WATU saba wamekufa katika mikoa ya Njombe na Pwani katika ajali za gari na mtoto kutumbukia kwenye ndoo.Kutoka Njombe, mtoto wa mwaka mmoja, Pendo Mbena amekufa baada ya kutumbukia kwenye ndoo ya maji.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani alisema mtoto huyo alikufa juzi saa tatu asubuhi katika Kijiji cha Igoma wilayani Njombe.Akielezea tukio hilo, Ngonyani alisema Upendo alikufa baada ya kutumbukia kwenye ndoo iliyokuwa jikoni baada ya kuachwa na mama yake, Agness Mbena (28) aliyekwenda kuchota maji.Katika tukio lingine, Ngonyani alisema mtoto wa miaka mitatu, Kelvin Kyando, mkazi wa Mtalawe amekufa baada ya kugongwa na pikipiki.Alisema ajali hiyo ilitokea mtaa wa Posta, Njombe Mjini baada ya pikipiki yenye namba za usajili T 112 CLX aina ya Fekon, mali ya Kelvin Chaula (21) kumgonga mtembea kwa miguu, mwanafunzi, Anthon Bruno (12) aliyekuwa amembeba Kelvin.“Jeshi la Polisi linamshikilia dereva wa pikipiki. Chanzo cha ajali ni uzembe wa mwendesha pikipiki kwani hakuweza kuchukua tahadhari kwani aneo hili lilikuwa na watoto wengi waliokuwa karibu na barabara,” alisema.Mkoani Pwani, watu wanne wamekufa katika matukio mawili tofauti, wakiwemo watu watatu waliopoteza maisha kwa ajali ya gari.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei alisema ajali hiyo ilitokea saa tano usiku eneo la Vigwaza, wilayani Bagamoyo baada ya Fuso lenye namba za usajili T 775 CHX kugongana na lori lenye namba za usajili T 627 ANA/T 386 ACE.Alitaja waliopoteza maisha kuwa ni dereva Kalista Mwigeni (23), mkazi wa Ilula Iringa, Gerald Muhanga (umri wake kati ya miaka 23-25) utingo wa Fuso, na Deseselia Daudi (50) mkulima wa Morogoro aliyekuwa abiria kwenye lori.Waliojeruhiwa katika ajali hiyo ni Noah Msalu (40), mkazi wa Iringa aliyekuwa amekodisha Fuso na Alani Philipo (60), mkazi wa Kipawa jijini Dar es Salaam ambaye ni dereva wa lori Katika tukio lingine, Matei alisema siku ya Jumanne saa 12 asubuhi, Mgaza Mbulu (61) mkazi wa Kijiji cha Kibindu, alikutwa amejinyonga juu ya mti kwa kutumia kamba.Alisema mwili wa marehemu ambaye alikuwa akiishi kijijini hapo bila ndugu wa karibu, ulikabidhiwa kwa viongozi wa kijiji baada ya kufanyiwa uchunguzi na daktari. “Marehemu hakuacha ujumbe wowote wa kueleza sababu za kujitoa maisha na upelelezi unaendelea,” alisema.
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

Comments
Post a Comment