1. A successful man is one who makes more money than his wife can spend. A successful woman is one who can find such a man. -
Lana Turner
2. Any girl can be glamorous. All you have to do is stand still and look stupid. -
Hedy Lamarr
3. Always remember that you are absolutely unique. Just like everyone else. -
Margaret Mead
4. If the facts don't fit the theory, change the facts.
Albert Einstein
5. Behind every great man is a woman rolling her eyes. -
Jim Carrey
6. My fake plants died because I did not pretend to water them. -
Mitch Hedberg
7. A woman's mind is cleaner than a man's: She changes it more often. -
Oliver Herford
8. Do not take life too seriously. You will never get out of it alive. -
Elbert Hubbard
9. I always wanted to be somebody, but now I realize I should have been more specific. -
Lily Tomlin
10. As a child my family's menu consisted of two choices: take it or leave it. -
Buddy Hackett
1. A successful man is one who makes more money than his wife can spend. A successful woman is one who can find such a man. -
Lana Turner
2. Any girl can be glamorous. All you have to do is stand still and look stupid. -
Hedy Lamarr
3. Always remember that you are absolutely unique. Just like everyone else. -
Margaret Mead
4. If the facts don't fit the theory, change the facts.
Albert Einstein
5. Behind every great man is a woman rolling her eyes. -
Jim Carrey
6. My fake plants died because I did not pretend to water them. -
Mitch Hedberg
7. A woman's mind is cleaner than a man's: She changes it more often. -
Oliver Herford
8. Do not take life too seriously. You will never get out of it alive. -
Elbert Hubbard
9. I always wanted to be somebody, but now I realize I should have been more specific. -
Lily Tomlin
10. As a child my family's menu consisted of two choices: take it or leave it. -
Buddy Hackett
KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: MADEREVA WA UMMA WAGOMA NA KUANDAMANA BRAZIL
Maafisa wa polisi nchini Brazil wametumia gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji katika siku ya pili ya mgomo wa wafanyikazi wa sekta ya uchukuzi ambao umesababisha uhaba mkubwa wa usafiri wa uma katika mji wa Sao Paulo.
Takriban nusu ya vituo vya treni vilifungwa na kusababisha msongamano mkubwa wa watu katika barabara za mji huo mkubwa ambao unatarajiwa kuandaa michuano ya kombe la dunia kuanzia alhamisi ijayo.
Wafanyakazi hao wa treni wanataka mishahara yao kuongezwa kwa asilimia kumi.
Awamu nyingine ya majadiliano imefeli na wafanyikazi hao wanasema kuwa mgomo huo utaendelea kwa mda usiojulikana.
QUOTES OF THE DAY JUNE 6, 2014
1. Wisdom, compassion, and courage are the three universally recognized moral qualities of men. -
Confucius
2. Imagination is more important than knowledge. -
Albert Einstein
3. Honesty is the first chapter in the book of wisdom. -
Thomas Jefferson
4. A man must be big enough to admit his mistakes, smart enough to profit from them, and strong enough to correct them. -
John C. Maxwell
5. A good head and a good heart are always a formidable combination. -
Nelson Mandela
6. The only true wisdom is in knowing you know nothing. -
Socrates
7. Experience is not what happens to you; it's what you do with what happens to you. -
Aldous Huxley
8. By three methods we may learn wisdom: First, by reflection, which is noblest; Second, by imitation, which is easiest; and third by experience, which is the bitterest. -
Confucius
9. Discipline is the bridge between goals and accomplishment. -
Jim Rohn
10. For beautiful eyes, look for the good in others; for beautiful lips, speak only words of kindness; and for poise, walk with the knowledge that you are never alone. -
Audrey Hepburn
KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: FIFA YATANGAZA IMANI KUHUSU MICHUANO HIYO BRAZIL
Rais wa shirikisho la soka duniani Fifa amesema kuwa ana imani kuwa kombe la dunia nchini Brazil litakuwa na ufanisi mkubwa.
Bwana Sepp Blatter ametoa wito kwa raia wa Brazil wajitolee vilivyo kusaidia kufanikisha mchezo huo mwaka huu.
Matamshi ya Bwana Blatter yamekuja huku hofu ikielezewa mjini Sao Paulo juu ya msongamano mkubwa wa watu na magari kufuatia mgomo wa wafanyakazi wa shirika la reli.
Maafisa wakuu wa Fifa wenyewe walikwama katika foleni ndefu ya magari barabarani.
Usafiri huo unatarajiwa kutatizika zaidi kufuatia kuvunjika kwa mazungumzo kati ya muungano wa wafanyikazi hao na serikali.
Orodha kamilifu ya timu zitakazoshiriki michuano ya Kombe la Dunia imetolewa. Majina ya makocha 32 ambao watasimamia mechi za mashindano hayo, pia majina ya wachezaji 736 watakaoshiriki mechi hizo zitakazochezwa kati ya Juni 12 hadi Julai 13 zimetangazwa..
Taarifa zaidi iliyotolewa ni kuwa timu zimepunguza idadi ya wachezaji, majeraha kukaguliwa na hali ya afya ya wachezaji kutathminiwa. Haya yote yakiwa ni matayarisho kwa michuano hayo yatakayo anza jijini Sao Paulo.
Timu zote zimetayarisha wachezaji 23 ambao kwa sasa watazingatia uwezo wa kufanikisha timu zao.
WAHUBIRI INJILI WAGEUKA KUWA WASHAMBULIAJI NIGERIA
Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Boko Haram, wameshambulia wanakijiji karibu na mji wa Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa Nigeria na kuwaua watu 45.
Walioponea kifo waliambia BBC kwamba washambuliaji hao walijidai kuwa walikuwa wamekuja kuwahubiria wanakijiji kabla ya kuanza kuwafyatulia risasi kiholea.
Wakati huohuo,wakazi pamoja na maafisa wakuu wanasema kuwa watu 200 waliuawa katika mashambulizi tofauti mapema wiki hii.
Mji wa Maiduguri na vitongoji vyake, haujaathirika sana na mashambulizi tangu kutangazwa kwa sheria ya hali ya hatari mwaka mmoja uliopita.
Maeneo ya mashinani ndio sasa hulengwa kwa mashambulizi
Serikali ya Nigeria imekuwa ikikabiliwa na shinikizo ndani ya nchi na kimataifa kuongeza juhudi za kukabiliana na kundi la Boko Haram tangu liwateke nyara wasichana zaidi ya miambili wa shule mwezi Aprili.
Kundi hilo limekuwa likiendesha harakati zake tangu mwaka 2009 katika juhudi za kudai uongozi wa kiisilamu.
Maelfu ya watu wameuawa katika mashambulizi mbali mbali ikiwemo maafisa wa usalama.
'Wanakijiji wahadaiwa'
Washambuliaji waliingia katika kijiji cha Barderi, karibu na chuo kikuu cha Maiduguri viungani mwa mji wa Maiduguri, wakiwaambia watu kuwa walikuwa wamekuja kuwahubiria, lakini baadaye wakaanza kuwashambulia kwa bunduki.
Wapiganaji hao wamewahi kutumia mbinu kama hizi za kijanja kuwahadaa wanakijiji na baadaye kuwashambulia.
QUOTES OF THE DAY JUNE 5, 2014
1. Success is not final, failure is not fatal: it is the courage to continue that counts. -
Winston Churchill
2. Coming together is a beginning; keeping together is progress; working together is success. -
Henry Ford
3. Success consists of going from failure to failure without loss of enthusiasm. -
Winston Churchill
4. In order to succeed, your desire for success should be greater than your fear of failure. -
Bill Cosby
5. The price of success is hard work, dedication to the job at hand, and the determination that whether we win or lose, we have applied the best of ourselves to the task at hand. -
Vince Lombardi
6. Always be yourself, express yourself, have faith in yourself, do not go out and look for a successful personality and duplicate it. -
Bruce Lee
7. Try not to become a man of success, but rather try to become a man of value. -
Albert Einstein
8. Take up one idea. Make that one idea your life - think of it, dream of it, live on that idea. Let the brain, muscles, nerves, every part of your body, be full of that idea, and just leave every other idea alone. This is the way to success. -
Swami Vivekananda
9. I've failed over and over and over again in my life and that is why I succeed. -
Michael Jordan
10. I don't measure a man's success by how high he climbs but how high he bounces when he hits bottom. -
George S. Patton.
MUME WA FROLA MBASHA ASEMA NI VIGUMU SANA NDOA YAO KUFIKIA MUAFAKA TENA
BAADA ya kudumu kwa zaidi ya miaka 10, imebainika kuwa ndoa ya mwanamuziki mahiri wa muziki wa Injili Bongo, Flora na mumewe Emmanuel Mbasha ipo chali kwa maana ya kuanguka huku ikidaiwa kuwa, kusimama imara tena inawezekana lakini ni kazi kubwa, Amani limefukunyua mazito
Hilo limejitokeza wiki moja baada ya madai ya mwanaume huyo kudaiwa kumbaka shemeji yake na kesi ipo polisi.
Imeelezwa Flora na mumewe ambao walifunga ndoa Agosti 22, 2002 wamepita katika migogoro mizito lakini wawili hao walikuwa wakiyamaliza kifamilia hadi kufikia hili la hivi karibuni ndilo lililoziba mataumaini ya wawili hao kuishi kama mume na mke.
Chanzo kilicho karibu na wawili hao kimeeleza kuwa, mzizi wa wawili hao kugombana ulichochewa na mwanamke mmoja (jina tunalo) ambaye alikuwa akikinzana na ushauri wa Mbasha mara kwa mara.
“Kuna vitu Mbasha alikuwa akimshauri huyo mama lakini walikuwa wakipishana Kiswahili na hapo ndipo tatizo lilipokua hadi kufikia hatua ya kumwagana,” kilisema chanzo.
TUJIUNGE NA MBASHA
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Emmanuel alizungumza na mwandishi wetu ambapo alikiri ndoa yake haina uhai tena na si rahisi kurejea katika hali ya kawaida licha ya kudai kuwa bado anampenda mkewe.
“Tulikuwa tunagombana sana na Flora lakini tulikuwa tukipatana ila mama… (anamtaja jina) alichangia ugomvi,
Flora naye alikuwa na nyendo zake mbaya, kuna wakati alikuwa anatoka kwenda gym (sehemu ya mazoezi) anachelewa kurudi ikafika wakati na nguvu ya ndugu wa mke ikawa kubwa kiasi cha kunizidi mimi na hapo ndipo mambo yalipofikia pabaya kabisa.”
FLORA ATIMKA NYUMBANI
Mbasha anaendelea: “Ugomvi ulizidi, ilifika wakati tulipishana kiasi cha yeye kuondoka nyumbani na kwenda kuishi katika nyumba ya wageni kwa miezi kadhaa wakati huo.
“Ndani ya ugomvi huo nilisikia mengi, baadhi ya watu wananiambia mke wangu anaonekana na Prado na mwanaume mwingine mwenye pesa, iliniuma sana ingawa sijawahi kumuona moja kwa moja,” alisema Emmanuel.
Kuhusu ugomvi huo, hivi karibuni Flora alikaririwa katika vyombo vya habari akisema hana tatizo na mumewe na ameshasamehe na kusahau yote yaliyopita hivyo ajitokeze tu ili akajibu mashitaka ya kudaiwa kubaka binti wa miaka 17 yaliyofunguliwa.
“Mimi sina tatizo kabisa na mume wangu, nimeshasamehe yote yaliyopita, kuhusu mashitaka ningeweza kuyafuta kama ningekuwa mimi ndiye niliyemshitaki,” alisema Flora.
FLORA ADAIWA KUHAMIA KWA GWAJIMA
Wakati gazeti hili likiendelea kusaka undani juu ya sakata hili, kuna chanzo kingine kilipenyeza data kuwa baada ya ugomvi kuwa mzito, Flora alihamia kwa Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Dar, Josephat Gwajima ambako ndiko alikuwa akisali kila Jumapili.
“Kwani nyinyi Global hamna habari? Flora amehamia kwa Gwajima Jumapili iliyopita, kwanza alihudhuria ibada jioni akaenda kuishi maana Gwajima ni mchungaji wake kwa sasa,” kilisema chanzo.
GWAJIMA ACHOMOA
Ili kupata mizani ya madai hayo, juzi Amani lilimpigia simu Mchungaji Gwajima na kumuuliza kama kweli Flora amehamia kwake kufuatia ugomvi kati yake na mumewe ambapo alikataa katakata.
“Flora hayupo hapa…mnataka niwaambiwe yuko hapa halafu vyombo vya habari muanze kuandika vibaya? Hakuna kitu kama hicho,” alisema Gwajima.
KWA NINI CHALI?
Ndoa kuwa chali ni ile ambayo imeanguka lakini inaweza kusimama tena tofauti na ndoa kuvunjika. Global iliwahi kuandika NDOA YA THEA CHALI baadaye ikasimama tena. Thea ni msanii wa filamu alifunga ndoa na Michael Sangu ‘Mike’ ambaye pia ni mwigizaji.
Wakati Emmanuel akizungumza na mwandishi wetu, alikiri kuwa Flora ameshamgeuka na nguvu kubwa imemuingia ndani ya moyo wake hivyo kuna ugumu sana wa kurudiana.
“Flora ambaye nilitegemea awe msaada katika hili lakini amefikia steji ya kuacha kunisikiliza, anasema haniamini, kwamba ninaweza kumfanyia lolote, sasa si bora kama anataka tuachane kwa heri kuliko kuniundia zengwe ambalo linataka kunipeleka mimi jela?” alihoji Mbasha.
Kutokana na mvutano huo pamoja na kesi hiyo ya kudaiwa kubaka inayomwandana Mbasha ni dhahiri kwamba kila mmoja hana imani na mwenzake tena hivyo suala la wawili hao kuishi kama zamani linakuwa gumu kuliko ngamia kupenya kwenye tundu la sindano.
Emmanuel Mbasha alishitakiwa katika Kituo cha Polisi cha Tabata Shule, Mei 30, mwaka huu kwa madai ya kumbaka shemejie.Uchunguzi juu ya tukio hilo unaendelea hadi sasa shitaka ambalo mwenyewe amelikanusha.
Canzo: GPL
KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: ENGLAND YATOKA SARE NA ECUADOR 2-2
Katika mechi za kirafiki kwa maandalizi ya michuano ya kombe la dunia, England ilitoka sare ya 2 - 2, dhidi ya Ecuador katika mechi iliyochezwa huko Miami.
Timu ya England iliongozwa na Frank Lampard.
Raheem Sterling ambaye huchezea klabu ya Liverpool, alibanduliwa uwanjani kwa kadi nyekundu katika dakika ya 11 baada ya mtafaruku kati yake na Antonio Valencia ambaye huchezea klabu ya Machester United. Sterling amepigwa marufuku kushiriki mechi ya kirafiki itakayofuata.
Ecuador iliikanda kanda England na kutumia fursa ya ulinzi mbovu huku ambapo Enner Valencia aliwaongoza kushambulia awali lakini Wayne Rooney akapata fursa ya kupenyeza bao lake la 39 kufaidi England kabla ya kwenda mapumziko.
Sasa England itabidi kujipiga msasa wakijiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Honduras siku ya Jumamozi kabl aya kusafiri kwenda Brazil kuanza ngoma ya kupigania kombe la dunia.
RAIS MTEULE WA MISRI KUAPISHWA JUMAPILI
Abdel Fatah al-Sisi ambaye amempinduwa kiongozi wa kwanza aliechaguliwa kwa njia ya demokrasia nchini Misri ataapishwa kuwa rais wa nchi hiyo Jumapili baada ya kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa rais wiki iliopita.
Tume ya uchaguzi hapo juzi imesema Sisi alishinda kwa asilimia 96.91 ya kura sawa na asilimia 47.5, ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kumpinduwa Mohamed Mursi wa itikadi kali za Kiislamu.
Ushindi wake huo mkubwa dhidi ya mpinzani pekee kiongozi wa sera za mrengo wa shoto Hamdeen Sabahi ulikuwa haukutiliwa mashaka kabisa kutokana na kupongezwa na watu wengi kwa jemedari huyo mkuu mstaafu kukomesha utawala wa mwaka mmoja wa Mursi uliowagawa wananchi miezi kumi na moja iliopita.
Sisi ataapishwa saa moja na nusu asubuhi hapo Jumapili katika baraza kuu la Mahakama Kuu ya Kikatiba.Sherehe za kuapishwa kwake zitahudhuriwa na rais wa kipindi cha mpito Adly Mansour, Waziri Mkuu Ibrahim Mahlab na baraza lake la mawaziri,Imamu Mkuu Ahmed al- Tayeb wa Taasisi kuu ya Kiislamu nchini humo Al Azhar,Papa wa Kanisa la Koptik Tawadros wa Pili na viongozi wengine wa kisiasa na wa serikali.
Sherehe hizo zitafuatiwa na tafrija itakayohudhuriwa na wafalme na wakuu wa nchi katika Kasri la Ittihadiya mjini Cairo.
Wananchi watekeleze wajibu wao
Rais wa mpito anayeondoka madarakani amesema wananchi lazima wasimame kutekeleza wajibu wao kutokana na changamoto kubwa zinazoikabili nchi hiyo ambayo imetibuliwa na ghasia za umwagaji damu, machafuko ya kisiasa na njama za kimataifa zenye kutishia utambulisho wake na heshima ya mamlaka ya dola.
Katika hotuba yake ya kuaga aliyoitowa leo hii Adly Mansour mara nyengine akionekana karibu kutokwa na machozi,ameorodhesha matatizo yanayoikabili Misri wakati alipochukuwa madaraka karibu mwaka mmoja uliopita.Amesema hivi sasa nchi hiyo iko katika hali nzuri baada ya kupitishwa kwa katiba na sasa kufanyika kwa uchaguzi ambapo mkuu wa majeshi wa zamani al-Sisi ameshinda.
Hotuba yake hiyo inalingana na ilani ya kampeni ya Sisi kwamba Wamisri lazima wakomeshe machafuko nchini humo na kuwezesha ujenzi mpya wa taifa hilo.
Changamoto ni nzito
Hapo jana Sisi alijaribu kupunguza wasi wasi ulioko nchini humo wakati aliporudia kauli mbiu ya uasi wa mwaka 2011 akiwataka wananchi wa Misri kufanya kazi kwa ajili ya kujipatia mkate,uhuru,utu wa binaadamu na haki ya kijamii.
Mashrika ya haki za binaadamu ,viongozi wa kimataifa na wataalamu wameonya kwamba changamoto nzito zinamkabili Sisi wakati akiongoza nchi hiyo iliogawika vibaya.
Marekani imesema inasubiri kwa hamu kushirikiana na Sisi lakini pia imeelezea wasi wasi wake juu ya mazingira ya kisiasa yenye vikwazo ambapo kwayo uchaguzi wa wiki uliopita ulifanyika.
Uchaguzi huo wa Mei 26 hadi 28 ulisusiwa na kundi la Mursi la Udugu wa Kiislamu na makundi ya vijana ya vuguvugu la uasi wa umma wa mwaka 2011 kutokana na ukandamizaji wa sauti za upinzani unaoendelea nchini humo.
KESI YA UMILIKI WA NYIMBO ZA BOB MARLEY YAMALIZIKA
Mzozo wa kisheria juu ya nani anayemiliki baadhi ya nyimbo maarufu za reggae duniani umemalizika mjini London.
Nyimbo hizo zilizotungwa na kuimbwa na msanii Bob Marley zimekuwa ziking'ang'aniwa na kampuni 2 pinzani juu ya umiliki wao.
Jaji katika mahakama kuu, Richard Meade alikata kesi ambapo kampuni ya Cayman Music ilikuwa inadai kumiliki nyimbo 13, miongoni mwao wimbo uliopata umaarufu 'No Woman, No Cry' kuwa haina haki nazo tena.
Kampuni hiyo ilikuwa imedai kuwa nyimbo hizo hazikujumuishwa walipouza baadhi ya haki zake kwa kampuni nyingine mnamo mwaka wa 1992.
Kampuni ya Cayman imesema kuwa Bob Marley aliandika nyimbo hizo chini ya majina tofauti, lakini Jaji ameamua kuwa bado kandarasi waliouzia inafunika nyimbo zote hizo.
Bob Marley alifariki mwaka wa 1981 baada ya kuugua maradhi ya saratani kwa muda.
DICAPRIO' JACK WA TITANIC' NA PARIS HILTON WASUSIA KUONEKANA KATIKA KIPINDI CHA KIM KADARSHIAN
Muigizaji maarufu nchini Marekani, Leonard DiCaprio au maarufu kama 'Jack' aliyeigiza katika muvi ya Titanic, amekata kurekodiwa na kipindi cha Kim Kadarshian 'Keeping Up With the Kadarshians' walipokuwa katika pati ya majira ya joto Jumapil mchana.
"Leo hakutaka kurekodiwa kwa ajili ya kipindi cha Kim na hakuwasili mpaka pale shughuli za kurekodi zilipokwisha" alisema mpasha habari mmoja.
Pia, Paris Hilton ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa Kim, naye hakupenda kuonekana katika kipindi hicho ambaye naye ameanzisha fani yake kama DJ.
KOCHA NOOIJ ASEMA HATOPANGUA KIKOSI CHA TAIFA STARS
KOCHA mkuu wa timu ya soka ya taifa ‘Taifa Stars’, Mholanzi Mart Nooij amesema kamwe hatakifanyia marekebisho kikosi chake kilichotinga raundi ya pili ya kuwania kushiriki fainali za Mataifa Afrika kwa kuifunga Zimbabwe jumla ya mabao 3-2.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salam, Stars ilipata ushindi wa bao 1-0 kabla ya kutoka sare ya 2-2 na wenyeji wao Zimbabwe Jumapili iliyopita Jijini Harare na kukata tiketi ya kucheza raundi hiyo ya pili na sasa itakutana na Msumbiji Julai 18.
Akizungumza baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Harare juzi usiku, kocha huyo alisema: “Mechi na Zimbabwe ilikuwa nzuri na ngumu kwetu, lakini nawapongeza vijana wangu walicheza kwa kujituma na kupata matokeo ambayo yametupeleka hatua nyingine, tuna muda mrefu kabla ya kucheza mechi inayofuata nitatumia muda huu kukirekebisha kikosi changu lakini siwezi kukibadilisha,” alisema Nooij.
Akiuzungumzia mchezo wao unaofuata dhidi ya Msumbiji aliyowahi kuifundisha siku za nyuma, Nooij alisema ni timu ngumu yenye wachezaji wengi wanaocheza soka la kulipwa Ulaya na Afrika, lakini anayajua vyema mapungufu yao na atayatumia ili kuweza kuiondosha kwenye kinyang’anyiro hicho kama ilivyokuwa kwa Zimbabwe.
“Hakuna asiyejua kama Msumbiji ni timu nzuri ina wachezaji wengi wenye uzoefu kutokana na kucheza soka Ulaya na wengine kwenye klabu kubwa Afrika, lakini hilo halinipi wasiwasi kwa sababu nawajua vyema wapinzani wetu na Watanzania watarajia kupata matokeo mazuri,” alisema Nooij.
Nooij alisema kitu kikubwa ambacho angependa kulishauri Shirikisho la soka Tanzania (TFF) ni kuiandaa timu mapema, ikiwa ni pamoja na kupata mechi za kirafiki za kimataifa ambazo zitawasaidia kujua mapungufu na uwezo waliokuwa nao kabla ya kuwavaa Msumbiji.
“Itafurahisha kuanza maandalizi mapema kwa sababu tutapumzika muda mrefu na kwa vile hakuna ligi kwa sasa, lengo ni kutaka kujifunza zaidi uwanjani na kupata mechi za majaribio ambazo zitarudisha ari ya vijana wangu kabla ya kumenyana na Msumbiji,” alisema Nooij.
Nooij, kocha mwenye uzoefu mkubwa na soka la Afrika, alianza kuifundisha Stars miezi mitatu iliyopita akichukua nafasi ya Kim Poulsen, siku za nyuma kuanzia mwaka 2007 hadi Septemba 2011 alikuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Msumbiji na kuiongoza kwenye michuano ya Mataifa Afrika yaliyofanyika Angola na timu hiyo kumaliza ya mwisho kwenye kundi lake baada ya kufungwa michezo miwili na kutoka sare mchezo mmoja.
KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: BLATTER AWASILI BRAZIL NA KUKUTANA NA RAIS WA NCHI HIYO, DILMA ROUSSEFF
Rais wa FIFA, Joseph S. Blatter amekutana na Rais wa Brazil, Dilma Rousseff huko Palacio do Planalto, Brasilia. Kwa msisimko wa kihistoria wa kombe hilo ambalo litatolewa kwa bibngwa wa dunia, kombe hilo limetolewa na Blatter na Cafu aliyekuwa nahodha wakati Brazil ilipotwaa kombe hilo mwaka 2002.
"Nilishasema kabla ya kuja Brazil, kwa mara ya kwanza itakuwa ni kuonana na Rais wa nchi hii. Hii yote ni kwa heshima na taadhima" alisema Blatter kabla ya kuanza kwa sherehe ambapo Rais Rousseff aliinua juu kombe la dunia ambalo huguswa na Marais na mabingwa pekee.
"Ni matumaini yangu na Wabrazil wenzangu zaidi ya milion 200, wanategemea hapo tarehe 13 Julai zaidi ya watu 23 wataweza kuligusa kombe hili" alisema Rousseff.Siku 10 kabla ya michuano kuanza.
Rais Dilma alishaitisha mkutano huko Brazil na wakuu wa majimbo kujadili juu ya mechi ya maandalizi ya ufunguzi kati ya Brazil na Croatia huko Palacio do Planato katika dimba la Arena de Sao Paulo. Baada ya sherehe za ufunguzi Blatter na Rais Dilma walihudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo pia alikuwepo Waziri wa Michezo wa Brazil, Aldo Rebelo.
Mwishoni mwa mwezi Januari Rais Blatter aliwkaribisha wakuu wa majimbo ya Brazil makao makuu ya FIFA huko Zurich."Ni matumaini yangu kwa zadi ya mwezi mmoja macho yote yataelekezwa Brazil katika kombe la dunia" alisema Blatter
QUOTES OF THE DAY JUNE 1, 2014
Education is what survives when what has been learned has been forgotten. -
B. F. Skinner
Love Quote of the Day:
I love you the more in that I believe you had liked me for my own sake and for nothing else.
-John Keats
Art Quote of the Day:
Every child is an artist. The problem is how to remain an artist once we grow up.
-Pablo Picasso
Nature Quote of the Day:
If the skies fall, one may hope to catch larks.
-Francois Rabelais
Funny Quote of the Day:
Only two things are infinite, the universe and human stupidity, and I'm not sure about the former.
-Albert Einstein
ASILILIA 25 YA WALIMU HUFUNDISHA MAMBO YASIYO YA MSINGI
Wakati Serikali ikiahidi kuboresha elimu nchini kwa kuhakikisha inaajiri walimu wa kutosha, imebainika kuwa asilimia 25 ya walimu huwafundisha wanafunzi mambo yasiyo ya msingi.
Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco), iliyozinduliwa Dar es Salaam hivi karibuni, imebainisha kuwa wakati wananchi wakilalamika kuwa elimu inayotolewa haimsaidii mwanafunzi kupata ajira nzuri, wanafunzi hawajifunzi mambo ya msingi yatakayowasaidia kupambana na changamoto za maisha.
Akizindua ripoti hiyo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa ripoti hiyo imeweka wazi ukubwa wa tatizo la ufundishaji, akieleza kwamba jumla ya watoto milioni 250, duniani wanakosa mafunzo ya msingi ya kusoma, kuandika na kuhesabu, ingawa wanaingia darasani.
“Tanzania kama sehemu ya dunia, haijakwepa tatizo hilo. Baadhi ya watoto wetu wamekuwa wakimaliza shule za misingi bila ya kuwa na ujuzi huo. Hii ni hali ya kushtua, inayohitaji nguvu za pamoja za wadau wote wa elimu duniani,” alisema Kawambwa.
Alibainisha kwamba ripoti hiyo imependekeza mpango wa elimu mwaka 2015, uzingatie ubora utakaotokana na mipango sahihi inayotekelezeka akitaka tatizo la walimu lipatiwe ufumbuzi wa kudumu kwa lazima ili kuwanusuru wanafunzi.
“Kama suala la walimu halitapatiwa ufumbuzi sasa, tofauti kwenye ufundishaji itakuwepo kwa vizazi vingi huku ikitoa tafsiri mbaya dhidi ya jitihada za kuondoa umaskini duniani na kufikiwa kwa maendeleo endelevu,” alisema Dk Kawambwa.
Aliongeza kuwa kwa namna hali ilivyo sasa, Serikali inalazimika kuhakikisha inaajiri walimu wenye dhamira ya kweli ya kufundisha na kutoa elimu bora.
Ripoti ya Unesco inaeleza kuwa licha ya kuwepo kwa mafanikio ya kuridhisha katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, wananchi masikini ndiyo walioathirika zaidi na tatizo la utoaji elimu mbaya sababu ikiwa kutokuwepo kwa walimu wenye mafunzo ya kutosha.
Unesco ilisema kuwa kutokana na matatizo ya walimu, wanafunzi 130 milioni wanaosoma shule za msingi duniani, hawana uwezo wa kusoma hata sentensi moja, jambo linalowafanya washindwe kujiunga na sekondari.
“Matatizo ya elimu siyo tu yanaathiri malengo ya watoto ya baadaye, lakini pia uchumi wa Serikali hizo. Gharama ya watoto 250 milioni kutosoma elimu ya msingi ni Dola 129 bilioni za Marekani,(Sh 212.85 bilioni), ambayo ni asilimia kumi ya matumizi ya dunia katika elimu,” inasema ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imelinukuu shirikali lisilo la Serikali la Uwezo, linaloeleza kuwa asilimia 26 ya wanafunzi wa darasa la tatu ndiyo wanaoweza kusoma vizuri hadithi ya Kiswahili ya darasa la pili.