JENERALI AUAWA KATIKA MAPIGANO SUDAN KUSINI

Mapigano makali yamezuka nje ya mji mkuu wa Sudan Kusini wa Bor na Jenerali mmoja wa jeshi la Sudan Kusini ameuawa.Mwandishi wa BBC anasema vikosi vya serikali vinazidi kuelekea karibu na mji wa Bor ambapo kumekuwa na mapigano ya kutegeana baina ya majeshi ya serikali na vikosi vya waasi vinavyomtii aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar.Mwandishi wa BBC amesema pia ameshuhudia miili ya watu ikiwa chini na vifaru vikiwa vimelipuliwa vibaya pembezoni mwa barabara.Pande pinzani nchini humo zinataraji kuanza mazungumzo ya ana kwa ana mjini Adis Ababa kujaribu kumaliza wiki tatu za mapigano.Kiongozi wa ujumbe wa serikali ya Sudan kusini Nial Deng Nial amesema kuwa ni muhimu kwamba viongozi kuzungumzia kuhusu kusitishwa kwa vita.

Comments

Popular Posts

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI