IRAN IMEFANYA JARIBIO LA KOMBORA LA NYUKLIA

Iran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.

Kombora hilo lilionyeshwa hadharani katika maonyesha ya kijeshi jana Ijumaa.

Iran imesema kuwa kombora hilo linaweza kusafiri mwendo wa kilomita 2,000.

Kituo cha runinga cha taifa hilo kilionyesha picha za sherehe hizo.

Kombora la kwanza la Khorram-Shahr lilirushwa angani Januari lakini likalipuka katikati ya mwendo.

Jaribio hilo lilifanywa siku chache baada ya Rais Trump wa Marekani kushambulia Iran katika hotuba yake katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Rais wa Iran, Hassan Rouhani, ametetea hatua ya taifa lake kuimarisha zana zake kwa lengo la kujitetea.



Chanzo

Comments

Popular Posts

CHEKI PICHA HIZI ALIZOWEKA NICKI MINAJ INSTAGRAM

MKUTAO WA G7 KUANGAZIA USALAMA NA MAZINGIRA

HISTORIA YA KOMBE LA DUNIA TANGU 1930, WAANDAAJI & WASHINDI

WAFAHAMU WAIGIZAJI 10 WA KIKE WA KOREA AMBAO NI WAREMBO KWA MWAKA 2017

WALIOCHAGULIWA CHUO CHA MIPANGO MAJINA HAYA HAPA

TEKNOLOJIA ZA KALE ZINAZOTUMIKA HADI SASA

ZIFAHAMU NCHI ZINAZOZUNGUMZA KISWAHILI BARANI AFRIKA

DEADMEN SPEAKS: A POEM