Posts

Showing posts with the label Historia

LEO AGOSTI 6 KATIKA HISTORIA

Image
Leo ni Agosti 6, 2018 ikiwa ni siku ya 218 katika mwaka 2018. Zimesalia siku 147 katika mwaka huu. Nakukaribisha tena katika muendelezo ya Leo Katika Historia. Kwa leo nimekuletea matukio kadhaa yaliyopata kutokea katika historia ya dunia, na tuanze kuyahesabu matukio hayo: MATUKIO 1787 - Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Marekani ilianza kujadiliwa huko Philadelphia. 1890 - Hukumu ya kuuawa kwa kiti cha umeme ilianza kutekelezwa katika gereza la Auburn huko New York, Marekani ambapo William Kemmier alihukumiwa kifo katika kiti cha umeme kwa kumuua mpenzi wake Matilda Ziegler kwa shoka. Adhabu hii ya kifo ilipendekezwa mwaka 1881 na Dk. Albert Southwick baada kushuhudia mlevi akiuawa kwa shoti ya umeme. Katika kutekeleza adhabu hii zilitumika volti 700 za umeme na katika sekunde 17 umeme ulifeli kabla Kemmier hajafariki na baadaye waliongeza umeme hadi volti 1,030 ndani ya dakika 2 na ndipo Kemmier alifariki. Kiti cha Umeme kilichotumika kutekeleza adhabu ya kifo kwa Kemmier.

MIAKA 5 YA VENANCE BLOG NAWASHUKURU SANA KUWEPO HAPA TANGU KUANZISHWA KWAKE MEI 2013

Image
VENANCE BLOG ilianzishwa Mei 2, 2013. Alhamis ya tarehe 2 Mei, 2013 nilitimiza kiu yangu ya kufungua Blog hii, lilikuwa ni wazo lililoishi toka mwaka 2012 nilipoanza kufahamu matumizi ya mtandao na tarehe hiyo lengo hili lilitimia. Huu ni mwaka wa 5 sasa nikiwa katika tasnia hii. Kuna wakati majukumu ya kitaaluma shuleni yanakaba sana mpaka nashindwa kuwa active kutokana na kufanya kazi hii nikiwa bado masomoni toka mwaka 2013 mpaka sasa. Kuwepo kwa Blog hii kumesaidia baadhi ya watu kupata taarifa na habari nyingine kwa mfano zile za kielimu hasa wakati wa selection za vyuo vikuu. VENANCE BLOG imekua msaada kwa baadhi ya watu, nimekua nikiwapa taarifa za habari hizi hasa wale walio katika mazingira ya kutokua na access ya mtandao. Pamoja na mengine mengi kama haya nimekua nikiitumia Blog hii kama platform ya kuchapisha mashairi yangu ambayo nimekua nikiyaandika kwa nyakati tofauti tofauti. Nawashukuruni sana wasomaji wangu kwa kutembelea Blog hii na kuyasoma mashai

MFAHAMU KARL MARX KWA UFUPI: DUNIA INAMKUMBUKA LEO

Image
Karl Mark alikuwa ni mwanafalsafa na mwanamapinduzi wa Ujerumani aliyeandika vitabu vya The Communist Manifesto na  Das Capital vitabu ambavyo vilikuwa vikipingana na mfumo wa kibepari na kuunda mfumo wa Ukomunisti ama Ujamaa kama alivyoutafsiri hayati Mwalimu JK Nyerere. Karl Marx alizaliwa Mei 5, 1818. Alianza kuchunguza nadharia za kijamii alipokuwa Chuo Kikuu na wenzie waliounda kikundi chao kilichoitwa Young Hegelians. Hiki kilikuwa ni kikundi kilichokuwa kinaamini katika falsafa za mwalimu wao aliyeitwa Hegel. Marx alikuwa mwandishi wa habari na machapisho yake kuhusu Ukomunisti vilipelekea yeye kufukuzwa Ujerumani na Ufaransa. Mwaka 1848 alichapisha kitabu chake cha The Communist Manifesto akiwa na Friedrich Engels ambacho kilipelekea kufukuzwa Ujerumani na kukimbilia London, Uingereza, huko pia aliandika kitabu cha Das Kapital ambako ndiko alikoishi mpaka alipoiaga dunia. Karl Marx alikuwa ni miongoni mwa watoto 9 wa Heinrich Marx na Henrietta Marx huko Trier Pruss

LEO SEPTEMBA 14 KATIKA HISTORIA

Image
Rapa Nas Escobar alizaliwa September 13, 1973. Leo ni Jumatano Septemba 14, 2016. Ni siku ya 258 katika mwaka 2016. Zimesalia siku 108 kuukamilisha mwaka 2016. MATUKIO 1960 - Iraq, Iran, Kuwait na Saudi Arabia ziliunda jumuiya ya OPEC. 1979 - Nur Muhammad Tarak, Rais na na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Afghanistan aliuawa katika mapinduzi ambapo Waziri Mkuu Hafizullah Amin alishika madaraka. KUZALIWA 1849 - Mwanasaikolojia wa Urusi, Ivan Pavlov. 1864 - Robert Cecil,  miongoni mwa waanzilishi wa Jumuiya ya Mataifa alizaliwa. 1879 - Margaret Sanger, wakili na muanzilishi wa Uzazi wa mpango. 1973 - Rapa Nas Escobar alizaliwa. 

LEO SEPTEMBA 13 KATIKA HISTORIA

Image
Tarehe kama ya leo Septemba 13' Tupac Shakur alifariki. Leo Septemba 13 siku ya 257 katika mwaka 2016, zimesalia siku 109 kuukamilisha mwaka 2016. MATUKIO 1759 - Vikosi vya majeshi ya Uingerza viliyashinda majeshi ya Ufaransa katija mapigano kwenye nyanda za Abraham huko Quebec. 1914 - Wanaharakati wa Ireland waliomba msaada kwa wajerumani. 1940 - Italia iliivamia Misri. 1945 - Vikosi vya majeshi ya Uingereza viliingia Japan kupunguza uwezo wa jeshi la Japan. 1993 - Mkataba wa amani kusitisha mapigano Israel na Palestina ulisainiwa. VIFO 1996 - Mwanamuziki 2Pac Shakur alifariki. KWA MSAADA WA MTANDAO.

LEO SEPTEMBA 12 KATIKA HISTORIA

Image
Tarehe kama ya leo Septemba 12, 1973 muigizaji wa Marekani, Paul Walker alizaliwa huko Glendale, Califonia.Alifariki Novemba 30, 2013. Leo ni tarehe 12 Septemba, siku ya 256 katika mwaka 2016, zimesalia siku 110 kuukamilisha mwaka 2016. MATUKIO Leo kuna matukio mengi sana hata hivyo tuyaangalie kama ifuatavyo: 1217 - Mfalme wa Ufaransa Prince Louis na Mfalme wa Uingerza Henry III walisaini mkataba wa amani. 1624 - Meli ya kwanza kupita chini ya maji ilijaribiwa katika Mto Thames kwa ajili ya kutumiwa na Mfalme James I huko Uingereza. 1662 - John Flamsteed aliona nusu ya kupatwa kwa jua na ikampelekea kuvutiwa na elimu ya anga (unajimu) 1703 - Jeshi la Uingereza chini ya Archiduke Charles wa Austria waliwasili nchini Ureno. 1722 - Vikosi vya Urusi viliteka Baku na Derbent huko Persia ambayo kwa sasa ni Iran. 1751 - Amsterdam ilikataa kuanzisha makazi ya Wayahudi. 1753 - Mnajimu wa Ufaransa Charles Messier bila kutarajia aligundua gesi ya miamba (crab

VIDEO: HII NDIYO MAANA HALISI YA SEPTEMBA 11 HUKO MAREKANI

Image
Mnamo mwaka 2001 ndege mbili za abiria za chini Marekani zilitekwa angani na magaidi wanaodhaniwa kuwa ni Al-Qaeda. Ndege hizo mbili aina ya Boeing 767 ziligonga katika majengo pacha ya Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililoko katika jiji la New York nchini Marekani. Hili lilikuwa ni shambulio kubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na magaidi wa Al-Qaeda ambao kwa kipindi hicho kundi hilo lilikuwa likiongozwa na Osama bin Laden ambaye aliuawa miaka ya hivi karibuni na wanajeshi wa jeshi la Marekani (wanavyodai wao Marekani).  Pia kundi la Al Qaeda lilikuwa limelenga kuteketeza jengo la Idara ya Ulinzi ya Marekani, The Pentagon ambako ndiyo makao makuu ya Idara ya Ulinzi ya nci ya Marekani. Lakini pia ililengwa Ikulu ya Marekani 'The White House'. Watu wapatao 2,996 pamoja na watekelezaji wa tukio hilo wakiwa 19 waliuawa. Watu zaidi ya 6,000 walijeruhiwa katika tukio hilo. Pia tukio hilo lilisababisha uharibifu wa mali hasa majengo na miundo mbinu uliofikia dola bilioni 10

LEO SEPTEMBA 11 KATIKA HISTORIA

Image
Leo ni tarehe 11 Septemba, siku ya 255 katika mwaka 2016, zimesalia siku 111 kumaliza mwaka huu 2016. MATUKIO 1740 - Daktari mweusi aliyetibu meno alitajwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la The Pennsylvania  1777 - Mapigano ya vita ya Brandywine yalianza huko Pennsylvania ambapo General George Washington na vikosi vyake walishindwa na General Sir William Howe wa Uingereza 1915 - Mkutano wa Zimmerwald uliitishwa kurejesha amani wakati wa vita ya kwanza ya Dunia. 1940 - Adof Hitler alituma vikosi vyake Mashariki mwa Romania katika vita ya pili ya dunia. 1944 - Vikosi vya Marekani viliingia Luxembourg. 1974 - Haile Selassie I aliondolewa madarakani huko Ethiopia. 1997 - Scotland ilipiga kura ya kuwa na Bunge lake kamili baada ya miaka 290 ya Muungano na England. Jengo la Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililolipuliwa Septemba 11, 2001 na kundi la Al-Qaeda. 2001 - Mnamo majira ya saa 2 na  dakika 45 asubuhi ikiwa siku ya Jumanne, ndege mbili za abiri

LEO SEPTEMBA 10 KATIKA HISTORIA

Image
George Washington, Rais wa Kwanza wa Marekani Leo ni tarehe 10 Septemba siku ya 254 katika mwaka 2016, zimesalia siku 112 kuumaliza mwaka huu 2016. TUANGALIE MATUKIO MUHIMU YALIYOTOKEA TAREHE KAMA YA LEO 210 K.K - Mtawala wa kwanza wa Dola ya Qin (Qin Dynasty) ya nchini China alifariki. 1776 - George Washington aliomba mpelelezi wa siri wa kujitolea, Nathan Hale akajitolea. 1993 - Israel ilisaini mkataba wa utambuzi na PLO. 1919 - Jiji la New York lilimkaribisha nyumbani Jenerali John J. Peshing na wanajeshi wengine 25,000 waliolitumikia jeshi la Marekanj katika vita ya kwanza ya Dunia katika divisheni ya kwanza. 1939 - Canada ilitangaza vita dhidi ya Ujerumani. 1945 - Vidkun Quisling alihukumiwa kifo kwa kushirikiana na jeshi la Ujerumani Nazi nchini Norway. Aliuawa kwa kupigwa risasi Oktoba 1945. 1963 - Wanafunzi weusi 20 (negro) waliruhusiwa kusoma katika shule za serikali za Alabama kufuatia makubaliano kati ya Serikali kuu na Gavana George C. W

HISTORIA KWA UFUPI KUHUSU NELSON MANDELA

Image
Rais Nelson Mandela amefariki baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya maambukizi ya pafu. Katika maisha yake Mandela alifungwa jela kifungo cha maisha lakini alikaa jela kwa miaka 27 katika gereza lililo katika kisiwa cha Robben huko Afrika Kusini na baadaye aliachiwa huru mwaka 1990. Mandela alipigania ukombozi na uhuru wa mwafrika kwa amani na iliposhindikana yeye pamoja na wanachama wenzie wa ANC waliamua kutumia nguvu ya mtutu wa bunduki mpaka walipofanikiwa. Mwaka 1994 alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini. Tofauti na viongozi wengine wa Afrika, Mandela alihudumu kwa miaka 5 tu kisha alistaafu mwaka 1999 na kubaki kama balozi wa Afrika Kusini dhidi ya UKIMWI. Alizaliwa mwaka 1918 Mashariki mwa Rasi ya Tumaini Jema na amefariki akiwa na umri wa miaka 95. Harakati zake katika kupigania ukombozi wa mwafrika zinafanana na zile za watu weusi huko Amerika. Enzi za uhai wake aliwahi kuyasema haya: "During my lifetime I have dedicated myself to this str