Skip to main content

MAMBO YA MUHIMU KUFAHAMU NA KUZINGATIA KABLA YA KUCHAGUA KOZI (TAALUMA) CHUO KIKUU

Picha kwa hisani ya Debt.org

1.0 UTANGULIZI

Nilipokuwa mwanafunzi wa chuo kikuu nilisikia manung'uniko miongoni mwa wanafunzi wenzangu wengi wa vyuo vikuu ambayo yalitokana na taaluma wanazosoma. Kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea manung'uniko hayo miongoni mwa wasomi hawa tukiachilia mbali suala la ucheleweshwaji wa mikopo miongoni mwa wasomi hawa (kwa sasa changamoto hii inapungua kadiri siku zinavyosonga). Tatizo lingine ambalo linawasumbua wasomi hawa ni suala la uchaguzi wa taaluma gani akaisome Chuo Kikuu.

Uchaguzi wa taaluma (career choice) ni jambo nyeti sana na la kuzingatia kwa muhitimu yeyote wa elimu ya kuanzia kidato cha nne. Jamii yetu ya Tanzania haifahamu kwa undani kuhusu umuhimu wajambo hili lakini huku ndiko msingi hundaliwa. Mtu anapohitimu kidato cha nne na kupata ufaulu wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ama ngazi ya astashahada (certificate) na stashahada (diploma) hapo ndipo uchanguzi wa taaluma huanza. Kwa kuandika makala haya ninakusudia kutoa hamasa kwa wazazi na walezi na jamii kwa ujumla kuwasaidia vijana hawa katika uchaguzi wa taaluma zao za baadaye kulingana na uwezo wao na mambo wanayoyapenda.

Uchaguzi wa taaluma huanza na uchaguzi wa michepuo/tahasusi (combination) anayokwenda kuisoma mwanafunzi shuleni. Hii huathiri kwa kiasi kikubwa taaluma yake kwa namna chanya ama hasi. Hapa ninamaanisha kwamba mchepuo atakaosoma una uhusiano mkubwa na taalumza zianzofundishwa chuo chuo kikuu ama kutokuwa na uhusiano kabisa. 

Kuna mambo kadhaa ambayo huwaathiri wanafunzi wawapo vyuo vikuu kwa kutozingatia uchaguzi wa taaluma. Mambo hayo yaweza kuwa; kutoendelea na masomo ya Chuo Kikuu kutokana na kufeli masomo (Discontinuation from studies), kufeli majaribio mara kwa mara kutokana na kutoridhika na kile wanachosomea ama ugumu wa masomo. Sababu kubwa hapa zaweza kuwa tatu; kwanza, uchaguzi wa taaluma kwa kufuata mkumbo wa marafiki pili, kushawishiwa ama kuchaguliwa taaluma na mzazi ama mtu yeyote aliyesoma taaluma husika na kupata mafanikio kwa hivyo na mchaguaji anaona naye asome taaluma husika ili afanikiwe na tatu, ni upepo wa upatikanaji wa mkopo kwa vyuo vikuu.

Tuwapo shuleni hasa kidato cha 5 & 6 wanafunzi wengi hua na ndoto kubwa sana wakati mwingine kuliko hata kutambua uwezo wao uko katika mambo yepi. Hili husababishwa na marafiki, suala hili linaitwa mkumbo. Kwa mfano wanafunzi wengi wa Kidato cha Sita hubagua taaluma za kusoma kutokana na matakwa yao bila kutambua uwezo wao. Wapo wengine ambao hawafikirii chochote zaidi ya kusikiliza marafiki zao wanataka kusoma taaluma zipi (mkumbo) matokeo yake baadaye wakiwa vyuoni huanza kujilaumu ama baadaye hushindwa kuendelea na masomo yaani 'Discontinuing from studies'.

Jambo lingine ni kushawishiwa ama kuchaguliwa taaluma ya kusoma na wazazi/mlezi; mara nyingi wazazi/mlezi huwalazimisha vijana wao wakasome taaluma fulani bila kutambua uwezo wa kijana husika. Lakini pia kwa sababu mzazi/mlezi kufanikiwa katika taaluma husika anamlazimisha kijana asome taaluma aliyosoma yeye. Wakati mwingine wazazi hualazimisha kabisa kwamba vijana wao wasipofuta maagizo wanayoambiwa watajijua wenyewe. Jambo hili huwa ni zito na changamoto sana kwa sababu wazazi/walezi mara nyingi ndiyo hugharamia fedha za masomo vijana wao wawapo masomoni.

Vilevile kuna suala la upatikanani wa mkopo. Hili ni suala ambalo linawalazimu wengi kusoma taaluma fulani Elimu/Ualimu wa Sayansi, Udaktari, Uuguzi na Uhandisi n. k. kwa sababu ya upatikanaji mkopo wa serikali ama ufadhili wa masomo. Wengi wao huchelewa kukubaliana na hali hii, lakini baadaye pia kutokana na ufadhili wa serikali hujikuta hawana namna kwa sababu ya hali ya familia kutoweza kugharamia masomo. Wengine hugundua mambo fulani katika taaluma husika na kuamua kukubaliana na hali na kuendelea na masomo. Huu ni mfano tu ila katika taaluma nyingine ambazo sijazitaja wapo wenye mambo kama haya.


2.0 MAMBO YA MUHIMU KUZINGATIA WAKATI WA KUCHAGUA TAALUMA

Kuna mambo kadhaa unaweza kuyazingatia katika suala zima la kuchagua taaluma ya kusoma Chuo Kikuu, mambo hayo yaweza kuwa yafuatayo:

2.1. UJUZI ULIO NAO AMA KIPAJI

Japokuwa kuna baadhi ya taaluma haziihitaji ujuzi sana ni muhimu kutambua kuwa suala la ujuzi ni la muhimu katika kipi usomee. Mathelani ujuzi katika lugha, hesabu ama kuwa na uwezo wa kuhifadhi kumbukumbu. Ujuzi ulio nao wewe utakusaidia kusoma vyema taaluma yako na kuifurahia huku ukiunoa zaidi ujuzi huo. hili pia linawahusu wenye vipaji, unaposoma taaluma inayokuza kipaji chako basi inekujenga zaidi kuwa na mtazamo mpana kuhusu kipaji na ndoto yako.

 2.2. MAMBO UPENDAYO

Baada ya kugundua ujuzi ama uwezo ulio nao, suala linalofuata ni kufahamu unapenda kufanya nini katika maisha yako baada ya kumaliza masomo. Lengo lako linatakiwa liwe kufanya jambo ambalo unalipenda, hii itakusaidia katika kuridhika na kuyafurahia masomo yako kwa kipindi chote utakochokuwa masomoni, utasoma kwa furaha sana na utakuwa umeridhika. Sanjari na hapo itakusaidia kujijenga vizuri kitaaluma na kukunoa vyema.

2.3. TAFUTA KITABU CHA CHUO KINACHOELEZEA KUHUSU CHUO (PROSPECTUS)

Prospectus ni kitabu kinachoelezea mambo yote ya msingi unayopaswa kuyafahamu kuhusu chuo. Kitabu hiki kinaelezea vizuri kuhusu taaluma mbalimbali zinazotolewa na chuo husika, hii inajumuisha na kozi ndogondogo ambazo hufundishwa kwa muda wote wa masomo kuanzia semista ya kwanza hadi ya mwisho. Kitabu hiki pia huonesha taarifa za kifedha kama ada inayotakiwa kulipwa kwa kila taaluma na michango mingine ya chuo. Muhimu zaidi kupitia kitabu hiki cha mwongozo ni kufahamu kuhusu taaluma utakayopenda kuisoma. Hapo utalinganisha  uwezo wako katika taaluma, yaani taaluma zipi utazimudu na zipi zinahitaji uongeze bidii. Pia kitabu hiki huwa na sifa za chini za kujiunga na masomo katika kila taaluma (mimimum entry qualification) hizi zinategea sana ufaulu wako wa Kidato cha Nne, Sita ama Diploma. Huna sababu ya kupata nakala ngumu ama kupiga simu kwenye chuo husika kwa sababu kitabu hiki huwekwa katika tovuti ya kila chuo.

2.4. PITIA KITABU CHA MWONGOZO CHA TCU (TCU GUIDEBOOK)

Kitabu hiki hutolewa kila mwaka wa masomo na Tume ya Vyuo Vikuu nchini. Hiki huwa na taaluma zinazotolewa na kila chuo pamoja na vigezo husika katika kila taaluma pamoja na ada yake. Taaluma ama chuo kisichokuwepo katika kitabu hiki huwa hakiruhusiwi kufanya udahili kwa mwaka husika. Katika kitabu hiki utakutana na vigezo vya chini ambavyo unatakiwa kukidhi ili kuingia katika ushindani wa taaluma husika. Mara nyingi ushindani unategemea na ufaulu wako kidato cha nne na kidato cha sita ama Diploma; jinsi ulivyofaulu vizuri ndivyo jinsi utakuwa katika nafasi za juu zaidi kuchaguliwa katika taaluma na chuo ulichotuma maombi. Vitabu vya Mwongozo hutolewa tofauti kwa Wahitimu wa Kidato cha Sita, Diploma wale wa Kutambuliwa kwa Kujifunza hapo Awali [Recognition for Prior Learning (RPL)]. Kila kimoja huainisha sifa kulingana na elimu husika.

2.5. CHAGUA TAALUMA UNAZOPENDA KULINGANA NA UWEZO NA VIPAUMBELE VYAKO

Katika hatua hii unatakiwa kuorodhesha taaluma unazotaka usoma. Kumbuka katika uchaguzi wako huo ni taaluma moja tu utatakiwa kusoma ama kwa kupangiwa na chuo kutokana na uchaguzi wako. Hili lisikupe shida kwa sababu wakati mwingine unaweza kubadili ukifika chuo ili mradi tu unavyo vigezo. Kuna baadhi ya vyuo huruhusu kubadili taaluma mwanzoni mwa semista ya kwanza. Vingine haviruhusu hivyo kama hujaipenda zaidi taaluma hiyo, unaweza kuahirisha mwaka wa masomo ama kuhama chuo. Nasisitiza kufanya uchaguzi sahihi zaidi ili kuepukana na kadhia hizo.

 2.6. USIFIKIRIE SANA KUHUSU UPATIKANAJI WA AJIRA

Wengi wetu tunasoma kwa kufikiria upatikanaji wa ajira, kwamba baada ya masomo tuuajiriwe ni sahihi pia lakini jambo la muhimu kwa sasa ni kusoma na kutengeneza wasifu mzuri katika masomo huku ukinoa kipaji na uwezo wako. Kumbuka umahiri wako ndiyo utakaokuajiri. Ukifika chuo masomo yawe kipaumbele wakati ukifanya mengine kama itakulazimu. Ukifikiria ajira kutokana na taaluma yako hutasoma kwa amani, soma mambo mazuri huja mbele ya safari.

2.7. CHAGUA CHUO NA TAALUMA KULINGANA NA UFAULU WAKO

Kumekuwepo na tabia ya watu kung'ang'ania kuchagua taaluma fulani ama vyuo fulani kutokana na jinsi wanavyopenda wao na sifa na hadhi za vyuo watakavyo pasipokuzingatia ufaulu wao. Wengi wamejikuta wakikosa nafasi za masomo kwa mwaka husika, hii inatokana na kung'ang'ania chuo kutokana na hadhi yake ilihali mtu ana ufalu mdogo kushindana na wenye ufaulu mkubwa. Hakikisha ufaulu wako unakidhi vigezo vya ushindani wa taaluma na vyuo unavyochagua. Kama ufaulu wako ni wa chini ni vyema kutafuta taaluma na vyuo ambazo entry qualifications zinaendana na ufaulu wako. Usipozingatia hili utapoteza muda kurudia zoezi la udahili ama utakosa kabisa nafasi kwa mwaka husika. Zingatia kwamba ufaulu wako ndiyo ushindani wako. Usipochaguliwa katika chuo na taaluma fulani hakikisha una mbadala mwingine wa chuo na si kung'ang'ania uchaguzi ambao hujachaguliwa. Na uzuri wa siku hizi ni kwamba usipochaguliwa taaluma fulani unapewa na sababu, usipuuze sababu hizo.

2.8. FANYA UAMUZI SAHIHI NA UTUME MAOMBI KATIKA VYUO UNAVYOVIPENDA

Baada ya kuridhika na machaguo yako ya taaluma, hakikisha umechagua machaguo sahihi bila kukurupuka na kisha tuma maombi vyuoni. Kwa sasa maombi yanatumwa kwenye vyuo husika ama kwa kupeleka maombi chuo moja kwa moja ama kwa kutumia njia ya mtandao na sio kupitia TCU kama ilivyokuwa miaka iliyopita. Njia ya mtandao ni rahisi sana ufatiliaji wake kuliko kupeleka maombi kwa njia ya barua.

 
3.0. MAMBO MENGINE YA KUZINGATIA

Hapo juu nimeainisha mambo ya muhimu kwa uchaguzi wa taaluma hasa vyuo vya ndani. Hapa chini nimeeleza kwa ufupi mambo ya jumla kuhusu uchaguzi utakaoufanya, sababu nyingine zaweza kukinzana na maelezo hapo juu kuliangana na mtazamo wa mtu.

3.1. SOKO LA AJIRA

Kama wewe ni mtu wa kuzingatia sana soko la ajira ni muhimu kwako kufanya utafiti kufahamu taaluma ambazo zina wigo mpana wa ajira ama zinazoajiri sana na hata zile ambazo zina uchache wa wataalamu. Wigo mpana wa ajira ni kuingia katika idara mbalimbali za ajira na kuweza kuendana na idara hizo bila kufundishwa sana au tena baada ya kumaliza masomo. Ajira zinazoajiri sana ni zile ambazo tasisi huhitaji watu wengi mara nyingi kulingana na umuhimu wake ingawa taaluma zote ni muhimu. Ajira zenye uchache wa wataalamu ni zile ambazo watu hawajasoma sana taaluma hizo kutokana na upya wake.

3.2. MSHAHARA NA MUDA

Ijapokuwa jambo unalolipenda ni muhimu zaidi, suala la mshahara ni la muhimu pia. Zingatia mshahara na malupulupu mengine na faida utakazozipata katika taaluma unayotaka kusoma kulingana na matarajio yako ya baadaye. Suala la muda pia ni muhimu kwa sababu zipo taaluma zitakuhitaji kupatikana hata katika muda wa zaida hata baada ya saa za kawaida za kazi.

3.3. UWIANO KATI YA KAZI NA MAISHA

Chunguza namna taaluma unayochagua itaathiri muda wa kazi na maisha yako binafsi , familia na matarajio yako mengine.

3.4. UKUAJI NA MAENDELEO

Zingatia ukuaji wako kitaaluma na maendeleo yako binafsi. Chagua taaluma ambayo itakupa wigo mpana wa kukua na kuendelea binafsi na kuendeleza taaluma husika yaani kuwa na mchango chanya katika maisha yako na taaluma yenyewe.

3.5. MALENGO ENDELEVU

Fikiria kuhusu malengo yako katika miaka ijayo. Je taaluma hiyo itakusaidia kufika huko ama utakuwa mtu wa kujilaumu tu na kujuta kwa nini uliichagua kuisoma? Fikiria kwa makini sana.

3.6. AFYA YAKO NA UZIMA

Hakikisha kwamba unakuwa katika taaluma ambayo inajali afya yako na uzima. Zipo baadhi ya taaluma huchosha mwili na akili pia, ni muhimu kuzifahamu ili ufahamu namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

3.7. MAZINGIRA NA UTAMADUNI WA KAZI

Baadhi ya taaluma zitakufanya uwe mtu wa kusafiri na kuhama hama sana. Hakikisha unakuwa tayari kumudu mambo hayo. Pia fikiria kuhusu utamaduni na miiko ya taaluma husika kama inaendana na tabia zako.

 

4.0. MUHTASARI NA MAELEZO MENGINE

Mara baada ya kufanya maombi kila Chuo hufanya utaratibu wa udahili kwa mfumo wa ushindani walioweka wenyewe lakini utaratibu huo lazima uendane na vigezo vya Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU). Katika zama hizi za kila Chuo kufanya udahili wenyewe kunawapa nafasi ya wao kuchagua wale wanaowataka kulingana na vigezo vyao, kwa hiyo unashauriwa kuangalia ufaulu wako hasa idadi ya alama ulizo nazo (cutting points) katika mchepuo/tahasusi uliyosoma Kidato cha Sita ama ufaulu wako katika ngazi ya Stashahada (Diploma) wakati mwingine hata matokeo ya Kidato cha Nne huangaliwa. Kwa ufupi ni kwamba wenye alama za juu huwa na uwezekano mkubwa wa kuchaguliwa ukilinganisha na wenye alama za chini.

Vyuo vinapomaliza uchambuzi na udahili hutangaza majina ya wale waliochaguliwa kujiunga na vyuo hivyo moja kwa moja ama waliochaguliwa hapo na kuchaguliwa kwingineko, kwa hiyo hapa mdahiliwa hutakiwa kuchagua chuo kimoja na taaluma moja na kisha kuthibitisha chuo na taaluma apendayo kuisoma. Aidha vyuo pia hutoa sababu za kwa nini wadahiliwa wengine hawakufanikiwa kuchaguliwa na mara nyingi sababu hizo si za kupuuzia hata kidogo hasa ukiambiwa hujafikisha alama za ushindani ama kutokidhi vigezo vya taaluma husika. Mdahiliwa hutakiwa kuzingatia sababu hizo za kutochaguliwa na kujaribu awamu nyingine. Utaratibu huwa ni uleule lakini katika awamu zinazofuata taaluma fulani huondolewa kwenye mfumo kutokana na kuuwa zimesjaa wadahiliwa na hii ndiyo maana unasisitizwa kusoma taarifa kwa kina kuhusu uchaguzi wako wa taaluma.

Utaratibu huendelea hivyo mpaka awamu zote zitakapokwisha. Jambo la muhimu ni kwamba kuna wakati usipozingatia baadhi ya maelezo unaweza kukosa nafasi ya chuo kwa mwaka husika hasa kutozingatia ufaulu wako ama niseme idadi ya alama ulizo nazo katika mchepuo ama Stashahada yako. Ni muhimu sana kuwa makini. Jambo lingine la muhimu tena ni kuhakikisha taarifa zako binafsi zinakua sahihi kwenye mfumo wa udahili. Zingatia yote niliyoyaeleza hapa kuepuka usumbufu.

Unaweza kumtafuta mtu mwenye ufahamu wa mambo haya akakuelekeza vizuri zaidi ama unaweza kuwasiliana name kwa namba nilizoweka hapa chini. Huwa natoa ushauri huu BURE kabisa niapokuwa na muda. Mawasiliano yangu yapo hapa chini.

 

Makala haya yameandaliwa na kuandikwa na

Venance Gilbert

Mwalimu, Shahada ya Kwanza ya Elimu katika Lugha na Menejimenti (BED-LM)

Chuo Kikuu Mzumbe

venancegilbert@gmail.com

0753400208.

Yalichapishwa mara ya kwanza 25/07/2017 yamefanyiwa marekebisho 05/06/2024.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

KUANZISHWA KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA Mafanikio ya michuano ya mpira wa miguu ya Olimpiki ndiyo yalikua mwanzo wa  FIFA kutamani kuwa na michuano yake ya Kombe la Dunia kwa mchezo wa mpira wa miguu. Ikumbukwe kwamba kipindi hicho mpira wa miguu wa wanaume pekee ndiyo ulikuwepo. Maswali yalitumwa kwa wahisani wa FIFA ili kuona kama wanakubaliana na uanzishwaji wa michuano hiyo na kwa masharti yapi? Kamati maalumu ilichunguza maswali hayo chini ya uongozi wa  Rais wa FIFA wa kipindi hicho Jules Rimet akishirikiana na Katibu wa Shirikisho la Soka nchini Ufaransa kwa wakati ule Henri Delaunay. Rais wa FIFA Jules Rimet aliyeanzisha na kusimamia Kombe la Dunia la kwanza . Kufuatia uwepo wa muswada wa Kamati Tendaji ya FIFA, lilifanyika kongamano la FIFA Mei 28, 1928 jijini Amsterdam nchini Uholanzi likiazimia kuwepo kwa michuano ya mabingwa wa soka duniani ambayo ilipangwa na shirikisho hilo la mpira duniani na sasa nchi waandaji wa michuano hiyo zilitakiwa ...

BAADHI MAMBO AMBAYO HUKUYAFAHAMU KUHUSU BARA LA AFRIKA

Ramani ya Afrika. Karibu tena mpenzi msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG. Leo katika safu yetu ya Fahamu napenda kukufahamisha mambo kadhaa ambayo huenda hukuyafahamu yote kuhusu bara la Afrika. Na tuanze sasa kuyahesabu mambo hayo: 1. Karibu nchi zote za Afrika zilitaliwa na wakoloni isipokuwa nchi mbili tu: Ethiopia na Liberia. 2. Kabla ya Ukoloni, Afrika ilikuwa na tawala zilizokaribia 10,000 (Kingdoms/Empire/State) na tawala hizi zilijiongoza kila moja kivyake zikiwa na lugha tofauti na mila na desturi tofauti tofauti. 3. Lugha ya kiarabu inazungumzwa na watu takribani milioni 170 ikifuatiwa na lugha ya kiingereza inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 130, Kiswahili kikiwa na wazungumzaji zaidi ya milioni 100, Kifaransa takribani wazungumzaji milioni milioni 115. Pia, kuna wazungumzaji wa lugha ya Xhosa wakiwa milioni 50. Kireno kinakadiriwa kuwa na wazungumzaji milioni 20 huku Kispanyola kikiwa na wazungumzaji wanaokadiriwa kuwa milioni 10. Vilevile takriba...

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

Nicki Minaja haishiwi vituko vya kupost picha mtandaoni akiwa uchi kabsa ama nusu uchi. Tazama hiyo picha hapo juu inayoonesha matako yake yakiwa wazi. Picha nyingine hii hapa japo amevaa nguo lakini mmmh!! Kwa wanaume so conducive kabisaaa. Cheki jinsi tako lilivyobinuliwa hapa hivi eti njiani anakopita kwa mavazi haya hawapi wanaume shida!!! Haya yote yanakuja wakati Nicki anajiandaa kuachia Album yake mpya ya Pink Friday Print. Album hiyo inapatikana kwenye iTune pia. Picha hizo ziko katika akaunti yake ya Instagram @nickiminaj.  WASILIANA NAMI:  Facebook: VENANCE BLOG  Twitter: @Venancetz  Instagram: venancegilbert  Asante kwa kutembelea VENANCE BLOG © 2014

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

Viongozi wa nchi tajiri zaidi duniani zinazounda kundi la G7 wanatarajiwa hii leo kutoa msimamo wa pamoja dhidi ya vitisho vya kiuslama vinavyoikumba dunia vikiwemo kitisho cha makundi ya wanamgambo wenye itikadi kali hadi kile Rais wa Marekani Barack Obama amelaani na kuutaja kama uchokozi wa Urusi nchini Ukraine. Kwa mara ya tatu mfululizo, viongozi hao wamemtenga Rais wa Urusi Vladimir Putin kutoka mkutano huo ulioanza hapo jana na unaokamilika hii leo katika mji wa Elmau nchini Ujerumani na badala yake wamewaalika viongozi kutoka kwingineko akiwemo waziri mkuu wa Iraq Haider al Abadi na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambao wote wawili wanakabiliwa na kitisho kutoka makundi ya wanamgambo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Ufaransa Francois Hollande wanatarajiwa kuangazia masuala ya mazingira katika mkutano huo hasa kuongezeka kwa viwango vya joto duniani na athari zake. Chanzo: DW

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

Lugha ya Kiswahili inazungumzwa katika nchi za Afrika Mashariki. Kiswahili hutumika nchini Tanzania, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji na Rwanda. Zaidi ya watu milioni 1 5 katika bara hili huitumia lugha hi i kama lugha ya kwanza na wazungumzaji wengine wakiitumia kama lugha ya pili au ya tatu. Ni lugha rasmi ya M uungano wa Afrika. Hii inafanya bara hili kuwa na idadi inayozidi milioni 100 ya wazungumzaji wa lugha hii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha kumi zinazoongoza kwa kua na idadi kubwa ya wazungumzaji barani Afrika. TANZANIA Kiswahili nchini Tanzania ni lugha rasmi na lugha ya Taifa. Ni lugha ya utambulisho kwa Mtanzanianainatumika kama lugha ya kuimarisha uelewano, ushirikiano na umoja wa kitaifa. Katika kuiendeleza, juhudi za usanifishaji zimefanyika kwa kuwatumia wataalamu wa fasihi na isimu, wadau wengine na wachapishaji vitabu. Taasisi mbalimbali zimebuniwa kuhusu lugha hii kama vile BAKITA, BAKIZA, Taasisi ya Elimu, UWAVI...

FRIENDSHIP QUOTES OF THE DAY MAY 26, 2018

Today I invite you to read these quotes of the day. Enjoy your day. 1.  One of the most beautiful qualities of true friendship is to understand and to be understood. ~Lucius Annaeus Seneca. 2.  Walking with a friend in the dark is better than walking alone in the light. ~Helen Keller. 3.  There is nothing on this earth more to be prized than true friendship. ~Thomas Aquinas. 4.  My best friend is the one who brings out the best in me. ~Henry Ford. 5.  It is one of the blessings of old friends that you can afford to be stupid with them. ~Ralph Waldo Emerson. 6.  The strong bond of friendship is not always a balanced equation; friendship is not always about giving and taking in equal shares. Instead, friendship is grounded in a feeling that you know exactly who will be there for you when you need something, no matter what or when. ~Simon Sinek. 7.  A friend is someone who gives you total freedom to be yourself. ~Jim Mo...

IDADI YA WATU WALIOFARIKI UGANDA YAFIKIA 33

Moto mkubwa uliowaka baada yaajali mbaya ya barabarani iliohusisha lori la mafuta, umewauwa takriban watu 33 mjini kampala Uganda. Watu wengine 30 wanadaiwa kujeruhiwa vibaya kufuatia tukiohilo. Maafisa wa polisi wanasema kuwa kati ya waliofariki ni raia waliokuwa wanakimbilia eneo hilo la mkasa kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwa lori hilo. maafisa wa serikali walikuwa katika harakati za kutambua mili ya waliofariki baada ya wengi wao kuchomeka vibaya. Idara ya polisi imesema kuwa waliofariki waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.

VITAMBULISHO VYA URAIA KUVUKIA MIPAKA KENYA, RWANDA NA UGANDA

Wananchi wa mataifa ya Rwanda, Uganda na Kenya wamepokea kwa shangwe kuanza kwa mpango wa kutumiwa kwa vitambulisho vya uraia kama cheti cha kuwaruhusu kuvuka mpaka na kuingia moja wapo wa nchi hizo.Mpango huu wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kusafiria katika nchi hizo tatu umeanza kutumiwa rasmi tarahe Mosi Januari 2014, kufuatia makubaliano kati ya viongozi wa mataifa hayo.Mpango wenyewe unatokana na makubaliano kati ya viongozi wa nchi tatu waliofikia wakati wa mkutano uliofanyika nchini Uganda mwezi Juni mwaka jana.Pia mpango huu unalenga kurahisisha usafiri wa watu wa jumuiya katika mataifa wanachama kama awamu ya pili ya ushirikiano kati ya mataifa wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.Hata hivyo siku moja tu baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutumia vitambulisho vya uraia kama hati ya kuwaruhusu raia wa nchini tatu, Uganda, Kenya na Rwanda kuvuka mpaka na kuingia mojawapo ya nchi hizo sasa inaonekana mpango huo huenda ukawanufaisha watu wachache peke yake.Sio ...

CHANGES QUOTES OF THE DAY MAY 23, 2018

Hello dear reader, welcome once again. Today I have gathered the quotes concerning changes in life. I should not write more since I am not not the speaker in this category, take your time to dive in and become intellectual with full equipped knowledge from the great men of history Remember, someday it might be you. Do not rely on inspiration from friends while you are needy, VENANCE BLOG is here for you. Welcome all the time by searching Quotes. Now proceed. 1. Every great dream begins with a dreamer. Always remember, you have within you the strength, the patience, and the passion to reach for the stars to change the world. ~Harriet Tubman. 2. Change your thoughts and you change your world. ~Norman Vincent Peale. 3.  If you don't like something, change it. If you can't change it, change your attitude. ~Maya Angelou 4.  Change will not come if we wait for some other person or some other time. We are the ones we've been waiting for. We are the change that...

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIUME WENYE MVUTO KOREA 2017

Uhali gani msomaji na mfuatiliaji wa VENANCE BLOG? Nakukaribisha katika darasa jipya la kufahamu mambo kadha wa kadha kama yanavyokuwa yakipigiwa kura na watu kutoka vyanzo tofauti kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, watu wenye ushawishi, majarida n.k. Basi kwa kuanza leo nakuletea orodha ya waigizaji 10 wa kiume wenye mvuto nchini Korea. Vigezo vilivyotumika husemwa na mtandao husika unaotoa orodha hiyo. Ili kurahisisha kazi hii, mimi kama Blogger ntakuletea orodha hizi kila siku kwa lugha ya Kiswahili. Na tuanze sasa, tunaanzia Korea Kusini kuangalia waigizaji wa kiume wenye mvuto kwa mwaka 2017: # 10. Lee Byung-Hun Lee Byung-Hyun ni muimbaji, mwanamitindo na muigizaji kutokea Korea ya Kusini. Anamiliki kampuni yake ya BH Entertainment. Ni muhitimu wa masuala ya filam na maigizo katika Chuo Kikuu Chung Ang. Anazungumza Kiingereza, Kifaransa, Kikorea na Kimandarin lakini pia ni mfuasi wa dini ya Budha. Alizaliwa Julai 12, 1972 katika jimbo la Gyeonggi Korea ya Kusini. Alianz...