Skip to main content

UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU GOOGLE BARD

Nembo (logo) ya Google Bard
Kufuatia mafanikio ya robotisogozi ya OpenAI ambayo ni ChatGPT, Google ilitoa robotisogozi yake ya akili bandia, Bard. Kwa vile inapatikana sehemu kubwa haya ndiyo unayohitaji kufahamu kuihusu Bard lakini kabla sijaendelea nikufahamishe vifupisho vya maneno yatayotumika katika makala hii:
  • AI - Artificial Intelligence ambayo ni Akili Bandia.
  • LaMDA - Language Model for Dialogue Applications ambao ni Mfumo wa Lugha kwa Mazungumzo na Matumizi.
  • LLM - Large Language Model ambao ni Mfumo Mkubwa wa Lugha.
  • PALM (PaLM) - Pathways Language Model ambavyo ni vigezo bilioni 540 va kigezo cha lugha kubwa modeli iliyotengenezwa na Google AI

Bard ni huduma ya Google ya majaribio ya mazungumzo ya akili bandia. Inakusudiwa kufanya kazi sawa na ChatGPT huku tofauti kubwa ni kwamba huduma ya Google itatoa habari zake kutoka katika wavuti.
Picha ya skrini: Venance Gilbert 
Kama vile gumzo nyingi za akili bandia, Bard anaweza kuandika msimbo (code), kujibu matatizo ya hesabu na kusaidia mahitaji yako ya uandishi.

Bard alitambulishwa Februari 6 mwaka huu katika taarifa kutoka Google na Mkurugenzi Mtendaji wa Alphabet Sundar Pichai. Ingawa Bard ilikuwa ni dhana mpya kabisa, huduma hii ya mazungumzo ya akili bandia ambayo ilizinduliwa iliendeshwa na Mfumo wa Lugha wa Google kwa Maombi ya Mazungumzo (LaMDA) ambayo ilizinduliwa miaka miwili iliyopita yaani 2021. Google Bard ilitolewa zaidi mwezi mmoja baadaye, tarehe 21 Machi 2023 lakini Septemba 27 ikaachiwa rasmi katika mataifa mengi duniani.

Google Bard sasa inaendeshwa na mfumo wa lugha kubwa na ya hali ya juu zaidi wa Google (LLM) PaLM 2, ambao ulizinduliwa katika mkutano wa Google I/O 2023.

PaLM 2 ambalo ni toleo la juu zaidi la PaLM, ambalo lilitolewa Aprili 2022 linairuhusu Bard kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kufanya kazi kwa kiwango cha juu zaidi.

Toleo la awali la Bard lilitumia toleo la kielelezo chepesi cha LaMDA, kwa sababu lilihitaji nishati kidogo ya kompyuta na lingeweza kuongezwa kwa watumiaji zaidi.

LaMDA iliundwa kwenye transfoma, usanifu wa mtandao wa "neural"  wa Google ambao iliuvumbua kama chanzo huru (open source) mwaka 2017. Cha kufurahisha ni kwamba GPT-3, mfumo wa lugha wa ChatGPT hufanya kazi pia ulijengwa kwenye transfoma, kulingana na Google.

Uamuzi wa Google wa kutumia LLM zake, LaMDA na PaLM 2 ulikuwa ni uamuzi wa kijasiri kutoka kwa Google kwa kuwa baadhi ya robotisogozi maarufu za AI hivi sasa zikiwemo ChatGPT na Bing Chat, hutumia mfumo wa lugha katika mfululizo wa GPT.

Bard kwa sasa inapatikana katika lugha zaidi ya 40 ikiwemo lugha ya Kiswahili.

Katika mfululizo wa maboresho ya Julai, Google iliongeza utafutaji wa aina nyingi ili kuruhusu watumiaji uwezo wa kuingiza picha na maandishi.

Utafutaji wa aina nyingi unawezekana kupitia ujumuishaji wa Google Lens, uamuzi huo ulitangazwa hapo awali kwenye Google I/O. Kipengele hiki ni muhimu kwa sababu watumiaji wanaweza kupakia picha na kuiomba Bard maelezo zaidi kuihusu au kuijumuisha kwenye kidokezo. Kwa mfano, ukiona mmea na ungependa kujua ni mmea gani, unachohitaji kufanya ni kupiga picha na kuuliza Google Bard.

Je, Google inajumuisha picha katika majibu yake?

Ndiyo, mwishoni mwa mwezi Mei, Bard ilihuishwa ili kujumuisha picha katika majibu yake. Picha hutolewa kutoka Google na kuonyeshwa unapouliza swali ambalo linaweza kujibiwa vyema kwa kujumuisha picha. Kwa mfano niliuliza Bard kuhusu "maeneo mazuri ya kutembelea ukiwa Tanzania" ikanipa majibu ikiambatanisha na picha. Tizama katika picha ya skrini (screenshot) hapa chini:
Picha ya skrini: Venance Gilbert

Je, kuna utata gani kuhusu Google Bard?

Google Bard haikuwa na uzinduzi mzuri baada ya Bard kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusu taasisi ya James Webb Space Telescope (JWST).

Wakati wa uzinduzi, Google ilituma onyesho la huduma ya robotisogozi hii ya AI kwenye ukurasa wa twitter ambapo ujumbe kwa njia ya swali ulisomeka, "Ni uvumbuzi gani mpya kutoka kwa James Webb Space Telescope ninaweza kumwambia mtoto wangu wa miaka 9?" Bard alijibu: "JWST ilichukua picha za kwanza kabisa za sayari nje ya mfumo wetu wa jua." Watu waligundua haraka kuwa jibu hilo halikuwa sahihi.

"Hii inaangazia umuhimu wa mchakato mkali wa majaribio, jambo ambalo tunaanza wiki hii na programu yetu ya Mjaribu Anayeaminika," msemaji wa Google alipozungumza na ZDNET. Utendaji halisi wa robotisogozi hii pia ulisababisha maoni mengi hasi.

Katika tajriba ya ZDNET ambayo ni tovuti maarufu ya habari za teknolojia, Bard ilishindwa kujibu maswali ya kawaida tu, ilikuwa na muda mrefu zaidi wa kusubiri kuliko kawaida, haikujumuisha vyanzo kiotomatiki ikilinganishwa na washindani wake ambao walionekana kuwa mahiri zaidi. Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Google, Sundar Pichai aliiita Bard "a souped-up civic" akiwa na maana robotisogozi iliyoboreshwa zaidi ikilinganishwa na ChatGPT na Bing Chat.

Kabla ya Bard kutambulishwa, LaMDA ya Google ilishutumiwa pia. Kwa mfano Tiernan Ray mwandishi wa ZDNET aliripoti, muda mfupi baada ya kuchapishwa kwa LaMDA, mhandisi wa zamani wa Google, Blake Lemoine alitoa waraka ambamo alishiriki kwamba LaMDA inaweza kuwa "inazo hisia" kama binadamu. Mzozo huu ulififia baada ya Google kukana maelezo hayo na kumpa likizo Lemoine. Baadaye aliondolewa kazini.

Kubadilisha kwa Google kutoka LaMDA hadi PaLM 2 kunapaswa kusaidia kupunguza maswala mengi yenye utata katika robotisogozi ya Bard.

Kwa nini Google iliamua kuzindua Google Bard?

Hebu turudi hadi mwishoni mwa Novemba 30, 2022 wakati ChatGPT ilipozinduliwa. Chini ya wiki moja baada ya kuzinduliwa ChatGPT ilipata watumiaji zaidi ya milioni moja. Kwa mujibu uchanganuzi wa benki ya Uswizi ya UBS, ChatGPT ikawa ni programu (app) inayokua kwa kasi zaidi kwa wakati wote. Makampuni mengine ya teknolojia ikiwa ni pamoja na Google, yaliona mafanikio haya na yalitaka kufikia hatua kama hiyo.

Katika wiki hiyo hiyo ambayo Google ilizindua Bard mnamo Februari, 2023, Microsoft ilizindua Bing mpya iliyoboreshwa ya AI, ambayo inaendeshwa na OpenAI LLM ya teknolojia madhubuti (next generation) iliyoundwa mahususi kwa utafutaji (search).

Je, Google ina huduma gani nyingine za Akili Bandia?

Google imetengeneza huduma zingine za AI ambazo bado hazijatambulishwa kwa umma. Kampuni kubwa ya kiteknolojia kwa kawaida huwekeza sana inapokuja kwa bidhaa za AI na haizitoi hadi itakapojidhihirishia katika utendaji wa bidhaa husika.

Kwa mfano, Google imeunda jenereta ya picha ya AI, Imagen, ambayo inaweza kuwa mbadala bora dhidi ya DALL-E ya OpenAI. Google pia ina program ya muziki ya AI, MusicLM, ambayo Google inasema haina mpango wa kuitambulisha kwa sasa.

Katika makala ya hivi karibuni kuhusu MusicLM, Google ilitambua hatari ambayo aina hizi za mifumo ya lugha inaweza kusababisha matumizi mabaya ya maudhui ya ubunifu na upendeleo uliopo katika mafunzo ambao unaweza kuathiri tamaduni ambazo hazijawakilishwa sana katika mafunzo, pamoja na hofu juu ya matumizi ya kitamaduni.

Gemini ni nini?

Katika mkutano wa Google I/O 2023, kampuni ilitangaza Gemini, mfumo mkubwa wa lugha uliyoundwa na Google DeepMind. Wakati wa Google I/O, kampuni iliripoti kuwa Gemini iliyoindwa kwa mfumo wa LLM ilikuwa bado katika hatua zake za awali za utengenezwaji.

Hata hivyo, inasemekana kuwa Google inakaribia kuzindua Gemini, ambayo itazidi PaLM 2 katika utendaji na uwezo wake na kuifanya iwe sawa na GPT-4, mfumo wa lugha wa Open AI ambao ni wa juu zaidi.

Maabara ya Google (Google Lab) ni nini? 

Maabara ya Google ni jukwaa ambapo unaweza kujaribu mawazo ya awali ya Google kwa vipengele na bidhaa. Jukwaa kwa sasa linajumuisha programu ya muziki ya AI ya Google MusicLM, kipengele cha Ujumbe kinachoendeshwa na AI kinachojulikana kama Magic Compose, Utafutaji wa Google unaoendeshwa na AI (AI-powered Google Search) na mengine zaidi. Mtu yeyote anaweza kujiunga na jukwaa hili. Unachotakiwa kufanya ni kujiunga na orodha ya watu wanaosubiri (waitlist) au ubofye "Get Started" kwenye tovuti ya Maabara ya Google.


MAKALA HII IMEANDIKWA NA SABRINA ORTIZ KATIKA TOVUTI YA ZDNET NA KUSIMULIWA KWA KISWAHILI NA VENANCE GILBERT.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

FRIENDSHIP QUOTES OF THE DAY MAY 26, 2018

Today I invite you to read these quotes of the day. Enjoy your day. 1.  One of the most beautiful qualities of true friendship is to understand and to be understood. ~Lucius Annaeus Seneca. 2.  Walking with a friend in the dark is better than walking alone in the light. ~Helen Keller. 3.  There is nothing on this earth more to be prized than true friendship. ~Thomas Aquinas. 4.  My best friend is the one who brings out the best in me. ~Henry Ford. 5.  It is one of the blessings of old friends that you can afford to be stupid with them. ~Ralph Waldo Emerson. 6.  The strong bond of friendship is not always a balanced equation; friendship is not always about giving and taking in equal shares. Instead, friendship is grounded in a feeling that you know exactly who will be there for you when you need something, no matter what or when. ~Simon Sinek. 7.  A friend is someone who gives you total freedom to be yourself. ~Jim Mo...

IDADI YA WATU WALIOFARIKI UGANDA YAFIKIA 33

Moto mkubwa uliowaka baada yaajali mbaya ya barabarani iliohusisha lori la mafuta, umewauwa takriban watu 33 mjini kampala Uganda. Watu wengine 30 wanadaiwa kujeruhiwa vibaya kufuatia tukiohilo. Maafisa wa polisi wanasema kuwa kati ya waliofariki ni raia waliokuwa wanakimbilia eneo hilo la mkasa kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwa lori hilo. maafisa wa serikali walikuwa katika harakati za kutambua mili ya waliofariki baada ya wengi wao kuchomeka vibaya. Idara ya polisi imesema kuwa waliofariki waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.

VITAMBULISHO VYA URAIA KUVUKIA MIPAKA KENYA, RWANDA NA UGANDA

Wananchi wa mataifa ya Rwanda, Uganda na Kenya wamepokea kwa shangwe kuanza kwa mpango wa kutumiwa kwa vitambulisho vya uraia kama cheti cha kuwaruhusu kuvuka mpaka na kuingia moja wapo wa nchi hizo.Mpango huu wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kusafiria katika nchi hizo tatu umeanza kutumiwa rasmi tarahe Mosi Januari 2014, kufuatia makubaliano kati ya viongozi wa mataifa hayo.Mpango wenyewe unatokana na makubaliano kati ya viongozi wa nchi tatu waliofikia wakati wa mkutano uliofanyika nchini Uganda mwezi Juni mwaka jana.Pia mpango huu unalenga kurahisisha usafiri wa watu wa jumuiya katika mataifa wanachama kama awamu ya pili ya ushirikiano kati ya mataifa wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.Hata hivyo siku moja tu baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kuwaruhusu raia wa nchini tatu, Uganda, Kenya na Rwanda kuvuka mpaka na kuingia mojawapo ya nchi hizo sasa inaonekana mpango huo huenda ukawanufaisha watu wachache peke yake.Sio ...

CHANGES QUOTES OF THE DAY MAY 23, 2018

Hello dear reader, welcome once again. Today I have gathered the quotes concerning changes in life. I should not write more since I am not not the speaker in this category, take your time to dive in and become intellectual with full equipped knowledge from the great men of history Remember, someday it might be you. Do not rely on inspiration from friends while you are needy, VENANCE BLOG is here for you. Welcome all the time by searching Quotes. Now proceed. 1. Every great dream begins with a dreamer. Always remember, you have within you the strength, the patience, and the passion to reach for the stars to change the world. ~Harriet Tubman. 2. Change your thoughts and you change your world. ~Norman Vincent Peale. 3.  If you don't like something, change it. If you can't change it, change your attitude. ~Maya Angelou 4.  Change will not come if we wait for some other person or some other time. We are the ones we've been waiting for. We are the change that...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...