TANZANIA BARA YATIMIZA MIAKA 52 YA UHURU

HAPPY INDEPENDENT DAY TANZANIA MAINLAND!!! 
HERI YA SIKU YA UHURU TANZANIA BARA!!! 
Mnamo tarehe 9 Desemba 1961, Baba wa taifa Mwl. Julius K. Nyerere pamoja na viongozi wenzie wa TANU walifanikiwa kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika kwa wakati ule (sasa Tanzania) kutoka katika utawala wa Waingereza chini ya Gavana Richard Turnbull. Siku hiyo bendera ya Uingereza ilishushwa na bendera ya Tanganyika huru ilianza kupepea nchini. Enzi za ukoloni Tanzania ambayo kipindi hicho iliitwa Tanganyika, iliwahi kutawaliwa na utawala wa kikatili wa Ujerumani, na baadaye Uingereza. Baada ya Uhuru Mwl. Nyerere alikuwa Waziri Mkuu na baadaye Rais wa kwanza. Katika miaka hii 52 ya uhuru Tanganyika iliungana na Zanzibar mnamo 26 Aprili 1964 na kuunda JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. Toka uhuru tumepitia Mawaziri Wakuu 10, wa sasa akiwa ni Mizengo Kayanza Peter Pinda na pia Marais 4 ambao ni 1. Mwl. Julius Kambarage Nyerere 2. Ali Hassan Mwinyi 3. Benjamin William Mkapa 4. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndo mtawala kwa sasa.
 WITO KWA WATANZANIA NI KUDUMISHA AMANI NA KUEPUKANA NA MIGOGORO YA KIDINI NA UKABILA INAWEZA KULIGAWA TAIFA PIA KUDUMISHA UMOJA,USHIRIKIANO NA MSHIKAMANO ILI TAIFA LETU LIWEZE KUSONGA MBELE. 
WITO KWA SERIKALI NI KUHAKIKISHA INAILINDA AMANI YETU KWA GHARAMA YOYOTE. MUNGU IBARIKI TANZANIA!!!!

0 comments:

Post a Comment