Bunge nchini Afrika Kusini, leo linatarajiwa kuwa na kikao maalum cha kumkumbuka Nelson Mandela, huku viongozi duniani wakijiandaa kwa misa ya wafu itakayofanyika Jumanne.Kikao cha leo kinafanyika mwonzoni wa wiki ya shughuli mbali mbali za kumuenzi Mandela kabla ya mazishi yake tarehe 15 Disemba.Zaidi ya viongozi miamoja wa sasa na wa zamani wanatarajiwa kuhudhuria misa hiyo au mazishi mwishoni mwa wiki hii.Mnamo siku ya Jumapili, mamilioni ya wanachi walijitokeza kuhudhuria maombi maalum ya kumkumbuka Mandela aliyekuwa rais wa kwanza mzalendo wa nchi hiyo.Kikao cha leo cha Bunge kitakuwa kikao maalum kwa ajili tu ya kumkumbuka Hayati Mandela.Mke wa zamani wa Mandela, Winnie Madikizela-Mandela na mjukuu wake Mandela Mandla, wote ni wabunge katika bunge la taifa, lakini haijulikani ikiwa watahudhuria kikao cha leo.Msemaji wa chama tawala, ANC, Moloto Mothapo amesema, anatumai kuwa baadhi ya jamaa za familia ya Mandela, watakuwepo bungeni.Rais wa zamani wa nchi hiyo, FW de Klerk, amealikwa kwa kikao hicho.
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...
Comments
Post a Comment