Skip to main content

WAFUNGAJI BORA NA WALIOCHEZA MECHI NYINGI KATIKA KOMBE LA DUNIA 1930-2014

WAFUNGAJI 5 WA MUDA WOTE

1. Miroslav Klose - Ujerumani

Klose wakati wa droo ya kombe la dunia mwaka jana 2017.
Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29.  Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002. Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil.
Klose wakati wa mechi ya robo fainali kati ya Ujerumani na Ufaransa katika dimba la Marakana Rio de Jeneiro Julai 4, 2014.


2. Ronaldo de Lima - Brazil

Ronaldo de Lima alipokabidhiwa tuzo ya Hall of Fame nchini Italia mwaka 2016
Amezaliwa Septemba 22, 1976. Amecheza mechi 45; 19 za kombe la dunia, 15 za kufuzu kombe la dunia, 5 za kombe la mabara na 6 za Olimpiki. Katika mechi hizi alifunga jumla ya magoli 34; 15 ya kombe la dunia, 10 ya kufuzu michuano hii, 4 ya kombe la mabara na 5 ya Olimpiki. Akiwa katika timu ya Brazil walishinda mechi 31, suluhu 8 na kufungwa mechi 6. Umaarufu wake ulianza kuonekana katika michuano ya Olympic mwaka 1996 iliyofanyika Atlanta dhidi ya Japan. Brazil iliifunga Japan 1-0. Amewahi kupewa kadi za njano mara 4 tu katika michuano yote. Alipokuwa Brazil walitwaa kombe la dunia mwaka 1994 na 2002. Mwaka 2002 ndiye aliyekua mchezaji bora wa michuano ya kombe la dunia FIFA. Mwaka 1997 akiwa na timu yake walishinda kombe la dunia la mabara. Ronaldo amewahi kushinda tuzo ya mpira wa dhahabu ya Adidas kama mchezaji bora. Mwaka 2002 pia alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas. Amewahi kushinda tuzo ya Balloon d'Or ya Ufransa mwaka 1997 na 2002.
Ronaldo enzi za Brazil.


    3. Gerd Mueller - Ujerumani

    Mueller alipokua kocha wa Bayern Munich  II
    Alizaliwa Novemba 3, 1945. Amecheza mechi 19 na timu yake ya Ujerumani; 13 zikiwa za kombe la dunia na 6 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi hizo alizokuwepo walishinda mechi 16, suluhu 1 na kufungwa 2. Ana magoli 23; 14 yakiwa ya kombe la dunia la 9 yakiwa ya kufuzu michuano hiyo. Amewahi kupewa kadi za njano 2 tu katika michuano ya kombe la dunia. Mwaka 1970 alishinda tuzo mbili; kiatu cha dhahabu cha Adidas pamoja tuzo ya Ballon d'Or. Pia ni miongoni mwa waliokuwepo katika kikosi cha Ujerumani kilichotwaa kombe la dunia mwaka 1974.
    Gerd Mueller mwaka 1974 waliposhinda fainali ya kombe la dunia.

    4. Just Fontaine - Ufaransa

    Fountaine mwaka 2017
    Alizaliwa Agosti 18, 1933. Yeye alicheza 8 tu 6 zikiwa zakombe la dunia na 2 zikiwa za kufuzu michuano hiyo, katika mechi hizi alifunga magoli 16; katika hayo 13 yalikua ya kombe la dunia na 3 yalikuwa ya mechi za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza 6 walishinda na hawakusuluhu ila walipoteza nchi 2 tu. Alionekana katika kombe la dunia kwenye mechi ya kati ya Ufaransa na Luxembourg ambapo waliifunga nchi hiyo 8-0 na hapo nyota yake iling'aa. Hakuwahi kupewa kadi katika mechi zote alizocheza. Mwaka 1958 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas. Katika kipindi chote alichocheza hawakuwahi kushinda ubingwa. Ufaransa illitwaa ubingwa baadaye mwaka 1998. Fontaine aliwahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Morocco ambapo aliiongoza timu hiyo katika kufuzu kucheza kombe la dunia. Kama kocha timu yake ya Morocco ilicheza mechi 4. Mwaka 1982 Morocco ilicheza na Zambia na waliifunga 2-0.
    Fontaine mwaka 1958

    5. Pele (Edson Arantes do Nascimento) - Brazil

    Pele mwaka 2017
    Alizaliwa Oktoba 23, 1940. Alicheza mechi 20 ambapo 14 zilikuwa za kombe la dunia na 6 zikiwa za kufuzu kucheza kombe la dunia. Alifunga magoli 18 katika michuano hiyo 12 yakiwa ya kombe la dunia na 6 yakiwa katika hatua za kufuzu. Pele anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji pekee duniani aliyeshuhudia timu yake ya Brazil ikishinda kombe la dunia mara 3 (1958, 1962, 1970) akiwepo katika kikosi cha timu hiyo mara 3 zote. Mwaka 1958 alishinda tuzo ya Hyundai ya mchezaji mdogo wakati ule akiwa na miaka 18 tu. Mwaka 2007 Pele alishinda tuzo ya heshima ya Rais wa FIFA. Katika mechi hizo 20 alizocheza, 18 walishinda, 1 walisuluhu na 1 walifungwa.
    Pele katika enzi zake kwenye soka.


    WACHEZAJI 5 WALIOCHEZA MECHI NYINGI

    1. Luthar Matthaus - Ujerumani

    Matthaus kwa sasa yupo Sky Sport.
    Amezaliwa Machi 21, 1961. Amecheza mechi 36; 25 zikiwa za kombe la dunia, 8 zikiwa za kufuzu michuano hiyo na 3 zikiwa za kombe la mabara. Umaarufu wake ulitokana na mechi ya kombe la dunia 1982 na Chile ambapo waliichapa timu hiyo 4-1. Katika mechi zote 36 alishinda 22, alisuluhu 8 na kufungwa 6. Mwaka 1990 alishinda Ballon d'Or pamoja na kuchukua ubingwa wa dunia na timu yake ya Ujerumani. Mwaka 1991 alikuwa mchezaji bora wa mwaka. Alifunga magoli 10; 6 yakiwa ya kombe la dunia, 3 yakufuzu michuano hiyo na 1 ikiwa kombe la mabara. Amewahi kupewa kadi za njano mara 9. Pia amewahi kua kocha wa timu ya Croatia, kama kocha aliifunga Hungaria magoli 3-0.
    Lothar akibusu kombe la dunia waliposhinda mwaka 1990.

    2. Miroslav Klose - Ujerumani

    Klose akiwa na wanaye baada ya Ujerumani kutwaa kombe la dunia mwaka 2014 dhidi ya Ajentina.
    Amezaliwa Juni 9, 1978. Ana jumla ya magoli 16 katika michuano ya kombe la dunia na magoli 23 katika mechi za kufuzu, hii inafanya jumla ya magoli kuwa 29. Aling'aa katika mechi ya awali kufuzu michuano hii ambapo Ujerumani iliichapa Abania 2-1 mwaka 2002. Amecheza mechi 43; 24 zikiwa za kombe la dunia na 19 zikiwa za kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza na timu yake wameshinda mechi 30 wamesuluhu mechi 8 na kupoteza mechi 5. Ana kadi 1 ya njano katika michuano ya FIFA na kadi 2 za njano katika hatua ya makundi kufuzu kucheza kombe la dunia. Mwaka 2006 alishinda kiatu cha dhahabu cha Adidas na mwaka 2014 alikuwepo katika kikosi cha Ujerumani walipotwaa kombe la dunia katika fainali dhidi ya Ajentina nchina Brazil.
    Klose katika kombe la dunia mwaka 2006.

    3. Paulo Maldini - Italia

    Maldin mwaka 2013.
    Alizaliwa Juni 26, 1968. Amecheza mechi 48; 23 zikiwa za kombe la dunia, 23 za kufuzu na 2 zikiwa za kombe la mabara. Alifunga magoli 3 tu katika mechi za kufuzu. Amewahi kupewa kadi za njano mara 3 tu. Katika mechi zote alizocheza 31 walishinda, 13 wakisuluhu na kupoteza 4. Mechi ya kombe la dunia mwaka 1990 wakati Italia ilipoifunga Austria 1-0 ilipelekea nyota yake kung'aa.
    Maldin mwaka 1998 katika robo fainalai ya kombe la dunia.

    4. Uwe Seeler - Ujerumani

    Seeler mwaka 2016
    Alizaliwa Novemba 5, 1936. Amecheza mechi 28; 21 zikiwa za kombe la dunia wakati 7 zikiwa za kufuzu. Amefunga magoli 23; 9 yakiwa ya kombe la dunia na 3 yakiwa ya kufuzu michuano hiyo. Katika mechi alizocheza 19 walishinda, 5 walisuluhu na 4 walifungwa. Nyota ilianza kung'aa katika kombe la dunia 1958 wakati Ujerumani ilipoifunga 3- 1 Ajentina. Hakuwahi kupewa kadi.

    5. Diego Maradona - Ajentina

    Maradona.
    Alizaliwa Oktoba 30, 1960. Alicheza mechi 35; 21 zikiwa za kombe la dunia, 8 zikiwa za kufuzu kombe la dunia na 6 zikiwa za kombe la dunia chini ya miaka 20 (U-20). Maradona alifunga magoli 17; 8 yakiwa ya kombe la dunia, 3 ya kufuzu na 6 kombe la dunia U-20. Katika mechi alizocheza 23 walishinda, 6 walisuluhu na 6 walifungwa. Nyota ya Maradona iling'aa wakati wa michuano ya vijana nchini Japan mwaka 1979 wakati Ajentina ilipoifunga 5-0 Indonesia. Mwaka 1979 alishinda mpira wa dhahabu wa Adidas, FIFA U-20 pamoja na kombe hilo mwaka huo huo. Mwaka 1986 alishinda kiatu cha dhahabu pamoja na kushinda kombe la dunia. Maradona amewahi kuwa kocha wa timu ya taifa lake ambapo mechi 13 zilichelezwa akiwa kocha. Alishinda mechi 8 na kufungwa 5. Umaarufu wake kama kocha ulitokana katika mechi ya kirafiki dhidi ya Venezuela mwaka 2010 ambapo waliichapa timu hiyo 4-0.
    Maradona akinyanyua kombe la dunia mwaka 1986 dhidi ya Ujerumani.


    MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA MTANDAO WA FIFA.

    Comments

    Popular posts from this blog

    HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

    KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

    WAFAHAMU MATAJIRI 10 WA TANZANIA MWAKA 2018

    10. YUSUF MANJI Manji ni mmiliki wa mali zisizohamishika hasa majengo kwa ajili ya makazi ya watu na biashara. Pia ni muanzilishi wa kampuni ya Quality Group of Companies. Anajihusisha pia na vipuli vya magari. Haya yamemfanya kua miongoni mwa matajiri wa juu zaidi nchini. 9. FIDA RASHID Fida ni muanzilishi wa kampuni ya Africarrier Group. Hii ni kampuni inayohusika na magari yaliyotumika. Pia kampuni hii inahusika na usambazaji wa magali ya kampuni ya Eicher na Golden Dragon hapa nchini. Hii imefanya kampuni yake kufanya vyema sana katika idara hii. Fida pia ni mmiliki wa mali zisizohamishika pamoja na majengo kama Zahra Tower na Raha Tower. Amekua mjasiriamali anayetengeneza zaidi mazingira mazuri ya biashara zake kama wafanyavyo wengine. 8. GHALIB SAID MOHAMMED Ghalib Mohammed alikua akifanya biashara ya korosho hapo awali na biashara nyingine akishirikiana na baba yake. Baadaye Ghalib Said aliamua kuanzisha kampuni yake na kuiita GSM Group ambayo inajihusisha...

    BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

    Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

    CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

    Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

    ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

    Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

    WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

    Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

    WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

    Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

    ZIFAHAMU TEKNOLOJIA 7 ZITAZOKAZOKUZA MAENDELEO YA MAJIJI MAKUBWA DUNIANI

    Fikiria ulikuwa unafanya kazi katika taasisi ya maendeleo na kupunguza umasikini mwanzoni mwa miaka ya 1990. Mwandishi wa makala hii, Abhas Jha anasema yeye aliwahi kufanya kazi zama hizi. Anasema kipindi hicho kulikuwa na tovuti moja tu iliyokuwepo duniani mpaka kufikia Agosti mwaka 1991 (leo kuna zaidi ya tovuti bilioni 1.5 duniani kote). Anasema kipindi hicho simu za mkononi zilikuwa ghali sana, chache na zilikuwa nzito na za kishamba sana ukilinganisha na hizi za sasa. Ni watu wachache wangetazamia kuhusu hali iliyopo nchini India kwa sasa kwamba kungekua na idadi kubwa ya simu za mkononi kuilko idadi ya vyoo. Bill Gates aliwahi kusema "tunayapa uzito sana mabadiliko ambayo yatatokea ndani ya kipindi cha muda mfupi sana na kuyapuuza yale yaliyotokea kwa muda mrefu sana". Teknolojia inakua kwa kasi sana na kufanya na mabadiliko makubwa sana kwenye majiji ili kufikisha huduma kwa jamii. Teknolojia inafanya hivi ili sio tu kufikisha huduma haraka kwa wateja bali pia kuk...

    HEZBOLLAH YATAJA SABABU YA KUUAWA KIONGOZI WAO

     Kundi la Waislamu wa madhehebu ya Kishia la Hezbollah nchini Lebanon limetaja sababu ya kifo cha kiongozi wake wa ngazi ya juu wa kijeshi, Mustafa Badreddine kuwa kimetokana na makombora ya mizinga liliofanyika karibu na uwanja wa ndege wa Damascus nchini Syria.  Hezbollah lilitangaza  kifo cha Badreddine hapo jana na alifanyiwa mazishi ya kijeshi siku hiyo hiyo katika eneo la ngome la kundi hilo huko kusini mwa Beirut. Taarifa ya kundi hilo imesema mashambulizi hayo yamefanywa na kundi linaloitwa Takfiri. Takfiri ni neno linalotumiwa na kundi hilo la Kisunni kwa kuonesha msimamo mkali, kundi lenye kujihami na silaha, lililo na itikadi kali. Badreddine alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa kundi la Hezbollah walioshutumiwa mwaka 2005 kuhusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanon Rafik Hariri. Chanzo: Deutsche Welle (DW)

    GWIJI WA RHUMBA TABU LEY AZIKWA KINSHASA

      Mazishi ya Gwiji wa Rumba nchini DRC, Tabu Ley Rochereau yalifanyika Jumatatu mjini Kinshasa.Mwili wake ukiwa ndani ya jeneza la rangi nyeupe lililotandwa bendera ya Jamhuri ya Congo, ulilazwa kwenye majengo ya Bunge ambako watu zaidi ya elfu kumi walifika kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Pascal Sinamoyi Tabu Ley.Viongozi wa serikali ya DRC walihudhuria mazishi hayo huku waakilishi kutoka nchi jirani ya Congo Brazaville pia wakihudhuria mazishi hayo. Tabu Ley alifariki mwezi Novemba akiwa na umri wa miaka 76 akipokea matibabu nchini Ubelgiji. Aidha gwiji huyo alikiri rasmi kwamba ana watoto 49. Lakini mwandishi wa BBC katika mazishi hayo Lubunga Byaombe, alisema kuwa zaidi ya watu 80 walijitokeza na kusema kuwa baba yao ni mwanamuziki huyo na kwamba wengi wao walitaka kupewa nafasi kuzungumza katika mazishi hayo. Tabu ley aliyejulikana kama mfalme wa muziki wa rumba aliaga dunia mwezi uliopita mjini Brussels, Ubelgiji akiwa na miaka sabini na sita.Wengi walimkumbuk...