Skip to main content

UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU GOOGLE BARD

Nembo (logo) ya Google Bard
Kufuatia mafanikio ya robotisogozi ya OpenAI ambayo ni ChatGPT, Google ilitoa robotisogozi yake ya akili bandia, Bard. Kwa vile inapatikana sehemu kubwa haya ndiyo unayohitaji kufahamu kuihusu Bard lakini kabla sijaendelea nikufahamishe vifupisho vya maneno yatayotumika katika makala hii:
  • AI - Artificial Intelligence ambayo ni Akili Bandia.
  • LaMDA - Language Model for Dialogue Applications ambao ni Mfumo wa Lugha kwa Mazungumzo na Matumizi.
  • LLM - Large Language Model ambao ni Mfumo Mkubwa wa Lugha.
  • PALM (PaLM) - Pathways Language Model ambavyo ni vigezo bilioni 540 va kigezo cha lugha kubwa modeli iliyotengenezwa na Google AI

Bard ni huduma ya Google ya majaribio ya mazungumzo ya akili bandia. Inakusudiwa kufanya kazi sawa na ChatGPT huku tofauti kubwa ni kwamba huduma ya Google itatoa habari zake kutoka katika wavuti.
Picha ya skrini: Venance Gilbert 
Kama vile gumzo nyingi za akili bandia, Bard anaweza kuandika msimbo (code), kujibu matatizo ya hesabu na kusaidia mahitaji yako ya uandishi.

Bard alitambulishwa Februari 6 mwaka huu katika taarifa kutoka Google na Mkurugenzi Mtendaji wa Alphabet Sundar Pichai. Ingawa Bard ilikuwa ni dhana mpya kabisa, huduma hii ya mazungumzo ya akili bandia ambayo ilizinduliwa iliendeshwa na Mfumo wa Lugha wa Google kwa Maombi ya Mazungumzo (LaMDA) ambayo ilizinduliwa miaka miwili iliyopita yaani 2021. Google Bard ilitolewa zaidi mwezi mmoja baadaye, tarehe 21 Machi 2023 lakini Septemba 27 ikaachiwa rasmi katika mataifa mengi duniani.

Google Bard sasa inaendeshwa na mfumo wa lugha kubwa na ya hali ya juu zaidi wa Google (LLM) PaLM 2, ambao ulizinduliwa katika mkutano wa Google I/O 2023.

PaLM 2 ambalo ni toleo la juu zaidi la PaLM, ambalo lilitolewa Aprili 2022 linairuhusu Bard kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kufanya kazi kwa kiwango cha juu zaidi.

Toleo la awali la Bard lilitumia toleo la kielelezo chepesi cha LaMDA, kwa sababu lilihitaji nishati kidogo ya kompyuta na lingeweza kuongezwa kwa watumiaji zaidi.

LaMDA iliundwa kwenye transfoma, usanifu wa mtandao wa "neural"  wa Google ambao iliuvumbua kama chanzo huru (open source) mwaka 2017. Cha kufurahisha ni kwamba GPT-3, mfumo wa lugha wa ChatGPT hufanya kazi pia ulijengwa kwenye transfoma, kulingana na Google.

Uamuzi wa Google wa kutumia LLM zake, LaMDA na PaLM 2 ulikuwa ni uamuzi wa kijasiri kutoka kwa Google kwa kuwa baadhi ya robotisogozi maarufu za AI hivi sasa zikiwemo ChatGPT na Bing Chat, hutumia mfumo wa lugha katika mfululizo wa GPT.

Bard kwa sasa inapatikana katika lugha zaidi ya 40 ikiwemo lugha ya Kiswahili.

Katika mfululizo wa maboresho ya Julai, Google iliongeza utafutaji wa aina nyingi ili kuruhusu watumiaji uwezo wa kuingiza picha na maandishi.

Utafutaji wa aina nyingi unawezekana kupitia ujumuishaji wa Google Lens, uamuzi huo ulitangazwa hapo awali kwenye Google I/O. Kipengele hiki ni muhimu kwa sababu watumiaji wanaweza kupakia picha na kuiomba Bard maelezo zaidi kuihusu au kuijumuisha kwenye kidokezo. Kwa mfano, ukiona mmea na ungependa kujua ni mmea gani, unachohitaji kufanya ni kupiga picha na kuuliza Google Bard.

Je, Google inajumuisha picha katika majibu yake?

Ndiyo, mwishoni mwa mwezi Mei, Bard ilihuishwa ili kujumuisha picha katika majibu yake. Picha hutolewa kutoka Google na kuonyeshwa unapouliza swali ambalo linaweza kujibiwa vyema kwa kujumuisha picha. Kwa mfano niliuliza Bard kuhusu "maeneo mazuri ya kutembelea ukiwa Tanzania" ikanipa majibu ikiambatanisha na picha. Tizama katika picha ya skrini (screenshot) hapa chini:
Picha ya skrini: Venance Gilbert

Je, kuna utata gani kuhusu Google Bard?

Google Bard haikuwa na uzinduzi mzuri baada ya Bard kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusu taasisi ya James Webb Space Telescope (JWST).

Wakati wa uzinduzi, Google ilituma onyesho la huduma ya robotisogozi hii ya AI kwenye ukurasa wa twitter ambapo ujumbe kwa njia ya swali ulisomeka, "Ni uvumbuzi gani mpya kutoka kwa James Webb Space Telescope ninaweza kumwambia mtoto wangu wa miaka 9?" Bard alijibu: "JWST ilichukua picha za kwanza kabisa za sayari nje ya mfumo wetu wa jua." Watu waligundua haraka kuwa jibu hilo halikuwa sahihi.

"Hii inaangazia umuhimu wa mchakato mkali wa majaribio, jambo ambalo tunaanza wiki hii na programu yetu ya Mjaribu Anayeaminika," msemaji wa Google alipozungumza na ZDNET. Utendaji halisi wa robotisogozi hii pia ulisababisha maoni mengi hasi.

Katika tajriba ya ZDNET ambayo ni tovuti maarufu ya habari za teknolojia, Bard ilishindwa kujibu maswali ya kawaida tu, ilikuwa na muda mrefu zaidi wa kusubiri kuliko kawaida, haikujumuisha vyanzo kiotomatiki ikilinganishwa na washindani wake ambao walionekana kuwa mahiri zaidi. Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Google, Sundar Pichai aliiita Bard "a souped-up civic" akiwa na maana robotisogozi iliyoboreshwa zaidi ikilinganishwa na ChatGPT na Bing Chat.

Kabla ya Bard kutambulishwa, LaMDA ya Google ilishutumiwa pia. Kwa mfano Tiernan Ray mwandishi wa ZDNET aliripoti, muda mfupi baada ya kuchapishwa kwa LaMDA, mhandisi wa zamani wa Google, Blake Lemoine alitoa waraka ambamo alishiriki kwamba LaMDA inaweza kuwa "inazo hisia" kama binadamu. Mzozo huu ulififia baada ya Google kukana maelezo hayo na kumpa likizo Lemoine. Baadaye aliondolewa kazini.

Kubadilisha kwa Google kutoka LaMDA hadi PaLM 2 kunapaswa kusaidia kupunguza maswala mengi yenye utata katika robotisogozi ya Bard.

Kwa nini Google iliamua kuzindua Google Bard?

Hebu turudi hadi mwishoni mwa Novemba 30, 2022 wakati ChatGPT ilipozinduliwa. Chini ya wiki moja baada ya kuzinduliwa ChatGPT ilipata watumiaji zaidi ya milioni moja. Kwa mujibu uchanganuzi wa benki ya Uswizi ya UBS, ChatGPT ikawa ni programu (app) inayokua kwa kasi zaidi kwa wakati wote. Makampuni mengine ya teknolojia ikiwa ni pamoja na Google, yaliona mafanikio haya na yalitaka kufikia hatua kama hiyo.

Katika wiki hiyo hiyo ambayo Google ilizindua Bard mnamo Februari, 2023, Microsoft ilizindua Bing mpya iliyoboreshwa ya AI, ambayo inaendeshwa na OpenAI LLM ya teknolojia madhubuti (next generation) iliyoundwa mahususi kwa utafutaji (search).

Je, Google ina huduma gani nyingine za Akili Bandia?

Google imetengeneza huduma zingine za AI ambazo bado hazijatambulishwa kwa umma. Kampuni kubwa ya kiteknolojia kwa kawaida huwekeza sana inapokuja kwa bidhaa za AI na haizitoi hadi itakapojidhihirishia katika utendaji wa bidhaa husika.

Kwa mfano, Google imeunda jenereta ya picha ya AI, Imagen, ambayo inaweza kuwa mbadala bora dhidi ya DALL-E ya OpenAI. Google pia ina program ya muziki ya AI, MusicLM, ambayo Google inasema haina mpango wa kuitambulisha kwa sasa.

Katika makala ya hivi karibuni kuhusu MusicLM, Google ilitambua hatari ambayo aina hizi za mifumo ya lugha inaweza kusababisha matumizi mabaya ya maudhui ya ubunifu na upendeleo uliopo katika mafunzo ambao unaweza kuathiri tamaduni ambazo hazijawakilishwa sana katika mafunzo, pamoja na hofu juu ya matumizi ya kitamaduni.

Gemini ni nini?

Katika mkutano wa Google I/O 2023, kampuni ilitangaza Gemini, mfumo mkubwa wa lugha uliyoundwa na Google DeepMind. Wakati wa Google I/O, kampuni iliripoti kuwa Gemini iliyoindwa kwa mfumo wa LLM ilikuwa bado katika hatua zake za awali za utengenezwaji.

Hata hivyo, inasemekana kuwa Google inakaribia kuzindua Gemini, ambayo itazidi PaLM 2 katika utendaji na uwezo wake na kuifanya iwe sawa na GPT-4, mfumo wa lugha wa Open AI ambao ni wa juu zaidi.

Maabara ya Google (Google Lab) ni nini? 

Maabara ya Google ni jukwaa ambapo unaweza kujaribu mawazo ya awali ya Google kwa vipengele na bidhaa. Jukwaa kwa sasa linajumuisha programu ya muziki ya AI ya Google MusicLM, kipengele cha Ujumbe kinachoendeshwa na AI kinachojulikana kama Magic Compose, Utafutaji wa Google unaoendeshwa na AI (AI-powered Google Search) na mengine zaidi. Mtu yeyote anaweza kujiunga na jukwaa hili. Unachotakiwa kufanya ni kujiunga na orodha ya watu wanaosubiri (waitlist) au ubofye "Get Started" kwenye tovuti ya Maabara ya Google.


MAKALA HII IMEANDIKWA NA SABRINA ORTIZ KATIKA TOVUTI YA ZDNET NA KUSIMULIWA KWA KISWAHILI NA VENANCE GILBERT.

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD  

LIST OF APPLICANTS SELECTED TO JOIN THE NATIONAL INSTITUTE OF TRANSPORT (NIT) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

To access the names of selected undergraduates click  HERE

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

SHAIRI: HEKO LIBERIA

Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

DEADMEN SPEAKS: A POEM

Image generated with OpenArt AI tool It has been longtime since I published my poems on this platform, today I'm humbly inviting you to our section of poems. As you enjoy reciting this creativity, please don't forget to leave your comment after this post or writing via my contacts after this poem. Poem: Deadmen Speaks Poet: Venance Gilbert Composition: July 30, 2023 DEADMEN SPEAKS: A POEM BY VENANCE GILBERT I heard deadmen tells no tale but these ones do They are burdened with a lots Weak folks who talks nothing just talking in mind in the streets I say so because one of them is me I speak for deadmen. Six years with no stable duties to perform while responsibilities have taken-off This week this job next week none and I have to survive regardless But how without money How can I count money without job? I speak for deadmen. While I'm enjoying my jobless survival Executive wants to collect from my pocket I have to pay tariff to buy light tariff to withdraw my hard-earned sav...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

NExT-GPT: MFUMO WA LUGHA WA AKILI BANDIA UNAOKUPA MAJIBU KWA MAANDISHI, PICHA, SAUTI NA PICHA MJONGEO

Picha hii imetengenezwa kwa Akili Bandia na Decrypt. Katika uwanda mpana wa teknolojia unaotawaliwa na makampuni makubwa kama OpenAI na Google, NExT-GPT ambao ni mfumo huria wa lugha pana ya Akili Bandia (AI) [Large Language M odel (LLM)] unaweza kuwa na kile kinachohitajika ili kushindana na miamba hii miwili katika teknolojia. ChatGPT imeusisimua ulimwengu kwa uwezo wake wa kuelewa maswali katika lugha asilia na kutoa majibu kama ya binadamu. Lakini wakati Akili Bandia inaendelea kusonga mbele kwa kasi ya umeme, watu wametaka kuwepo na maendeleo zaidi. Zama za maandishi pekee zimekwisha sasa mifumo ya lugha ya Akili Bandia imeanza kuwa mingi kuleta ushindani. NExT-GPT imetengenezwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha taifa cha Singapore (NUS) na Chuo Kikuu cha Tsinghua. Inaweza kuchakata na kutoa majibu kwa kuchanganya maandishi, picha, sauti na picha mjongeo (video). Hii inaruhusu majibizano ya asili zaidi kuliko miundo ya maandishi pekee kama ilivyo kwenye ChatGPT. T...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA

Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz . Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika. Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya  HAPA  ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya  HAPA  ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa: 1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3) SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno ku...