Skip to main content

MVUA ZINAZOENDELEA DAR ES SALAAM KUPUNGUA MAKALI JUMAMOSI HII

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mvua za mfululizo zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam zitaendelea kunyesha na kwamba zinatarajia kupungua mwishoni mwa wiki hii.

Taarifa hiyo inaweza kuwa habari njema kwa wakazi wa Dar es Salaam na miji mingine iliyoathirika kwa kiasi kikubwa na mvua hizo zilizonyesha mfululizo na kusababisha vifo, uharibifu wa mali na miundombinu, huku hali ya usafiri, upatikanaji wa bidhaa hasa za vyakula ikiwa ngumu katika maeneo mengi.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mkuu wa  Huduma za Hali ya Hewa kwa Jamii wa TAM, Hellen Msemo alisema mvua hizi zinatarajia kupungua mwishoni mwa wiki hii; lakini sio kuisha kabisa na kwamba kwa sasa wananchi waendelee kufuatilia taarifa zinazotolewa.

“Mvua hizi zitaendelea kunyesha mpaka Ijumaa ya wiki hii na tunaweza kuona jua kidogo Jumamosi lakini sio mvua za kukatika kabisa zitaendelea kunyesha kidogo kidogo,” alisema Msemo.

Shule zajaa maji

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msasani ‘B’, Jane Reuben alisema mvua zinazoendelea kunyesha zimeathiri kwa kiasi kikubwa mahudhurio ya wanafunzi shuleni hapo huku wengine wakichelewa kufika darasani.

Gazeti hili lilishuhudia hali tete katika shule ya Msingi Msasani ‘A’ ambapo baadhi ya madarasa yamejaa maji na kushindwa kutumika na kuwalazimu wanafunzi kuchangia vyumba vya madarasa.

Kutokana na hali hiyo, wanafunzi wengi wanaosoma katikati ya jiji wameshindwa kufika shuleni kwa kuhofia usumbufu wa usafiri kutokana na mvua ambayo imekuwa ikiendelea kunyesha.

Baadhi ya shule katika Kata ya Goba zimefungwa kwa muda kutokana na athari za mvua hizo. Foleni zawa kero Mvua hizo pia zimeendelea kuleta usumbufu mkubwa katika barabara nyingi za Dar es Salaam kutokana na kuharibika na kusababisha msongamano unaowafanya wakazi wa jiji hilo kupata wakati mgumu wa kuyafikia maeneo mbalimbali ama kikazi au shughuli binafsi.

HabariLeo ilishuhudia maeneo ya Posta Mpya katika barabara za Samora Avenue, Mkwepu, Ocean Road, Uhuru na zile zinazoelekea Magomeni na Mwenge zikiwa na msongamano wa magari.

Bidhaa bei juu Kwa upande wa bidhaa katika masoko, bei zimepaa na kusababisha kuongezeka kwa ukali wa maisha miongoni mwa wakazi wa Dar es Salaam.

Katika soko la Kariakoo, mfanyabiashara Baraka Lisulile anayeuza karoti alisema kabla ya mvua kilo moja ilikuwa inauzwa kwa Sh 2,000 lakini sasa imefikia Sh 3,000.

“Vile vile kabla ya mvua hizi kunyesha tenga la nyanya lilikuwa ni kati ya Sh 20,000 hadi Sh 35,000 lakini hivi sasa ni kuanzia Sh 48,000 hadi Sh 50,000,” alisema mfanyabiashara huyo.

Bidhaa za unga, mchele, maharage na aina nyingine za vyakula, nazo ziko juu. Nyumba zabomoka Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Musa Natty alisema mvua hizo zimefanya wananchi kukumbwa na uharibifu mkubwa ambao ni nyumba kufurika maji, kubomoka na barabara na madaraja kukatika.

Alisema katika manispaa hiyo maiti nne za wanaume na mwanamke moja zimepatikana na zimeripotiwa kata za Wazo Kunduchi na Mbezi beach.

Katika manispaa hiyo pia eneo la Africana nyumba zimejaa maji huku maeneo ya Nyaishozi kaya 151 zinahitaji msaada wa haraka ikiwemo mahema na chakula.

Alisema kata ya Tandale maeneo ya bondeni maji yameingia katika mitaa ya Pakacha, kwa Tumbo, Mahalitani, Sokoni, Mtogole na kwa Mkunduge.

Nyumba 14 ndizo zilizoathirika kwa kubomoka ambapo wakazi wake wamehifadhiwa na majirani.

Kata ya Kwembe watu 23 wamepata majeraha baada ya nyumba kuezuliwa paa, Shule ya Msingi King’azi ambayo inamilikiwa na Manispaa nayo imepata maafa ya kutitia na kutoa ufa kati ya lenta na paa.

Kata ya Mbweni familia 128 zimeathirika kwa kuzungukwa na maji na kukosa makazi na kuhifadhiwa na majirani na kata ya Magomeni mwili wa mtu mmoja umeopolewa akiwa amekufa, katika mtaa wa Suna watu 450 wamekosa makazi na mtaa wa Makuti A watu 250 hawana makazi na wanahifadhiwa na majirani.

Mtaa wa Idrisa watu 180 hawana makazi na nyumba nyingine 450 kuzingirwa na maji Kata ya Mabwepande daraja la mto Nyakasangwa mtaa wa Mbopo limekatika na kutitia hakuna mawasiliano kati ya pande mbili na barabara ya kwenda Mabwepande imekatika karibu na njia panda iendayo kwa waathirika wa Mji Mpya na nyumba 20 zimezingirwa na maji.

Kata ya Hananasif nyumba 400 ambazo ziko mabondeni zimezungukwa na maji na wakazi wa nyumba hizo wamehama makazi yao. Nyumba hizo ni zile zilizopo bondeni ambazo zilizobaki baada ya kubomolewa na wamiliki kupelekwa Mabwepande.

Kata ya Mabibo daraja la Tasaf linalounganisha Kata ya Mabibo na Makuburi limekatika kwa sababu ya wingi wa maji pamoja na nyumba tisa na vyoo.

Kata ya Manzese kumeripotiwa kifo cha mtu mmoja na kubomoka kwa nyumba moja. Daraja la linalounganisha kata ya Mbezi juu kwa Londa na Makongo kukatika.

Kata ya Wazo mtaa wa Mivumoni nyumba 13 zimeezuliwa na upepo mkali na Kata ya Kawe Mtaa wa Mzimuni nyumba 64 zimebomoka na nyingine kuzunguka na maji.

Kata ya Makumbusho mwili wa mtu mzima miaka 45 umeokotwa na waathirika 109 waliobomokewa na nyumba na zingine kujaa maji wamehifadhiwa shule ya msingi Kisiwani ambao wanahitaji msaada.

Kata ya Msasani Shule ya msingi msasani A imejaa maji katika madarasa 7 na nyumba za walimu na shule imefungwa kwa muda, Kata ya Sinza maji yamejaa yanaelekea katika makazi ya watu huku mtaa wa Barafu nyumba 3 zimebomoka na watu kukosa makazi huku nyumba 275 zimezungukwa na maji na kuhatarisha makazi.

Kata ya Mwananyamala katika mitaa ya Msisiri A na Msisiri B, Bwawani na mtaa wa Mwinyijuma jumla ya nyumba 150 zimezingirwa na maji na kuleta taabu kwa wakazi wake.

Kata ya Makuburi nyumba mbili zimebomoka na daraja la waenda kwa miguu linalounganisha Kata za Makuburi na Kimara kusombwa.

Kata ya Kimara familia saba zimehamia katika Kituo cha Polisi cha Kilungule A baada ya nyumba yao kujaa maji na kukatika, Kata ya Mizimuni nyumba tano zimevunjika kuta na kaya 15 zimehamia kwa majirani huku kaya 30 nyumba zake zimezingirwa na maji.

Kufuatia maafa hayo, Halmashauri imechukua jitihada mbalimbali ili kuokoa maisha ya watu na kuwawezesha kurudi katika makazi yao. Jitihada hizo ni pamoja ni kununua pampu za kunyonya maji ambayo yamezunguka makazi ya watu.Kazi hiyo ya kunyonya maji imeanza pamoja na kuzibua mitaro.




Chanzo: Habari Leo

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

MAANDALIZI MEMA YA SIKUKUU YA KRISMAS

Kwanza namshukuru Mungu toka tukiwa wadogo mpaka sasa anaendelea kutulinda. Uongozi mzima wa Venance Blog tunawatakieni maandalizi mema ya Krismas hapo kesho, wale wa kanisani tukafurahi kwani bwana atazaliwa. Msali salama katika misa za mkesha kubwa zaidi kudumisha amani na usalama kuanzia leo mpaka sikuku itakapoisha. MAANDALIZI MEMA YA KRISMAS!!!

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

AJALI: BASI LAUA WATU 12 PAPO HAPO

Watu 12 wamekufa papo hapo na wengine zaidi ya 90 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Korogwe, Tanga kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka. Ajali hiyo ilitokea jana saa 1.30 asubuhi kwenye barabara kuu ya Segera-Chalinze katika kijiji cha Kwalaguru kata ya Kwedizinga wilayani hapa. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alithibitisha jana kutokea kwa ajali hiyo ya basi la Burudani namba T 610 ATR aina ya Nissan. Majeruhi walipelekwa katika hospitali ya wilaya ya Korogwe ya Magunga, kwa matibabu ya awali na miili ya marehemu, akiwamo dereva wa gari hilo, Luta Mpenda (35) imehifadhiwa hospitalini hapo.  “Tukiwa tunakaribia kwenye kona ile, tulipishana na lori hilo likiwa kasi upande wetu, dereva wetu akajitahidi kulikwepa lakini kutokana na ile kona kuwa kali, gari lilimshinda na kupinduka,” alisema Bendera. Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo walisema walisikia kishindo kutoka eneo hilo wakaenda na kukuta gari limepinduka na baadh...

FAHAMU MAMBO HAYA 20 KUHUSU TANZANIA

Leo nakufahamisha baadhi ya mambo ambayo huenda hukuyafahamu ama ulichukulia kawaida tu. Mambo hayo ni hapahapa Tanzania.  Tanzania ina eneo la kilomita za mraba 945,087. Ina jumla mikoa 31 kote bara na visiwani. Mpaka kufikia mwaka 2017 idadi ya watu nchini ilikadiriwa kuwa milioni 52.554 kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya takwimu. Twende sasa tuanze kuhesabu moja baada ya jingine #1 . Wimbo wa taifa "Mungu Ibariki Tanzania"  ni wimbo unaofanana na nyimbo za mataifa ya Afrika Kusini na Zambia. Wimbo huu ulitungwa na Enock Sontonga kwa lugha ya Xhosa "Nkosi Sikelel iAfrika" . Wimbo huu pia uliwahi kutumiwa na nchi za Zimbabwe na Namibia. Enock Sontonga mtunzi wa wimbo Mungu Ibariki Afrika #2. Ni Tanzania pakee ambako kunapatikana Simba wenye uwezo wa kupanda juu ya miti. Simba hawa wanapatikana katika hifadhi ya taifa ya Ziwa Manyara. Simba wenye uwezo wa kupanda miti hifadhi ya Ziwa Manyara. #3. Tanzania ni nchi ambako fuvu la mtu wa kale z...

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA: FIFA IMESEMA ITAZIPA DOLA MILIONI 2 NCHI ZA AFRIKA ZINAZOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA

FIFA itatoa zawadi ya dola milioni mbili kwa kila mojawapo ya timu tano za Afrika zilizofuzu kucheza kombe la dunia kuzisaidia katika maandalizi, amesema rais wa shirikisho la kandanda barani Afrika CAF. Misri, Morocco, Nigeria, Senegal na Tunisia, zimefuzu kushiriki katika michuano ya kombe la dunia itakayofanyika nchini Urusi, na rais wa shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF, Ahmad Ahmad, alismea katika taarifa kwamba fedha hizo zitatumika "kushughulikia mapema, suala la bonasi za wachezaji." "Migogoro juu ya malipo katika michuano iliyopita ilipelekea kuwepo na hali zilizoathiri vibaya taswira ya soka barani Afrika, ikiwa ni pamoja na kuathiri kwa kiwango kikubwa utendaji wa timu viwanjani," aliongeza. Mwaka uliopita, shirikisho la kandanda la Nigeria (NFF) lilisaini makubaliano na wachezaji wake wakiahidi kujiepusha na migogoro ya bonasi na malipo ambayo imeharibu kampeni zao za nyuma za kombe la dunia. Wachezaji wa timu ya Nigeria, Sup...

LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

The following applicants have been selected to join various programmes offered by Tanzania Institute of Accountancy for the Academic year 2018/2019. Selected candidates should report to their respective campuses on 29 th  OCTOBER 2018. Joining instructions and admission letters can be downloaded through our website www.tia.ac.tz The Institute has limited accommodation facilities for students. Those who wish to stay at the Institute’s Hostels should apply in advance to their respective campuses before commencement of an academic year. Applicants with status  “PENDING FOR SELECTION’’  are advised to communicate with the institute through mobile numbers  062577774 OR O677777746 OR 0764777746.  Applicants with  ‘‘Prior admission status’’  in their accounts are advised to clear their prior admission status through filling TCU prior admission clearance form .  Unsuccessful applicants for the second round are advised to re-apply for third ro...