Abdel-Fattah al-Sisi ameapishwa kuwa rais mpya wa Misri katika seherehe iliyofanywa kwenye mahakama makuu ya katiba mjini Cairo.
Baada ya kaapishwa, Rais Sisi alikwenda ikulu kwa ajili ya sherehe iliyohudhuriwa na viongozi kutoka nchi kadha.
Kiongozi wa muda, Adly Mansour na Bwana al-Sisi walitia saini waraka wa kukabidhi madaraka kwake rais mpya - kwa mara ya kwanza katika historia ya Misri.
Rais mpya alisema hilo ni tukio la kihistoria.
Mkuu huyo wa zamani wa jeshi alishinda katika uchaguzi wa mwezi uliopita kwa asili-mia-97, ingawa upinzani ulisusia uchaguzi huo.
Wafuasi wa Rais al-Sisi walisherehekea katika medani ya Tahrir mjini Cairo.
Mfuasi mmoja wa al-Sisi, Fakhri Gamel Abdul Khaleq, alisema anatumai sherehe za leo ndio zitamaliza matatizo yaliyopita:
"nampongeza Bwana rais anapoapishwa leo.
Mungu ajaalie uwe mwaka wa furaha kwetu na kwa Wamisri wote.
Na tunaomba Mungu atunusuru na yale yaliyotokea kabla, na tutakuwa watu wema.
Mungu akipenda, kama alivosema rais, tutakuwa mfano mzuri wa ustaarabu".
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...
Comments
Post a Comment