Skip to main content

MOHAMMED SALAH: ILIKUAJE AKAIMARIKA HARAKA? MAJIBU HAYA HAPA

Mohammed Salah
Huku wachezaji wakisherehekea kwa fujo baada 4-0 dhidi ya ENPPI, kocha Said Al Shesheni aliangalia upande mmoja na kugundua kwamba mchezaji mmoja wa kikosi cha al-Mokawloon wa kikosi cha wachezaji wasiozidi umri wa miaka 16 hakuwa akifurahia michuano iliokuwa Cairo. Alikuwa akibubujikwa na machozi kwamba jina lake halikuwa katika orodha ya wafungaji mabao. Akicheza kama beki wa kushoto ilikuwa vigumu kuchukua jukumu kubwa kama alivyotaka.
Akiwa mzaliwa wa eneo la Nagrig, kijiji kimoja kilichopo kilomita 130 Kaskazini mwa mji mkuu wa Misri, mchezaji huyo alilazimika kupitia tatizo la kusafiri kwa saa tisa kila siku mara nyingine akilazimika kutumia mabasi 10, ili kuweza kufika mazoezini mbali na kushiriki mechi.
Na baada ya kufurahishwa na ari ya kijana huyo Al Sheheni alimpatia fursa na kumpeleka safu ya mbele. Tangu wakati huo Mohammed Salah hajarudi nyuma tena.
Kijana katika uwanja wa Mo salah
Mchezaji huyo wa Liverpool alilazimika kulipia uwanja mpya katika shule yake ya zamani.

Habari hiyo ni jibu kwa swali ambalo limekuwa katika fikra za mashabiki wa soka duniani: Mchezaji ambaye hakuwa na athari yoyote kimchezo katika ligi kuu za Ulaya mara moja amekuwa mfungaji bora akilinganishwa na Lionel Messi na Christiano Ronaldo.
Katika soka inasaidia wakati mchezaji anapojikuta katika eneo analohitajika kuwa na katika wakati ufaao. Lakini ni watu wachache waliokuwa na hilo wakati Liverpool ilipotangaza usajili wa Salah kutoka klabu ya Italia ya Rome mwaka uliopita .
Kitita cha $55.7m kinaonekana kuwa cha juu kwa mchezaji ambaye alikuwa amefeli kuonyesha umahiri wake katika soka ya Uingereza baada ya kuhudumu kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa Chelsea 2015.
Pia ni muhimu kuona kwamba Misri sio timu yenye umaarufu mkubwa katika soka duniani, ijapokuwa ina umaarufu mkubwa barani Afrika, baada ya kushinda taji la kombe la Afrika mara saba.
Lakini The Pharaoh wamecheza katika michuano miwili ya kombe la dunia 1934 na 1990 na hadi Salah alipoimarika, ilikuwa rahisi kutajwa kwa kuwa kipa Essam El-Hadary yuko katika harakati za kuwa mchezaji mkongwe zaidi kushirki katika kombe la dunia, wakati Misri iliporejea katika kinyang'anyiro hicho nchini Urusi.
Timu ya taifa ya Misri
Misri imeshiriki katika michuano miwili pekee ya kombe la dunia lakini wamefaulu kushiriki Urusi 2018

Ni nini kilichofanyika kimakosa kwa Salah mapema alipocheza Uingereza? Kwanza Salah alishiriki katika ligi ya Switzerland, ambayo haina ushindani mkubwa kama ile ya Uingereza.
Akiwa Chelsea pia alikabiliwa na ushindani mkubwa kutoka kwa wachezaji walioimarika na hakupata fursa za kutosha kuonyesha umahiri wake.
Raia huyo wa Misri alicheza mechi 19 kwa klabu hiyo ya London huku akianzishwa katika mechi tisa pekee. Ni mara mbili pekee alipocheza dakika zote 90. Salah baadaye alipelekwa kwa mkopo kwa vilabu vya Italia kabla ya kusainiwa na Roma kwa msimu wa 2015/16
Ni wakati huo ambapo Salah alionyesha umahiri wake na kufunga mabao 34 katika misimu miwili kabla ya kuelekea Liverpool.
Image result for mohamed salah with mourinho at chelsea
Salah hakuweza kufanya vizuri chini ya usimamizi wa Mourinho akiwa Chelsea: Alicheza mechi 19 na kufunga mabao 2 pekee.
"Alikuwa mtoto alipowasili Chelsea na Chelsea ilikuwa na kikosi kizuri hivyo basi ilikuwa vigumu'', alisema mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp akizungumza na runinga ya Ujerumani wiki hii.
"Nadhani sote lazima tukubaliane kwamba Jose Mourinho ni kocha mzuri kwa hivyo mara nyengine mambo huwa hivyo. Kwa hivyo iwapo haiwezekani jiondoe ujaribu tena na hivyo ndivyo ilivyokuwa na Mohamed."
Katika ziara ya hivi karibuni Anfield, Mourinho, ambaye sasa ni mkufunzi wa Manchester United alionekana akimkumbatia raia huyo wa Misri.
Na mahojiano na ESPN Brasil yaliorushwa hewani Jumapili iliopita, raia huyo wa Ureno alizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na mchezaji huyo.
''Ni mimi ndiye niliyemsaini Salah na uamuzi wa kumuuza haukuwa wangu, bali ulikuwa wa Chelsea''.
''Ni mtu mzuri , lakini alikuwa mdogo na hakuwa amejiandaa kimaungo na kifikra wakati alipwasili. Pia alipata utamaduni tofauti. Nafurahi sana kumuona anaendelea vyema, hususan kwa sababu hajafunga dhidi ya United'', alifanya mzaha.
Image result for mohamed salah with klopp
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp akimkumbatia Mohammed Salah
Inawezekana kwamba magoli aliyofunga katika msimu wa 2017/18 yalipita kiwango ambacho mchezaji huyo alikuwa ametaka kuafikia. Katika mechi 48 alizochezea Liverpool katika mashindano yote, raia huyo wa Misri alifunga mabao 43 na kusaidia pasi za mabao 15.
Amekuwa nyota katika kombe la vilabu bingwa Ulaya ambapo ameisaidia Liverpool kukaribia kufika fainali ya kombe hilo kwa mara ya kwanza tangu 2007.
Raia huyo wa Misri ni baraka kwa aina ya mchezo wa Klopp kwa kasi na mashambulio.
Mbali na mafanikio yake, Salah anaweza kufanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza wa Afrika kushinda taji la mfungaji bora Ulaya, taji analokabidhiwa mfungaji bora katika ligi ya Ulaya.
Na msimu wa Salah hautakamilika katika wikendi ya mwisho ya ligi kuu ya Uingerza. Timu ya taifa imefanikiwa kufuzu katika kombe la dunia la 2018 ikiwa ni mara kwanza katika kipindi cha miaka 28 baada ya kampeni ya kuwania kufuzu ambapo Salah alifunga mabao matano kati ya manane huku akitoa usaidizi wa mabao mawili.
Ushujaa wake ulihusisha penalti ya dakika 94 dhidi ya Congo ambayo ilikamilisha kufuzu kwa taifa hilo katika kombe la dunia .
Mo Salah akiichezea Egypt
Salah alifunga mabao matano kati ya magoli ya Misri katika kombe la kombe la dunia.
Na kudhania kwamba kuimarika kwake kulianza kwa bahati. Mnamo mwezi Machi 2012, soka la Misri lilikuwa limedorora: ligi ya taifa hilo ilisitishwa kutokana na janga la uwanja wa Port Said - maandamano ambayo mapema takriban watu 70 walifariki huku wengine 500 wakijeruhiwa.
Huku wakitafuta kushiriki katika mechi kwa maandalizi ya michezo ya Olimpiki mjini London, timu hiyo ya Misri yenye wachezaji wasiozidi umri ya miaka 23 walipanga mechi za kirafiki hidi ya vilabu vya Ulaya.
Mojawapo ni klabu ya Uswizi ya Basel, ambaye rais wake, Bernhard Heusler, alimsajili Salah hapo kwa hapo.
"Kulikuwa na baridi kali lakini alionyesha mchezo mzuri. Alicheza kipindi cha pili pekee lakini sijaona mchezaji mwenye kasi katika maisha yangu yote'', alisema Heusler.
Wachezaji wenza wa Basel wanakumbuka kwamba Salah hakuchezshwa mara moja. Katika mwaka wake wa kwanza katika klabu hiyo mchezaji huyo alitumiwa kama mchezaji wa ziada na ni katika mechi 10 pekee kati ya 29 ambapo alicheza kwa zaidi ya saa moja.
Mchezaji mwenza Philipp Degen, aliambia Sky Sports habari kuhusu Salah alivyomshangaza kila mtu baada ya kufunga bao la ushindi dhidi ya Chelsea katika mechi ya kombe la vilabu bingwa.
Salah akiichezea Basel
Salah alijiunga na Basel mwaka 2012 baada ya kucheza kipindi kimoja pekee ya mechi dhidi ya timu ya Usiwzi
"Tulijaribu kumpa hongera lakini hakukubali. Anasema kuwa alipiga nje mikwaju sita na ni wa saba tu pekee kwa kuwa klabu ilimuamini. Umaruufu wake pia unatokana na kuwa mfuasi mkuu wa dini ya Kiislamu.
Anapendwa sana nchini Misri wakati ambapo taifa hilo limegawanyika katika misingi ya kisiasa ilioanzishwa mika michache iliopita na maandamano ya Uarabuni na mapinduzi ya 2013, lakini Salah anapenda mizizi yake.



Amelipia ujenzi wa shule na hospitali na kuweka jina lake katika mashirika ya hisani ikiwemo kuchangisha $280,000 kwa hazina ya serikali inayolenga kuimarisha kiuchumi familia za Wamisri masikini.
Picha ya Mo Salah mjini Cairo
Mchezaji huyo ni shujaa wa taifa lake la Misri.
Utata unaozunguka jina la Salah unashirikisha madai kwamba alikataa kusalimiana na wachezaji kutoka klabu ya Israel ya Maccabi Tel-Aviv katika mechi dhidi ya Basel mwaka 2013 - alienda kubadili viatu vyake kabla ya mechi kuanza wakati huo raia wengi wa Misri walikuwa wamepinga vitendo vyake na hata kumtaka mchezaji huyo kutoshirikishwa katika mechi ya ugenini ya Israel.
Hata hivyo mbali na kuzomewa na mashabiki wa Maccabi Salah alicheza mechi ya ugenini na kufanikiwa kufunga bao.
Wiki iliopita baada ya raia huyo wa Misri kuisaidia Liverpool kushinda 5-2 dhidi ya Roma katika kombe la vilabu bingwa, Waziri wa Ulinzi Avigdor Lieberman alituma ujumbe katika mtandao wa Twitter kwamba atampigia mkuu wa utumishi wa umma kumsaini Mohammed Salah kwa mkataba wa kudumu na jeshi la Israel.

Chanzo: BBC
Picha: Getty Images

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

FRIENDSHIP QUOTES OF THE DAY MAY 26, 2018

Today I invite you to read these quotes of the day. Enjoy your day. 1.  One of the most beautiful qualities of true friendship is to understand and to be understood. ~Lucius Annaeus Seneca. 2.  Walking with a friend in the dark is better than walking alone in the light. ~Helen Keller. 3.  There is nothing on this earth more to be prized than true friendship. ~Thomas Aquinas. 4.  My best friend is the one who brings out the best in me. ~Henry Ford. 5.  It is one of the blessings of old friends that you can afford to be stupid with them. ~Ralph Waldo Emerson. 6.  The strong bond of friendship is not always a balanced equation; friendship is not always about giving and taking in equal shares. Instead, friendship is grounded in a feeling that you know exactly who will be there for you when you need something, no matter what or when. ~Simon Sinek. 7.  A friend is someone who gives you total freedom to be yourself. ~Jim Mo...

IDADI YA WATU WALIOFARIKI UGANDA YAFIKIA 33

Moto mkubwa uliowaka baada yaajali mbaya ya barabarani iliohusisha lori la mafuta, umewauwa takriban watu 33 mjini kampala Uganda. Watu wengine 30 wanadaiwa kujeruhiwa vibaya kufuatia tukiohilo. Maafisa wa polisi wanasema kuwa kati ya waliofariki ni raia waliokuwa wanakimbilia eneo hilo la mkasa kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwa lori hilo. maafisa wa serikali walikuwa katika harakati za kutambua mili ya waliofariki baada ya wengi wao kuchomeka vibaya. Idara ya polisi imesema kuwa waliofariki waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.

VITAMBULISHO VYA URAIA KUVUKIA MIPAKA KENYA, RWANDA NA UGANDA

Wananchi wa mataifa ya Rwanda, Uganda na Kenya wamepokea kwa shangwe kuanza kwa mpango wa kutumiwa kwa vitambulisho vya uraia kama cheti cha kuwaruhusu kuvuka mpaka na kuingia moja wapo wa nchi hizo.Mpango huu wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kusafiria katika nchi hizo tatu umeanza kutumiwa rasmi tarahe Mosi Januari 2014, kufuatia makubaliano kati ya viongozi wa mataifa hayo.Mpango wenyewe unatokana na makubaliano kati ya viongozi wa nchi tatu waliofikia wakati wa mkutano uliofanyika nchini Uganda mwezi Juni mwaka jana.Pia mpango huu unalenga kurahisisha usafiri wa watu wa jumuiya katika mataifa wanachama kama awamu ya pili ya ushirikiano kati ya mataifa wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.Hata hivyo siku moja tu baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kuwaruhusu raia wa nchini tatu, Uganda, Kenya na Rwanda kuvuka mpaka na kuingia mojawapo ya nchi hizo sasa inaonekana mpango huo huenda ukawanufaisha watu wachache peke yake.Sio ...

CHANGES QUOTES OF THE DAY MAY 23, 2018

Hello dear reader, welcome once again. Today I have gathered the quotes concerning changes in life. I should not write more since I am not not the speaker in this category, take your time to dive in and become intellectual with full equipped knowledge from the great men of history Remember, someday it might be you. Do not rely on inspiration from friends while you are needy, VENANCE BLOG is here for you. Welcome all the time by searching Quotes. Now proceed. 1. Every great dream begins with a dreamer. Always remember, you have within you the strength, the patience, and the passion to reach for the stars to change the world. ~Harriet Tubman. 2. Change your thoughts and you change your world. ~Norman Vincent Peale. 3.  If you don't like something, change it. If you can't change it, change your attitude. ~Maya Angelou 4.  Change will not come if we wait for some other person or some other time. We are the ones we've been waiting for. We are the change that...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...