TIMU ZA SEVILLA NA DNIPOPETROVSK ZATINGA FAINALI EUROPA LIGI

Mashabiki wa timu ya Dnipopetrovsk wakiishangilia timu yao.
Nusu fainali ya pili ya Europa ligi iliendelea usiku wa kuamkia leo wakati Dnipopetrovsk ilipomenyana na Napoli huku Fiorentina ikiialika Sevilla. Hadi mwisho wa michezo yote miwili, Dnipro imeingia fainali kwa jumla ya bao 2 kwa 1 bada ya jana kushinda bao 1-0.
Nayo Fiorentina imetupwa nje kwa jumla ya bao 5-0 baada jana kuzabuliwa bao mbili nyumbani walipocheza dhidi ya Sevilla.
Fainali itapigwa mnamo May 27 huko nchini Poland kati ya Sevilla dhidi ya Dnipropetrovsk.

0 comments:

Post a Comment