TCU IMERUHUSU UDAHILI VYUO VIKUU AWAMU YA PILI

Tume ya Vyuo Vikuu nchini Tanzania (TCU) imeruhusu awamu ya pili ya udahili kwa wanafunzi waliokosa vyuo kwa kukosa sifa katika udahili wa awamu ya kwanza na wale ambao hawakuomba kudahiliwa kabisa.

Aidha TCU inakumbusha kwamba wale waliokwisha omba na hawakupangiwa kwa kukosa sifa stahiki za vyuo walivyopangiwa hawatatakiwa kulipia tena.

Pia wadahiliwa wapya wanatakiwa kulipia kiasi cha fedha za kitanzania Tsh. Elfu Hamsini (50,000/=) kama gharama za udahili. Fedha hii huwa hairudishwi.

Vilevile TCU inakumbusha kwamba kozi ambazo zimejaa tayari hazitaonekana kwenye mfumo wa Udahili (CAS).

Aidha TCU inawakumbusha waombaji kuwa mwisho wa kutuma maombi ya udahili ni Septemba 23 na hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza kwa wale watakaoshindw kuomba vyuo katika muda huo ulioongezwa.


MAELEZO ZAIDI BOFYA HAPA

Comments

Popular Posts

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

VIFAA VYA KUWATAMBUA WENYE UGONJWA WA EBOLA VYAINGIZWA NCHINI

TAZAMA HAPA MAGOLI 10 BORA YA KOMBE LA DUNIA 2018