JENERALI AUAWA KATIKA MAPIGANO SUDAN KUSINI

Mapigano makali yamezuka nje ya mji mkuu wa Sudan Kusini wa Bor na Jenerali mmoja wa jeshi la Sudan Kusini ameuawa.Mwandishi wa BBC anasema vikosi vya serikali vinazidi kuelekea karibu na mji wa Bor ambapo kumekuwa na mapigano ya kutegeana baina ya majeshi ya serikali na vikosi vya waasi vinavyomtii aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar.Mwandishi wa BBC amesema pia ameshuhudia miili ya watu ikiwa chini na vifaru vikiwa vimelipuliwa vibaya pembezoni mwa barabara.Pande pinzani nchini humo zinataraji kuanza mazungumzo ya ana kwa ana mjini Adis Ababa kujaribu kumaliza wiki tatu za mapigano.Kiongozi wa ujumbe wa serikali ya Sudan kusini Nial Deng Nial amesema kuwa ni muhimu kwamba viongozi kuzungumzia kuhusu kusitishwa kwa vita.

Comments

Popular Posts

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

MFAHAMU KARL MARX KWA UFUPI: DUNIA INAMKUMBUKA LEO

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018