Venance Blog inawakutakia HERI YA MWAKA MPYA 2014 sherehekea kwa amani na utulivu kama ujuavyo ndo mwanzo wa mwaka hivyo unachotakiwa kufanya usilewe sana kama ni mtumiaji wa vileo eti kisa unafurahia kuumaliza mwaka 2013 na kukaribisha mwaka 2014 pia usitumie pesa hovyo kwani mwezi huu huwa mgumu sana. Mwisho nakutakia mafanikio mema katika mwaka huu 2014, uwe mwaka wa neema kwako na Mungu akutangulie katika kila jambo.. HERI YA MWAKA MPYA!!
Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

Comments
Post a Comment