MKAZI wa Kijiji cha Kakese-Mkwajuni, wilayani Mpanda, Shoma Salum (78) ameuawa kwa kuchinjwa kwa kile kinachodaiwa ni kutokana na imani za kishirikina.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema mauaji hayo yalifanyika Desemba 29 , mwaka jana saa 2:30.Alikutwa nyumbani kwake mwili ukiwa na majeraha makubwa sikioni na kichwani. Mwanamke huyo inadaiwa alikuwa mganga wa kienyeji na mfinyanzi maarufu wa vyungu.Kwa mujibu wa Kamanda, siku moja kabla ya tukio, akiwa kwenye shughuli hizo, jirani na nyumbani kwake, walifika vijana wawili waliotajwa ni Shigela Majinja (25) na Mhoja Shilinde (18). Inadaiwa vijana hao ambao ni wakazi wa kijijini hapo.Walifika kwa kwa mama huyo wakijifanya kuwa ni wateja wake, ambapo walikuwa wakiulizia bei ya vyungu. Pia, walimwomba awasaidie kuwapatia tiba ya kienyeji .“Ndipo vijana hao walipoanza kumhoji juu ya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutaka kujua mahali , alikokuwa akiishi na chumba alichokuwa akilala na alikuwa akilala na nani. Inadaiwa aliwajibu vijana hao kwa ufasaha bila kuwa na shaka nao huku mazungumzo hayo yakiwa yanasikilizwa kwa siri na Tausi Mlitoni, ambaye naye alikuwa karibu na eneo hilo ,” alisema Kamanda.Kwa mujibu wa Kamanda, Desemba 29 saa 2:30 asubuhi mke wa Lameck Mboka, aitwaye Zamda Militone, baada ya kuona mama mkwe amechelewa kuamka, alienda na kujaribu kufungua mlango wa chumba chake.Lakini, alibaini kuwa kilikuwa kimefungwa kwa nje. Kidavashari alisema Zamda alipofungua mlango huo wa chumba cha mama mkwe wake na kuingia ndani , alimkuta mama akiwa ameuawa.Kamanda alisema watu watatu wanashikiliwa kwa mahojiano, nao ni Majija, Shilinde na Masanja Ngasa (31), wote wakazi wa kijijini hapo. Watuhumiwa wengine wanne wanaendelea kusakwa baada ya kukimbia kusikojulikana.
Chanzo: Habari Leo
Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

Comments
Post a Comment