Basi la kampuni ya SASEBOSSA liliondoka Tabora stand saa 2 asubuhi tukiwa safarini saa sita na dakika 48 mchana basi lilisimama katika kituo cha Rungwa kwa masaa 4 baada ya kupata hitilafu, mafundi walijaribu kulitengeneza na walifanikisha saa kumi na moja na dakika 40 jioni ambapo basi lilianza kuondoka, majira ya saa 6 usiku gari lilipasuka exozi na kusababisha mafuta yote kumwagika chini hapo tulilazimika kusubiri kwa saa zima na nusu kusubiri konda alete mafuta kwa kurudi kituo cha nyuma, mpaka saa 7 na nusu usiku hapo tulikuwa katika mlima wa kuzunguka zunguka a.k.a NYOKA NYOKA kama wanavyouita wenyeji baada ya konda kuleta mafuta tulizunguka mlima huo na hatimaye kuuacha, gari likaendelea mpaka tulipofika Mbeya stand saa kumi usiku.
"NAMSHUKURU MUNGU KWA KUNIFANYA NIFIKE SALAMA BINAFSI LICHA YA KUPATA UGUMU WA SAFARI KAMA HIVYO NA ASANTENI WOTE MLIOSHIRIKIANA NA MIMI KWA NAMNA YOYOTE ILE TOKA MWANZO WA SAFARI #UKEREWE HADI #MBEYA KUPITIA #TABORA MUNGU AWABARIKI"
© #Venancetz
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...
Comments
Post a Comment