Showing posts with label Historia. Show all posts
Showing posts with label Historia. Show all posts

LEO AGOSTI 6 KATIKA HISTORIA

Leo ni Agosti 6, 2018 ikiwa ni siku ya 218 katika mwaka 2018. Zimesalia siku 147 katika mwaka huu. Nakukaribisha tena katika muendelezo ya Leo Katika Historia. Kwa leo nimekuletea matukio kadhaa yaliyopata kutokea katika historia ya dunia, na tuanze kuyahesabu matukio hayo:

MATUKIO

1787 - Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Marekani ilianza kujadiliwa huko Philadelphia.

1890 - Hukumu ya kuuawa kwa kiti cha umeme ilianza kutekelezwa katika gereza la Auburn huko New York, Marekani ambapo William Kemmier alihukumiwa kifo katika kiti cha umeme kwa kumuua mpenzi wake Matilda Ziegler kwa shoka. Adhabu hii ya kifo ilipendekezwa mwaka 1881 na Dk. Albert Southwick baada kushuhudia mlevi akiuawa kwa shoti ya umeme. Katika kutekeleza adhabu hii zilitumika volti 700 za umeme na katika sekunde 17 umeme ulifeli kabla Kemmier hajafariki na baadaye waliongeza umeme hadi volti 1,030 ndani ya dakika 2 na ndipo Kemmier alifariki.
Kiti cha Umeme kilichotumika kutekeleza adhabu ya kifo kwa Kemmier.

1904 - Jeshi la Japan lililokua nchini Korea lilizunguka Jeshi la Urusi ambalo lilizidiwa nguvu na kuamua kurudi nyuma katika jimbo la Manchuria.

1945 - Ndege ya Marekani B-29 ikiongozwa na rubani Paul Tibbets ilidondosha bomu la nyuklia katika jimbo la Hiroshima. Bomu hilo liliua watu waliofikia 80,000 na pia watu 35,000 walijeruhiwa na inakadiriwa kua baadaye mwishoni mwa mwaka huo watu wengine 60,000 walifariki kwa madhara ya bomu hilo. Kulikua na majengo 90,000 katika mji wa Hiroshima lakini baada ya bomu kulipuka yalibaki majengo 28,000 tu, madakatari walikua 200 lakini waliosalia walikua 20 tu, manesi walikua 1,754 lakini walisalia 150 tu.
Ndege aina ya B-29 iliyodondosha bomu la nyuklia huko Hiroshima.
Baada ya bomu kudondoshwa hali ilikua hivi. 

Hivi ndiyo Hiroshima ilivyojengwa kwa sasa. 

1962 - Jamaica ilipata Uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza baada ya kutawaliwa kwa miaka 300.

1973 - Mwanamuziki wa Marekani Steve Wonder alipata ajali ya gari iliyopelekea kupoteza fahamu kwa siku 4.

1993 - Papa John Paul II alichapisha makala iliyohusu Umuhimu wa Kanisa Katoliki katika kufundisha maadili.

KUZALIWA

1809 - Mtunzi wa mashairi wa Uingereza Alfred Lord Tennyson alizaliwa. Moja kati ya mashairi yake maarufu ni "The Charge of the Light Bregade" la mwaka 1850.

1881 - Alexander Flemming mgunduzi wa dawa aina ya Penicillin mwaka 1928 alizaliwa.

1911 - Muigizaji na mchekeshaji wa Marekani Lucille Ball alizaliwa. 

1934 - Piers Anthony Dillingham Jacob mwandishi wa riwaya za kisayansi na matukio ya ajabu na ya kusimumua alizaliwa. 

MIAKA 5 YA VENANCE BLOG NAWASHUKURU SANA KUWEPO HAPA TANGU KUANZISHWA KWAKE MEI 2013

VENANCE BLOG ilianzishwa Mei 2, 2013.

Alhamis ya tarehe 2 Mei, 2013 nilitimiza kiu yangu ya kufungua Blog hii, lilikuwa ni wazo lililoishi toka mwaka 2012 nilipoanza kufahamu matumizi ya mtandao na tarehe hiyo lengo hili lilitimia. Huu ni mwaka wa 5 sasa nikiwa katika tasnia hii.

Kuna wakati majukumu ya kitaaluma shuleni yanakaba sana mpaka nashindwa kuwa active kutokana na kufanya kazi hii nikiwa bado masomoni toka mwaka 2013 mpaka sasa.

Kuwepo kwa Blog hii kumesaidia baadhi ya watu kupata taarifa na habari nyingine kwa mfano zile za kielimu hasa wakati wa selection za vyuo vikuu. VENANCE BLOG imekua msaada kwa baadhi ya watu, nimekua nikiwapa taarifa za habari hizi hasa wale walio katika mazingira ya kutokua na access ya mtandao.

Pamoja na mengine mengi kama haya nimekua nikiitumia Blog hii kama platform ya kuchapisha mashairi yangu ambayo nimekua nikiyaandika kwa nyakati tofauti tofauti. Nawashukuruni sana wasomaji wangu kwa kutembelea Blog hii na kuyasoma mashairi hayo na pia kutumia muda wenu kutoa maoni kadiri inavyowapendeza. Asanteni sana.

Aidha nimekua nikiandika habari za kitaifa, kimataifa, siasa, udaku, nyimbo mpya, video mpya, habari za masuala ya anga, Teknolojia, Michezo, nimekua nikiandika pia nukuu kutoka kwa wanafalsafa wakubwa dunia na watu wengineo kama vile wanasiasa, wanamuziki, wanaharakati wa masuala tofauti tofauti n.k. Aidha nimekua nikiandika habari za mitindo na mambo mengine kadha wa kadha.

Habari, Picha, Matukio na mambo mengine ninayoyachapisha hapa nimekua nikipitia kwa ukaribu katika vyanzo makini kama vile Habari Leo, Mwananchi, BBC, DW, VoA, Jarida la Mitindo la Vogue, Forbes, Kitabu cha kumbukumbu cha rekodi za dunia Guinness, Blogs za watu binafsi, taasisi na kadhalika.

Katika mwaka huu wa 5 naahidi kuendelea kufanya kazi hii kwa ukaribu kabisa na watu, moja ya mpango wa hivi karibuni ni kuanza kuandika habari za matangazo ya kazi pamoja na kuongeza zaidi taarifa za nafasi za masomo ya nje ya nchi (scholarship) ambayo hii tayari nimeanza kuifanyia kazi. Pia kuna mengine mengi yanakuja katika Blog hii. Endelea kufuatilia VENANCE BLOG na nakushukuru sana kuendelea kuwa msomaji wa Blog hii.


Kwa maoni na mengineyo, wasiliana nami kwa moja kati ya njia hizi:
barua pepe: venancegilbert@gmail.com

Simu ya mkononi: 0753400208.

MFAHAMU KARL MARX KWA UFUPI: DUNIA INAMKUMBUKA LEO

Karl Mark alikuwa ni mwanafalsafa na mwanamapinduzi wa Ujerumani aliyeandika vitabu vya The Communist Manifesto na Das Capital vitabu ambavyo vilikuwa vikipingana na mfumo wa kibepari na kuunda mfumo wa Ukomunisti ama Ujamaa kama alivyoutafsiri hayati Mwalimu JK Nyerere.

Karl Marx alizaliwa Mei 5, 1818. Alianza kuchunguza nadharia za kijamii alipokuwa Chuo Kikuu na wenzie waliounda kikundi chao kilichoitwa Young Hegelians. Hiki kilikuwa ni kikundi kilichokuwa kinaamini katika falsafa za mwalimu wao aliyeitwa Hegel. Marx alikuwa mwandishi wa habari na machapisho yake kuhusu Ukomunisti vilipelekea yeye kufukuzwa Ujerumani na Ufaransa. Mwaka 1848 alichapisha kitabu chake cha The Communist Manifesto akiwa na Friedrich Engels ambacho kilipelekea kufukuzwa Ujerumani na kukimbilia London, Uingereza, huko pia aliandika kitabu cha Das Kapital ambako ndiko alikoishi mpaka alipoiaga dunia.

Karl Marx alikuwa ni miongoni mwa watoto 9 wa Heinrich Marx na Henrietta Marx huko Trier Prussia ya zamani (kwa sasa Ujerumani) Baba yake alikuwa mwanasheria aliyefanikiwa sana na alikuwa mwanaharakati aliyependa mabadiliko nchini Prussia. Japokuwa wazazi wake walikuwa na asili ya Kiyahudi, baba yake Marx alihamia katika Ukristu mwaka 1816 alipokuwa na umri wa miaka 3.

Marx alikuwa ni mwanafunzi wa kawaida. Alisomea nyumbani hadi alipokuwa na umri wa miaka 12 na kisha alipelekwa Jesuit High School alikosoma kwa muda wa miaka 5 kuanzia 1830 hadi 1835.

Mwaka 1835 Marx alijiunga na Chuo Kikuu cha Bonn. Chuo hiki kilikuwa na Itikadi za kuipinga serikali. Marx alijiunga na maisha ya uanafunzi katika chuo hiki. Katika semista mbili chuoni hapo, alifungwa kwa ulevi na kuvuruga amani chuoni hapo, kuwa na madeni lakini pia kushiriki katika falsafa zilizokinzana na chuo. Mwisho wa mwaka baba yake Marx alimsisitiza kuwa serious na masomo katika Chuo Kikuu cha Berlin.

Katika Chuo Kikuu Berlin alisomea fani ya sheria na falsafa ambako alikutana na falsafa za mwalimu wake George Hegel ambaye alikuwa profesa katika chuo hicho mpaka alipofariki mwaka 1895. Baadaye Marx alijiunga na kikundi cha Young Hegelians ambacho pia kulikuwa na Bruno Bauer na Ludwig Feuerbach ambao walikosoa kuanzishwa kwa siku za kisiasa na kidini nchini humo. Kuna mengi yalijiri Marx alipokuwa Berlin.
Tokeo la picha la marx and bruno bauer
Bruno Bauer
Marx hakutulia wala kuishia hapo. Mwaka 1841 alitunukiwa Shahada yake ya Uzamivu ya Chuo Kikuu cha Jena lakini harakati zake za kisiasa zilipelekea yeye kutokuaminiwa na kuwa mwalimu katika chuo chochote nchini Ujerumani. Alianza kufanya kazi kama mwandishi wa habari na mwaka 1842 alikuwa Mhariri wa Rheinische Zeitung ambalo lilikuwa ni gazeti la wanaharakati wa usawa huko Cologne, Ujerumani. Mwaka mmoja baadaye serikali ililifuta gazeti hilo kuanzia April 1, 1843. Marx aliacha kazi hapo Machi 18. Miezi mitatu baadaye alimuoa Jenny von Westephalen  na Oktoba walihamia Paris, Ufaransa.
Tokeo la picha la karl marx and his family
Marx akiwa na mkewe Jenny von Westephalen
Mji wa Paris ulikuwa ni kitovu cha harakati za kisiasa barani Ulaya mwaka 1843. Huko Marx akiwa na Arnold Ruge, walianzisha gazeti la uchambuzi wa kisiasa lilioitwa Deutsch-Franzosische Jahrbucher (German-French Annals) jambo moja tu ndilo lilikuwa likichapishwa katika gazeti hili kabla Marx na Ruge hawajatofautiana kiitikadi hadi kupelekea gazeti hilo kupotea kwenye ramani lakini Agosti 1844, gazeti hilo liliwaleta pamoja Marx na Friedrich Engels kama mwandishi mshiriki ambaye alikuwa msaidizi wake na rafiki yake hadi kifo. Pamoja, wawili hao walianza kuandika makala za kukosoa mawazo ya Bruno Bauer ambaye alikuwa ni mshiriki katika kikundi cha Young Hegelians. Mwaka 1845 Marx na Engels walichapisha makala yao iliyojulikana kama The Holy Family.


Baadaye katika mwaka huo, Marx alihamia Ubeligiji baada ya kufukuzwa nchini Ufaransa ambako aliandika katika gazeti la Vorwarts! ambalo lilikuwa na itikadi ambazo baadaye zingepelekea kuanzishwa kwa Jumuiya ya Kikomunisti. Alipokuwa Ubeligiji, Marx alipokelewa na Moses Hess, na baadaye aliachana kabisa na siasa za Young Hegelians. Alipokuwa nchini humo aliandika The German Ideology ambako ndiko alipoandika nadharia yake inayojulikana kama Historical Materialism. Marx hakupata mtu wa kuruhusu kuchapisha makala yake. The German Ideology na Theses on Feuerbach hayakuchapisha makala hiyo hadi alipofariki. Nadharia hii inawataka watu kushiriki kwa vitendo kupinga uonevu.


Tokeo la picha la Karl marx and engels
Karl Marx & Friedrich Engels
Mwanzoni mwa mwaka 1846, Mark alianzisha Communist Correspondence Committee katika juhudi zake za kuunganisha ukomunisti barani Ulaya. Waingereza walivutiwa na sera zake na kuitisha mkutano na kuunda shirikisho lao Communist League na mwaka 1847 katika mkutano wao mkuu uliofanyika London, shirikisho hilo liliwaomba Marx na Engels kuandika Manifest der Kommunistischen Partei (Manifesto of the Communist Party)

The Communist Manifesto ni miongoni mwa kazi maarufu za Marx ambayo ilichapishwa mwaka 1848 na baadaye mwaka 1849 Marx alifukuzwa nchini Ubeligiji. Alikwenda Ufaransa ambako alianzisha vuguvugu la Mapinduzi nchini humo ambako pia alifukuzwa. Prussia ilikataa kumpokea Marx na hivyo alihamia London japokuwa Uingerza ilikataa kumpa uraia nchini humo hadi kifo chake.

Marx alipokuwa London alisaidia kuundwa kwa shirikisho la wanataaluma wa Ujerumani German Workers' Educational Society lakini pia Shirikisho la Kikomunisti The Communist League. Aliendelea kufanya kazi kama mwandishi japokuwa safari hii alizuiwa na baadhi ya itikadi zake. Alifanya kazi katika The New York Daily Tribune kwa miaka 10 kuanzia 1852-1862 lakini hakulipwa , aliishi kwa kusaidiwa na rafiki yake Engels.

Marx aliutazama mfumo wa kibepari zaidi na mwaka 1867 alichapisha toleo la kwanza la kitabu chake Das Kapital. Baadaye alitumia muda wake kupitia chapisho hilo na akawa akilifanyia masahihisho na kuongeza baadhi ya vitu. Matoleo mawili yaliyofuata baadaye ambayo hata hakuyakamilisha yaliunganishwa na kuchapishwa na Engels.

Marx alifariki kwa ugonjwa wa mapafu unaojulikana kitaalamu kama pleurisy alipokuwa London Machi 14, 1883. Katika kaburi lake kuna maandishi ya kitabu chake The Communist Manifesto yenye maana wafanyakazi wote waungane.



MAKALA HII IMEANDALIWA KWA MSAADA WA MTANDAO INAWEZA KUFANYIWA MAREKEBISHO MUDA WOWOTE PANAPOHITAJIKA.

LEO SEPTEMBA 14 KATIKA HISTORIA

Rapa Nas Escobar alizaliwa September 13, 1973.
Leo ni Jumatano Septemba 14, 2016. Ni siku ya 258 katika mwaka 2016. Zimesalia siku 108 kuukamilisha mwaka 2016.

MATUKIO

1960 - Iraq, Iran, Kuwait na Saudi Arabia ziliunda jumuiya ya OPEC.

1979 - Nur Muhammad Tarak, Rais na na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Afghanistan aliuawa katika mapinduzi ambapo Waziri Mkuu Hafizullah Amin alishika madaraka.



KUZALIWA

1849 - Mwanasaikolojia wa Urusi, Ivan Pavlov.

1864 - Robert Cecil,  miongoni mwa waanzilishi wa Jumuiya ya Mataifa alizaliwa.

1879 - Margaret Sanger, wakili na muanzilishi wa Uzazi wa mpango.

1973 - Rapa Nas Escobar alizaliwa. 

LEO SEPTEMBA 13 KATIKA HISTORIA

Tarehe kama ya leo Septemba 13' Tupac Shakur alifariki.
Leo Septemba 13 siku ya 257 katika mwaka 2016, zimesalia siku 109 kuukamilisha mwaka 2016.


MATUKIO

1759 - Vikosi vya majeshi ya Uingerza viliyashinda majeshi ya Ufaransa katija mapigano kwenye nyanda za Abraham huko Quebec.

1914 - Wanaharakati wa Ireland waliomba msaada kwa wajerumani.

1940 - Italia iliivamia Misri.

1945 - Vikosi vya majeshi ya Uingereza viliingia Japan kupunguza uwezo wa jeshi la Japan.

1993 - Mkataba wa amani kusitisha mapigano Israel na Palestina ulisainiwa.


VIFO

1996 - Mwanamuziki 2Pac Shakur alifariki.


KWA MSAADA WA MTANDAO.

LEO SEPTEMBA 12 KATIKA HISTORIA

Tarehe kama ya leo Septemba 12, 1973 muigizaji wa Marekani, Paul Walker alizaliwa huko Glendale, Califonia.Alifariki Novemba 30, 2013.
Leo ni tarehe 12 Septemba, siku ya 256 katika mwaka 2016, zimesalia siku 110 kuukamilisha mwaka 2016.

MATUKIO

Leo kuna matukio mengi sana hata hivyo tuyaangalie kama ifuatavyo:

1217 - Mfalme wa Ufaransa Prince Louis na Mfalme wa Uingerza Henry III walisaini mkataba wa amani.

1624 - Meli ya kwanza kupita chini ya maji ilijaribiwa katika Mto Thames kwa ajili ya kutumiwa na Mfalme James I huko Uingereza.

1662 - John Flamsteed aliona nusu ya kupatwa kwa jua na ikampelekea kuvutiwa na elimu ya anga (unajimu)

1703 - Jeshi la Uingereza chini ya Archiduke Charles wa Austria waliwasili nchini Ureno.

1722 - Vikosi vya Urusi viliteka Baku na Derbent huko Persia ambayo kwa sasa ni Iran.

1751 - Amsterdam ilikataa kuanzisha makazi ya Wayahudi.

1753 - Mnajimu wa Ufaransa Charles Messier bila kutarajia aligundua gesi ya miamba (crab nebula) na akaanza utafiti wake (Messier Catalogue)

1848 - Uswisi iliunganisha mataifa yake kupata taifa moja la Uswisi.

1878 - Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alifungua Mkutano wa Kongo.

1885 - Rekodi ya kwanza ya magoli 35 katika mechi ya ligi daraja la kwanza iliwekwa.

1890 - Cecil Rhodes alifika Harare, Zimbabwe kwa wakati ule ikiitwa Fort Salisbury.

1909 - Waarabu walivamia Gedara Palestina.

1919 - Adolf Hitler aliungana na Chama cha Wafanyakazi wa Ujerumani akiwa mwanachama wa saba lakini hakukubaliana na lengo la chama hicho badala yake alisisitiza Utaifa (Harakati za nchi binafsi) na kusisitiza chuki dhidi ya Wayahudi.

1922 - Mwanariadha Paavo Nurmi aliweka rekodi ya dunia kwa kukimbia umbali wa mita 5000 sawa na kilomita 5 kwa daika 14:35.4

1928 - Kimbunga Hurricane kiliua watu 6,000.

1934 - Estonia, Lativia & walisaini mkataba wa Baltic Entente dhidi ya Muungano wa nchi za Kisovieti.

1941 - Meli ya kwanza ya kijerumani katika vita ya pili ya Dunia ilitekwa na meli za Marekani.

1943 - Taifa la Skorzeny lilimuachia Benito Nussolini huko Gran Sasso.

1944 - Vikosi vya Marekani viliingia nchini Ujerumani kwa mara ya kwanza.

1950 - Serikali ya Ubelgiji iliwafukuza wafanyakazi wote wa kikomunisti.

1956 - Wanafunzi weusi waliruhusiwa kusoma shule ya Ckay Ky huko Marekani.

1958 - Marekani ilifanya jaribio lake la Nyuklia katika uwanja wa majaribio wa Nevada.

1958 - Muhandisi Jack Kilby alifanya jaribio la sakiti ya kompyuta aliyogundua kwa msimamizi wake.

1959 - Muungano wa nchi za kisovieti (USSR) ulituma chombo Luna 2 kwenda kwenye mwezi.

1961 - Urusi ilifanya jaribio lake la nyuklia huko Novaya Zemlya.

1971 - Urusi ilituma chombo chake kwenye mwezi Luna 16.

1973 - Urusi ilifanya tena jaribio la Nyuklia huko Novaya Zemlya.

1974 - Mfalme Haile Sellasie alipinduliwa nchini Ethiopia.

1978 - Fidel Castro alitembelea Addis Ababa Ethiopia.

1979 - Indonesia ilikumbwa na tetemeko la ardhi ambalo lilikuwa na ukubwa wa 8.1 katika kipimo cha Richter.

1984 - Ethiopia iliunda Jamhuri ya Kisoshalisti.

1987 - Ethiopia ilianza kufuata utawala wa Katiba.

1992 - Mae Jemison alikuwa mwanamke wa kwanza Mmarwkani mweusi kwenda angani.

1999 - Indonesia ilisema itaruhusu walinzi wa amani Mashariki mwa Timor.

2005 - Israel iliondosha majeshi na vikosi vyake kutoka ukanda wa Gaza.

2007 - Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe alitangaza nia yake ya kujiuzulu wadhifa huo.

2007 - Rais wa zamani wa Ufilipino Joseph Estrada kwa kosa na wizi wa fedha za serikali.

2010 - Lady Gaga na Eminem walichukua tuzo za MTV Video Music.

2012 - Kampuni ya Apple ilitangaza na kuonesha simu zao iPhone 5 na iOS 6.

2015 - Watalii 12 waliuawa bila kukusudia na Jeshi la Misri Magahribi mwa Jangwa la Misri wakidhaniwa kuwa ni waasi.




KUZALIWA

1575 -  Mtafiti wa Uingereza Henry Hudson.

1913 - Mwanaridha Jesse Owen.

1973 - Muigizaji Paul Walker.

1977 - Muigizaji Connor Frante.

1978 - Muigizaji Benjamin McKenzie.

1981 - Muigizaji na Mwanamuziki Jennifer Hudson.



IMEANDALIWA KWA MSAADA WA MTANDAO.

VIDEO: HII NDIYO MAANA HALISI YA SEPTEMBA 11 HUKO MAREKANI

Mnamo mwaka 2001 ndege mbili za abiria za chini Marekani zilitekwa angani na magaidi wanaodhaniwa kuwa ni Al-Qaeda. Ndege hizo mbili aina ya Boeing 767 ziligonga katika majengo pacha ya Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililoko katika jiji la New York nchini Marekani. Hili lilikuwa ni shambulio kubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na magaidi wa Al-Qaeda ambao kwa kipindi hicho kundi hilo lilikuwa likiongozwa na Osama bin Laden ambaye aliuawa miaka ya hivi karibuni na wanajeshi wa jeshi la Marekani (wanavyodai wao Marekani). 

Pia kundi la Al Qaeda lilikuwa limelenga kuteketeza jengo la Idara ya Ulinzi ya Marekani, The Pentagon ambako ndiyo makao makuu ya Idara ya Ulinzi ya nci ya Marekani. Lakini pia ililengwa Ikulu ya Marekani 'The White House'.

Watu wapatao 2,996 pamoja na watekelezaji wa tukio hilo wakiwa 19 waliuawa. Watu zaidi ya 6,000 walijeruhiwa katika tukio hilo.

Pia tukio hilo lilisababisha uharibifu wa mali hasa majengo na miundo mbinu uliofikia dola bilioni 10. Jumla kuu ya uharibifu ilikadiriwa kuwa dola za kimarekani trilioni 3. 

Katika kutekeleza tukio hilo la ugaidi magaidi 19 walihusika ambapo 15 walikuwa ni raia wa Saudi Arabia, 2 kutoka Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE), 1 kutoka Misri na 1 kutoka Lebanon.

Historia ya Al Qaeda inarudi nyuma katika mwaka 1979 ambapo Muungano wa Kisoviet uliivamia Afghanistan. Osama alisafiri hadi Afghanistan na kuunda kikundi cha kiarabu cha wajahideen kupingana na Wasoviet. Osama aliendelea kuwa kinyume na Wamarekani na mwaka 1996 alitoa tamko lililotaka majeshi ya Marekani kuondoka Saudia Arabia

Shambulio hili lilkuwa kama ifuatavyo:
  • Ndege ya Shirika la Marekani (American Airlines Flight 11) aina ya Boeing 767 iliondoka Logan airpot ikiwa na crew ya watu 11 pamoja na abiria 76 (watekaji 5 hawakuhesabiwa) ndege hiyo iligeuzwa ruti ikiwa angani na kugonga katika kituo cha biashara Duniani saa 8:46 am saa za Marekani.
  • Ndege ya pili ya Marekani (American Airlines Flight 77) Boeing 757 iliondoka Washington Dulles Airport kuelekea Los Angels, California ikiwa na crew ya watu 6 na abiria 53 (watekaji wameondolewa katika hesabu hiyo). Watekaji walifanikiwa kuiteka na kugonga jengo la ulinzi la Marekani The Pentagon saa 9:37 am saa za Marekani.
  • Ndege ya tatu (United Airlines Flight 93) Boing 757 iliondoka  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa New York ikielekea San Fransisco kabla ya kutekwa angani na kugonga Stonycreek Township  karibu na Shanksville, Pennsylvania saa 10:03 am saa za Marekani. Abiria walikuwa 33 na crew ya watu 7 huku watekaji wakiwa 4.
  • Ndege nyingine American Airline Flight 11 Boeing 767 ilikuwa na abiria 51 crew ya watu 9 na watekaji 5 iliondoka Los Angels na kutekwa angani hadi WTC saa 9:03 am dakika chache mara baada ya Shambulio la awali.



Hizi ni baadhi ya picha za tukio hilo



WTC kabla ya shambulio


WTC kabla ya shambulio



WTC kabla ya shambulio



Nimekuwekea video pia ambapo unaweza kutazama tukio hilo





Makala hii imeandaliwa kwa Msaada wa Mtandao (Wikipedia, Britannica na YouTube)

LEO SEPTEMBA 11 KATIKA HISTORIA

Leo ni tarehe 11 Septemba, siku ya 255 katika mwaka 2016, zimesalia siku 111 kumaliza mwaka huu 2016.

MATUKIO

1740 - Daktari mweusi aliyetibu meno alitajwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la The Pennsylvania 

1777 - Mapigano ya vita ya Brandywine yalianza huko Pennsylvania ambapo General George Washington na vikosi vyake walishindwa na General Sir William Howe wa Uingereza

1915 - Mkutano wa Zimmerwald uliitishwa kurejesha amani wakati wa vita ya kwanza ya Dunia.

1940 - Adof Hitler alituma vikosi vyake Mashariki mwa Romania katika vita ya pili ya dunia.

1944 - Vikosi vya Marekani viliingia Luxembourg.

1974 - Haile Selassie I aliondolewa madarakani huko Ethiopia.

1997 - Scotland ilipiga kura ya kuwa na Bunge lake kamili baada ya miaka 290 ya Muungano na England.

Jengo la Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililolipuliwa Septemba 11, 2001 na kundi la Al-Qaeda.

2001 - Mnamo majira ya saa 2 na
 dakika 45 asubuhi ikiwa siku ya Jumanne, ndege mbili za abiria za Marekani Boeing 767 zilitekwa angani na kugonga katika jengo la Kituo cha Biashara duniani (WTC) ambapo watu wengi waliuawa. Inasidikika kuwa tukio hilo la ugaidi liliungwa mkono na magaidi wa Kiislamu kutoka Saudi Arabia na kundi la Al Qaeda ilililokuwa chini ya Osama bin Laden kwa kipindi hicho.

2005 - Israel iliwaondoa wananchi wake na vikosi vyake vya jeshi katika mapiagano dhidi ya Palestina katika Ukanda wa Gaza.

2007 - Urusi ilifanya jaribio la kulipua bomu la Nano lililoitwa "Father of Bombs" yaani Baba la Mabomu yote ambalo lilikuwa ni bomu lisilo la nyuklia kuwahi kutengenezwa.

2012 - Ofisi za Ubalozi wa Mareani nchini Libya katika mji wa Benghazi zilichomwa moto na kupelekea vifo vya watu 4 akiwemo balozi wa Marekani nchini Libya, Christopher Stevens


KUZALIWA

1700 - Mshairi wa Scotland, James Thomson.

1877 - Mwanasayansi James Jeans.

1862 - Mwandishi wa Marekani O. Henry (William Sydney Porter) alizaliwa.

1939 - Charles M. Chuck Geschke muanzilishi wa Adobe System Inc.

1965 - Rais wa Syria Bashal al-Assad. Yupo madarakani tangu mwaka 2000.

1977 - Rapa Ludacris.
Rapa Ludacris alizaliwa mwaka 1977.


VIFO

1971 - Nikita Khrushchev moja kati ya viongozi wa kisoshalist alifariki akiwa na miaka 77 katika kipindi cha vita baridi.

NUKUU

"Kama mtu ameishi katika vita, umaskini na upendo, ameishi maisha kamili" - O. Henry.


KWA MSAADA WA MTANDAO.

LEO SEPTEMBA 10 KATIKA HISTORIA

George Washington, Rais wa Kwanza wa Marekani
Leo ni tarehe 10 Septemba siku ya 254 katika mwaka 2016, zimesalia siku 112 kuumaliza mwaka huu 2016.

TUANGALIE MATUKIO MUHIMU YALIYOTOKEA TAREHE KAMA YA LEO


210 K.K - Mtawala wa kwanza wa Dola ya Qin (Qin Dynasty) ya nchini China alifariki.

1776 - George Washington aliomba mpelelezi wa siri wa kujitolea, Nathan Hale akajitolea.

1993 - Israel ilisaini mkataba wa utambuzi na PLO.


1919 - Jiji la New York lilimkaribisha nyumbani Jenerali John J. Peshing na wanajeshi wengine 25,000 waliolitumikia jeshi la Marekanj katika vita ya kwanza ya Dunia katika divisheni ya kwanza.

1939 - Canada ilitangaza vita dhidi ya Ujerumani.

1945 - Vidkun Quisling alihukumiwa kifo kwa kushirikiana na jeshi la Ujerumani Nazi nchini Norway. Aliuawa kwa kupigwa risasi Oktoba 1945.

1963 - Wanafunzi weusi 20 (negro) waliruhusiwa kusoma katika shule za serikali za Alabama kufuatia makubaliano kati ya Serikali kuu na Gavana George C. Wallace.

1974 - Guinea-Bissau ilipata uhuru wake kamili kutoka kwa Ureno.

1979 - Wanaharakati wanne wa Puerto Rico walihukumiwa kwenda jela kwa kosa la kufanya shambulizi katika Bunge la Wawakilishi nchini Marekani mwaka 1953 na jaribio la kutaka kumuua Rais wa Marekani, Harry S. Truman mwaka 1950. Waliachiwa baadae kwa msaha kutoka kwa Rais Jimmy Carter.

2008 - Jaribio lililoitwa Hadron Collider ambalo ni jaribio kunwa kiwahi kufanyika katika historia ya binadamu lilifanywa huko Geneva, Uswisi.


KUZALIWA

1638 - Malikia Maria Theresa akiwa mke wa Mfalme Lous XIV wa Hispania maarufu kama "Maria Theresa wa Hispania" alizaliwa huko El Escorial nchini Hispania.

1928 - Mwanafalsafa wa Canada, Jean Vanier alizaliwa.

1931 - Muigizaji wa Matekani Philip Baker Hall alizaliwa.

1940 - Mwanamuziki wa Marekani Roy Ayers alizaliwa.

1953 - Muigizaji wa kike wa Marekani Amy Irving alizaliwa.

1957 - Mwanamuziki wa Uingereza Siobhan Fahey alizaliwa.

1958 - First lady wa Canada Margaret Trudeau alizaliwa.

1960 - Muigizaji wa Uingereza Colin Firth alizaliwa.

1968 - Muongozajj wa filamu wa Uingereza Guy Ritchie alizaliwa.

1974 - Muigizaji wa Marekani Ryan Phillippe alizaliwa.

1979 - Muigizaji wa Marekani Jacob Young alizaliwa.


KWA MSAADA WA MTANDAO

HISTORIA KWA UFUPI KUHUSU NELSON MANDELA

Rais Nelson Mandela amefariki baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya maambukizi ya pafu. Katika maisha yake Mandela alifungwa jela kifungo cha maisha lakini alikaa jela kwa miaka 27 katika gereza lililo katika kisiwa cha Robben huko Afrika Kusini na baadaye aliachiwa huru mwaka 1990. Mandela alipigania ukombozi na uhuru wa mwafrika kwa amani na iliposhindikana yeye pamoja na wanachama wenzie wa ANC waliamua kutumia nguvu ya mtutu wa bunduki mpaka walipofanikiwa. Mwaka 1994 alichaguliwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini. Tofauti na viongozi wengine wa Afrika, Mandela alihudumu kwa miaka 5 tu kisha alistaafu mwaka 1999 na kubaki kama balozi wa Afrika Kusini dhidi ya UKIMWI. Alizaliwa mwaka 1918 Mashariki mwa Rasi ya Tumaini Jema na amefariki akiwa na umri wa miaka 95. Harakati zake katika kupigania ukombozi wa mwafrika zinafanana na zile za watu weusi huko Amerika. Enzi za uhai wake aliwahi kuyasema haya: "During my lifetime I have dedicated myself to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination". Alishinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1993 iliyompa heshima kubwa ulimwenguni kote licha kuwa aliwahi kufungwa jela miaka 27. Alishiriki katika juhudi za kutafuta amani nchini Burundi, DRC na kwingeneko barani Afrika. Hakika atakumbukwa kwa mengi sana.
MWENYEZI MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI.