CLAIRE FOY KUPAMBA JARIDA LA MITINDO LA VOGUE MWEZI UJAO

Claire Foy ambaye ni muigizaji maarufu nchini Uingereza, ataonekana kwenye ukurasa wa mbele kabisa wa Jarida la Mitindo nchini humo la Vogue. Taarifa hii inakuja rasmi kabisa kutoka katika mtandao wa Vogue.

Claire alizaliwa April 4, 1984 huko Stockport Uingereza. Anafahamika kwa kuigiza vema kabisa katika "Season of the Witch" (2011), "Going Postal" (2010) na "Wreckers" (2011). Amefunga ndoa na Stephen Campbell More toka Desemba 2014 na wana mtoto mmoja katika ndoa yao.

Claire amewahi kushinda tuzo za Golden Globes kama Muigizaji wa Kike aliyefanya vizuri katika maigizo kupitia series ya The Crown (2016), BAFTA/La Britania Awards kama Muigizaji bora wa mwaka nchini Uingereza (2017) na Screen Actor Guild Awards kama muigizaji bora wa kike (2017). Alitajwa pia katika tuzo za Primetime Emmy Awards, BAFTa Awards, Chritics Choice Television Awards, Broadcasting Press Guild Awards

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017:

#10. Lee Byung-Hun

Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianza kuigiza katika televisheni ya KBS katika baadhi ya matukio ya mchezo wa kuigiza "Asphalt My Hometown" Aliendelea kuigiza hadi mwaka 2000 alipoigiza muvi iliyompa umaarufu zaidi na kuuza sana nchini humo, muvi hiyo iliitwa "Joint Security Area" Lee ni mwanachama wa Academy of Motion Picture Arts and Science huko Hollywood Marekani.


#9. Jang Geun-Suk


Jang anapenda kutereza kwenye barafu, kuimba na kucheza. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maonesho ya jukwaani katika Chuo Kikuu cha Yang Han nchini Korea Kusini. Alianza kuigiza mwaka 2008 katika Kdrama ambapo aliigiza katika "Beethon Virus" aliigiza pia mwaka 2009 katika "You are Beautiful" na mwaka 2010 "Marry Stayed Out All Night" yote akifanya Kdrama. Kwa sasa anafanya kazi kama muigizaji na muongozaji. Jang alizaliwa Agost 4, 1987 na ameonekana vyema katika maonesho zaidi ya 20 aliyowahi kuigiza. Jang anafahamika kama muigizaji anayejituma sana katika Kdrama. Mwaka jana 2016 aliachia albam zake kadhaa za muziki zikiwemo mbili za "Just Crazy" na "Lounge H". Mnamo Julai mwaka jana 2016 aifanya ziara yake ya kimuziki barani Asia ikiwemo Seoul nchini Korea Kusini, China na Japan ambako alipata mafanikio makubwa katika ziara yake hiyo ya "It's Show Time"  kwa sasa anashughilika na kipindi cha maisha halisi kinachoitwa "My Ear's Candy"


#8. Gong Yoo

Alizaliwa Julai 10, 1979. Ni muhitimu wa Chuo Kikuu cha Kyung Hee akiwa na Shahada ya Sanaa na Maonesho. Anafahamika zaidi kwa kucheza michezo ya Martial Art ya Urusi, pamoja na kupanda kwenye miamba kama alivyoigiza katika "The Suspect" (2013). Alitajwa kama muigizaji maarufu zaidi nchini Korea Kusini mwaka jana 2016. Amewahi kuigiza katika muvi ya mazombi "Train to Busan" alipoambiwa atoe maoni kuhusu muvi hiyo alisema "nilidhani muvi za mazombi na kupigana ni rahisi sana, nilihangaika mno"

#7. Song Joong-Ki

Song alianza kuigiza kama utani tu katika shindano la Kdarama ambalo lililenga kutafuta vipaji "Descendants of the Sun" Kuuigiza haikuwa chaguo lake. Amewahi kushiriki katika michezo ya kutereza kwenye barafu ngazi ya taifa lakini alishindwa kuendelea kutokana na majeraha ambapo alishindwa kushiriki Olympic. Mwaka 2010 aliandika kitabu cha "Beatiful Skin Project" Mwaka 2008 aliigiza katka "A Frozen River" japokuwa igizo lililompa umaarufu sana ni "Sungkyunkwun Scandal" Mwaka 2017 ameigiza katika "Battleship Island"

#6. Park Yoo-Chun

Park ni muigizaji mwenye tuzo nyingi katika tasnia hii ya filamu naa uigizaji nchini Korea Kusini. Anafahamika pia kwa jina la Micky Yoo-Chun, jina la kiingereza alilopewa alipokuwa Virginia nchini Marekani. Alizaliwa Juni 8, 1986 Seoul mji mkuu wa Korea Kusini. Ni mtuzi wa nyimbo, muimbaji na muigizaji, nyimbo zake zipo katika maadhi ya Kpop, rhythm naa blues. Amewahi kuwa mshiriki katika kundi la DBSK toka 2003 hadi 2009 na kwa sasa yupo ktk kundi la JYJ. Ameigiza katika "Sungkyunkwan Scandal", "Miss Ripley" na "Rooftop Prince" Anafahamika pia kwa jina la "Gland Slam" kutokana na kushinda tuzo kutoka SBS, MBC na KBS ambazo ni maarufu nchini Korea Kusini.

#5. Hyun Bin

Hyun ni mmoja kati ya washindi wa tuzo kadhaa nchini humo. Anapendelea mpira wa kikapu, kuogelea na kwenda maonesho ya filamu. Amezaliwa Septemba 25, 1982 Seuol Korea Kusini. Ni muigizaji katka Kdrama ambapo amekuwa maarufu kupitia "My Name is Kim Sam-soon" ambayo ilimpa umaarufu sana na kumfanya ashinde tuzo za MBC Drama, Top Excellence. Ameigiza pia katika "The Secret Garden" Mwaka 2010 aliachia wimbo wake "Dream In my Heart", mwaka 2011 alitoa "Cant Have You" na "That Man" Mwaka 2010 alishinda tuzo ya Netizen Popularity Award.

#4. Kim Woo-Bin

Kabla hajawa muigizaji katika Kdarama, Kim alikuwa ni mwanamitindo aliyekuwa anatokea katika maonesho ya Seoul Fashion Week nchini Korea Kusini mwaka 2009. Anapenda sana mitindo lakini aliambiwa ili aongeze uzuri katika kazi yake hiyo ashiriki katika uigizaji, alikubali. Aliigiza katika "White Christmas" na baadaye mwaka 2013 aliigiza katika "School 2013" na "The Heirs" ambazo zilifanya aanze kutazamwa na Netizen. Mwaka 2012 alionekana katika fiamu tano zikiwemo "The Con Artist" na "Twenty". Mwaka 2016 aliigiza katika filamu ya uhalifu ya "Master" kama Park Jong-goon.

#3. Lee Jong Suk

Yeye anapenda sana kucheza games. Katika muda wake wa mapumziko anapenda kucheza Taekwondo na kupiga piano. Amezaliwa Septemba 14, 1989 ni muhitimu wa Chuo Kikuu Konkum akiwa na shahada ya filamu. Alianza kazi zake katika tasnia ya burudani kama mwanamitindo akitokea katika Seoul Fashion Week mwaka 2005. Mwaka 2010 alionekana katika "Prosecutor Princess" na baadaye akaonekana pia katika "The Secret Garden" na "School 2013"


#2. Lee Min Ho

Lee Min Ho alizaliwa Juni 22, 1987, anapenda sana filamu, kucheza game, na kucheza soka la miguu. Alihitimu Chuo Kikuu Konkuk akisomea filamu, na pia ana mdogo mmoja wa kike. Kwa mujibu wa IMDB, Min Ho alipokua mdogo alikuwa na ndoto za kuwa mcheza soka mkubwa lakink ndoto hizo zilipotea baada ya kuumia katika mchezo huo. Ameanza kuonekana Kdeama mwaka 2006 katika "Secret Campus" Hakua maarufu sana mpaka alipoigiza kama Goo Jon Pyo kwenye "Boys Over Flowers", na hapo ndipo alipoanza kuwa maarufu katika tasnia ya maigizo. Mwaka 2009 alishinda tuzo kama chipukizi bora kwenye tuzo za KBS Drama Acting Awards. Mafanikio zaidi yalifuata alipoigiza "Personal Tatse", "City Hunter" na "Faith" mwaka 2016 alionekana katika "The Legend of the Blue Sea" pia ni mpiga piano mzuri na muimbaji mwenye voko zake.

#1. Kim Soo-yun

Kim soo-hyun alizaliwa Februari 16, 1988. Ni muhitimu kutoka Chuo Kikuu Chung-Ang. Alionekana kwa mara ya kwanza 2013 kwenye "My Love From Another Star" japokuwa haikua na mwisho mzuri lakini ndiyo hii iliyompa umaarufu katika tasnia hii. Amekuwa akifanya kazi mbali mbali katika tasnia ya burudani nchini Korea Kusini kama vile kuimba, kuigiza, kufanya matamasha na hata kuwa balozi kuiwakilisha nchi yake. Mwaka 2014 alikuwa Balozi wa Goodwill kwa jiji la Seoul. Ameshinda tuzo kadhaa kama vile SBS New Star mwaka 2010, KBS New Actor mwaka 2011, na tuzo ya Popularity and Best Couple Awards.



Chanzo: Trending Top Most

Je, una lolote ungependa kusikia kuhusu chochote kinachohusiana na haya? Niandikie kupitia moja ya njia hizi:
WhatsApp: +255 712 586 027
Facebook: VENANCE BLOG
Instagram: @venanceblog
Twitter: @Venancetz
Barua pepe: venancegilbert@gmail.com

MSHAMBULIAJI WA MANCITY SERGIO AGUERO AJERUHIWA KATIKA AJALI

Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amejeruhiwa katika ajali ya barabarani mjini Amsterdam, saa chache baada ya kuhudhuria tamasha.
Raia huyo wa Argentina, mwenye umri wa miaka 29, anaarifiwa kuwa ndani ya taxi akielekea katika uwanja wa ndege baada ya kuhudhuria tamasha la muimbaji Maluma.
City imesema "alikuwa Uholanzi katika siku yake ya mapumziko na amepata majeraha".
Sergio Aguero
Image captionSergio Aguero
Aguero anatarajiwa kurudi Manchester Ijumaa na atakaguliwa na kikosi cha madaktari wa City kabla ya kuelekea kwa mchuano wa Premier League watakapokaribishwa na Chelsea Jumamosi.
Polisi Amsterdam wameithibitishia BBC kwamba watu wawili walikuwa ndaniya taxi iliyohusika katika ajali katika eneo la De Boelelaan mjini humo.

Chanzo: BBC

MTANDAO WA TWITTER KUONGEZA MANENO HADI 280

Mtandao wa Twitter kwa sasa upo katika majaribio ya kuongeza maandishi yake kutoka 140 hadi 280 hii ikiwa ni mara mbili ya hayo ya awali.

Sababu za kuongeza idadi hiyo ya maneno ni kwamba kuna wakati mtu unaweza kuwa na hoja fulani inayozidi ukomo wa maneno lakini ukashindwa kuiandika ama ukapunguza idadi ya maneno ambayo wakati mwingine huwa ni ya muhimu sana katika tweet husika.
Huu ni mfano wa vile tweet ya sasa ilivyo na vile ambavyo ongezeko litakuwa kwa maneno 280.

Afisa Masoko Aliza Rosen wa Twitter na Mhandisi wa Twitter Japan  Ikuhiro Ihara wamesema kuwa katika mchakato wa kuruhusu jambo hili watu wachache watachaguliwa kwa majaribio na pia watakuwa wakikusanya maoni na kupata mrejesho kutoka kwa watumiaji wa Twitter kabla hawajafikia uamuzi wa kuruhusu ongezeko hilo la maneno.

Jinsi tweet za Kiingereza na Kispanyola zinavyokuwa ukilinganisha na Kijapan.

Zipo lugha ambazo hazitahusika kabisa katika jaribio ambazo ni Kichina, Kijapan na Kikorea sababu ni kwamba karibia 0.4% ya watu wanaotweet kwa lugha hizo hasa kijapan ndiyo hufikia ukomo wa sasa uliopo wakati lugha kama Kifaransa, Kiingereza, Kispanyora na nyinginezo 9% ya wanaotweet hufika ukomo wa maneno 140 kwa hiyo wakaona umuhimu wa kuongeza maneno.

Aidha utafiti uliofanywa na mtandao huo unadai kuwa watu wengi wanakasirishwa na ukomo wa idadi hiyo ya maneno.

IRAN IMEFANYA JARIBIO LA KOMBORA LA NYUKLIA

Iran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.

Kombora hilo lilionyeshwa hadharani katika maonyesha ya kijeshi jana Ijumaa.

Iran imesema kuwa kombora hilo linaweza kusafiri mwendo wa kilomita 2,000.

Kituo cha runinga cha taifa hilo kilionyesha picha za sherehe hizo.

Kombora la kwanza la Khorram-Shahr lilirushwa angani Januari lakini likalipuka katikati ya mwendo.

Jaribio hilo lilifanywa siku chache baada ya Rais Trump wa Marekani kushambulia Iran katika hotuba yake katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Rais wa Iran, Hassan Rouhani, ametetea hatua ya taifa lake kuimarisha zana zake kwa lengo la kujitetea.



Chanzo

AUDIO | HUNTER & D FLEVA FEAT BARNABA-FURSA | DOWNLOAD


Ngoma mpya kutoka kwa Hunter & D Fleva wakimpa shavu Baarnaba Boy Classic. Ngoma imefanyika Combination sound ukiwa ni mono wa fundi Man Water. VENANCE BLOG inakupa nafasi ya kudownload na kusikiliza.

DOWNLOAD

KAMPUNI YA ACACIA KUPUNGUZA SHUGHULI NA WAFANYAKAZI NCHINI

Kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia imesema itapunguza wafanyakazi na shughuli zake za migodini ikiwa ni sehemu ya athari ya uzuiaji wa usafirishwaji wa makinikia uliowekwa na serikali ya Tanzania mwezi Machi mwaka huu.

Kampuni hiyo inasema wakati baadhi ya shughuli ndani ya mashimo yake ya dhahabu zitasimama, ndani ya wiki nne, uchenjuaji wa makininia pia nao utasimama.

"Kwa masikitiko, mpango huu utapelekea kupunguzwa kwa ajira kati ya wafanyakazi 1,200 waliopo hivi sasa na wanakandarasi 800" kampuni hiyo imesema kwenye taarifa.

Hata hivyo Acacia hawajasema ni wafanyakazi wangapi hasa watakaopunguzwa kazini.

Kampuni hiyo ambayo imeorodheshwa katika soko la hisa la London nchini Uingereza inasema kusimamishwa kwa usafirishwaji wa makinikia kumekuwa kukiikosesha takribani $15 milioni (Dola milioni kumi na tano) kwa mwezi.

Acacia wanasema hali hiyo imesababisha uendeshaji wa siku hadi siku wa moja ya migodi yake mikubwa Bulyanhulu kuathiriwa kwa kiasi kikubwa.

Acacia imekuwa katika mgogoro na serikali ya Tanzania kwa takribani miezi sita sasa tangu serikali ya Tanzania izuie usafirishwaji wa makinikia ya kampuni hiyo nje ya nchi.

Lakini serikali ya Tanzania pia imekuwa ikiishutumu kampuni ya Acacia kwa kukwepa kulipa kodi inayostahili, tuhuma ambazo kampuni hiyo imezikanusha.

Mazungumzo yanayolenga kutatua mgogoro huu bado yanaendelea.

"Kampuni ina matumaini kwamba majadiliano yanayoendelea kati ya Barrick na serikali ya Tanzania yatatatua kuzuiwa kwa usafirishaji wa makinikia na kurudisha mazingira ya uendeshaji wa mgodi wa Bulyanhulu katika hali nzuri" inasema taarifa ya Acacia.

Mapema mwaka huu Rais John Magufuli aliamuru uchunguzi wa kina katika sekta ya madini nchini Tanzania huku akiamini kwamba Tanzania hainufaiki vya kutosha kutokana na sekta ya madini.


Chanzo: BBC

VIDEO | TAZAMA ROMA-ZIMBABWE WIMBO MPYA

Huu ni wimbo mpya wa Roma Mkatoliki. VENANCE BLOG inakupa nafasi ya kuutazama hapa chini:




RAIS PUTIN AMEAGIZA WANADIPLOMASIA 755 WA MAREKANI KUONDOKA URUSI

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameagiza wafanyakazi 755 wa ubalozi wa Marekani nchini Urusi kusitisha shughuli zao kufikia Septemba mosi mwaka huu.

Urusi imeidhinisha hatua hiyo kwa ghadhabu kufuatia vikwazo vipya vilivyopitishwa na bunge la Marekani dhidi yake, kwa tuhuma za kuingilia uchaguzi wa taifa hilo mwaka jana.
Marekani kwa upande wake, inasema imesikitishwa na uamuzi huo, na inapima athari na kutafakari namna ya kujibu hatua hiyo.

Hatua hii ya Urusi imekuja baada ya vikwazo vipya dhidi ya Urusi kuidhinishwa kwa wingi wa kura na mabunge yote ya congress nchini Marekani Jumanne, licha ya kwamba Ikulu ya White house ilipinga kura hiyo.

Rais huyo wa Urusi ameapa kuwa upo uwezekano wa kuongeza vikwazo zaidi dhidi ya serikali ya Marekani.

Akizungumza kwenye televisheni ya taifa ya Urusi, rais Putin alisema kuwa alitarajia uhusiano baina ya Moscow na Washington ungebadilika na kuwa mzuri, lakini hilo haliwezekani kwa sasa.

Akizungumza wakati wa ziara yake nchini Estonia, makamu wa rais wa Marekani, Mike Pence, alisema anatumai kwamba mienendo ya serikali ya Urusi itabadilika.

Mashirika ya ujasusi nchini Marekani yanaamini kuwa Urusi ilijaribu kuingilia uchaguzi wa urais wa mwaka 2016 kwa lengo la kumsaidia Donald Trump kupata ushindi.
Urusi imekuwa ikikanusha kuingilia kwa vyovyote uchaguzi huo.


Chanzo: BBC

MMILIKI WA NGURDOTO HOTEL AFARIKI DUNIA


Mfanyabiashara maarufu nchini, Maleu Mrema amefariki dunia jana akiwa kwenye matibabu nchini Afrika Kusini.

Akizungumza na Mwananchi ndugu wa marehemu,Vincent Laswai alithibitisha msiba huo akiwa nyumbani kwa marehemu eneo la Uzunguni jijini Arusha.

Akihojiwa na gazeti la Mwananchi Laswai amesema kwamba alipokea taarifa za kifo cha marehemu jana saa 12 jioni na uongozi wa familia utatoa taarifa za kifo cha mfanyabiashara huyo leo.

Laswai, amesema kwamba ni mapema kuzungumzia chanzo cha kifo kwa sababu bado hawajapata taarifa kutoka katika hospitali aliyokuwa akitibiwa nchini humo.

Hivi karibuni marehemu Mrema alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya ambapo Juni mwaka huu alipelekwa Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu.



Chanzo: Mwananchi

PICHA 20 KUTOKA KWA DIAMOND NA ZARI WAKIWA KENYA WALIZOPOST INSTAGRAM

Diamond na Zari wameendelea na starehe zao huko Mombasa Kenya huku team ya WCB ikitia mguu pia mahali hapo; Harmonize na Sallam walihusika pia. Hizi ni baadhi ya picha kutoka katika mapumziko hayo.

Hapa Zari aliamua kumtania shemeji yake Harmonize.

mkubwa Simba na Zari katika starehe zao



Harmonize alipata nafasi ya kusema chochote BClub



Katika picha hii Diamond kaandika caption ya kiingereza ambayo Kiwashili chake ni "namwambia Harmonize kwamba wenye chuki wote hawana maana. Tuna uwezo na ni matarijiri"

Unamuona Zari anavyozidi kupendeza kama ndo kwanza ana miaka 12

Kila mtu apambane na mahusiano yake tu.



Huu mkao sasa Zari alivyomtegea Mond afu anajifanya kama hana habari yuko busy na simu


Sallam alihusika pia B Club

Wanapendeza hawa wapendanao



unamuona Zari?



KWA PICHA, MATUKIO, HABARI NA MAELEZO KAMA HAYA NA MENGINE MENGI USISITE KUTEMBELEA VENANCE BLOG:
Facebook: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venanceblog
email: venancegilbert@gmail.com

DIAMOND AWAJIA JUU WANAOMSEMA ZARI KUHUSU MSIBA WA MAMA YAKE

Mwanamuziki wa Tanzania aliyeikamata Afrika na Dunia kwa uimbaji wake wa lugha ya Kiswahili, Diamond Platnumz a.k.a Chibu Dangote, Baba Tee, Simba na majina mengineyo usiku wa leo amewajia juu hasa wadada wanaomsema mpenzi wake Zarina Hassan kufuatia kifo cha mama yake kilichotokea majuzi tu. Zari ameonekana na Diamond wakiwa katika starehe za mahusiano yao kitu kilichopelekea wadau na mashabiki wao kuliongelea suala hilo.

Kwa tamaduni za kiafrika na jinsi tulivyozoea, mtu anapofiwa hasa na Mama yake mzazi humchukua muda sana kabla ya kurudi katika utaratibu wa kawaida, hii imekuwa tofauti kwa Zari ambaye siku chache tu baada ya msiba ameonekana na Diamond wakiponda raha huku wakijirekodi video na kuzituma katika mtandao wa Instagram hali iliyopelekea mashabiki kuliongelea sana suala hilo.

Diamond Platnumz amefunguka baada ya kuonekana kukerwa na maneno ya watu katika mtandao wa Instgram na kuyaandika haya:
"Kuna vichupi kunuka wanajifanya wanajua sana uchungu wa misiba ya watu.... Mtoto wa watu katoka katika matatizo mfululizo, anatakiwa apelekwe sehemu tulivu apetiwepetiwe apate faraja!...sasa kama nyie hamna mabwana wa kuwafanyia hayo, Msijifanye ni Tamaduni na kulazimisha kila mtu awe kama nyie, eti kutwa nzima ajifungie chumbani kulia... Pambaneni na mahusiano yenu...! Nina siku 5 za kumpetipeti...! leo ndio kwanza Ya kwanza 😛"

Hii ni screenshoot ya ujumbe huo aliotuma Diamond Platnumz kwenye mtandao wa Instagram huku akiwa ametag eneo Mombasa, Kenya.


WASILIANA NA VENANCE BLOG:
Facebook page: VENANCE BLOG
Twitter: @Venancetz
Instagram: @venanceblog
email: venancegilbert@gmail.com

MAMBO YA MUHIMU KUFAHAMU NA KUZINGATIA KABLA YA KUCHAGUA KOZI (TAALUMA) CHUO KIKUU

Picha kwa hisani ya Debt.org

1.0 UTANGULIZI

Nilipokuwa mwanafunzi wa chuo kikuu nilisikia manung'uniko miongoni mwa wanafunzi wenzangu wengi wa vyuo vikuu ambayo yalitokana na taaluma wanazosoma. Kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea manung'uniko hayo miongoni mwa wasomi hawa tukiachilia mbali suala la ucheleweshwaji wa mikopo miongoni mwa wasomi hawa (kwa sasa changamoto hii inapungua kadiri siku zinavyosonga). Tatizo lingine ambalo linawasumbua wasomi hawa ni suala la uchaguzi wa taaluma gani akaisome Chuo Kikuu.

Uchaguzi wa taaluma (career choice) ni jambo nyeti sana na la kuzingatia kwa muhitimu yeyote wa elimu ya kuanzia kidato cha nne. Jamii yetu ya Tanzania haifahamu kwa undani kuhusu umuhimu wajambo hili lakini huku ndiko msingi hundaliwa. Mtu anapohitimu kidato cha nne na kupata ufaulu wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ama ngazi ya astashahada (certificate) na stashahada (diploma) hapo ndipo uchanguzi wa taaluma huanza. Kwa kuandika makala haya ninakusudia kutoa hamasa kwa wazazi na walezi na jamii kwa ujumla kuwasaidia vijana hawa katika uchaguzi wa taaluma zao za baadaye kulingana na uwezo wao na mambo wanayoyapenda.

Uchaguzi wa taaluma huanza na uchaguzi wa michepuo/tahasusi (combination) anayokwenda kuisoma mwanafunzi shuleni. Hii huathiri kwa kiasi kikubwa taaluma yake kwa namna chanya ama hasi. Hapa ninamaanisha kwamba mchepuo atakaosoma una uhusiano mkubwa na taalumza zianzofundishwa chuo chuo kikuu ama kutokuwa na uhusiano kabisa. 

Kuna mambo kadhaa ambayo huwaathiri wanafunzi wawapo vyuo vikuu kwa kutozingatia uchaguzi wa taaluma. Mambo hayo yaweza kuwa; kutoendelea na masomo ya Chuo Kikuu kutokana na kufeli masomo (Discontinuation from studies), kufeli majaribio mara kwa mara kutokana na kutoridhika na kile wanachosomea ama ugumu wa masomo. Sababu kubwa hapa zaweza kuwa tatu; kwanza, uchaguzi wa taaluma kwa kufuata mkumbo wa marafiki pili, kushawishiwa ama kuchaguliwa taaluma na mzazi ama mtu yeyote aliyesoma taaluma husika na kupata mafanikio kwa hivyo na mchaguaji anaona naye asome taaluma husika ili afanikiwe na tatu, ni upepo wa upatikanaji wa mkopo kwa vyuo vikuu.

Tuwapo shuleni hasa kidato cha 5 & 6 wanafunzi wengi hua na ndoto kubwa sana wakati mwingine kuliko hata kutambua uwezo wao uko katika mambo yepi. Hili husababishwa na marafiki, suala hili linaitwa mkumbo. Kwa mfano wanafunzi wengi wa Kidato cha Sita hubagua taaluma za kusoma kutokana na matakwa yao bila kutambua uwezo wao. Wapo wengine ambao hawafikirii chochote zaidi ya kusikiliza marafiki zao wanataka kusoma taaluma zipi (mkumbo) matokeo yake baadaye wakiwa vyuoni huanza kujilaumu ama baadaye hushindwa kuendelea na masomo yaani 'Discontinuing from studies'.

Jambo lingine ni kushawishiwa ama kuchaguliwa taaluma ya kusoma na wazazi/mlezi; mara nyingi wazazi/mlezi huwalazimisha vijana wao wakasome taaluma fulani bila kutambua uwezo wa kijana husika. Lakini pia kwa sababu mzazi/mlezi kufanikiwa katika taaluma husika anamlazimisha kijana asome taaluma aliyosoma yeye. Wakati mwingine wazazi hualazimisha kabisa kwamba vijana wao wasipofuta maagizo wanayoambiwa watajijua wenyewe. Jambo hili huwa ni zito na changamoto sana kwa sababu wazazi/walezi mara nyingi ndiyo hugharamia fedha za masomo vijana wao wawapo masomoni.

Vilevile kuna suala la upatikanani wa mkopo. Hili ni suala ambalo linawalazimu wengi kusoma taaluma fulani Elimu/Ualimu wa Sayansi, Udaktari, Uuguzi na Uhandisi n. k. kwa sababu ya upatikanaji mkopo wa serikali ama ufadhili wa masomo. Wengi wao huchelewa kukubaliana na hali hii, lakini baadaye pia kutokana na ufadhili wa serikali hujikuta hawana namna kwa sababu ya hali ya familia kutoweza kugharamia masomo. Wengine hugundua mambo fulani katika taaluma husika na kuamua kukubaliana na hali na kuendelea na masomo. Huu ni mfano tu ila katika taaluma nyingine ambazo sijazitaja wapo wenye mambo kama haya.


2.0 MAMBO YA MUHIMU KUZINGATIA WAKATI WA KUCHAGUA TAALUMA

Kuna mambo kadhaa unaweza kuyazingatia katika suala zima la kuchagua taaluma ya kusoma Chuo Kikuu, mambo hayo yaweza kuwa yafuatayo:

2.1. UJUZI ULIO NAO AMA KIPAJI

Japokuwa kuna baadhi ya taaluma haziihitaji ujuzi sana ni muhimu kutambua kuwa suala la ujuzi ni la muhimu katika kipi usomee. Mathelani ujuzi katika lugha, hesabu ama kuwa na uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu. Ujuzi ulio nao wewe utakusaidia kusoma vyema taaluma yako na kuifurahia huku ukiunoa zaidi ujuzi huo. hili pia linawahusu wenye vipaji, unaposoma taaluma inayokuza kipaji chako basi inekujenga zaidi kuwa na mtazamo mpana kuhusu kipaji na ndoto yako.

 2.2. MAMBO UPENDAYO

Baada ya kugundua ujuzi ama uwezo ulio nao, suala linalofuata ni kufahamu unapenda kufanya nini katika maisha yako baada ya kumaliza masomo. Lengo lako linatakiwa liwe kufanya jambo ambalo unalipenda, hii itakusaidia katika kuridhika na kuyafurahia masomo yako kwa kipindi chote utakochokuwa masomoni, utasoma kwa furaha sana na utakuwa umeridhika. Sanjari na hapo itakusaidia kujijenga vizuri kitaaluma na kukunoa vyema.

2.3. TAFUTA KITABU CHA CHUO KINACHOELEZEA KUHUSU CHUO (PROSPECTUS)

Prospectus ni kitabu kinachoelezea mambo yote ya msingi unayopaswa kuyafahamu kuhusu chuo. Kitabu hiki kinaelezea vizuri kuhusu taaluma mbalimbali zinazotolewa na chuo husika, hii inajumuisha na kozi ndogondogo ambazo hufundishwa kwa muda wote wa masomo kuanzia semista ya kwanza hadi ya mwisho. Kitabu hiki pia huonesha taarifa za kifedha kama ada inayotakiwa kulipwa kwa kila taaluma na michango mingine ya chuo. Muhimu zaidi kupitia kitabu hiki cha mwongozo ni kufahamu kuhusu taaluma utakayopenda kuisoma. Hapo utalinganisha  uwezo wako katika taaluma, yaani taaluma zipi utazimudu na zipi zinahitaji uongeze bidii. Pia kitabu hiki huwa na sifa za chini za kujiunga na masomo katika kila taaluma (mimimum entry qualification) hizi zinategea sana ufaulu wako wa Kidato cha Nne, Sita ama Diploma. Huna sababu ya kupata nakala ngumu ama kupiga simu kwenye chuo husika kwa sababu kitabu hiki huwekwa katika tovuti ya kila chuo.

2.4. PITIA KITABU CHA MWONGOZO CHA TCU (TCU GUIDEBOOK)

Kitabu hiki hutolewa kila mwaka wa masomo na Tume ya Vyuo Vikuu nchini. Hiki huwa na taaluma zinazotolewa na kila chuo pamoja na vigezo husika katika kila taaluma pamoja na ada yake. Taaluma ama chuo kisichokuwepo katika kitabu hiki huwa hakiruhusiwi kufanya udahili kwa mwaka husika. Katika kitabu hiki utakutana na vigezo vya chini ambavyo unatakiwa kukidhi ili kuingia katika ushindani wa taaluma husika. Mara nyingi ushindani unategemea na ufaulu wako kidato cha nne na kidato cha sita ama Diploma; jinsi ulivyofaulu vizuri ndivyo jinsi utakuwa katika nafasi za juu zaidi kuchaguliwa katika taaluma na chuo ulichotuma maombi. Vitabu vya Mwongozo hutolewa tofauti kwa Wahitimu wa Kidato cha Sita, Diploma wale wa Kutambuliwa kwa Kujifunza hapo Awali [Recognition for Prior Learning (RPL)]. Kila kimoja huainisha sifa kulingana na elimu husika.

2.5. CHAGUA TAALUMA UNAZOPENDA KULINGANA NA UWEZO NA VIPAUMBELE VYAKO

Katika hatua hii unatakiwa kuorodhesha taaluma unazotaka usoma. Kumbuka katika uchaguzi wako huo ni taaluma moja tu utatakiwa kusoma ama kwa kupangiwa na chuo kutokana na uchaguzi wako. Hili lisikupe shida kwa sababu wakati mwingine unaweza kubadili ukifika chuo ili mradi tu unavyo vigezo. Kuna baadhi ya vyuo huruhusu kubadili taaluma mwanzoni mwa semista ya kwanza. Vingine haviruhusu hivyo kama hujaipenda zaidi taaluma hiyo, unaweza kuahirisha mwaka wa masomo ama kuhama chuo. Nasisitiza kufanya uchaguzi sahihi zaidi ili kuepukana na kadhia hizo.

 2.6. USIFIKIRIE SANA KUHUSU UPATIKANAJI WA AJIRA

Wengi wetu tunasoma kwa kufikiria upatikanaji wa ajira, kwamba baada ya masomo tuuajiriwe ni sahihi pia lakini jambo la muhimu kwa sasa ni kusoma na kutengeneza wasifu mzuri katika masomo huku ukinoa kipaji na uwezo wako. Kumbuka umahiri wako ndiyo utakaokuajiri. Ukifika chuo masomo yawe kipaumbele wakati ukifanya mengine kama itakulazimu. Ukifikiria ajira kutokana na taaluma yako hutasoma kwa amani, soma mambo mazuri huja mbele ya safari.

2.7. CHAGUA CHUO NA TAALUMA KULINGANA NA UFAULU WAKO

Kumekuwepo na tabia ya watu kung'ang'ania kuchagua taaluma fulani ama vyuo fulani kutokana na jinsi wanavyopenda wao na sifa na hadhi za vyuo watakavyo pasipokuzingatia ufaulu wao. Wengi wamejikuta wakikosa nafasi za masomo kwa mwaka husika, hii inatokana na kung'ang'ania chuo kutokana na hadhi yake ilihali mtu ana ufalu mdogo kushindana na wenye ufaulu mkubwa. Hakikisha ufaulu wako unakidhi vigezo vya ushindani wa taaluma na vyuo unavyochagua. Kama ufaulu wako ni wa chini ni vyema kutafuta taaluma na vyuo ambazo entry qualifications zinaendana na ufaulu wako. Usipozingatia hili utapoteza muda kurudia zoezi la udahili ama utakosa kabisa nafasi kwa mwaka husika. Zingatia kwamba ufaulu wako ndiyo ushindani wako. Usipochaguliwa katika chuo na taaluma fulani hakikisha una mbadala mwingine wa chuo na si kung'ang'ania uchaguzi ambao hujachaguliwa. Na uzuri wa siku hizi ni kwamba usipochaguliwa taaluma fulani unapewa na sababu, usipuuze sababu hizo.

2.8. FANYA UAMUZI SAHIHI NA UTUME MAOMBI KATIKA VYUO UNAVYOVIPENDA

Baada ya kuridhika na machaguo yako ya taaluma, hakikisha umechagua machaguo sahihi bila kukurupuka na kisha tuma maombi vyuoni. Kwa sasa maombi yanatumwa kwenye vyuo husika ama kwa kupeleka maombi chuo moja kwa moja ama kwa kutumia njia ya mtandao na sio kupitia TCU kama ilivyokuwa miaka iliyopita. Njia ya mtandao ni rahisi sana ufatiliaji wake kuliko kupeleka maombi kwa njia ya barua.

 
3.0. MAMBO MENGINE YA KUZINGATIA

Hapo juu nimeainisha mambo ya muhimu kwa uchaguzi wa taaluma hasa vyuo vya ndani. Hapa chini nimeeleza kwa ufupi mambo ya jumla kuhusu uchaguzi utakaoufanya, sababu nyingine zaweza kukinzana na maelezo hapo juu kuliangana na mtazamo wa mtu.

3.1. SOKO LA AJIRA

Kama wewe ni mtu wa kuzingatia sana soko la ajira ni muhimu kwako kufanya utafiti kufahamu taaluma ambazo zina wigo mpana wa ajira ama zinazoajiri sana na hata zile ambazo zina uchache wa wataalamu. Wigo mpana wa ajira ni kuingia katika idara mbalimbali za ajira na kuweza kuendana na idara hizo bila kufundishwa sana au tena baada ya kumaliza masomo. Ajira zinazoajiri sana ni zile ambazo tasisi huhitaji watu wengi mara nyingi kulingana na umuhimu wake ingawa taaluma zote ni muhimu. Ajira zenye uchache wa wataalamu ni zile ambazo watu hawajasoma sana taaluma hizo kutokana na upya wake.

3.2. MSHAHARA NA MUDA

Ijapokuwa jambo unalolipenda ni muhimu zaidi, suala la mshahara ni la muhimu pia. Zingatia mshahara na malupulupu mengine na faida utakazozipata katika taaluma unayotaka kusoma kulingana na matarajio yako ya baadaye. Suala la muda pia ni muhimu kwa sababu zipo taaluma zitakuhitaji kupatikana hata katika muda wa zaida hata baada ya saa za kawaida za kazi.

3.3. UWIANO KATI YA KAZI NA MAISHA

Chunguza namna taaluma unayochagua itaathiri muda wa kazi na maisha yako binafsi , familia na matarajio yako mengine.

3.4. UKUAJI NA MAENDELEO

Zingatia ukuaji wako kitaaluma na maendeleo yako binafsi. Chagua taaluma ambayo itakupa wigo mpana wa kukua na kuendelea binafsi na kuendeleza taaluma husika yaani kuwa na mchango chanya katika maisha yako na taaluma yenyewe.

3.5. MALENGO ENDELEVU

Fikiria kuhusu malengo yako katika miaka ijayo. Je taaluma hiyo itakusaidia kufika huko ama utakuwa mtu wa kujilaumu tu na kujuta kwa nini uliichagua kuisoma? Fikiria kwa makini sana.

3.6. AFYA YAKO NA UZIMA

Hakikisha kwamba unakuwa katika taaluma ambayo inajali afya yako na uzima. Zipo baadhi ya taaluma huchosha mwili na akili pia, ni muhimu kuzifahamu ili ufahamu namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

3.7. MAZINGIRA NA UTAMADUNI WA KAZI

Baadhi ya taaluma zitakufanya uwe mtu wa kusafiri na kuhama hama sana. Hakikisha unakuwa tayari kumudu mambo hayo. Pia fikiria kuhusu utamaduni na miiko ya taaluma husika kama inaendana na tabia zako.

 

4.0. MUHTASARI NA MAELEZO MENGINE

Mara baada ya kufanya maombi kila Chuo hufanya utaratibu wa udahili kwa mfumo wa ushindani walioweka wenyewe lakini utaratibu huo lazima uendane na vigezo vya Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU). Katika zama hizi za kila Chuo kufanya udahili wenyewe kunawapa nafasi ya wao kuchagua wale wanaowataka kulingana na vigezo vyao, kwa hiyo unashauriwa kuangalia ufaulu wako hasa idadi ya alama ulizo nazo (cutting points) katika mchepuo/tahasusi uliyosoma Kidato cha Sita ama ufaulu wako katika ngazi ya Stashahada (Diploma) wakati mwingine hata matokeo ya Kidato cha Nne huangaliwa. Kwa ufupi ni kwamba wenye alama za juu huwa na uwezekano mkubwa wa kuchaguliwa ukilinganisha na wenye alama za chini.

Vyuo vinapomaliza uchambuzi na udahili hutangaza majina ya wale waliochaguliwa kujiunga na vyuo hivyo moja kwa moja ama waliochaguliwa hapo na kuchaguliwa kwingineko, kwa hiyo hapa mdahiliwa hutakiwa kuchagua chuo kimoja na taaluma moja na kisha kuthibitisha chuo na taaluma apendayo kuisoma. Aidha vyuo pia hutoa sababu za kwa nini wadahiliwa wengine hawakufanikiwa kuchaguliwa na mara nyingi sababu hizo si za kupuuzia hata kidogo hasa ukiambiwa hujafikisha alama za ushindani ama kutokidhi vigezo vya taaluma husika. Mdahiliwa hutakiwa kuzingatia sababu hizo za kutochaguliwa na kujaribu awamu nyingine. Utaratibu huwa ni uleule lakini katika awamu zinazofuata taaluma fulani huondolewa kwenye mfumo kutokana na kuuwa zimesjaa wadahiliwa na hii ndiyo maana unasisitizwa kusoma taarifa kwa kina kuhusu uchaguzi wako wa taaluma.

Utaratibu huendelea hivyo mpaka awamu zote zitakapokwisha. Jambo la muhimu ni kwamba kuna wakati usipozingatia baadhi ya maelezo unaweza kukosa nafasi ya chuo kwa mwaka husika hasa kutozingatia ufaulu wako ama niseme idadi ya alama ulizo nazo katika mchepuo ama Stashahada yako. Ni muhimu sana kuwa makini. Jambo lingine la muhimu tena ni kuhakikisha taarifa zako binafsi zinakua sahihi kwenye mfumo wa udahili. Zingatia yote niliyoyaeleza hapa kuepuka usumbufu.

Unaweza kumtafuta mtu mwenye ufahamu wa mambo haya akakuelekeza vizuri zaidi ama unaweza kuwasiliana name kwa namba nilizoweka hapa chini. Huwa natoa ushauri huu BURE kabisa niapokuwa na muda. Mawasiliano yangu yapo hapa chini.

 

Makala haya yameandaliwa na kuandikwa na

Venance Gilbert

Mwalimu, Shahada ya Kwanza ya Elimu katika Lugha na Menejimenti (BED-LM)

Chuo Kikuu Mzumbe

venancegilbert@gmail.com

0753400208.

Yalichapishwa mara ya kwanza 25/07/2017 yamefanyiwa marekebisho 05/06/2024.

SCHOLARSHIPS FOR UNDERGRADUATE, GRADUATE AND PhD STUDIES

Tokeo la picha la VENANCE BLOG
The listed Universities below offer various scholarship programmes across the world. If you are interested you may follow the instruction basing on your status of education and interests of the course you wish to perform.



Rhodes Trust, Oxford University
Application Deadline: Various

China Three Gorges University, China
Application Deadline: July 7, 2017

Nanjing University of Information Science & Technology, China
Application Deadline: June 15, 2017

Beijing Sport University, China
Application Deadline: July 10, 2017

The Southeast Asian Regional Center for Graduate Study and Research in Agriculture (SEARCA)
Application Deadline: July 31, 2018

Durham University, United Kingdom
Application Deadline: July 28, 2017

University of New Mexico
Course Starts on June 12, 2017 

Queen Mary University of London, United Kingdom
Application Deadline: January 15, 2018

University of Ghana
Application Deadline: November 3, 2017

Plymouth University in United Kingdom
Application Deadline: June 30, 2017

University of Cape Town, South Africa
Application Deadline: July 31, 2017

Humboldt University of Berlin, Germany
Application Deadline: June 15, 2017

University of Maryland
Course Starts on August 21, 2017

European Commission
Application Deadline: September 8, 2017

Charles Sturt University, Australia
Application Deadline: June 12, 2017

Sapienza University of Rome, Italy
Application Deadline: July 31, 2017

University of Melbourne in Australia
Application Deadline: July 16, 2017

University of Zaragoza, Spain
Application Deadline: June 15, 2017

Trinity College Dublin, Ireland
Application Deadline: June 14, 2017

Penn State University and Coursera
MOOC starts from June 5, 2017

The Radio Television Digital News Association
Application Deadline: June 30, 2017

Government of Hong Kong
Application Deadline: June 19, 2017

University of Lausanne, Switzerland
Application Deadline: June 30, 2017

Uppsala University ,Sweden
Application Deadline: June 30, 2017

University of Greenwich, United Kingdom
Application Deadline: June 28, 2017

The Japan Foundation
Application Deadline: June 1, 2017

Government of Belize
Application Deadline: June 16, 2017

University of Sao Paulo, Brazil
Application Deadline: July 25, 2017

Oxford Internet Institute, UK
Application Deadline: June 26, 2017

University of North Carolina, USA
Application Deadline: August 2, 2017

University of Bristol, United Kingdom
Application Deadline: July 7, 2017

University of Newcastle, Australia
Application Deadline: June 30, 2017

Dublin City University, Ireland
Application Deadline: June 30, 2017

University of Cape Town, South Africa
Application Deadline: Open

University of Oslo, Norway
Application Deadline: June 26, 2017

University of New South Wales, Australia
Application Deadline: July10, 2017

Department of Science & Technology, India
Application Deadline: June 30, 2017

John S. Latsis Public Benefit Foundation
Application Deadline: June 7, 2017

Indian Institute of Management, Bangalore
Course Starts on August 3, 2017

RWTH Aachen University
Course Starts on July 19, 2017




Source: Scholarship Position