Skip to main content

UNAYOPASWA KUFAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA YA 5G

Logo rasmi ya teknolojia ya mtandao wa 5G.
Katika teknolojia za mitandao ya simu iliyopita kulikua na suluhisho la matumizi ya sauti pekee katika mtandao wa 1G, sauti na jumbe za maneno katika mtandao wa 2G, kuliongezeka kufungua tovuti mbalimbali katika mtandao wa 3G na kuongezeka kwa kasi zaidi ya mtandao na kutazama video za moja kwa moja katika mtandao wa 4G. Mabadiliko kutoka 4G kwenda 5G yatasaidia si watumiaji wa mtandao tu bali pia wamiliki wa viwanda mbalimbali.

Mabadiliko katika teknolojia ya simu na mtandao.

Kwa teknolojia ya mtandao huu wa simu za mkononi kasi ya mtandao inatarajiwa kuwa mara 8 ya hii ya sasa mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2023 huku kukiwa na uhitaji wa teknolojia imara, viwango vikubwa vya data na wigo mpana wa matumizi ya mtandao huu tofauti na hii iliyopo sasa (4G). Vitumizi vipya kama vile 4K/8K vya kutazamia video mtandaoni moja kwa moja, uwezo wa mtandao ambao umeongezwa karibia na uhalisia pamoja matumizi ya data ambao kwa sasa yanachipukia kwa kasi, yote haya yatahitaji vipimo vikubwa vya data, uwezo wa hali ya juu, ulinzi pamoja na utulivu wa kusafirisha data katika mtandao. Haya yote ni miongoni mwa yatakayokuwa katika mtandao wa 5G. Mtandao huu utaleta fursa mpya kwa watu, jamii na biashara.

Ericsson pamoja na washirika wake wamekuwa wakifanya kazi katika teknolojia ya mtandao wa 5G kwa miaka mingi sasa katika maabara za mtandao na katika miaka 2 iliyopita waliamua kuijaribu teknolojia hii kuiweka katika matumizi. Pia, tayari wameshaingia ubia wa kusaini mikataba ya mtandao huu wa 5G kwa awamu ya kwanza ambapo mpaka kufikia sasa kampuni 39 tu duniani zimesaini mkataba wa matumizi ya teknolojia hii.

Kiwango cha teknolojia hii ya mtandao kimepelekea uwepo wa redio mpya ya mtandao wa 5G "5G New Radio" ambayo tayari imekamilika tangu Desemba mwaka jana 2017 na inatarajiwa kuanza kupatikana katikati mwa mwaka huu 2018. Mitandao ya kwanza ya kibiashara pamoja na vifaa vyenye teknolojia hii (simu, kompyuta, iPad, tablets n.k.) vya teknolojia hii vitakamilika  mwakani 2019 kwa mujibu wa Mpango wa Ushirikiano wa Mtandao wa Kizazi cha tatu "3GPP" lakini yote haya yataanza kutumika kuanzia 2020. Ericsson imekadiria idadi ya watumiaji wa teknolojia hii kwamba watafika bilioni 1 mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2023.

UFAHAMU NA TAARIFA KUHUSU TEKNOLOJIA HII

Mtandao huu utafanya mambo mengi sana na ndiyo sababu ukaitwa Mtandao wa Muunganiko wa Vitu (Internet of Things) utakuwa na mengi sana ya kufanya kupitia teknolojia hii. Haya ni baadhi ya mambo ambayo Ericsson inayataja kuwepo katika teknolojia hii:

ULINZI 

Vifaa vilivyounganishwa pamoja na vitumizi vitahitaji kuunganishwa katika mtandao ambao ni stahimilivu, wenye ulinzi na wenye uwezo wa kulinda siri na faragha za mtumiaji. Teknolojia hii imetengenezwa kwa kuyafanikisha haya.


BIASHARA KWA NJIA YA MTANDAO ULIOIMARISHWA

Modem za mtandao chini ya teknolojia hii zitakuwa na nguvu zaidi ili kuimarisha biashara za wateja. Tafiti zilizofanywa na Ericsson zinaonesha kwamba mabadiliko kuelekea 5G yanaweza kupunguza karibia mara 10 ya gharama ya mtandao kwa kila gigabaiti moja tofauti na ilivyo kwa mtandao wa sasa wa 4G.

UFIKISHWAJI WA TEKNOLOJIA HII KWA NJIA YA MODEM KWANZA


Ericsson wanadai kwamba jambo la kwanza litakuwa ni kuboresha modem za sasa ili ziendane na kasi ya 5G.

MTANDAO HUU UTATEKA SOKO LA BIASHARA

Ericsson wanadai kwamba mtandao huu utakuwa wa matumizi ya vitu kwa mfano vifaa vya kujiendesha venyewe kama vile magari. Wametaja fursa, changamoto pamoja mifano ya baadhi ya mambo yanayotokea katika usasa wa viwanda.

VIWANDA VINAISUBIRIA TEKNOLOJIA HII

Je ni kwa namna gani kampuni kubwa zitaitumia teknolojia hii katika biashara zao? Ericsson imewauliza wafanya maamuzi 900 katika viwanda 10 na ripoti hiyo ipo nitaizungumzia siku nyingine. 

5G KWA VIWANDA

Teknolojia hii itawawezesha wamiliki wa kampuni za simu za mikononi fursa ya kuwasaidia wamiliki wa viwanda kuwa viwanda vya kisasa na kuangalia faida za teknolojia hii kama vile utumiaji wa mitambo inayojiendesha (automation), akili bandia (artificial intelligence), ukweli thabiti (augmented reality) pamoja na mtandao wa muunganiko wa vitu (Internet of Things "IoT")

FURSA KWA WATOA HUDUMA ZA AFYA

Teknolojia hii itawasaidia watoa huduma za afya kwa urahisi zaidi kwa wateja wao. Hii itawezesha njia za mtandao kuwa kasi zaidi hivyo itawezesha hata kuwasiliana moja kwa moja kwa njia ya video bila mushkeri ya mtandao. Hii pia itawafanya watoa huduma kupanua huduma zao zaidi kuliko kusubiriana ofsini tu.

MUHTASARI KUHUSU UTAYARI WA TEKNOLOJIA HII
Ericsson wanadai kwamba utafiti mfupi uliofanywa mwaka jana 2017 unaonesha kwamba mtandao huu utakuwa na watumiaji bilioni 1 mpaka kufikia mwisho mwa mwaka 2023 kama nilivyosema hapo juu.


KUONGEZA IDADI YA WATAZAMAJI WA MPIRA

Watazamaji wa mpira wanaotumia simu hupenda kuangalia mpira bila kuwa na shida ya mtandao. Ericsson wanadai kwamba teknolojia hii ya 5G itamfanya mtazamaji kujihisi yuko uwanjani yani itakua kana kwamba anauzunguka uwanja wa mpira yeye mwenywe. Ongezeko la watu kuangalia mpira kwa njia ya mtandao utatokana na uimara wa mtandao ambao ulifanyiwa tafiti mwaka 2016 huko Rio de Jeneiro.


MAJARIBIO YA TEKNOLOJIA YA MTANDAO WA 5G


KOREA KUSINI

Mwezi Februari mwaka huu 2018, Ericsson, Shirika la mawasiliano la Korea Kusini na Intel walifanya majaribio ya mtandao huu katikati ya jiji la Seoul ambapo kuna idadi ya watu milioni 25. Teknolojia ya 4K video ilijaribiwa ili kutoa picha kwa watumiaji kuona uwezo wake. Matumizi ya data yalifikia 900Mbps kwa upande wa kupakua (downloading) huku yale ya kupakia (uploding) yakifikia 600Mbps. Kwa kutumia bendi 28Ghz uunganishwaji wa mtandao ulikua imara kabisa licha ya kuwepo changamoto ya uenezi wa mtandao.

ESTONIA

Telia, Ericsson na Intel walifanya majaribio ya mtandao katika kampuni ya usafirishaji ya Tallink ambayo husafirisha watu na mizigo. Kila meli hubeba hadi kufikia watu 2,000. Mafanikio bado yalionekana kwa mtandao huu. Abiria waliweza kutumia mtandao huu safarini bila kuwepo na mushkeri ya aina yoyote ile.


KASI MPYA YA 5G

Ericsson wakishirikiana na SK Telecom na BMW Korea walitumia teknolojia hii ya 5G iliyoboreshwa kuangalia gari iliyounganishwa na mtandao huu kwa kuangalia mwendokasi wa gari iliyosafiri kilomita 170 kwa saa. Matumizi yalifikia uwezo wa kupakua hadi GB 3.6. Jaribio hili lilihusisha radio 4 tofauti za kusambaza mawasiliano. Pia, kulifanyika jaribio la kuhama kutoka radio moja ya mawasiliano kwenda nyingine na bado kasi ya mtandao ilifikia zaidi ya GB 1.5. Majaribio haya yote yalifanyika katika 28Ghz bendi.


KAMPUNI ZILIZOINGIA UBIA NA ERICSSON

Mpaka kufikia mwezi April mwaka huu 2018 ni kampuni 39 tu duniani ambazo zimeingia mkataba wa matumizi ya mtandao huu wa 5G kama jinsi inavyoonekana. Kwa bara la Afrika ni kampuni 2 tu za mawasiliano ambazo tayari zimesaini mkataba wa ubia na Ericsson. Kampuni hizo ni MTN ya Afrika Kusini na Etisalat ya nchini Misri. Unaweza kuziangalia nchi hizo kama jinsi kampuni zinavyoonekana kwenye ramani ya dunia akatika picha hii:

MAKALA HII IMEANDALIWA KWA HISANI YA MTANDAO WA ERICSSON.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI

Kansela Angela Merkel akihutubia bungeni siku ya Jumatano (7 Septemba 2016). Licha ya chama cha CDU kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi la kwao la Mecklenburg-Vorpommern kutokana na sera yake ya wahamiaji, Kansela Angela Merkel anasema sera yake ni sahihi na kamwe hatarudi nyuma. Vichwa vya habari katika magazeti na ripoti za televisheni na redio mara tu baada ya CDU kushindwa uchaguzi huo wa Jumapili, zilitazamiwa kumrejesha Kansela Merkel nyuma, na hotuba ya leo ilidhaniwa kuwa ingekuwa nyepesi na laini. Lakini hivyo sivyo ilivyokuwa, kwani kwenye hotuba ya bungeni ya leo Jumatano (7 Septemba 2016), ambapo alionekana kusimama imara. "Hali yetu leo ni bora zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka mmoja uliopita kwetu sote. Hapana shaka, bado kuna mambo ya kufanywa. Changamoto kubwa ikiwa kuwarejesha nyumbani wahamiaji ambao hawawezi kubakia hapa na sisi. Na kwa uadilifu kuwahudumia raia wetu, huku tukiwafahamisha kuwa tunapaswa kuwasiaidia wale wenye haki ya kusaidiwa," aliwaambi...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

PICHA 20 KUTOKA KWA DIAMOND NA ZARI WAKIWA KENYA WALIZOPOST INSTAGRAM

Diamond na Zari wameendelea na starehe zao huko Mombasa Kenya huku team ya WCB ikitia mguu pia mahali hapo; Harmonize na Sallam walihusika pia. Hizi ni baadhi ya picha kutoka katika mapumziko hayo. Hapa Zari aliamua kumtania shemeji yake Harmonize. mkubwa Simba na Zari katika starehe zao Harmonize alipata nafasi ya kusema chochote BClub Katika picha hii Diamond kaandika caption ya kiingereza ambayo Kiwashili chake ni "namwambia Harmonize kwamba wenye chuki wote hawana maana. Tuna uwezo na ni matarijiri" Unamuona Zari anavyozidi kupendeza kama ndo kwanza ana miaka 12 Kila mtu apambane na mahusiano yake tu. Huu mkao sasa Zari alivyomtegea Mond afu anajifanya kama hana habari yuko busy na simu Sallam alihusika pia B Club Wanapendeza hawa wapendanao unamuona Zari? KWA PICHA, MATUKIO, HABARI NA MAELEZO KAMA HAYA NA MENGINE MENGI USISITE KUTEMBELEA VENANCE BLOG: Facebook: VENANCE BLOG Twitter: @Venan...

LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

The following applicants have been selected to join various programmes offered by Tanzania Institute of Accountancy for the Academic year 2018/2019. Selected candidates should report to their respective campuses on 29 th  OCTOBER 2018. Joining instructions and admission letters can be downloaded through our website www.tia.ac.tz The Institute has limited accommodation facilities for students. Those who wish to stay at the Institute’s Hostels should apply in advance to their respective campuses before commencement of an academic year. Applicants with status  “PENDING FOR SELECTION’’  are advised to communicate with the institute through mobile numbers  062577774 OR O677777746 OR 0764777746.  Applicants with  ‘‘Prior admission status’’  in their accounts are advised to clear their prior admission status through filling TCU prior admission clearance form .  Unsuccessful applicants for the second round are advised to re-apply for third ro...