Skip to main content

WAZIRI MGIMWA AFARIKI

RAIS Jakaya Kikwete amepokea kwa mshituko na huzuni kubwa taarifa za kifo cha Waziri wa Fedha, William Mgimwa, aliyekuwa pia Mbunge wa Kalenga kupitia CCM.

Rais katika taarifa ya Ikulu jana, alisema Taifa limepoteza Waziri huyo katika kipindi lilipokuwa linamhitaji zaidi kutokana na mchango wake mkubwa, ambao amekuwa akiutoa kupitia nafasi zake za Waziri wa Serikali na mwakilishi wa wananchi wa Kalenga. Kifo cha Mgimwa kilitangazwa jana na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue kwa niaba ya Serikali. Katika tangazo lake, Balozi Sefue alisema Waziri Mgimwa aliaga dunia jana saa 5.20 (Saa za Afrika ya Kati) katika Hospitali ya Kloof Medi- Clinic, Pretoria, Afrika Kusini ambako alilazwa kwa muda kidogo.

Balozi Sefue alisema maandalizi ya kurudisha nyumbani mwili wa marehemu yanafanywa na Serikali kwa kushirikiana na familia yake na taarifa zaidi zitatolewa baadaye kwa kadri zinavyopatikana na maandalizi yanavyoendelea. Katika salamu zake kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na familia ya Mgimwa, Rais Kikwete alisema: “Sina maneno ya kutosha kuelezea mshituko na huzuni yangu kubwa kutokana na taarifa za kifo cha Mgimwa.

“Binafsi nilimtembelea mara mbili hospitalini alikokuwa amelazwa na mara ya mwisho hali yake ilikuwa imeimarika. Tulizungumza kwa kiasi cha dakika 10 hivi akanielezea nia na tamaa yake ya kurejea nyumbani kwa sababu hali yake ilikuwa nzuri.”Rais Kikwete aliongeza: “Sote tunajua mchango wake katika Serikali. Sote tulitamani kuendelea kuwa naye, lakini haya ni mapenzi ya Mungu. “Napenda kutoa pole nyingi na rambirambi zangu za dhati kwa wanafamilia wote kwa kuondokewa na mhimili wao. Naungana nanyi katika kuomboleza msiba huo mkubwa. Napenda mjue kuwa msiba huu ni wangu pia. Machungu yenu ni majonzi yangu,” alisema Rais Kikwete.

Rais pia aliwatumia rambirambi wananchi wa Kalenga akisema wamempoteza mwakilishi na mtetezi mahiri wa maslahi yao. Kifo cha Mgimwa kinafanya wizara tano sasa kukosa mawaziri baada ya wengine wanne kuondoka, kutokana na sakata la ujangili kwa utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili, kukiuka haki za binadamu kwa baadhi ya raia kuuawa na wengine kupata ulemavu huku mifugo pia ikiuawa. Wakati Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki alijiuzulu, mawaziri wengine watatu walitenguliwa vyeo vyao, ambao ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David Mathayo.

Wasifu wake Mgimwa alizaliwa Kalenga Januari 20, 1950 na kupata elimu ya msingi katika Shule ya Wasa kati ya mwaka 1961 na 1967 kabla ya kujiunga na Seminari ya Tosa kati ya mwaka 1966 na 1967. Baada ya hapo alijiunga na Seminari ya Tosamaganga kati ya mwaka 1968 na 1969 kisha Seminari ya Mafinga kati ya mwaka 1970 na 1971. Mwaka 1975 alijiunga na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) hadi mwaka 1978 ambapo alipata Stashahada ya Juu katika masuala ya benki.Alirudi IFM mwaka 1983 na kusoma hadi mwaka 1984 na kutoka na Stashahada ya Uzamili katika fedha na mwaka 1989 alijiunga na Chuo cha Uongozi Mzumbe kusomea Shahada ya Uzamili katika fedha, ambayo aliipata mwaka 1991.

Kuhusu ajira, Mgimwa alifanya kazi Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kati ya mwaka 1980 hadi mwaka 2000, akishika nafasi za Mhasibu mwaka 1980 hadi 1981; mwaka 1981 hadi 1989 alikuwa mhadhiri katika Chuo cha NBC na mwaka 1996 hadi 1997 alikuwa Meneja katika benki hiyo. Kuanzia mwaka 1997 hadi 2000 alikuwa Mkurugenzi wa NBC kabla ya kuwa Mkuu wa Chuo cha Benki Mwanza kati ya mwaka 2000 na 2010, alipochaguliwa kuwa Mbunge wa Kalenga, akichukua nafasi ya Stephen Galinoma.

Mei 7 mwaka juzi aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Waziri wa Fedha, akichukua nafasi ya Mustafa Mkulo.Ndani ya CCM Mgimwa kati ya mwaka 2008 na 2010 alikuwa Mlezi wa Kata ya Wasa, mwaka 1994 hadi 1995 alikuwa Kamanda Msaidizi wa Vijana wa CCM wakati mwaka 1991 hadi 1994 alipata kuwa Diwani wa Kata ya Gangilonga. Katika uhai wake aliandika machapisho mengi kuhusu masuala ya benki na fedha. Wakati huo huo, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtumia Rais Jakaya Kikwete salaam za rambirambi, kutokana na kifo hicho cha Waziri Mgimwa.

Aidha, kimetuma salaam kwa familia na uongozi wa CCM, kutokana na msiba huo wa kuondokewa na mmoja wa wanachama na mbunge.Taarifa iliyotolewa jana, ilisema chama hicho kimepokea kwa mshituko na majonzi makubwa taarifa za kifo hicho.“Kwa masikitiko makubwa, CHADEMA kinatuma salaam za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kwa kuondokewa na msaidizi wake wa karibu na mtumishi mwenzake serikalini,” ilisema taarifa ya chama.

Chanzo: Habari Leo

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

10. YUSUF MANJI Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini. 9. FIDA RASHID Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine. 8. GHALIB SAID MOHAMMED Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

ZIFAHAMU TEKNOLOJIA 7 ZITAZOKAZOKUZA MAENDELEO YA MAJIJI MAKUBWA DUNIANI

Fikiria ulikuwa unafanya kazi katika taasisi ya maendeleo na kupunguza umasikini mwanzoni mwa miaka ya 1990. Mwandishi wa makala hii, Abhas Jha anasema yeye aliwahi kufanya kazi zama hizi. Anasema kipindi hicho kulikuwa na tovuti moja tu iliyokuwepo duniani mpaka kufikia Agosti mwaka 1991 (leo kuna zaidi ya tovuti bilioni 1.5 duniani kote). Anasema kipindi hicho simu za mkononi zilikuwa ghali sana, chache na zilikuwa nzito na za kishamba sana ukilinganisha na hizi za sasa. Ni watu wachache wangetazamia kuhusu hali iliyopo nchini India kwa sasa kwamba kungekua na idadi kubwa ya simu za mkononi kuilko idadi ya vyoo. Bill Gates aliwahi kusema "tunayapa uzito sana mabadiliko ambayo yatatokea ndani ya kipindi cha muda mfupi sana na kuyapuuza yale yaliyotokea kwa muda mrefu sana". Teknolojia inakua kwa kasi sana na kufanya na mabadiliko makubwa sana kwenye majiji ili kufikisha huduma kwa jamii. Teknolojia inafanya hivi ili sio tu kufikisha huduma haraka kwa wateja bali pia kuk...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

HEZBOLLAH YATAJA SABABU YA KUUAWA KIONGOZI WAO

 Kundi la Waislamu wa madhehebu ya Kishia la Hezbollah nchini Lebanon limetaja sababu ya kifo cha kiongozi wake wa ngazi ya juu wa kijeshi, Mustafa Badreddine kuwa kimetokana na makombora ya mizinga liliofanyika karibu na uwanja wa ndege wa Damascus nchini Syria.  Hezbollah lilitangaza  kifo cha Badreddine hapo jana na alifanyiwa mazishi ya kijeshi siku hiyo hiyo katika eneo la ngome la kundi hilo huko kusini mwa Beirut. Taarifa ya kundi hilo imesema mashambulizi hayo yamefanywa na kundi linaloitwa Takfiri. Takfiri ni neno linalotumiwa na kundi hilo la Kisunni kwa kuonesha msimamo mkali, kundi lenye kujihami na silaha, lililo na itikadi kali. Badreddine alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa kundi la Hezbollah walioshutumiwa mwaka 2005 kuhusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanon Rafik Hariri. Chanzo: Deutsche Welle (DW)

GWIJI WA RHUMBA TABU LEY AZIKWA KINSHASA

  Mazishi ya Gwiji wa Rumba nchini DRC, Tabu Ley Rochereau yalifanyika Jumatatu mjini Kinshasa.Mwili wake ukiwa ndani ya jeneza la rangi nyeupe lililotandwa bendera ya Jamhuri ya Congo, ulilazwa kwenye majengo ya Bunge ambako watu zaidi ya elfu kumi walifika kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Pascal Sinamoyi Tabu Ley.Viongozi wa serikali ya DRC walihudhuria mazishi hayo huku waakilishi kutoka nchi jirani ya Congo Brazaville pia wakihudhuria mazishi hayo. Tabu Ley alifariki mwezi Novemba akiwa na umri wa miaka 76 akipokea matibabu nchini Ubelgiji. Aidha gwiji huyo alikiri rasmi kwamba ana watoto 49. Lakini mwandishi wa BBC katika mazishi hayo Lubunga Byaombe, alisema kuwa zaidi ya watu 80 walijitokeza na kusema kuwa baba yao ni mwanamuziki huyo na kwamba wengi wao walitaka kupewa nafasi kuzungumza katika mazishi hayo. Tabu ley aliyejulikana kama mfalme wa muziki wa rumba aliaga dunia mwezi uliopita mjini Brussels, Ubelgiji akiwa na miaka sabini na sita.Wengi walimkumbuk...