Showing posts with label Burudani. Show all posts
Showing posts with label Burudani. Show all posts

KUELEKEA MWISHONI 2016 LADY JAY DEE KAYAANDIKA HAYA INSTAGRAM



Kuelekea mwisho wa mwaka 2016 msanii mkongwe Lady Jay Dee ameyaandika haya katika mtandao wa Instagram:

"Kiukweli comeback yangu ya 2016 ilikuwa kubwa sana kuliko watu wengi walivyoitegemea mbali na changamoto ngumu na nyingi nilizowahi kupitia na ninazoendelea kuzipitia kuliko msanii yeyote yule wa kike wala wa kiume Tanzania nadiriki kusema bado nimesimama Imara *Kejeli *Dhihaka *Mabezo *Kutengwa *Story za kusingiziwa ikiwemo kuambiwa nyumba yangu inauzwa sijui inapigwa mnada na mengine yote mnayoyajua ni vitu vinavyovunja moyo sana. Ila Wa Tanzania ninawaheshimu sana linapokuja swala la kupigania kitu mnachokipenda. Hivi bila nyie si ningekuwa marehemu??? Bila fans JayDee ni nani??? Ninawashukuru kwa kuniamsha. Ninawashukuru kwa kuniamini. Ninawashukuru kwa kunipa nguvu na jeuri. Kuanzia Ndindindi mpaka Together *Mliijaza Mlimani City *Mkajaza mikoa niliyopita. Nawaomba muendelee kujaa 2017. Ili kuwadhihirishia wanadamu kuwa Mungu huwa ni mmoja tu. Happy new year to my fans all around the world. Nawapenda hata nikinuna. Kaeni tayari kwa album ya WOMAN 2017."

Hiyo ilikuwa ni sehemu ya kwanza, aliyoiandika jana na hii hapa chini ni sehemu ya pili:

"Kama nilivyoeleza hapo awali mwaka 2015 vitu vingi  vilisimama ili nijpange upya. Na 2016 vitu vingi vilianza kurudi Ikiwemo kuendelea kuperform na Band yangu THE BAND ambayo niliondoa jina la MACHOZI BAND na tulizunguka sehemu nyingi nchini. Mwaka 2017 nitarudisha kitu kingine ambacho kimekuwa kikiulizwa na watu wengi sana kutokana na kutokuwepo hewani kwa takribani mwaka na nusu. DIARY YA LADY JAYDEE Itarudi tena kwa mfumo na muonekano wa tofauti na wa mwanzo ukizingatia maisha yangu pia yamebadilika Hivyo naomba sponsor kujitokeza kwa wingi pia kwani mambo yakuwa ni moto sana. Itakuwa ni kuhusu misha yangu binafsi ya kimuziki, kibiashara, mapenzi na kila kinachonizunguka. Kaeni tayari kwa Msimu mpya wa Diary ya Lady JayDee yenye production bora zaidi ya jana. Diary ya Lady JayDee pia itapatikana kwenye YouTube channel yangu fanya kusubscribe"

Hii ni sehemu ya pili aliyoiandika katika mtandao wa Instagram. Kama kuna lolote usikose kutembelea VENANCE BLOG kwa mengine zaidi. Jay Dee anapatikana Instagram @jidejaydee





 Unaweza kulike VENANCE BLOG facebook kwa kubofya HAPA
Nifolo kwenye Twitter @Venancetz au bofya HAPA
Nipo Instagram pia @venancegilbert au bofya HAPA

VENANCE BLOG INAWATAKIA HERI YA CHRISTMAS 2014

VENANCE BLOG inapenda kuwatakia heri ya Christmas kwa mwaka huu 2014 tusherekee kwa amani na upendo huku tukimtanguliza Mungu katika kila jambo kwani yeye ndo muweza wa yote. Heri ya Krismas na pia Heri ya Mwaka mpya 2015!!







WASILIANA NAMI: 
Facebook: VENANCE BLOG 
Twitter: @Venancetz 
Instagram: venancegilbert
Simu: +255712586027/+255753400208 
Email: venancegilbert@gmail.com

CHRISTMAS PHOTOS

MERRY CRISTMAS

HAPPY CRISTMAS

GREAT CHRISTMAS

ENJCHRISTMAS

FANTASTIC CHRISTMAS

NICE CHRISTMAS

JUST FOR YOU

JUST FOR YUOU



MERRY CHRISTMAS & HAPPY CHRISTMAS

SALAAMU ZA SIKUKUU YA KRISMASI


Venance Blog inawatakieni HERI YA KRISMAS. Mpendwa msomaji wa blog hii, leo Wakristu duniani kote wanaadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwokozi wao, Yesu Kristu aliyezaliwa takribani miaka 2000 iliyopita. Venance Blog inakukumbusha katika sikukuu hii kama ni mnywaji usilewe sana na pia ukumbuke ugonjwa hatari wa UKIMWI hasa siku kama hii ya leo kuwa makini sana, pia tuwasaidie watoto wetu au wadogo zetu kuvuka mabarabara salama huko mitaani kwetu. Krismasi ni siku ya furaha na kuoneshana upendo, hivyo tupendane wote kwa pamoja. HERI YA KRISMAS NA KRISMAS YENYE FURAHA SHEREHEKEA KWA AMANI NA UPENDO!!!

CHRISTMAS GREETINGS

 

Venance Blog is grateful to wish you a MERRY CHRISTMAS. Venance Blog wishes you a nice celebration, one thing to remember is to keep our national peace and avoiding other evils, if you drink don't take too much remember there is HIV/AIDS so be careful help the children to cross the road along the streets because its a day for happiness and loving each other.. MERRY CHRISTMAS & HAPPY CHRISTMAS!!!

MAANDALIZI MEMA YA SIKUKUU YA KRISMAS

Kwanza namshukuru Mungu toka tukiwa wadogo mpaka sasa anaendelea kutulinda. Uongozi mzima wa Venance Blog tunawatakieni maandalizi mema ya Krismas hapo kesho, wale wa kanisani tukafurahi kwani bwana atazaliwa. Msali salama katika misa za mkesha kubwa zaidi kudumisha amani na usalama kuanzia leo mpaka sikuku itakapoisha. MAANDALIZI MEMA YA KRISMAS!!!

UNGEKUWA WEWE UNGEFANYA NINI?


House girl alitandika kitanda cha bosi wake Kama Sehemu ya jukumu lake la kila siku. Alipomaliza akakitazama sana kile kitanda cha bosi wake akasema naweza kufa bure bila ya kulalia kitanda kama hiki. Akasema ngoja nijaribu kulala angalau kidogo.
 Akavua nguo zote akaziweka chini, akabaki na gagulo tu akawasha AC akajifunika brangeti gubigubi akalala. Kwa bahati mbaya usingizi ukampitia kweli akalala fofofo.
Ghafla Mume wa bosi akarudi na haikuwa kawaida yake kurudi Muda huo. Alipoingia chumbani, akajua hakika huyu ni mke wangu na kwa kuwa jana tulikwaruzana atakuwa amekasirika tu. Akaogopa kumwamsha. Mwanamme akasaula, akabaki na msuli naye akajifunika hilo hilo blanketi kwa taratibu sana kwa hofu ya kumwamsha mke wake. Kwa bahati mbaya naye usingizi ukampitia, akalala fofofo .
Bosi aliporudi, akaingia chumbani, akakuta watu wawili wamelala fofofo. Akafunua blanketi kwa nguvu, akawakuta wote wawili; yaani yule mfanyakazi na mume wake wamelala pamoja. Walipoulizwa kila mtu akaeleza ukweli wake. Je ungekuwa wewe ni bosi, housegirl au huyo mume ungefanya nini????

HAPPY FAMILY DAY

Nawatakieni siku njema ya familia duniani zidisheni upendo katika familia zenu na Mungu awabariki mkue katika imani ya kumtegemea yeye.

HAPPY FAMILY DAY!

HAPO KWELI SERA YA KILIMO KWANZA ITATIMIA KAMA BWANA SHAMBA ANAINGIA SHAMBA NA SUTI??

BWANA SHAMBA

KARIBU VENANCE BLOG

Karibu VENANCE BLOG, hapa utapata habari za kitaifa, kimataifa, michezo, burudani, matukio na nukuu za watu maarufu duniani pamoja na mengine mengi bila kusahau nyanja ya elimu. Unachotakiwa kufanya ni kuwa karibu na VENANCE BLOG kila wakati kwa sababu ni haki yako kupata habari kama chakula cha ubongo. Ungana nami kwa njia zifuatazo:


2. Twitter

3. Instagram 






VENANCE BLOG © May 2013.