Venance Blog inawakutakia HERI YA MWAKA MPYA 2014 sherehekea kwa amani na utulivu kama ujuavyo ndo mwanzo wa mwaka hivyo unachotakiwa kufanya usilewe sana kama ni mtumiaji wa vileo eti kisa unafurahia kuumaliza mwaka 2013 na kukaribisha mwaka 2014 pia usitumie pesa hovyo kwani mwezi huu huwa mgumu sana. Mwisho nakutakia mafanikio mema katika mwaka huu 2014, uwe mwaka wa neema kwako na Mungu akutangulie katika kila jambo.. HERI YA MWAKA MPYA!!
Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

Comments
Post a Comment