RAIS MTEULE WA MISRI EL-SISI AAPISHWA NA KUKABIDHIWA MADARAKA

Abdel-Fattah al-Sisi ameapishwa kuwa rais mpya wa Misri katika seherehe iliyofanywa kwenye mahakama makuu ya katiba mjini Cairo. Baada ya kaapishwa, Rais Sisi alikwenda ikulu kwa ajili ya sherehe iliyohudhuriwa na viongozi kutoka nchi kadha. Kiongozi wa muda, Adly Mansour na Bwana al-Sisi walitia saini waraka wa kukabidhi madaraka kwake rais mpya - kwa mara ya kwanza katika historia ya Misri. Rais mpya alisema hilo ni tukio la kihistoria. Mkuu huyo wa zamani wa jeshi alishinda katika uchaguzi wa mwezi uliopita kwa asili-mia-97, ingawa upinzani ulisusia uchaguzi huo. Wafuasi wa Rais al-Sisi walisherehekea katika medani ya Tahrir mjini Cairo. Mfuasi mmoja wa al-Sisi, Fakhri Gamel Abdul Khaleq, alisema anatumai sherehe za leo ndio zitamaliza matatizo yaliyopita: "nampongeza Bwana rais anapoapishwa leo. Mungu ajaalie uwe mwaka wa furaha kwetu na kwa Wamisri wote. Na tunaomba Mungu atunusuru na yale yaliyotokea kabla, na tutakuwa watu wema. Mungu akipenda, kama alivosema rais, tutakuwa mfano mzuri wa ustaarabu".

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI