Skip to main content

WAFUNGAJI BORA NA WALIOCHEZA MECHI NYINGI KATIKA KOMBE LA DUNIA 1930-2014

WAFUNGAJI 5 WA MUDA WOTE

1. Miroslav Klose - Ujerumani

Klose wakati wa droo ya kombe la dunia mwaka jana 2017.
Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29.  Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002. Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil.
Klose wakati wa mechi ya robo fainali kati ya Ujerumani na Ufaransa katika dimba la Marakana Rio de Jeneiro Julai 4, 2014.


2. Ronaldo de Lima - Brazil

Ronaldo de Lima alipokabidhiwa tuzo ya Hall of Fame nchini Italia mwaka 2016
Amezaliwa Septemba 22, 1976. Amecheza mechi 45; 19 za kombe la dunia, 15 za kufuzu kombe la dunia, 5 za kombe la mabara na 6 za Olimpiki. Katika mechi hizi alifunga jumla ya magoli 34; 15 ya kombe la dunia, 10 ya kufuzu michuano hii, 4 ya kombe la mabara na 5 ya Olimpiki. Akiwa katika timu ya Brazil walishinda mechi 31, suluhu 8 na kufungwa mechi 6. Umaarufu wake ulianza kuonekana katika michuano ya Olympic mwaka 1996 iliyofanyika Atlanta dhidi ya Japan. Brazil iliifunga Japan 1-0. Amewahi kupewa kadi za njano mara 4 tu katika michuano yote. Alipokuwa Brazil walitwaa kombe la dunia mwaka 1994 na 2002. Mwaka 2002 ndiye aliyekua mchezaji bora wa michuano ya kombe la dunia FIFA. Mwaka 1997 akiwa na timu yake walishinda kombe la dunia la mabara. Ronaldo amewahi kushinda tuzo ya mpira wa dhahabu ya Adidas kama mchezaji bora. Mwaka 2002 pia alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas. Amewahi kushinda tuzo ya Balloon d'Or ya Ufransa mwaka 1997 na 2002.
Ronaldo enzi za Brazil.


    3. Gerd Mueller - Ujerumani

    Mueller alipokua kocha wa Bayern Munich  II
    Alizaliwa Novemba 3, 1945. Amecheza mechi 19 na timu yake ya Ujerumani; 13 zikiwa za kombe la dunia na 6 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi hizo alizokuwepo walishinda mechi 16, suluhu 1 na kufungwa 2. Ana magoli 23; 14 yakiwa ya kombe la dunia la 9 yakiwa ya kufuzu michuano hiyo. Amewahi kupewa kadi za njano 2 tu katika michuano ya kombe la dunia. Mwaka 1970 alishinda tuzo mbili; kiatu cha dhahabu cha Adidas pamoja tuzo ya Ballon d'Or. Pia ni miongoni mwa waliokuwepo katika kikosi cha Ujerumani kilichotwaa kombe la dunia mwaka 1974.
    Gerd Mueller mwaka 1974 waliposhinda fainali ya kombe la dunia.

    4. Just Fontaine - Ufaransa

    Fountaine mwaka 2017
    Alizaliwa Agosti 18, 1933. Yeye alicheza 8 tu 6 zikiwa zakombe la dunia na 2 zikiwa za kufuzu michuano hiyo, katika mechi hizi alifunga magoli 16; katika hayo 13 yalikua ya kombe la dunia na 3 yalikuwa ya mechi za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza 6 walishinda na hawakusuluhu ila walipoteza nchi 2 tu. Alionekana katika kombe la dunia kwenye mechi ya kati ya Ufaransa na Luxembourg ambapo waliifunga nchi hiyo 8-0 na hapo nyota yake iling'aa. Hakuwahi kupewa kadi katika mechi zote alizocheza. Mwaka 1958 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas. Katika kipindi chote alichocheza hawakuwahi kushinda ubingwa. Ufaransa illitwaa ubingwa baadaye mwaka 1998. Fontaine aliwahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Morocco ambapo aliiongoza timu hiyo katika kufuzu kucheza kombe la dunia. Kama kocha timu yake ya Morocco ilicheza mechi 4. Mwaka 1982 Morocco ilicheza na Zambia na waliifunga 2-0.
    Fontaine mwaka 1958

    5. Pele (Edson Arantes do Nascimento) - Brazil

    Pele mwaka 2017
    Alizaliwa Oktoba 23, 1940. Alicheza mechi 20 ambapo 14 zilikuwa za kombe la dunia na 6 zikiwa za kufuzu kucheza kombe la dunia. Alifunga magoli 18 katika michuano hiyo 12 yakiwa ya kombe la dunia na 6 yakiwa katika hatua za kufuzu. Pele anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji pekee duniani aliyeshuhudia timu yake ya Brazil ikishinda kombe la dunia mara 3 (1958, 1962, 1970) akiwepo katika kikosi cha timu hiyo mara 3 zote. Mwaka 1958 alishinda tuzo ya Hyundai ya mchezaji mdogo wakati ule akiwa na miaka 18 tu. Mwaka 2007 Pele alishinda tuzo ya heshima ya Rais wa FIFA. Katika mechi hizo 20 alizocheza, 18 walishinda, 1 walisuluhu na 1 walifungwa.
    Pele katika enzi zake kwenye soka.


    WACHEZAJI 5 WALIOCHEZA MECHI NYINGI

    1. Luthar Matthaus - Ujerumani

    Matthaus kwa sasa yupo Sky Sport.
    Amezaliwa Machi 21, 1961. Amecheza mechi 36; 25 zikiwa za kombe la dunia, 8 zikiwa za kufuzu michuano hiyo na 3 zikiwa za kombe la mabara. Umaarufu wake ulitokana na mechi ya kombe la dunia 1982 na Chile ambapo waliichapa timu hiyo 4-1. Katika mechi zote 36 alishinda 22, alisuluhu 8 na kufungwa 6. Mwaka 1990 alishinda Ballon d'Or pamoja na kuchukua ubingwa wa dunia na timu yake ya Ujerumani. Mwaka 1991 alikuwa mchezaji bora wa mwaka. Alifunga magoli 10; 6 yakiwa ya kombe la dunia, 3 yakufuzu michuano hiyo na 1 ikiwa kombe la mabara. Amewahi kupewa kadi za njano mara 9. Pia amewahi kua kocha wa timu ya Croatia, kama kocha aliifunga Hungaria magoli 3-0.
    Lothar akibusu kombe la dunia waliposhinda mwaka 1990.

    2. Miroslav Klose - Ujerumani

    Klose akiwa na wanaye baada ya Ujerumani kutwaa kombe la dunia mwaka 2014 dhidi ya Ajentina.
    Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29. Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002. Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil.
    Klose katika kombe la dunia mwaka 2006.

    3. Paulo Maldini - Italia

    Maldin mwaka 2013.
    Alizaliwa Juni 26, 1968. Amecheza mechi 48; 23 zikiwa za kombe la dunia, 23 za kufuzu na 2 zikiwa za kombe la mabara. Alifunga magoli 3 tu katika mechi za kufuzu. Amewahi kupewa kadi za njano mara 3 tu. Katika mechi zote alizocheza 31 walishinda, 13 wakisuluhu na kupoteza 4. Mechi ya kombe la dunia mwaka 1990 wakati Italia ilipoifunga Austria 1-0 ilipelekea nyota yake kung'aa.
    Maldin mwaka 1998 katika robo fainalai ya kombe la dunia.

    4. Uwe Seeler - Ujerumani

    Seeler mwaka 2016
    Alizaliwa Novemba 5, 1936. Amecheza mechi 28; 21 zikiwa za kombe la dunia wakati 7 zikiwa za kufuzu. Amefunga magoli 23; 9 yakiwa ya kombe la dunia na 3 yakiwa ya kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza 19 walishinda, 5 walisuluhu na 4 walifungwa. Nyota ilianza kung'aa katika kombe la dunia 1958 wakati Ujerumani ilipoifunga 3- 1 Ajentina. Hakuwahi kupewa kadi.

    5. Diego Maradona - Ajentina

    Maradona.
    Alizaliwa Oktoba 30, 1960. Alicheza mechi 35; 21 zikiwa za kombe la dunia, 8 zikiwa za kufuzu kombe la dunia na 6 zikiwa za kombe la dunia chini ya miaka 20 (U-20). Maradona alifunga magoli 17; 8 yakiwa ya kombe la dunia, 3 ya kufuzu na 6 kombe la dunia U-20. Katika mechi alizocheza 23 walishinda, 6 walisuluhu na 6 walifungwa. Nyota ya Maradona iling'aa wakati wa michuano ya vijana nchini Japan mwaka 1979 wakati Ajentina ilipoifunga 5-0 Indonesia. Mwaka 1979 alishinda mpira wa dhahabu wa Adidas, FIFA U-20 pamoja na kombe hilo mwaka huo huo. Mwaka 1986 alishinda kiatu cha dhahabu pamoja na kushinda kombe la dunia. Maradona amewahi kuwa kocha wa timu ya taifa lake ambapo mechi 13 zilichelezwa akiwa kocha. Alishinda mechi 8 na kufungwa 5. Umaarufu wake kama kocha ulitokana katika mechi ya kirafiki dhidi ya Venezuela mwaka 2010 ambapo waliichapa timu hiyo 4-0.
    Maradona akinyanyua kombe la dunia mwaka 1986 dhidi ya Ujerumani.


    MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA MTANDAO WA FIFA.

    Comments

    Popular posts from this blog

    SHAIRI: HEKO LIBERIA

    Picha kwa hisani ya Freepik Shairi hili linakuja kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka huu nchini Liberia. Katika hali isiyo ya kawaida George Weah aliyekuwa akitetea nafasi yake ali kubali kusindwa na mpinzani wake Joseph Boakai katika Uchaguzi huo pasipo mvutano na migogoro kama ilivyozoeleka katika mataifa mengi ya bara hili . Kama mshairi niliwiwa kuandika ili kupongeza kitendo hiki cha uungwana kukubali kukabidhi madaraka pasipo mvutano ambao mara nyingi hupelekea umwagaji damu. Karibu katika shairi letu kwa lugha adhimu ya Kiswahili. Shairi: Heko Liberia Mtunzi: Venance Gilbert Mpate Mwaka: 19 Novemba 2023 HEKO LIBERIA Heko Liberia naisifu yenu demokrasia, Wenu ukomavu yote Afrika imeshuhudia, Tupeni maarifa darasani tupate kujifunzia, Afrika matokeo mshindani hawezi kuridhia, Uchaguzi mtawala hakubali kupoteza felia, Ninyi metuonesha mtawala aweza kuwa felia, Mpinzani akashika dola imani ikaendelea, Heko Liberia naisifu yenu demokrasia. Mtawala aku...

    BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

    Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

    WAHAMIAJI 239 WAHOFIWA KUZAMA KATIKA AJALI YA MELI WAKITOKEA LIBYA

    Wahamiaji 239 wamehofiwa kuzama katika ajali ya meli wakitokea nchini Libya. Hii ni kwa mujibu wa habari kutoka shirika la Wakimbizi UNHCR. Msemaji wa UNHCR mjini Roma Italia amesema kuwa taarifa hizo zimethibitishwa na manusura wa ajali walipofikishwa katika ukingo wa bahari katika kisiwa cha Lampedusa. Mpaka sasa hakuna ambaye amekwishapatikana katika hao 239. Sami alisema kuwa watu 31 wamenusurika katika ajali za meli mbili zilizopata ajali baharini kufuatia dhoruba kali. Walisema kuwa watu 29 walinusurika katika meli ya kwanza huku wengine 120 hawajulikani walipo. Katika jitihada za kuokoa watu, wanawake 2 waliokuwa wakiogelea kujinusuru waliwambia waokoaji kuwa watu hao 120 walikufa katika meli hiyo. Katika matukio yote mawili, wengi wa wahamiaji hao wanaonekana kuwa ni raia kutoka eneo la Jangwa la Sahara. Leonard Doyle, msemaji mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) amesema kuwa watu 4,220 wamepoteza maisha katika mwaka huu 2016 kwenye ajali za meli katik...

    CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

    Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

    ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

    Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

    DEADMEN SPEAKS: A POEM

    Image generated with OpenArt AI tool It has been longtime since I published my poems on this platform, today I'm humbly inviting you to our section of poems. As you enjoy reciting this creativity, please don't forget to leave your comment after this post or writing via my contacts after this poem. Poem: Deadmen Speaks Poet: Venance Gilbert Composition: July 30, 2023 DEADMEN SPEAKS: A POEM BY VENANCE GILBERT I heard deadmen tells no tale but these ones do They are burdened with a lots Weak folks who talks nothing just talking in mind in the streets I say so because one of them is me I speak for deadmen. Six years with no stable duties to perform while responsibilities have taken-off This week this job next week none and I have to survive regardless But how without money How can I count money without job? I speak for deadmen. While I'm enjoying my jobless survival Executive wants to collect from my pocket I have to pay tariff to buy light tariff to withdraw my hard-earned sav...

    MFAHAMU WOLE SOYINKA GWIJI WA FASIHI YA KIAFRIKA MWENYE TUZO YA NOBEL KATIKA FASIHI 1986

    Picha kwa hisani ya Oasis Magazine Bila shaka jina la Wole Soyinka sio geni masikioni mwako kwa sababu wengi wetu tumesoma tamthiliya (play) yake ya The Lion and The Jewel sekondari hasa kidato cha tatu na cha nne na The Trials of Brother Jero kwa wale waliosoma miaka ya nyuma. Hapa nitamzungumzia Wole Soyinka, mwafrika wa kwanza kushinda tuzo ya Nobel katika fasihi. Haya ni mambo ambayo huwezi kufundishwa kwenye mitaala ya shuleni, hivyo unapaswa kuyafahamu nje ya mtaala wa shule kwa muda wako mwenyewe. Awali ya yote, ni kwamba wasifu huu niliuandika kwa mara ya kwanza katika mtandao wa Twitter Julai 13, 2020 kabla sijaamua kuuleta hapa. MAISHA YA MWANZO Soyinka alizaliwa Julai 13, 1934 huko Abeokuta jirani na Ibadan nchini Naijeria. Majina yake halisi ni Akinwande Oluwole Babatunde Soyinka lakini anafahamika sana kama Wole Soyinka. Alisoma Fasihi, Ibadan. Mwaka 1954 alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds nchini Uingereza mara baada ya kumaliza masomo yake katika Chuo cha Serikali, Ibadan...

    UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU GOOGLE BARD

    Nembo (logo) ya Google Bard Kufuatia mafanikio ya robotisogozi ya OpenAI ambayo ni ChatGPT, Google ilitoa robotisogozi yake ya akili bandia, Bard. Kwa vile inapatikana sehemu kubwa haya ndiyo unayohitaji kufahamu kuihusu Bard lakini kabla sijaendelea nikufahamishe vifupisho vya maneno yatayotumika katika makala hii: AI - Artificial Intelligence ambayo ni Akili Bandia. LaMDA - Language Model for Dialogue Applications ambao ni Mfumo wa Lugha kwa Mazungumzo na Matumizi. LLM - Large Language Model ambao ni Mfumo Mkubwa wa Lugha. PALM (PaLM) - Pathways Language Model ambavyo ni vigezo bilioni 540 va kigezo cha lugha kubwa modeli iliyotengenezwa na Google AI Bard ni huduma ya Google ya majaribio ya mazungumzo ya akili bandia. Inakusudiwa kufanya kazi sawa na ChatGPT huku tofauti kubwa ni kwamba huduma ya Google itatoa habari zake kutoka katika wavuti. Picha ya skrini: Venance Gilbert  Kama vile gumzo nyingi za akili bandia, Bard anaweza kuandika msimbo (code), kuj...

    TANGAZO LA AJIRA 289 ZA WATUMISHI KADA ZA AFYA KUTOKA WIZARA YA AFYA

    Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/” B”/75 cha tarehe 04 Mei, 2023 na Kumb. Na FA.97/128/01”B”/78 cha tarehe 09 Agosti, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 289 za Kada za Afya. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz . Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika. Unaweza kutazama tangazo hilo kwa kubofya  HAPA  ama kwa kulidownload moja kwa moja kwa kubofya  HAPA  ama kwa kusoma hapa chini nafasi zilizotangazwa: 1. Daktari wa Meno Daraja la II – TGHS E (NAFASI 3) SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa waliohitimu na kufaulu Kidato cha Nne/Sita/Stashahada, wenye Shahada ya Udaktari/Udaktari wa Meno ku...

    VALENTINE DAY'S QUOTES

    1. Today is Valentine's Day - or, as men like to call it, Extortion Day! -Jay Leno  2. We are most alive when we're in love. -John Updike 3. So, fall asleep love, loved by me... for I know love, I am loved by thee. -Robert Browning 4. Each time you love, love as deeply as if it were forever. -Audre Lorde 5. I love bringing roses to a woman when she least expects it. -Esai Morales 6. Soul meets soul on lovers' lips. -Percy Bysshe Shelley 7. I'd kiss a frog even if there was no promise of a Prince Charming popping out of it. I love frogs. -Cameron Diaz 8. It is the passion that is in a kiss that gives to it its sweetness; it is the affection in a kiss that sanctifies it. -Christian Nestell Bovee 9. Romance is thinking about your significant other, when you are supposed to be thinking about something else. -Nicholas Sparks 10. Harmony is pure love, for love is a concerto. -Lope de Vega 11. They invented hugs to let people know you love them without...