Posts

Showing posts from December, 2017

VIDEO: FID Q FT DIAMOND PLATNUMZ & RAYVANNY - FRESH REMIX | WATCH & DOWNLOAD

Image
DOWNLOAD

FAHAMU MAKALA BORA ZA KISAYANSI ZILIZOSAIDIA JAMII 2017

Image
Karibu ndugu msomaji wa VENANCE BLOG. Leo nimekuletea makala fupi zakisayansi ambazo zilipata umaarufu kwa mwaka huu kwa ufupi sana, na tuanze sasa Biashara ya siri kuuzwa sokwe Afrika Magharibi David Shukman na Sam Piranty walifanya utafiti mrefu Afrika Magharibi na BBC kugundua mipango ya siri inayohusiana na uuzwaji wa wanyamapori hasa sokwe. Hii ilisaidia kunusurika kwa sokwe aitwaye Nemley Jr ambaye alikuwa na umri wa mwaka mmoja. Mtambo wa Kupunguza Kabonidayoksaidi angani Katika mwaka 2017, riport zilionesha kwamba kuna mrundikano mwingi wa gesi ya kabonidayoksaidi angani mpaka kufikia wingi huo kuvunja rekodi huku juhudi za kimataifa zikishindwa kutatua changamoto hiyo ili kuepuka hatari ya kuongezeka kwa joto duniani. Je teknolojia hiyo inaweza kuondoa gesi hiyo ya kabonidayoksaidi ili kujibu maswali mengi ambayo juhudi za kimataifa zimekua zikishinwa kujibu? Hii iliandikwa na Matt McGrath. Misheni ya Anga ya Cassini kuitafiti sayari ya Sarateni ili

ZIFAHAMU GAUNI BORA 20 ZA MWAKA 2017

Image
Uhali gani msomaji wa VENANCE BLOG? Natumai u mzima, leo nakukaribisha kuzifahamu gauni 20 bora za mwaka 2017 zilizovaliwa na nyota wa fasheni na mitindo uli mwenguni.  Tuanze uchambuzi wetu. Huyuy ni Natalie Potman. Muigizaji maarufu katika kiwanda cha filamu Marekani Hollywood. Huenda miezi tisa ya ujauzito huwa migumu sana lakini Natalie hakuchoka katika hilo. Gauni hili ni ubunifu wa Prada na alilivaa katika tuzo za Golden Globe Awrds, unaweza kuona gauni lilivo zuri na kumpendeza mjamzito na mimba yake hapo juu. Unapenda fasheni na mitindo? Basi hili litamfaa zaidi mjamzito. Mwingine huyu. Anaitwa Brie Leson muigizaji mwingine kutoka kiwanda cha filamu Marekani. Brie alivaa gauni hili katika katika tuzo za 89 za Academy Awards. Ni ubunifu wa mwanamitindo Oscar de la Renta. Unaionaje gauni hiyo? Bila shaka kimpasuo hiko kidogo kinapendeza sana pamoja na mchanuo ule wa nyuma kama maua. Haya kazi kwako kupendeza na mtindo huu kwenye red carpet. Huwezi kushindwa kumt

TETESI ZA UHAMISHO ULAYA: NANI WANATARAJIWA KUHAMIA KLABU MPYA JANUARI?

Image
Ni wakati mwengine wa mwaka ambapo uvumi utaanza kusambaa. Uhamisho wa mwaka uliopita haukuwa na changamoto nyingi kutoka kwa timu sita bora katika ligi ya Uingereza huku timu zote za ligi hiyo zikitumia £215m mwezi Januari. Wakati huu itakuwaje, Je timu kubwa zitagharamika kununua wachezaji? Barani Ulaya ... Dirisha la uhamisho katika ligi tano kuu litafungwa kwa wakati mmoja. Dirisha la uhamisho la klabu za Uingereza, Ufaransa , Ujerumani , Italia  na Uhispania litafungwa Desemba 31 mwaka huu DIEGO LOPEZ ( klabu : Espanyol; Safu : kipa ; Umri : 36)   Anahusishwa na uhamisho wa : Crystal Palace. Ni kipa anayejulikana kwa kupigania nafasi ya kipa na Iker Casillas katika klabu ya Real Madrid, alikuwa katika benchi wakati Reala Madrid iliposhinda kombe la vilabu bingwa 2014 na amekuwa mchezaji wa Ziada wa Espanyol kwa kipindi kirefu cha msimu. Pia aliichezea Villarreal, Sevilla na AC Milan. KEVIN TRAPP (Paris St-Germain; kipa ; 27) Anahusishwa na

UNICEF: WATOTO WALISHAMBULIWA KWA KIWANGO KIKUBWA SANA MWAKA 2017

Image
  Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto UNICEF, limesema mwaka 2017 ulikuwa miongoni mwa miaka mibaya zaidi kwa watoto wanaoishi katika maeneo ya vita na mizozo duniani. Ripoti ya shirika hilo la UNICEF imesema pande zinazozozana katika vita duniani zilikiuka wazi wazi sheria za kimataifa linapokuja suala la kuwalinda watozo. Mkurugenzi wa UNICEF kuhusu mipango ya dharura Manuel Fontaine amesema watoto walilengwa na kuwekwa katika hatari ya mashambulizi wakiwa nyumbani, shuleni na wakicheza. Fontaine ameongeza kusema ulimwengu haupaswi kuyafumbia macho mashambulizi haya akisisitiza maovu dhidi ya watoto hayapaswi kuwa matukio ya kawaida katika ulimwengu wa sasa. Maovu dhidi ya Watoto ni makubwa Watoto katika mataifa yanayoshuhudia vita wamekuwa waathirika wakubwa wakiuawa, kulemazwa, kusajiliwa kwa lazima kuwa wapiganaji, kuolewa kwa lazima, kutekwa nyara, kutumikishwa na kubakwa. Wapiganaji watoto wa Sudan Kusini. Wengi wa watoto ha