tayari imemalizika nchini Urusi jana Julai 15, 2018 ambapo Ufaransa ilii chapa 4 - 2 Croatia. Leo nakupa nafasi ya kuangalia magoli 10 bora yaliyofungwa katika michuano hii, magoli haya ni kama ifuatavyo: 10: Cristiano Ronaldo, Portugal vs Spain 09: Toni Kroos, Germany vs Sweden 08: Lionel Messi, Argentina vs Nigeria 07: Ricardo Quaresma, Portugal vs IR Iran 06: Nacho, Spain vs Portugal 05: Aleksandar Kolarov, Serbia vs Costa Rica 04: Angel Di Maria, Argentina vs France 03: Philippe Coutinho, Brazil vs Switzerland 02. Benjamin Pavard, France vs Argentina 01. Denis Cheryshev, Russia vs Croatia. Unaweza kutazama magoli hayo katika video hii hapa chini: Magoli haya ni kwa hisani ya Kwesé Sports ambao walikua ni washirika rasmi wa FIFA wa kuonesha michuano hii ya Kombe la Dunia 2018.

WAFUNGAJI BORA NA WALIOCHEZA MECHI NYINGI KATIKA KOMBE LA DUNIA 1930-2014

Image
WAFUNGAJI 5 WA MUDA WOTE 1. Miroslav Klose - Ujerumani Klose wakati wa droo ya kombe la dunia mwaka jana 2017. Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29.   Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002.  Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil. Klose wakati wa mechi ya robo fainali kati ya Ujerumani na Ufaransa katika dimba la Marakana Rio de Jeneiro Julai 4, 2014.

TAKWIMU ZA MUDA WOTE ZA KOMBE LA DUNIA LA FIFA: TIMU, MECHI, KADI NA MAGOLI 1930-2022

Image
TIMU, MECHI & IDADI YA MAGOLI 1. Mwaka 1930 jumla ya timu 13 zilicheza jumla ya mechi 18 na yalipatikana jumla ya magoli 70 hii ikiwa ni wastani wa magoli 3.9 katika kila mechi. 2. Mwaka 1934 jumla ya timu 16 zilicheza jumla ya mechi 17 na yalipatikana jumla ya magoli 70 hii ikiwa ni wastani wa magoli 4.9  katika  kila mechi. 3. Mwaka 1938 jumla ya timu 15 zilicheza jumla ya mechi 18 na yalipatikana jumla ya magoli 84 hii ikiwa ni wastani wa magoli 4.7  katika  kila mechi. 4. Mwaka 1950 jumla ya timu 13 zilicheza jumla ya mechi 22 na yalipatikana jumla ya magoli 88 hii ikiwa ni wastani wa magoli 4.0  katika  kila mechi. 5. Mwaka 1954 jumla ya timu 16 zilicheza jumla ya mechi 26 na yalipatikana jumla ya magoli 140 hii ikiwa ni wastani wa magoli 5.4  katika  kila mechi. 6. Mwaka 1958 jumla ya timu 16 zilicheza jumla ya mechi 35 na yalipatikana jumla ya magoli 126 hii ikiwa ni wastani wa magoli 3.6  katika  kila mechi. 7. Mwaka 1962 jumla ya timu 16 ziliche

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

Image
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa kuchaguli