Venance Blog inawakutakia HERI YA MWAKA MPYA 2014 sherehekea kwa amani na utulivu kama ujuavyo ndo mwanzo wa mwaka hivyo unachotakiwa kufanya usilewe sana kama ni mtumiaji wa vileo eti kisa unafurahia kuumaliza mwaka 2013 na kukaribisha mwaka 2014 pia usitumie pesa hovyo kwani mwezi huu huwa mgumu sana. Mwisho nakutakia mafanikio mema katika mwaka huu 2014, uwe mwaka wa neema kwako na Mungu akutangulie katika kila jambo.. HERI YA MWAKA MPYA!!
KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

Comments
Post a Comment