Bunge nchini Afrika Kusini, leo linatarajiwa kuwa na kikao maalum cha kumkumbuka Nelson Mandela, huku viongozi duniani wakijiandaa kwa misa ya wafu itakayofanyika Jumanne.Kikao cha leo kinafanyika mwonzoni wa wiki ya shughuli mbali mbali za kumuenzi Mandela kabla ya mazishi yake tarehe 15 Disemba.Zaidi ya viongozi miamoja wa sasa na wa zamani wanatarajiwa kuhudhuria misa hiyo au mazishi mwishoni mwa wiki hii.Mnamo siku ya Jumapili, mamilioni ya wanachi walijitokeza kuhudhuria maombi maalum ya kumkumbuka Mandela aliyekuwa rais wa kwanza mzalendo wa nchi hiyo.Kikao cha leo cha Bunge kitakuwa kikao maalum kwa ajili tu ya kumkumbuka Hayati Mandela.Mke wa zamani wa Mandela, Winnie Madikizela-Mandela na mjukuu wake Mandela Mandla, wote ni wabunge katika bunge la taifa, lakini haijulikani ikiwa watahudhuria kikao cha leo.Msemaji wa chama tawala, ANC, Moloto Mothapo amesema, anatumai kuwa baadhi ya jamaa za familia ya Mandela, watakuwepo bungeni.Rais wa zamani wa nchi hiyo, FW de Klerk, amealikwa kwa kikao hicho.
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...
Comments
Post a Comment