Skip to main content

PINDA: CCM ITAELEZA HAYA KWENYE KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, jana alihitimisha mjadala wa makadirio ya Bajeti ya Ofisi yake ya Sh trilioni 5.7 ambayo ilipitishwa na Bunge, huku akifafanua hoja zitakazotumiwa na CCM kuomba kura za wananchi katika Uchaguzi Mkuu ujao.


Pinda alisema hakuna haja ya kuandikia mate wakati wino upo na kufafanua kuwa katika Uchaguzi Mkuu, CCM itatakiwa kueleza mafanikio ya Serikali katika nishati ya umeme vijijini, miundombinu ya barabara, elimu, maji na afya.


Alitaka waliokuwa wakijiuliza nani atashinda katika uchaguzi huo, wapitie kidogo historia kuanzia mwaka 1995 mpaka katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika Desemba mwaka jana, ili waelewe nani alipata kipigo.


Elimu


Akifafanua kwa ufupi mafanikio yaliyopatikana katika elimu, Pinda alisema watakapoulizwa katika sekta hiyo nini kimefanyika, wataweka wazi kuwa ingawa bado kuna changamoto lakini yapo pia mafanikio makubwa.


“Wacha tubebe lawama katika changamoto, lakini tutaeleza kuwa katika vyuo vya ufundi mwaka 1995 na 1996, udahili katika vyuo vya ufundi ulikuwa 7,700 tu, mwaka 2005 wanafunzi 78,000 lakini takwimu za 2013, waliodahiliwa walikuwa wanafunzi 145,000,” alisema.


Katika vyuo vikuu, alisema mwaka 2005 walikuta vyuo vikuu vikiwa 23 lakini takwimu za 2013, zinaonesha kuwa vyuo vikuu vimefikia 50 na ongezeko hilo lisingewezekana kama si kuwepo kwa sera nzuri na usimamizi mzuri wa Serikali.


Kuhusu idadi ya wanafunzi waliodahiliwa katika vyuo hivyo, Pinda alisema mwaka 2005 walikuta wanafunzi 40,000 katika vyuo vikuu lakini mwaka 2015 wanaiacha nchi ikiwa na wanafunzi 200,000 waliopo katika vyuo vikuu mbalimbali.


Kuhusu ubora wa elimu aliosema kuwa una changamoto, lakini alikumbusha kuwa utafiti uliofanyika wa vyuo vikuu 100 bora Afrika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),kiliibuka namba nne kwa ubora Afrika na kufuatiwa na Chuo Kikuu cha Capetown Afrika Kusini.


Katika elimu ya msingi, alisema alipokwenda Marekani alipatwa na mshangao kukabidhiwa Tuzo ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa katika Uandikishaji wa Wanafunzi wa Elimu ya Msingi.


Afya


Katika sekta ya afya, Pinda alisema umri wa kuishi wa Mtanzania umeongezeka huku vifo vya watoto chini ya miaka mitano vikipungua. “Tanzania ni miongoni mwa nchi tano barani Afrika, zilizofanya vizuri katika kupunguza vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano,” alisema.


Miundombinu ya barabara


Kuhusu miundombinu ya barabara, Pinda alihoji ni nani anayeweza kusimama kwa wananchi na kusema Serikali haijafanya chochote katika sekta hiyo.


“Hivi kuna anayeweza kusema kuwa katika barabara hatujafanya kitu na akasimama kwa wananchi kuomba kura? Njooni kule Rukwa nenda Kigoma useme hakuna kitu, nawahakikishia hamtapata kura,” alisema.


Aliwasema wabunge wa Kigoma ambao tangu Uhuru wamekuwa wakilalamika kuwa mkoa huo umetengwa na kushangazwa kwa hatua yao ya kutosema chochote kuhusu ujenzi mkubwa wa barabara kwenda katika mkoa huo na daraja kubwa la Kikwete.


Mbali na Daraja la Kikwete, Pinda alisema madaraja zaidi ya 20 yaliyokuwa kikwazo katika miundombinu ya barabara yamejengwa huku vivuko vingi katika mito, maziwa na bahari vikinunuliwa.


Maji, umeme


Kwa upande wa huduma ya maji, Pinda alisema kuna kazi kubwa imefanyika katika miaka miwili iliyopita na kutoa mfano wa Mradi wa Maji Karatu.


“Inasikitisha hata rafiki yangu wa Karatu akija hapa hasemi mradi huu ni mzuri. Wamejenga shule nzuri lakini hawasemi, lakini mimi nilipofika pale niliwasifia shule nzuri kwa kuwa najua wanatekeleza Ilani ya CCM,” alisema Pinda.


Kuhusu umeme vijijini, Pinda alisema ingawa hawajamaliza vijiji vyote lakini kazi imefanyika na kwa kuwa anaamini kuwa Serikali ijayo ni ya CCM, kazi hiyo itaendelezwa na Serikali ijayo.Kilimo
Katika kilimo, Pinda alisema changamoto kubwa iliyokuwa ikisumbua Taifa ilikuwa kukosekana kwa usalama wa chakula, jambo alilosema ilikuwa aibu kwa taifa kuomba chakula nje ya nchi.

Alisema Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, imejitahidi na leo Tanzania inatamba kuwa hata mikoa yenye njaa, italishwa kwa kutumiachakula kilichozalishwa ndani ya nchi.

AlisemaTanzania ni nchi ya nne barani Afrika kwa kuzalisha mahindi, duniani inashika nafasi ya 12 katika uzalishaji wa zao hilo huku akiongeza kuwa mwaka 2005 kulikuwa na matrekta 4, 000, sasa matrekta yaliyopo ni zaidi ya 10,000.

“Tusingewekeza katika uzalishaji wa mazao ya kilimo, tusingekuwa na jeuri ya kulisha mikoa yote yenye njaa. Kwa sasa tunaweza kulisha hata nje ya nchi na hivi karibuni, Sudan walikuja kuomba tuwasaidie. “Hata Kenya mwaka jana walikuja kuomba tuwasaidie tani 240,000 na tukawapa…nasema lazima tuone jeuri katika hilo,” alisema Pinda.

Uchumi


Pinda alisema yapo mambo mengi yanafanyika katika uchumi wa nchi na kutoa mfano wa utafiti wa wataalamu wa Benki ya Dunia (WB) wa mwaka 2012 kwa kushirikiana naTaasisi ya Business Insider kuhusu nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi.

Kwa kutumia vigezo vya ukuaji wa uchumi, Pinda alisema utafiti huo ulikuja na nchi 29 duniani ambazo zina uchumi unaokua kwa kasi na Tanzania ilishika namba 15.

Mbali na utafiti huo, mwingine ulifanywa na taasisi ya KPMJ ya Afrika Kusini kutafuta nchi kumi zenye uchumi unaokuwa barani Afrika na Tanzania ikashika nafasi ya sita.

Pia alitaja utafiti wa kikanda uliofanywa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) Aprili mwaka huu, ikabainishwa kuwa Tanzania inafanya vizuri. “Katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, sisi ndio tunaong’ara na hata hao watafiti wakija wanaona viashiria vilivyo bayana kabisa vya ukuaji wa uchumi,” alisema Pinda.

Alitoa mfano wa Mkoa wa Dodoma, kwamba alipokuwa anakuja na Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere miaka ya 1980 na mkoa huo ulivyo sasa ni vitu viwili tofauti.

Ujenzi wa madarasa Pinda alisema anajua mafanikio hayo lazima yawaume Kambi ya Upinzani kwa kuwa wamenyang’anywa hoja za kuwaeleza wananchi katika uchaguzi mkuu.

Alisema hata kama inawauma hivyo, lakini ni vyema wanapojadili waheshimiane kuliko ilivyokuwa wakati wa kujadili makadirio ya Bajeti ya ofisi yake, ambapo baadhi ya wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani, walifikia hatua ya kuacha kuheshimiana na kuwaita mawaziri hawana akili.

“Ah! Inaonekana upande huo mna akili sana, lakini hivi Mbowe mkija kushika madaraka na sisi tukakaa huko tuache kuwaheshimu mtafurahi? Msiwatendee wenzenu lile msilopenda kutendewa,” alisema Pinda.

Alimtaka Mbowe na kundi lake la Umoja wa Katiba ya Wananchi(UKAWA), katika mikutano yao ya kuchangisha fedha, wajaribu hata kujenga darasa moja ili wajue anachozungumzia cha kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo nini maana yake.



Chanzo: Habari Leo

Comments

Popular posts from this blog

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CELEBRITY WA SIKU: PAUL WALKER

Leo katika kipengele cha Celebrity wa siku tunaye Paul Walker ambaye kwa sasa ni maremu. Kwa nini Paul Walker leo? Kwa sababu leo ni tarehe ambayo alizaliwa mwaka 1973 huko California. Na tuangalie historia yake ili kumfahamu zaidi. KUZALIWA Paul Walker alizaliwa Septemba 12, 1973 huko Glendale, Calfornia nchini Marekani.  ELIMU Alipata Elimu yake katika Village Christian School. KAZI Paul Walker alikuwa muigizaji nchini Marekani ambapo alianza kazi hiyo katika televisheni mbalimbali kama vile katika vipindi vya The Young and the Restless na Touched by an Angel. Alipata umaarufu katika movie za vijana kama vile She's All That na Varsity Blues. Walker alipata umaarufu zaidi katika movie za Brian O'Conner ambapo zinahusisha uendeshaji wa magari mitaani 'The Fast and the Furious'. Alishiriki pia katika filamu kama vile Eight Below, Timeline, Into the Blue, Joy Ride na Running Scared. Mbali na uigizaji, Walker pia alikuwa mtangazaji wa kipindi cha ...

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MOVIE: X-MEN APOCALYPSE RELEASED TODAY

  Release date: May 27, 2016 Director: Bryan Singer Starring: James McAvoy Jennifer Lawrence Oscar Isaac Michael Fassbender Rose Byrne Sophie Turner Synopsis: In this comic-book adventure set in the 1980s, the X-Men are forced to confront an ancient mutant called Apocalypse (Oscar Isaac). After the resurrected beast recruits a super-team to take over the world and destroy hunmanity, Professor X (James McAvoy) and his charges must come to the rescue for the fate of the planet. The film co-stars Michael Fassbender, Jennifer Lawrence and Olivia Munn.

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

Chuo cha Mipango ama Institute of Rural Development Planning kimetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali za shahada (Bachelor Degree) chuoni hapo mwa mwaka wa masomo 2016/207. BOFYA HAPA KUANGALIA MAJINA HAYO IMPORTANT NOTICES TO SELECTED STUDENTS The selected candidates must report at the Institute’s main campus Miyuji area on Monday 17 th October, 2016 ready for orientation program. Joining instructions can be downloaded from the website www.irdp.ac.tz and can also be collected from the main campus admission office. Tuition fees for Bachelor Degree courses 850,000/= Registration fee is 50,000/=, Students organization fee 20,000/= sports and games is 10,000/= and NACTE Quality Assurance Fee 20,000/=. Students are required to pay atleast half of the tuition fee and 100,000/= for registration, students organization, sports and games and NACTE Quality Assurance Fee. The payment should be made through CRDB Bank account no. 01J1082678600 before 1...

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

Jana nilikuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea Kusini, leo tuangalie upande wa pili kwa akina dada ambao ni warembo zaidi. #10. Han Ye Seul   Han Ye Seul alizaliwa chini Marekani japokuwa ana asili ya Korea. Anaigiza series na filamu za kawaida. Alionekana katika Nonstop 4 na pia ameigiza katika muvi kama vile Couple or Truble, Birth of a Beauty, Miss Gold Digger na Penny Pincher. Baada ya kupata umaarufu nchini Korea aliamua kufuta uraia wake wa Marekani na kuamua kuwa raia wa Korea Kusini. #9. Song Hye Kyo Song Hye Kyo alipata umaarufu katika tasnia ya muvi nchini Korea katika muvi kama vile Autumn in My Heart, All In, Full House, The World They Live In na nyinginezo. Ni mwenye furaha na amekuwa akiigiza muvi zake vizuri sana. #8. Lee Da Hae Lee Da Hae ni muigizaji maarufu nchini Korea Kusini. Ameigiza katika My Girl, Green Rose, The Slave Hunter, Miss Ripley na Hotel King. Ameigiza pia katika muvi za Kichina kama vile Actually Lob...

DOWNLOAD AUDIO KUTOKA UPRISE MUSIC: JVP SQUAD-HUSTLE ZA KITAA

Ngoma imefanywa Uprise Music na producer Fragger. Ngoma inaitwa Hustle za Mtaa imefanywa na JVP Squad ndani kasimama Ng'itu the Hustler na Fizzo. Sikiliza na kudownload kisha toa maoni yako hapa.  BOFYA HAPA KUSIKILIZA NA KUDOWNLOAD