Venance Blog inawatakieni kila la heri katika kuumaliza mwaka huu 2013 na kuuanza mwaka mpya 2014. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetulinda toka Januari 1 mpaka leo hii Desemba 31 muda na wakati kama huu, tumuombe pia atualie uzima tuweze kuufikia mwaka mpya 2014 tukiwa wazima wa afya ili pia tuendelee na ujenzi wa taifa letu Tanzania. Kwa hayo machache, Venance Blog inakutakia kila la heri na maandalizi mema ya kuupokea mwaka mpya, tusherehekee kwa amani na utulivu bila kuvuja sheria zilizowekwa... KARIBU 2014 KWA HERI 2013!!!
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

Comments
Post a Comment