MADAGASCAR YAPATA RAIS MPYA

Maafisa nchini Madagascar wanasema kuwa matokeo ya mwanzo mwanzo ya duru ya pili ya uchaguzi wa Rais uliofanyika mwezi Disemba, yanaonyesha mshindi kuwa waziri wa zamani wa fedha Hery Rajaonarimampianina.Tume ya uchaguzi ya nchi hiyo inasema kuwa bwana Hery Rajaonarimampianina alishinda asilimia hamsini na tatu (53%) ya kura zilizopigwa.Mshindani wake, Jean Louis Robinson anasema kuwa uchaguzi ulikumbwa na wizi wa kura na sasa anasema sharti shughuli ya kuhesabu kura irejelewe.Uchaguzi huo ulikuwa mpango wa kurejesha utulivu kwa nchi hiyo baada ya mapinduzi ya kijeshi kufanyika miaka minne iliyopita.Bwana Rajaonarimampianina alikuwa mgombea aliyeungwa mkono na kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi, Rais wa zamani Andry Rajoelina. Chanzo: BBC Swahili

Comments

Popular Posts

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

CELEBRITY: SHANIA TWAIN ANATIMIZA MIAKA 53 LEO AGOSTI 28, 2018

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI