Posts

Showing posts with the label Celebrity

MFAHAMU WOLE SOYINKA GWIJI WA FASIHI YA KIAFRIKA MWENYE TUZO YA NOBEL KATIKA FASIHI 1986

Image
Picha kwa hisani ya Oasis Magazine Bila shaka jina la Wole Soyinka sio geni masikioni mwako kwa sababu wengi wetu tumesoma tamthiliya (play) yake ya The Lion and The Jewel sekondari hasa kidato cha tatu na cha nne na The Trials of Brother Jero kwa wale waliosoma miaka ya nyuma. Hapa nitamzungumzia Wole Soyinka, mwafrika wa kwanza kushinda tuzo ya Nobel katika fasihi. Haya ni mambo ambayo huwezi kufundishwa kwenye mitaala ya shuleni, hivyo unapaswa kuyafahamu nje ya mtaala wa shule kwa muda wako mwenyewe. Awali ya yote, ni kwamba wasifu huu niliuandika kwa mara ya kwanza katika mtandao wa Twitter Julai 13, 2020 kabla sijaamua kuuleta hapa. MAISHA YA MWANZO Soyinka alizaliwa Julai 13, 1934 huko Abeokuta jirani na Ibadan nchini Naijeria. Majina yake halisi ni Akinwande Oluwole Babatunde Soyinka lakini anafahamika sana kama Wole Soyinka. Alisoma Fasihi, Ibadan. Mwaka 1954 alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds nchini Uingereza mara baada ya kumaliza masomo yake katika Chuo cha Serikali, Ibadan

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

Image
KUZALIWA  Celebrity wetu wa leo ni Shania Twain. Jina lake la kuzaliwa ni  Eilleen Regina Edwards lakini umaarufu wake umetokana na jina lilizoeleka la Shania Twain. Wengine wanamuita Malkia wa Muziki wa Country.  Alizaliwa mnamo Agosti 28, 1965 leo anatimiza miaka 53 ya kuwepo duniani. Alizaliwa huko  Windsor, Ontario, Canada akiwa ni mmoja kati ya mabinti 3 wa Clarence na Sharon (Morison) Edwards. Yeye ndiye mkubwa. Alipokua na miaka 6 mama yake aliolewa tena na Jerry Twain ambaye alimchukua kama mwanaye. Alianza kuimba katika vilabu vya pombe na alipokua na miaka 13 alionekana katika The Tommy Hunter Show. Alipokua na umri wa miaka 22 wazazi wake waliuawa katika ajali na hivyo akaacha sanaa muziki ili awalee wadogo zake Mark na Darryl pamoja na dada zake wawili aliozaliwa nao kwa baba yake na mama yake mzazi. Mwaka 1991 alibadilisha jina lake alilopewa na wazazi wake na kujiita Shania Twain na hapo ndipo jina hili lilipokua.  Mwaka huo huo pia alisaini mkataba na lebo ya muziki

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI ATIMIZA MIAKA 93: TUJIKUMBUSHE HISTORIA YAKE KWA UFUPI

Image
Mei 8, 1925 wkati huo Tanganyika ikiwa ni koloni la Uingereza alizaliwa Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mzee Ali Hassan Mwinyi.   Alipoingia madarakani kumpokea aliyekuwa Rais wa Awamu ya kwanza,Mwalimu Julius Nyerere mnamo tarehe 5 Novemba mwaka 1985, watanzania wachache sana (kama wapo) waliweza kutabiri kwamba miaka kumi baadaye na zaidi baada ya kustaafu rasmi, ataibuka kuwa mmojawapo wa maraisi wa Tanzania ambao watabakia kupendwa na kuheshimika kwa namna ya kipekee kabisa. Tunadiriki kusema “namna ya kipekee” kwa sababu ukweli unabakia kwamba inapofanyika tathmini ya uongozi wake, bado mtu au watu mbalimbali wanakuwa na maoni yao tofauti tofauti kuhusiana na suala hilo. Utoaji huo wa tathmini ni suala ambalo haliwezi kukoma leo wala kesho, ni tukio linaloendea na litakaloendelea, vizazi mpaka vizazi. Huo ndio uzuri au ubaya wa historia na muda (history and time) huwa vina jinsi ya kipekee katika kutoa hukumu zao. Mp

MOHAMMED SALAH: ILIKUAJE AKAIMARIKA HARAKA? MAJIBU HAYA HAPA

Image
Mohammed Salah Huku wachezaji wakisherehekea kwa fujo baada 4-0 dhidi ya ENPPI, kocha Said Al Shesheni aliangalia upande mmoja na kugundua kwamba mchezaji mmoja wa kikosi cha al-Mokawloon wa kikosi cha wachezaji wasiozidi umri wa miaka 16 hakuwa akifurahia michuano iliokuwa Cairo.  Alikuwa akibubujikwa na machozi kwamba jina lake halikuwa katika orodha ya wafungaji mabao.  Akicheza kama beki wa kushoto ilikuwa vigumu kuchukua jukumu kubwa kama alivyotaka. Akiwa mzaliwa wa eneo la Nagrig, kijiji kimoja kilichopo kilomita 130 Kaskazini mwa mji mkuu wa Misri, mchezaji huyo alilazimika kupitia tatizo la kusafiri kwa saa tisa kila siku mara nyingine akilazimika kutumia mabasi 10, ili kuweza kufika mazoezini mbali na kushiriki mechi. Na baada ya kufurahishwa na ari ya kijana huyo Al Sheheni alimpatia fursa na kumpeleka safu ya mbele. Tangu wakati huo Mohammed Salah hajarudi nyuma tena. Mchezaji huyo wa Liverpool alilazimika kulipia uwanja mpya katika shule yake ya zamani. Haba