WATU 10 WAMEKUFA KATIKA AJALI YA MOTO KIWANDANI HUKO BANGLADESH

Takribani watu 10 wamekufa katika mlipuko mkubwa wa moto huko Bangladesh kufuatia kulipuka kwa kontena la kuchemshia maji ya moto.

 Polisi wamesema kuwa takribani watu 100 walikuwa ndani ya kiwanda hicho chenye jengo la ghorofa 4 ambapo mlipuko ulisikika katika mji wa Tongi.

Takribani watu 30 wamejeruhiwa  kutokana na moto huo kusambaa kwa haraka katika jengo hilo.

Huduma za dharura zinadai kuwa moto bado unaendelea kuwaka na inasemekana idadi ya watu kufariki katika ajali hiyo inaweza kuongezeka.

"Mpaka sasa tumepata uhakika wa watu 10 kufariki. Lakini bado idadi inaweza kuongezeka kwa sababu moto bado ni mkali kushindwa kuzimwa." Inspekta wa Polisi Sirajul Islam aliiambia AFP.

Kumekuwa na majanga mengi ya moto viwandani nchini Bangladesh kufuatia kutokuwa na usalama wa kuzuia majanga hayo katika nchi hiyo.


Canzo: BBC

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

DIAMOND AISIFIA NGOZI YA WEMA ASEMA INA MVUTO NA INANG'ARA KULIKO KITU CHOCHOTE

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA