ASTON VILLA YAPIGWA FAINI


Chama cha soka cha England FA, kimeipiga faini ya pound 200,000 klabu ya soka ya Aston Villa, kwa kitendo cha mashabiki kuvamia uwanja kwenye mechi ya robo fainali ya FA Cup dhidi ya West Bromwich Albion.
Katika mtanange huo uliopigwa March 7 kwenye dimba la Villa Park, mashabiki wa Aston Villa waliingia uwanjani wakati wachezaji walipopata majeraha na hata mwisho wa mchezo huku viti vikirushwa kutoka kwa mashabiki waliokuwa wamesimama mbali.
FA inasema klabu hiyo imeonywa vikali hasa juu ya mwenendo wake katika siku zijazo. Lakini kwa upande wao Villa waliomba msamaha baada ya mechi kuisha na kuongeza kuwa ushindi wao walioupata siku hiyo ulitiwa doa na vitendo vya wale walioshindwa kujizuia wao wenyewe.
Naye boss wa West Brom Tony Pulis amewakosoa walinda usalama wa uwanja huo na kuongeza kuwa usalam wa wachezaji wake ulikuwa mashakani.

Comments

Popular Posts

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

LIST OF UNDERGRADUATES SELECTED TO JOIN TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) 2018/2019 ROUNDS 1 & 2

VIFAA VYA KUWATAMBUA WENYE UGONJWA WA EBOLA VYAINGIZWA NCHINI

TAZAMA HAPA MAGOLI 10 BORA YA KOMBE LA DUNIA 2018