Bunge nchini Afrika Kusini, leo linatarajiwa kuwa na kikao maalum cha kumkumbuka Nelson Mandela, huku viongozi duniani wakijiandaa kwa misa ya wafu itakayofanyika Jumanne.Kikao cha leo kinafanyika mwonzoni wa wiki ya shughuli mbali mbali za kumuenzi Mandela kabla ya mazishi yake tarehe 15 Disemba.Zaidi ya viongozi miamoja wa sasa na wa zamani wanatarajiwa kuhudhuria misa hiyo au mazishi mwishoni mwa wiki hii.Mnamo siku ya Jumapili, mamilioni ya wanachi walijitokeza kuhudhuria maombi maalum ya kumkumbuka Mandela aliyekuwa rais wa kwanza mzalendo wa nchi hiyo.Kikao cha leo cha Bunge kitakuwa kikao maalum kwa ajili tu ya kumkumbuka Hayati Mandela.Mke wa zamani wa Mandela, Winnie Madikizela-Mandela na mjukuu wake Mandela Mandla, wote ni wabunge katika bunge la taifa, lakini haijulikani ikiwa watahudhuria kikao cha leo.Msemaji wa chama tawala, ANC, Moloto Mothapo amesema, anatumai kuwa baadhi ya jamaa za familia ya Mandela, watakuwepo bungeni.Rais wa zamani wa nchi hiyo, FW de Klerk, amealikwa kwa kikao hicho.
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment