Venance Blog inawatakieni kila la heri katika kuumaliza mwaka huu 2013 na kuuanza mwaka mpya 2014. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetulinda toka Januari 1 mpaka leo hii Desemba 31 muda na wakati kama huu, tumuombe pia atualie uzima tuweze kuufikia mwaka mpya 2014 tukiwa wazima wa afya ili pia tuendelee na ujenzi wa taifa letu Tanzania. Kwa hayo machache, Venance Blog inakutakia kila la heri na maandalizi mema ya kuupokea mwaka mpya, tusherehekee kwa amani na utulivu bila kuvuja sheria zilizowekwa... KARIBU 2014 KWA HERI 2013!!!
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

Comments
Post a Comment