(NEW VIDEO) SNURA - NIMEVURUGWA
BONY M-MARYS BORN CHILD SONG LYRICS
And man will live forevermore because of Christmas Day
Long time ago in Bethlehem, so the Holy Bible said
Mary's boy child, Jesus Christ, was born on Christmas Day
Hark, now hear the angels sing, a king was born today
And man will live forevermore because of Christmas Day
Mary's boy child, Jesus Christ, was born on Christmas Day
While shepherds watch their flocks by night
They see a bright new shining star
They hear a choir sing a song, the music seemed to come from afar
Hark, now hear the angels sing, a king was born today
And man will live forevermore because of Christmas Day
Mmh-mmh
Mmh-hmm
Mmh-mmh
Mmh-mmh-hmm
Mmh-mmh-mmh-hmm
Mmh-hmm-mmh-mmh
For a moment the world was aglow, all the bells rang out
There were tears of joy and laughter, people shouted
"Let everyone know, there is hope for all to find peace"
Oh my Lord
You sent Your son to save us
Oh my Lord
Your very self You gave us
Oh my Lord
That sin may not enslave us
And love may reign once more
Oh my Lord
When in the crib they found Him
Oh my Lord
A golden halo crowned Him
Oh my Lord
They gathered all around Him
To see Him and adore (this day will live forever)
Oh my Lord (so praise the Lord)
They had become to doubt You
Oh my Lord (He is the truth forever)
What did they know about You?
Oh my Lord (so praise the Lord)
But they were lost without You
They needed You so bad (His light is shining on us)
Oh my Lord (so praise the Lord)
With the child's adoration
Oh my lord (He is a personation)
There came great jubilation
Oh my Lord (so praise the Lord)
And full of admiration
They realized what they had (until the sun falls from the sky)
Oh my Lord (oh praise the Lord)
You sent Your son to save us
Oh my Lord (this day will live forever)
Your very self You gave us
Oh my Lord (so praise the Lord)
Watch Mary's Boy Child Official Music Video 👇🏿
KNOW ABOUT BIG RESULTS NOW ON EDUCATION IN TANZANIA
Improving education is of high importance to Tanzania – it is a
strategic agent for development for the country. With this perspective,
significant efforts have been made to increase access for all, resulting
in a huge enrollment expansion over the last ~10 years. Over the same
period of time quality of education dropped significantly. To address
this challenge and reverse the trend, the education lab has focused on
finding ways to raise the quality of basic education, and has set a very
ambitious target to improve pass rates1 in primary and secondary
schools to 60% in 2013, 70% in 2014 and 80% in 2015
Among several drivers of quality, the lab team has analyzed the most important challenges, and gone through an extensive prioritization effort to determine the focus areas that will give Big Results Now. Among the top issues we have addressed are lack of accountability, availability of teaching and learning materials, low support for struggling students and poor school management
To address the core issues, the lab recommends a business unusual quality transformation programme built on 4 integrated levers: Create performance transparency, motivate through incentives, provide support where needed the most and improve the teacher conditions
The lab has outlined each initiative in detail, including 3 feet implementation plans, budgets and a comprehensive set of KPIs to track progress and results
A cross-functional team of 34 members from 31 organizations worked together as a team for 6 weeks to develop the solutions. After the lab, the Education Ministry Delivery Unit, overseen by the Presidents’ Delivery Bureau, will keep the strong momentum and drive the end-to-end implementation
The Government of Tanzania has decided to prioritise the available resources to strategic sectors so as to realise the Big Results Now (BRN). The Education Sector is among the six prioritised sectors, which has developed 9 key initiatives to improve the quality of basic education and thereby increasing the pass rates in Primary and Secondary Schools. The Official School Ranking as per examination results according to the performance and improvement is among the 9 initiatives. In this ranking, schools are classified into bands of three major groups namely Green, Yellow and Red representing High, Medium and Lowperforming schools respectively. The schools' information will bring community awareness and engagement as well as improve transparency and accountability.
SOURCE: moe.go.tz
Among several drivers of quality, the lab team has analyzed the most important challenges, and gone through an extensive prioritization effort to determine the focus areas that will give Big Results Now. Among the top issues we have addressed are lack of accountability, availability of teaching and learning materials, low support for struggling students and poor school management
To address the core issues, the lab recommends a business unusual quality transformation programme built on 4 integrated levers: Create performance transparency, motivate through incentives, provide support where needed the most and improve the teacher conditions
The lab has outlined each initiative in detail, including 3 feet implementation plans, budgets and a comprehensive set of KPIs to track progress and results
A cross-functional team of 34 members from 31 organizations worked together as a team for 6 weeks to develop the solutions. After the lab, the Education Ministry Delivery Unit, overseen by the Presidents’ Delivery Bureau, will keep the strong momentum and drive the end-to-end implementation
The Government of Tanzania has decided to prioritise the available resources to strategic sectors so as to realise the Big Results Now (BRN). The Education Sector is among the six prioritised sectors, which has developed 9 key initiatives to improve the quality of basic education and thereby increasing the pass rates in Primary and Secondary Schools. The Official School Ranking as per examination results according to the performance and improvement is among the 9 initiatives. In this ranking, schools are classified into bands of three major groups namely Green, Yellow and Red representing High, Medium and Lowperforming schools respectively. The schools' information will bring community awareness and engagement as well as improve transparency and accountability.
SOURCE: moe.go.tz
QUOTES BY BRUCE LEE
1. Love is like a friendship caught on fire. In the beginning a flame, very pretty, often hot and fierce, but still only light and flickering. As love grows older, our hearts mature and our love becomes as coals, deep-burning and unquenchable.
2. Always be yourself, express yourself, have faith in yourself, do not go out and look for a successful personality and duplicate it.
3. Mistakes are always forgivable, if one has the courage to admit them.
4. I fear not the man who has practiced 10,000 kicks once, but I fear the man who has practiced one kick 10,000 times.
5. If you love life, don't waste time, for time is what life is made up of.
6. A wise man can learn more from a foolish question than a fool can learn from a wise answer.
7. If you always put limit on everything you do, physical or anything else. It will spread into your work and into your life. There are no limits. There are only plateaus, and you must not stay there, you must go beyond them.
8. I'm not in this world to live up to your expectations and you're not in this world to live up to mine.
9. A goal is not always meant to be reached, it often serves simply as something to aim at.
10. Knowledge will give you power, but character respect.
11. Ever since I was a child I have had this instinctive urge for expansion and growth. To me, the function and duty of a quality human being is the sincere and honest development of one's potential.
12. To hell with circumstances; I create opportunities.
13. Showing off is the fool's idea of glory.
14. As you think, so shall you become.
15. A quick temper will make a fool of you soon enough.
16. The key to immortality is first living a life worth remembering.
17. If you spend too much time thinking about a thing, you'll never get it done.
18. Notice that the stiffest tree is most easily cracked, while the bamboo or willow survives by bending with the wind.
19. You just wait. I'm going to be the biggest Chinese Star in the world.
20. To me, the extraordinary aspect of martial arts lies in its simplicity. The easy way is also the right way, and martial arts is nothing at all special; the closer to the true way of martial arts, the less wastage of expression there is.
21. Obey the principles without being bound by them.
22. The possession of anything begins in the mind.
23. The less effort, the faster and more powerful you will be.
24. If you spend too much time thinking about a thing, you'll never get it done.
25. The key to immortality is first living a life worth remembering.
26. Take things as they are. Punch when you have to punch. Kick when you have to kick.
27. Real living is living for others.
28. Ever since I was a child I have had this instinctive urge for expansion and growth. To me, the function and duty of a quality human being is the sincere and honest development of one's potential.
29. To hell with circumstances; I create opportunities.
30. Showing off is the fool's idea of glory.
31. As you think, so shall you become.
32. A quick temper will make a fool of you soon enough. 33. Man, the living creature, the creating individual, is always more important than any established style or system. 34. It's not the daily increase but daily decrease. Hack away at the unessential.
35. To know oneself is to study oneself in action with another person.
36. All fixed set patterns are incapable of adaptability or pliability. The truth is outside of all fixed patterns.
37. Take no thought of who is right or wrong or who is better than. Be not for or against.
QUOTES BY BOB MARLEY
1. My music fights against the system that teaches to live and die.
2. Get up, stand up, Stand up for your rights. Get up, stand up, Don't give up the fight.
3. Me only have one ambition, you know. I only have one thing I really like to see happen. I like to see mankind live together - black, white, Chinese, everyone - that's all.
4. The good times of today, are the sad thoughts of tomorrow.
5. I don't stand for the black man's side, I don' t stand for the white man's side. I stand for God's side.
6. If you're white and you're wrong, then you're wrong; if you're black and you're wrong, you're wrong. People are people. Black, blue, pink, green - God make no rules about color; only society make rules where my people suffer, and that why we must have redemption and redemption now.
7. The greatness of a man is not in how much wealth he acquires, but in his integrity and his ability to affect those around him positively.
8. Don't gain the world and lose your soul; wisdom is better than silver or gold.
9. People want to listen to a message, word from Jah. This could be passed through me or anybody. I am not a leader. Messenger. The words of the songs, not the person, is what attracts people.
10. Bob Marley isn't my name. I don't even know my name yet.
MWILI WA NELSON MANDELA KUZIKWA LEO KIJIJINI KWAKE QUNU
NDEGE ya kijeshi aina ya C-130 Hercules iliyobeba mwili wa Rais wa Kwanza Mzalendo wa Afrika Kusini, ilitua Uwanja wa Ndege wa Mthatha jana majira ya saa 6.37.Ikisindikizwa na ndege nyingine mbili za kijeshi, iliruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kijeshi wa Waterkloof, Pretoria saa 4:58, tayari kwa safari ya mwisho ya kuuhifadhi mwili wa Mandela kwa maziko kijijini kwake Qunu katika Jimbo la Eastern Cape.Mwili wa mwanamapinduzi huyo kipenzi cha dunia, unatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya familia ya Mandela, shughuli inayotarajiwa kuanza saa 3 asubuhi.Shujaa huyo wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi, alifariki dunia Alhamisi ya Desemba 5, 2013 saa 2:50 usiku nyumbani kwake, Mtaa wa Laa Namba 12, Houghton jijini Johannesburg akiwa amezungukwa na wanafamilia wote, wakiwemo mkewe Graca Machel na mtalaka wake, Winnie Medikizela –Mandela na mtoto wake mkubwa, Makaziwe Mandela.Tayari Serikali imetangaza leo kuwa siku ya mapumziko, ili kuwawezesha wananchi kufuatilia maziko ya kiongozi huyo ambaye tangu kufa kwake siku kumi zilizopita, amekuwa gumzo kubwa kutokana na heshima aliyojiwekea kote duniani.Kama ilivyokuwa katika miji ya Soweto na Pretoria ulikoagwa mwili wa shujaa huyo aliyeaga dunia akiwa na umri wa miaka 95, Mji wa Mthatha nao ulifurika umati wa wananchi ambao bila kutarajia, walijikuta wakitengeneza mstari mrefu kutoka katikati ya mji hadi uwanja wa ndege kuulaki mwili wa shujaa wao.Na baada ya kutua, mwili huo ulizunguka katika mitaa ya Mthatha na baadaye kusafirishwa kwa msafara mkubwa wa magari na pikipiki za kijeshi hadi Qunu, umbali wa kilomita 31 kutoka Mthatha, huku anga lote la barabara iliyotumika kusafirisha mwili huo ikilindwa kwa helikopta za kijeshi.Akizungumza kutoka Qunu mapema, mmoja wa watu walioteuliwa na familia kusimamia maandalizi ya mazishi, Phathekile Holomisa kabla na kupaa kwa ndege na wakati wote wa safari angani, wazee wa familia walizungumza na mwili wa marehemu mithili ya mtu anayesikia, wakiutaarifu juu ya safari nzima kuelekea Qunu.“Wanazungumza na Mandela kama mtu aliye hai,” alisema Holomisa na kuongeza;” Hii ni kwa sababu tunaamini kiroho bado yu hai.” Mwili wa Mandela uliwasili kijijini Qunu saa 9:26 alasiri, huku mji wote ukiwa na umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza kumlaki shujaa wao. Mara baada ya ujio wa mwili huo, helikopta nne za kijeshi zilionekana zikizunguka anga la Qunu.Tutu kutomzika `swahiba’ wakeLicha ya kuwa rafiki wa siku nyingi wa Mzee Mandela, taarifa za kushangaza zinasema kuwa, Askofu mashuhuri mstaafu wa Kanisa la Anglikana Afrika Kusini, Desmond Tutu ambaye pia ni Mshindi wa Nishani ya Amani ya Nobel, hatashiriki katika shughuli ya kuupumzisha kaburini mwili wa Mandela leo kijijini Qunu.“Hakuna taarifa zaidi zitakazotolewa kuhusiana na Askofu Tutu kutomzika Mandela,” anasema Mpho Tutu, binti wa Askofu Tutu ambaye ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa taasisi ya Desmond Tutu na mkewe Leah. “Askofu hakualikwa, hivyo hatakwenda,” alikaririwa na kusisitiza kutozama katika kuelezea suala hilo.Taarifa za baadaye kutoka Ikulu ya Afrika Kusini zinasema, Askofu Tutu amealikwa kwenda Qunu. “Askofu Tutu si mtu wa kawaida, ana nguvu na ushawishi ndani na nje. Ni mtu muhimu nchini mwetu, yupo katika orodha yetu,” anasema Mac Maharaj wa Ikulu ya Afrika Kusini.Hata hivyo, vyombo vya habari vimedokeza kuwa, huenda hakualikwa kutokana na misimamo yake `migumu’ dhidi ya serikali ya sasa inayoongozwa na Jacob Zuma.Vyombo hivyo vimeongeza kuwa, Tutu hakuwamo katika orodha ya wasemaji siku ya mazishi ya kitaifa ya Mzee Mandela kwenye Uwanja wa Soka wa FNB, Soweto Jumanne wiki hii.Hata hivyo, katika dakika za mwisho aliombwa kutoa `neno’ baada ya umati wa waombolezaji kumzomea Rais Zuma. Askofu Tutu aliweza kupoza hasira za wananchi hao wa Afrika Kusini, baada ya kuzungumza kwa ukali akisema; “Tuioneshe dunia tumekuja hapa kumuaga shujaa wetu.Lazima tuoneshe kuwa sisi ni watu wenye nidhamu, tutulie na ikiwezekana kwa ukimya wenu nisikie sauti ya pini ikidondoka.”Alimmwagia sifa Mandela kuwa alikuwa mtu wa maajabu na alionesha maajabu akiwa hai kutokana na matendo yake yanayopaswa kuigwa na hata baada ya kuaga dunia, kwani licha ya kuiliza dunia nzima, amefanikiwa pia kuwakutanisha viongozi mahasimu wa kisiasa duniani katika uwanja mmoja wakimuaga.Miongoni mwa viongozi mahasimu waliokutana ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe aliyekutana na Rais Barack Obama na Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron.Obama na Cameron waliweka vikwazo vya kiuchumi kwa Zimbabwe wakipinga matokeo ya uchaguzi uliompa Mugabe ushindi wa asilimia 61 dhidi ya wapinzani wake, wakidai kuwa kiongozi huyo alichakachua kura.Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Natanyahu ambaye awali aliripotiwa kutokwenda, alifika na kukaa katika uwanja mmoja na Rais wa Mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, licha ya kuwa na ugomvi wa muda mrefu na unaoendelea baina yao.Pia Rais Obama, alikutana na hasimu wa nchi yake wa siku nyingi, Rais Raul Castrol wa Cuba, ambao uhusiano wao umekuwa ukidorora tangu Mapinduzi ya Cuba ya mwaka 1959.Kutokana na uhusiano mbovu kati ya nchi hizo, mpaka leo Marekani haina uhusiano wa kibalozi na Cuba, huku nchi hiyo ikiweka katika sheria zake vizuizi kwa kampuni za Marekani kufanya biashara na Cuba.Nchini Marekani, wachambuzi wa kisiasa walishangazwa na uamuzi wa familia za kisiasa za Obama, George W. Bush na Bill Clinton, kupanda ndege moja kwenda Afrika Kusini kumuaga Mandela.
BBC YALAUMIWA KUVUNJA VIPINDI KWA AJILI YA MSIBA WA MANDELA

Wakati Dunia ikifuatilia kwa karibu safari ya mwisho ya Mandela hapa duniani, Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) limeripotiwa kuingia lawamani kutokana na uamuzi wake wa kupangua vipindi vingi na kuweka matangazo ya moja kwa moja ya mazishi ya kiongozi huyo wa zamani wa Afrika Kusini ambaye kabla ya kuingia Ikulu, alisota gerezani kwa miaka 27 kutokana na harakati zake zilizowakera makaburu.
Gazeti la Daily Mail la Uingereza limeripoti kuwa, watazamaji na wasikilizaji 1,834 wa redio na televisheni za BBC, wamelalamikia matangazo mfululizo ya mazishi ya Mandela. Mmoja wa wabunge wa chama cha Conservative, Conor Burns amekaririwa akisema hakukuwa na ulazima wa BBC kutumia muda mwingi na pia kupoteza fedha za walipa kodi kutuma wanahabari wanane kwenda Johannesburg, Afrika Kusini kwa ajili ya vipindi vya mahojiano katika shughuli ya kumuaga Mzee Mandela.“Tunafahamu heshima ya Mzee Mandela, alikuwa mmoja wa viongozi wa kipekee katika karne ya 20 na 21. Ametufundisha mengine juu ya amani na kuheshimu wengine, lakini BBC wamekurupuka na kutumia fedha nyingi badala ya kuwaeleza walipa kodi umuhimu wa safari hiyo na hata kukata vipindi zaidi ya 100 kwa wiki moja sasa,” anasema Burns.
Chanzo: BBC
ZITTO AKERWA KUITWA MUONGO BUNGENI
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, amesema anatarajia kuwasilisha maelezo binafsi kuhusu, kauli ya Mwanasheria Mkuu aliyoitoa juzi bungeni dhidi yake na kumuita muongo kuhusu suala la kuwa na orodha ya watu wanaodaiwa kuficha fedha nje ya nchi.Zitto, aliyasema hayo bungeni juzi, ikiwa ni siku moja tu baada ya Mwanasheria Mkuu (AG), Jaji Frederick Werema, kudai mbele ya Bunge kuwa Serikali inashughulikia kisheria suala la Zitto kudanganya Bunge na Kamati kuhusu majina ya watu walioficha mabilioni ya fedha Uswisi.Akizungumza na HabariLeo Jumapili, Zitto alisema kwa sasa hataki kuzungumzia suala hilo, ila ukweli wote ataubainisha kwenye maelezo yake binafsi ambayo atayawasilisha wiki ijayo kwenye mkutano wa 14 wa Bunge unaoendelea.“Nimeamua hili suala nilizungumzie ndani ya Bunge, kwa hiyo tayari nimewasilisha maelezo yangu kwenye Ofisi ya Bunge, na wameniambia kuwa nitapangiwa kuwasilisha maelezo hayo wiki ijayo, kila kitu nitakibainisha siku hiyo, sina zaidi,” alisisitiza Zitto.Wakati akitoa majumuisho ya mjadala wa taarifa zilizowasilishwa bungeni juzi, ambazo ni taarifa ya Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, Werema alisema katika suala hilo, Zitto amezidi kuwa mzito.AG huyo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya kuchunguza madai ya mabilioni hayo amesema ili kumalizia uchunguzi wa fedha hizo ameomba Spika wa Bunge kuongezea kamati hiyo miezi sita.Werema alisema alishangaa kitendo cha Zitto kutaka suala hilo liangalie mfumo na siyo majina ya watu walioficha mabilioni hayo. Alisema awali yeye alishauri kuangalia mfumo wa uwekaji wa fedha hizo, lakini Zitto alikataa na kusema anataka kutoa dukuduku kwa kutaja majina ya watu walioficha fedha hizo.Alisema mwezi Februari Kamati ilikutana na Zitto na kuwaeleza kuwa ana taarifa na nyaraka na kutoa masharti lakini aliondoka kwenda katika kambi ya Jeshi ambako Kamati ilimfuata lakini bado aliwataka kukutana Dar es Salaam.Alisema Mei mwaka huu hadi aliposema hakuwa na jina wala akaunti ya mtu yeyote ambaye ana akaunti nje ya nchi kwa kiapo maalumu.“Jambo la kushangaza ni leo kudai Serikali haina dhamira na suala la walioficha fedha Uswisi? Kwa kweli Zitto Kabwe ni mzigo na sasa tunaingia kufanya kazi hiyo ya uchunguzi kama Serikali kwa kutafuta taarifa bila kumuonea mtu,” alisema Werema.
POLISI WAKAMATA BASTOLA NYUMBA YA KULALA WAGENI
JESHI la Polisi wilayani Igunga mkoani Tabora limefanikiwa kukamata bastola katika nyumba ya kulala wageni ambayo inadhaniwa imesahaulika na majambazi.Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Tabora, Peter Ouma alisema silaha hiyo imekamatwa juzi katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Sophia Lodge iliyopo mtaa wa Bank, Igunga mjini.Alisema kuwa bastola hiyo yenye namba za usajili 224335 aina ya Browing Court ilidakwa na risasi 38 pamoja na magazini 4.
KENYA YASHEREHEKIA MIAKA 50 YA UHURU
Kenya jana ilisherehekea miaka 50 ya uhuru walioupata chini ya utawala wa Uingereza.Mamia ya raia na wageni mbali mbali wamehudhuria katika sherehe hizo zilizofanyika katika mji mkuu wa Nairobi.Wageni mbali mbali pamoja marais wa mataifa mbali mbali wamehudhuria sherehe hizo akiwemo Rais Godluck Jonathan wa Nigeria, Jakaya Kikwete wa Tanzania, Joseph Kabila wa DRC, Pierre Nkurunziza wa Burundi, Ali Bongo wa Gabon, Mahinda Rajapaksa wa Sri Lanka.Usiku wa kuamkia Alhamis bendera ya Kenya ilipandishwa katika eneo hilo hilo siku bendera ya uhuru ilipopandishwa wakati nchi hiyo inapata uhuru katika bustani ya Uhuru Desemba 12, 1963.Siku hiyo ya uhuru Rais Jomo Kenyatta, baba yake rais wa sasa Uhuru Kenyatta alitawazwa kuwa kiongozi wa nchi hiyo.
KINGEREZA CHAMCHANGANYA MKALIMANI AFRIKA KUSINI

Wataalamu wa lugha za ishara wamesema mtafsiri huyo wa lugha za ishara, Thamsanqa Dyanty, alikuwa "akitapatapa" wakati wa ibada hiyo siku ya jumanne. Naibu Waziri wa Afrika Kusini Hendrietta Bogopane - Zulu amesema hakuna suala lolote la kukiuka taratibu za kiusalama wakati mtafsiri huyo alipokuwa akisimama kwani alikuwa na vibali halali.
Katika maoni yake mtafsiri huyo anayelalamikiwa, Bwana Dyanty , amesema alipatwa ugonjwa wa kuchanganyikiwa. Kwa upande wake mmiliki wa kampuni iliyomtoa mtafsiri huyo imetupilia mbali madai ya Naibu waziri Bogopane Zulu.
Awali Naibu Waziri huyo aliwaomba radhi jamii ya viziwi kwa kiwango cha chini cha kutafsiri kilichofanywa na Bwana Dyanty kutoka kampuni ya SA Interpreters."Mtafsiri huyo anazungumza lugha ya Xhosa hivyo kiingereza kilikuwa kigumu sana kwake," alisema Waziri huyo.
AJALI: BASI LAUA WATU 12 PAPO HAPO
Watu 12 wamekufa papo hapo na wengine zaidi ya 90 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Korogwe, Tanga kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka. Ajali hiyo ilitokea jana saa 1.30 asubuhi kwenye barabara kuu ya Segera-Chalinze katika kijiji cha Kwalaguru kata ya Kwedizinga wilayani hapa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alithibitisha jana kutokea kwa ajali hiyo ya basi la Burudani namba T 610 ATR aina ya Nissan. Majeruhi walipelekwa katika hospitali ya wilaya ya Korogwe ya Magunga, kwa matibabu ya awali na miili ya marehemu, akiwamo dereva wa gari hilo, Luta Mpenda (35) imehifadhiwa hospitalini hapo.
“Tukiwa tunakaribia kwenye kona ile, tulipishana na lori hilo likiwa kasi upande wetu, dereva wetu akajitahidi kulikwepa lakini kutokana na ile kona kuwa kali, gari lilimshinda na kupinduka,” alisema Bendera. Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo walisema walisikia kishindo kutoka eneo hilo wakaenda na kukuta gari limepinduka na baadhi ya watu wamekufa. “Sisi tulikuwa tumekaa huku, ghafla tukasikia kishindo kikubwa tukakimbia kuangalia tukakuta ni basi la Burudani limepinduka, kusema kweli ile ajali ni mbaya sana,” alisema Zablon Mbaga.
Baadhi ya wakazi wa Korogwe waliofurika katika hospitali ya Magunga kutambua miili na majeruhi waliofikishwa hapo walisema idadi kubwa ya abiria waliokuwa wakisafiri katika basi hilo ni wafanyabiashara.“Wengi hapa ni wafanyabiashara ndio wanaotumia basi hili kwa sababu wana uhakika wakiondoka alfajiri saa 12, wanafika Dar es Salaam mapema na kugeuza jioni,” alisema Fatuma Bakari.
Mganga Mkuu wa Magunga, Dk Simon Mngiwa, alisema alipokea majeruhi ambao hali zao ni mbaya kutokana na kupasuka vichwa, kuvunjika miguu, mikono na kupata maumivu ya kifua.Baadhi ya majeruhi kwa mujibu wa Dk Mngiwa, walikimbizwa katika hospitali ya Bombo, KCMC Moshi na Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu ya Muhimbili (MOI). Rambirambi ya JK Kutokana na ajali hiyo, Rais Jakaya Kikwete, alimtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa. “Nimepokea kwa mshituko na masikitiko makubwa taarifa za vifo vya watu 12 vilivyotokea na majeruhi baada ya basi la kampuni ya Burudani walilokuwa wakisafiria kutoka Korogwe kwenda Dar es Salaam kupinduka katika kijiji cha Taula,” alisema Rais Kikwete katika taarifa iliyotumwa jana na Ikulu.
Rais alisema vifo vya watu hao ni pigo kubwa si tu kwa familia za waliopoteza ndugu zao, bali pia Taifa kwa ujumla ambalo limepoteza nguvukazi muhimu iliyokuwa bado inahitajika kwa ujenzi wa Taifa. Rais Kikwete alimwomba Mkuu wa Mkoa kumfikishia salamu zake kwa familia, ndugu na jamaa waliopotelewa na wapendwa wao. Aliwahakikishia wafiwa kwamba yuko pamoja nao katika kipindi hiki cha maombolezo na kuwaomba wawe na uvumilivu, ujasiri na subira katika kipindi hiki kigumu wanachopitia wakiomboleza vifo vya ndugu zao. Aidha, aliwaombea kwa Mungu majeruhi wapone haraka na kurejea katika hali zao za kawaida, ili waungane na ndugu na jamaa zao na kuendesha maisha yao kama ilivyokuwa kabla ya kutokea kwa ajali.
Waliopoteza maisha katika ajali hiyo wametambuliwa kuwa ni dareva wa basi hilo, Luta Kimar, mkazi wa Kwasamangube Korogwe, aliyetajwa kwa jina la Mama Ally, mkazi wa National Housing Korogwe, Joyce Mokiwa (36) na mkazi wa Kambi ya Maziwa, Rehema Mandondo.Wengine ni Mwalimu wa Shule ya Mgombezi Korogwe, Msoke Mosha,mkazi wa Kilole Korogwe, Bashiri Shafii, mkazi wa Lutherani Korogwe, aliyetajwa kwa jina moja la Bryton, mkazi wa Bagamoyo Kilole Korogwe, Rehema Nassoro (23), Agnes Linus ambaye ni mkazi wa Mandera na Mariamu Juma ambaye hakutajwa eneo anakotoka.
Chanzo: Habari Leo
PINDA: NITAFURAHI NIKIONDOLEWA
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda uwaziri mkuu ni mzigo anaobeba kama Msalaba na ikiwa ataondolewa, atafurahi kwa kuwa atapumzika. Alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Rukia Kassim Mohamed (CUF), katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo.“Rais akiniambia nimeshindwa majukumu nitaondoka, huku nikiwa na kicheko, hata ninyi wabunge mna nafasi ya kuniondoa, mnaweza kufanya hivyo mkiona inafaa kwani nitafurahi na kupumzika,” alisema.Rukia katika swali lake, alimtaka Pinda kutoa ufafanuzi kuhusu kauli za wabunge wa CCM kuwa yeye ndiye mzigo. Alisema licha ya jitihada anazofanya kutekeleza wajibu wake kwa kusimamia wizara 20, anashangaa kuhukumiwa kwa upungufu unaotokea katika wizara moja au mbili.Alifafanua, kuwa anasimamia wizara kama 20 na zote zinafanya kazi vizuri, lakini kama kuna wizara moja au mbili hazijafanya vizuri sana, hiyo haitoshi kudai atimuliwe kazi.Alisema uzuri wa nafasi ya uwaziri mkuu, mtu haombi, bali anateuliwa na Rais kwa majaaliwa ya Mwenyezi Mungu, hivyo isipompendeza, ni kazi rahisi kwa Rais ambaye atamwambia kuwa ameshindwa jukumu lake na kumwondoa.“Bunge pia mnaweza kumwondoa Waziri Mkuu kwa uwezo wenu, hivyo dada Rukia kama unafikiri hilo na wabunge wote wakaona sawa, nipo tayari, tena nitafurahi kweli kweli angalau nimeutua Msalaba huu, mana’ke hii kazi ni ngumu,” alisema.Katika swali la msingi, Mbunge huyo alitaka kujua kauli ya Waziri Mkuu iliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuwa kuna baadhi ya mawaziri ni mizigo alipokuwa katika ziara yake mkoani Mbeya.Akijibu swali hilo, Pinda alisema hata yeye alisikia kauli hiyo kwenye vyombo vya habari akasema ni vema kumsubiri Kinana arudi kutoka katika ziara na kumsikiliza alichosema alikuwa na nia gani, ndipo wataona namna ya kwenda mbele zaidi.Hata hivyo, aliyesema bungeni kuwa Pinda ni mzigo kwa Serikali alikuwa Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM) akisema ndiye ambaye anastahili aondolewe kwenye nafasi yake hiyo.Pia Waziri Mkuu alimwahidi Mbunge wa Mkanyageni, Habib Juma Mnyaa (CUF), kufuatilia kwa nini suala la kupeleka fedha za chenji ya rada hazijafikishwa Zanzibar. Alisema suala hilo lilishazungumzwa ndani ya Serikali wakakubaliana na likaisha.Aliongeza kuwa suala hilo ni la kisekta na litatolewa ufafanuzi zaidi na waziri husika. Katika swali lake la awali, Mnyaa alimwuliza Waziri Mkuu ni kwa nini hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya kauli iliyotolewa bungeni ya kushughulikia suala la chenji ya rada kupelekwa Tanzania Bara pekee.
UGANDA YAANZA KUILIPA TANZANIA FIDIA
SERIKALI ya Uganda tayari imeshaanza kulipa deni lake kwa Tanzania la dola za Marekani milioni 9.6 kati ya dola za Marekani milioni 18.4 ikiwa ni fidia kwa Tanzania kwa mchango wake katika kumuondoa Idd Amin Dada Uganda mwaka 1978.Hayo yalibainishwa bungeni jana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Shamsi Vuai Nahodha, wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Mbinga, John Komba (CCM).Katika swali lake Komba alitaka kujua kama Tanzania ilishaanza kudai fidia kwa Serikali ya Uganda kutokana na mchango wake wa kuisaidia nchi hiyo kumuondoa Idd Amin na kumfanya Rais wa sasa Yoweri Museveni kutawala kwa amani nchini humo.Akijibu swali hilo, Nahodha alikiri kuwa Tanzania ilipigana vita na Uganda kuanzia mwaka 1978 hadi mwaka 1979 kutokana na uvamizi uliofanywa na Uganda chini ya utawala wa Idd Amin aliyevamia na kukalia sehemu ya ardhi ya Tanzania mkoani Kagera.“Kwa kuwa vita hivyo vilitokana na uvamizi wa Idd Amin, baada ya vita kumalizika Serikali ya Tanzania iliitaka Uganda kulipa fidia. Serikali hiyo nayo ilikubali kuilipa Tanzania fidia hiyo,” alisema Nahodha.Alisema kwa bahati mbaya Serikali ya Uganda haikutekeleza makubaliano hayo yaliyofanyika mwaka 1979 hivyo Serikali ya awamu ya tatu ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Mstaafuma William Benjamin Mkapa ilifanya majadiliano tena na Uganda.Alisema kutokana na majadiliano hayo Serikali ya Uganda ilitakiwa kulipa fidia dola za Marekani milioni 18.4 na hadi sasa Serikali hiyo imeshalipa dola za Marekani milioni 9.6 fedha ambazo ziliwekwa katika Mfuko Mkuu wa Serikali na nchi hiyo kubakiwa na deni la dola za Marekani milioni 8.8.Nahodha alisema majadiliano baina ya Tanzania na Uganda yanaendelea ili sehemu ya fidia iliyobaki iweze kulipwa chini ya Wizara ya Fedha ambayo ndio inayofuatilia deni hilo.Akijibu swali la nyongeza la Komba la kuitaka Tanzania imkumbushe Museveni juu ya namna Tanzania ilivyosaidia nchi yake hivyo aache kuihujumu kwa kusaidiana na Rais wa Rwanda Paul Kagame, Nahodha alisema siku zote Tanzania haimsaidii mtu ili kupata shukurani. Tanzania ni nchi ya kipekee sana, imebahatika kupata viongozi wenye sifa kubwa duniani kama Nyerere (Mwalimu Julius), kiongozi huyu aliwahi kusema Waafrika ni ndugu na Afrika yetu sote, tuliwasaidia Uganda kwa utu hatutegemei zaidi,” alisisitiza.Alisema hata juzi baada ya kifo cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Tanzania ilitoa tamko la kumuenzi kwa kusisitiza uvumilivu, jambo ambalo limeipatia sifa kubwa Tanzania. “Naomba tuendelee kuitunza sifa hii na si vinginevyo.”