Mwanamzuki mwenye vionjo vya kipekee Ali Kiba a.k.a. King Kiba amethibitisha katika ukurasa wake wa Facebook kuwa ataperform katika tuzo za MTV MAMA zitakazofanyika Johanesburg Afrika Kusini Octoba 22 mwaka huu.
ALI KIBA KUTUMBUIZA TUZO ZA MTV MAMA OKTOBA 22
Mwanamzuki mwenye vionjo vya kipekee Ali Kiba a.k.a. King Kiba amethibitisha katika ukurasa wake wa Facebook kuwa ataperform katika tuzo za MTV MAMA zitakazofanyika Johanesburg Afrika Kusini Octoba 22 mwaka huu.
KATY PERRY AMESEMA ATAFANYA COLLABO NA TAYLOR SWIFT KAMA ATAOMBA MSAMAHA
![]() |
Katy Perry na Taylor Swift wakiwa Berley Hilton Hotel Januari 30, 2010 |
Katy Perry na Taylor Swift kufanya collabo?
Collabo hiyo inaweza kutokea lakini kwa sharti moja tu kutoka kwa Katy Perry, kama Taylor Swift atakubali kumuomba msamaha.Hili linakuja baada ya shabiki mmoja wa Katy Perry kuuliza katika mtandao wa Twitter kama Katy Perry anaweza kufanya collabo na Swift, Perry akajibu kwa kifupi "hakika, kama ataomba msamaha"
Mgogoro kati ya mastaa hawa wawili wa Pop ulianza mwaka 2014 kufuatia Swift kumteta Katy katika Mtandao wa The Rolling Stone kuwa wimbo wake "Bad blood" ulikuwa unamhusu Swift.
"Alifanya kitu kibaya sana" alisema Swift. "Ilikuwa kama hivyo. Tumekuwa maadui. Na sababu haikuwa mwanaume. Ni kazi tu. Alijaribu hata kuvuruga tamasha langu. Alijaribu hata kuwapa hela vijana waje kunitoa jukwaani"
JE, KATY PERRY AMETHIBITISHA KUWA WIMBO WA 'BAD BLOOD' UNAMHUSU SWIFT?
Mtandao wa The Internet ulisema kwamba Katy Perry ndiye mwenye makosa, kufuatia baadhi ya madansa wa Swift kuondoka kwenye tour ya Swift kufuatia mpango ulofanywa na Katy Perry.Muda mfupi baada ya Mahojiano na The Rolling Stone yaliyokuwa ya moja kwa moja, Katy alitweet katika mtandao wa Twitter "Kaa tayari kwa kipindi cha Regina George kuhusu nguo za kondoo".
Baadaye kwenye mahojiano mwaka 2015 na Billboard Perry alisema "kama kuna mtu atajaribu kuniharibia sifa yangu, mtamsikia tu"
Chanzo: Billboard
WALIOKUFA KATIKA TETEMEKO WAFIKIA 16
![]() |
Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kuaga miili ya waliokufa katika tetemeko la ardhi mkoani Kagera. |
Maafa zaidi yameripotiwa katika janga la tetemeko la ardhi, lililotokea juzi mkoani Kagera, ambapo imeripotiwa idadi ya vifo kuongezeka na kufikia watu 16, huku wengine 253 wakijeruhiwa na kusababisha simanzi na masikitiko kwa familia nyingi. Katika tukio hilo, pia nyumba 840 za makazi zimeanguka, nyumba 1,264 zimepata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule yameanguka.
Tukio hilo limemfanya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kulazimika kufanya ziara ya ghafla ya kuwatembelea waathirika wa tetemeko hilo, ambalo limedaiwa kusababisha tafrani pia katika nchi jirani za ukanda wa Afrika Mashariki za Kenya na Rwanda.
Katika hatua nyingine, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimeeleza mpango wa kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga hayo kutokea.
Katika mradi huo maalumu chini ya Kitengo cha Utafiti wa Miamba na Volcano, chuo hicho kitashirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo Ulaya na Marekani, hasa Chuo Kikuu cha Glasgow kilichopo Scotland, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Burton Mwamila. Ziara ya Waziri Mkuu
Akitoa taarifa kwa Waziri Mkuu jana katika Uwanja wa Kaitaba ulioko mjini Bukoba ambapo umeandaliwa maalumu kwa ajili ya kuaga miili ya watu waliopoteza maisha katika tukio hilo la kusikitisha, Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu alisema tukio hilo ni la kwanza kutokea mkoani humo na kwamba limeleta madhara makubwa kwa wananchi na kuacha majonzi makubwa.
Kijuu alisema mpaka taarifa inaandaliwa watu 16 waliripotiwa kupoteza maisha na kusababisha majeruhi 253, huku 170 wakiwa wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo na 83 wakitibiwa na kuruhusiwa.
Alisema pia tetemeko hilo limesababisha nyumba 840 za makazi kuanguka, nyumba 1,264 kupata nyufa kubwa na majengo 44 ya taasisi mbalimbali zikiwemo shule kuanguka.
Alisema tetemeko hilo lenye ukubwa wa alama 5.7 uliopimwa kwa kipimo cha Ritcher cha kisayansi cha kupima matetemeko, limeleta madhara makubwa ambapo Serikali ya Mkoa inaendelea kutathmini kwa kina athari zaidi zilizosababishwa na tetemeko hilo na pia uharibifu uliojitokeza kisha kupeleka katika Ofisi ya Waziri Mkuu waone jinsi ya kusaidia.
Alisema hatua zilizochukuliwa na mkoa mpaka sasa ni kuwaokoa na kuwapeleka watu hospitali kwa ajili ya matibabu na kuwapatia makazi ya muda baadhi ya wananchi wenye nyumba zilizoathirika, wakati mipango mingine ikiandaliwa.
Taarifa hiyo ya Mkuu wa Mkoa, ilimfanya Waziri Mkuu kueleza masikitiko yake na serikali kutokana na janga hilo na kutoa salamu za pole kwa wananchi waliopatwa na madhara na kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa na pia maeneo yote yaliyoathirika.
"Leo si siku nzuri kwetu, nimekuja kumwakilisha Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye anawapa pole sana wana Kagera wote na Watanzania kwa ujumla. Pia Makamu wa Rais anawapa pole kwa msiba huu mkubwa, lengo la safari yangu ni kuja kuwapa pole, tukio hili ni kubwa na halijawahi kutokea Tanzania, tumekuwa tukisikia kutoka mataifa ya nje lakini leo limetupata nchini kwetu," alisema Majaliwa.
Aliwasihi na kuwataka wananchi kuwa wavumilivu, kuonesha umoja na ushirikiano, lakini pia kujitokeza kuwafariji wenzao wakati wote wa majonzi, huku akisema Watanzania kwa miaka mingi wamekuwa wakishuhudia mitikisiko midogo, lakini juzi tumeshuhudia mtikisiko mkubwa kabisa ambao umeleta madhara makubwa kwetu.
"Mpaka sasa hatuna uhakika mtikisiko huu utakuwa endelevu kwa kiasi gani, nataka niwahakikishie Watanzania wote, Serikali tunafanya mawasiliano na taasisi zenye uwezo wa kubaini mtikisiko huu ili tuweze kujua jambo hili litakuwa endelevu kwa kiasi gani na kuona dalili na ukubwa wake utakuwaje ili tujipange katika kutoa elimu lakini pia tahadhari pindi jambo kama hili linapoweza kutokea au tunapoona viashiria au dalili za jambo hili," alisema Waziri Mkuu.
Alisema kuwa Mkuu wa Mkoa katika taarifa yake alimweleza kwamba tathmini inaendelea na kwamba ameiagiza Kamati ya Maafa ya Ofisi ya Waziri Mkuu kufika mkoani Kagera mara moja na kuzunguka mkoa mzima kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa kwa lengo la kufanya tathmini ya jumla.
Alisema baada ya tathmini hiyo, utaratibu utafuatwa kwani serikali haiwezi kuwatupa mkono wananchi hao, pia alitumia fursa hiyo kuwaambia wafiwa kuwa Watanzania nchini kote wako pamoja nao katika janga hilo.
Akielezea mkasa huo, majeruhi Happines Apolinary ambaye ni mkazi wa kata ya Buyekera aliyelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera kwa kuumia kichwani na mgongoni, alisema alishtuka kusikia mtikisiko mkubwa wakati akiwa ndani ya nyumba yake na ghafla aliangukiwa na kuta na kumsababishia majeraha. Pamoja na kueleza kuumia vibaya kutokana na tukio hilo, Happines aliwashukuru wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Kagera kwa huduma nzuri waliyompatia tangu juzi alipofikishwa hospitalini hapo.
Majeruhi mwingine, Paulina Spilian aliyelazwa hospitalini hapo akiwa amejeruhiwa miguu alisema akiwa ndani ya nyumba yake ghafla alisikia mtikisiko mkubwa ulioambatana na kishindo cha kuanguka kwa kuta za nyumba na akiwa katika harakati za kutaka kukimbia nje aliangukiwa na ukuta miguuni.
Majeruhi huyo aliiomba Serikali kuwasaidia kwa kuwajengea nyumba na pia kuwapa elimu kuhusiana na matukio kama hayo ili waweze kujiokoa baada ya kuona dalili au viashiria tofauti na ilivyotokea juzi.
Advela Respicius ambaye ni mama wa marehemu, Verdiana Respicius aliyekufa baada ya kufunikwa na kifusi cha nyumba, akizungumza kwa niaba ya familia za wafiwa wa tukio hilo, alitoa shukrani kwa serikali kwa kutoa majeneza, sanda na usafiri wa kuwapeleka marehemu hao mpaka vijijini kwa ajili ya maziko.
Vifaa vya kutabiri kufungwa Wakati hofu ikiwa bado imetawala kutokana na tukio hilo hasa kutokana na wananchi wa Kagera kueleza kutofahamu lolote kabla ya kutokea kwa tetemeko kutokana na kutopewa taarifa zozote na mamlaka za serikali, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo eneo la Tengeru, mkoani Arusha kimesema kinatarajia kuanza kufunga vifaa vitakavyotoa ishara ya matukio ya matetemeko ya ardhi kabla majanga hayo kutokea.
Katika mradi huo maalumu chini ya Kitengo cha Utafiti wa Miamba na Volcano, chuo hicho kitashirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu zilizopo Ulaya na Marekani, lakini hasa Chuo Kikuu cha Glasgow kilichopo Scotland, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Burton Mwamila.
Katika mradi huo wa kwanza nchini unaolenga kutoa utabiri wa matukio ya matetemeko na ulipukaji wa volcano nchini, vifaa maalumu vitakavyokuwa vinapima uwezekano wa kutokea majanga hayo, vitafungwa katika maeneo nyeti kama milima, vilima na sehemu ambazo huwa na volcano hai.
Mtaalamu wa miamba ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya 'Eco Science' inayoshughulika na utafiti wa miamba pamoja na milipuko ya volcano, Dk Ben Beeckmans amefafanua kuwa 'Mlima wa Mungu' (Oldonyo Lengai) uliopo eneo la Ngaresero, wilayani Ngorongoro ndio chanzo kikubwa cha matetemeko ya ardhi katika eneo lote la Afrika Mashariki. Mlima huo wenye volkano hai pia umekuwa ukilipuka mara kwa mara na tukio la mwisho lilirekodiwa mwaka 2007.
Vifaa hivyo vya kutabiri matetemeko ya ardhi vitafungwa kuzunguka eneo la mlima huo, Ziwa Natron, Mlima Meru na hata Mlima Kilimanjaro pamoja na maeneo mengine nchini.
Lakini hatua hiyo si kwamba imetokana na matukio ya tetemeko yaliyoyakumba maeneo mengi ya nchi juzi bali ni mpango uliobuniwa na wataalamu mapema mwaka huu na kwamba kilichobaki ni utekelezaji tu.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), Karimu Meshaki alisema atatoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya mpango huo wiki hii.
Hivi karibuni Serikali ilijenga maabara kubwa kabisa ya utafiti wa kisayansi katika Chuo cha Nelson Mandela, Arusha ambayo ilizinduliwa miezi miwili iliyopita.
Serikali ya India pia ilitoa mchango wake kwa kukipatia chuo hicho kompyuta kubwa na yenye uwezo mkubwa zaidi nchini ijulikanayo kama 'Param Kilimanjaro,' ambayo pamoja na shughuli nyingine pia inatarajiwa kutumika katika tafiti za miamba, gesi asilia na pia kwenye huu mradi mpya wa kufuatilia matukio ya tetemeko la ardhi na milipuko ya volkano.
Chanzo: Habarileo
VIDEO: HII NDIYO MAANA HALISI YA SEPTEMBA 11 HUKO MAREKANI
Mnamo mwaka 2001 ndege mbili za abiria za chini Marekani zilitekwa angani na magaidi wanaodhaniwa kuwa ni Al-Qaeda. Ndege hizo mbili aina ya Boeing 767 ziligonga katika majengo pacha ya Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililoko katika jiji la New York nchini Marekani. Hili lilikuwa ni shambulio kubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na magaidi wa Al-Qaeda ambao kwa kipindi hicho kundi hilo lilikuwa likiongozwa na Osama bin Laden ambaye aliuawa miaka ya hivi karibuni na wanajeshi wa jeshi la Marekani (wanavyodai wao Marekani).
Pia kundi la Al Qaeda lilikuwa limelenga kuteketeza jengo la Idara ya Ulinzi ya Marekani, The Pentagon ambako ndiyo makao makuu ya Idara ya Ulinzi ya nci ya Marekani. Lakini pia ililengwa Ikulu ya Marekani 'The White House'.
Watu wapatao 2,996 pamoja na watekelezaji wa tukio hilo wakiwa 19 waliuawa. Watu zaidi ya 6,000 walijeruhiwa katika tukio hilo.
Pia tukio hilo lilisababisha uharibifu wa mali hasa majengo na miundo mbinu uliofikia dola bilioni 10. Jumla kuu ya uharibifu ilikadiriwa kuwa dola za kimarekani trilioni 3.
Katika kutekeleza tukio hilo la ugaidi magaidi 19 walihusika ambapo 15 walikuwa ni raia wa Saudi Arabia, 2 kutoka Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE), 1 kutoka Misri na 1 kutoka Lebanon.
Historia ya Al Qaeda inarudi nyuma katika mwaka 1979 ambapo Muungano wa Kisoviet uliivamia Afghanistan. Osama alisafiri hadi Afghanistan na kuunda kikundi cha kiarabu cha wajahideen kupingana na Wasoviet. Osama aliendelea kuwa kinyume na Wamarekani na mwaka 1996 alitoa tamko lililotaka majeshi ya Marekani kuondoka Saudia Arabia
Shambulio hili lilkuwa kama ifuatavyo:
- Ndege ya Shirika la Marekani (American Airlines Flight 11) aina ya Boeing 767 iliondoka Logan airpot ikiwa na crew ya watu 11 pamoja na abiria 76 (watekaji 5 hawakuhesabiwa) ndege hiyo iligeuzwa ruti ikiwa angani na kugonga katika kituo cha biashara Duniani saa 8:46 am saa za Marekani.
- Ndege ya pili ya Marekani (American Airlines Flight 77) Boeing 757 iliondoka Washington Dulles Airport kuelekea Los Angels, California ikiwa na crew ya watu 6 na abiria 53 (watekaji wameondolewa katika hesabu hiyo). Watekaji walifanikiwa kuiteka na kugonga jengo la ulinzi la Marekani The Pentagon saa 9:37 am saa za Marekani.
- Ndege ya tatu (United Airlines Flight 93) Boing 757 iliondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa New York ikielekea San Fransisco kabla ya kutekwa angani na kugonga Stonycreek Township karibu na Shanksville, Pennsylvania saa 10:03 am saa za Marekani. Abiria walikuwa 33 na crew ya watu 7 huku watekaji wakiwa 4.
- Ndege nyingine American Airline Flight 11 Boeing 767 ilikuwa na abiria 51 crew ya watu 9 na watekaji 5 iliondoka Los Angels na kutekwa angani hadi WTC saa 9:03 am dakika chache mara baada ya Shambulio la awali.
Hizi ni baadhi ya picha za tukio hilo
![]() |
WTC kabla ya shambulio |
![]() |
WTC kabla ya shambulio |
![]() |
WTC kabla ya shambulio |
Nimekuwekea video pia ambapo unaweza kutazama tukio hilo
Makala hii imeandaliwa kwa Msaada wa Mtandao (Wikipedia, Britannica na YouTube)
LEO SEPTEMBA 11 KATIKA HISTORIA
Leo ni tarehe 11 Septemba, siku ya 255 katika mwaka 2016, zimesalia siku 111 kumaliza mwaka huu 2016.
2001 - Mnamo majira ya saa 2 na
dakika 45 asubuhi ikiwa siku ya Jumanne, ndege mbili za abiria za Marekani Boeing 767 zilitekwa angani na kugonga katika jengo la Kituo cha Biashara duniani (WTC) ambapo watu wengi waliuawa. Inasidikika kuwa tukio hilo la ugaidi liliungwa mkono na magaidi wa Kiislamu kutoka Saudi Arabia na kundi la Al Qaeda ilililokuwa chini ya Osama bin Laden kwa kipindi hicho.
MATUKIO
1740 - Daktari mweusi aliyetibu meno alitajwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la The Pennsylvania
1777 - Mapigano ya vita ya Brandywine yalianza huko Pennsylvania ambapo General George Washington na vikosi vyake walishindwa na General Sir William Howe wa Uingereza
1915 - Mkutano wa Zimmerwald uliitishwa kurejesha amani wakati wa vita ya kwanza ya Dunia.
1940 - Adof Hitler alituma vikosi vyake Mashariki mwa Romania katika vita ya pili ya dunia.
1944 - Vikosi vya Marekani viliingia Luxembourg.
1974 - Haile Selassie I aliondolewa madarakani huko Ethiopia.
1997 - Scotland ilipiga kura ya kuwa na Bunge lake kamili baada ya miaka 290 ya Muungano na England.
1997 - Scotland ilipiga kura ya kuwa na Bunge lake kamili baada ya miaka 290 ya Muungano na England.
![]() |
Jengo la Kituo cha Biashara Duniani (WTC) lililolipuliwa Septemba 11, 2001 na kundi la Al-Qaeda. |
dakika 45 asubuhi ikiwa siku ya Jumanne, ndege mbili za abiria za Marekani Boeing 767 zilitekwa angani na kugonga katika jengo la Kituo cha Biashara duniani (WTC) ambapo watu wengi waliuawa. Inasidikika kuwa tukio hilo la ugaidi liliungwa mkono na magaidi wa Kiislamu kutoka Saudi Arabia na kundi la Al Qaeda ilililokuwa chini ya Osama bin Laden kwa kipindi hicho.
2005 - Israel iliwaondoa wananchi wake na vikosi vyake vya jeshi katika mapiagano dhidi ya Palestina katika Ukanda wa Gaza.
2007 - Urusi ilifanya jaribio la kulipua bomu la Nano lililoitwa "Father of Bombs" yaani Baba la Mabomu yote ambalo lilikuwa ni bomu lisilo la nyuklia kuwahi kutengenezwa.
2012 - Ofisi za Ubalozi wa Mareani nchini Libya katika mji wa Benghazi zilichomwa moto na kupelekea vifo vya watu 4 akiwemo balozi wa Marekani nchini Libya, Christopher Stevens
2007 - Urusi ilifanya jaribio la kulipua bomu la Nano lililoitwa "Father of Bombs" yaani Baba la Mabomu yote ambalo lilikuwa ni bomu lisilo la nyuklia kuwahi kutengenezwa.
2012 - Ofisi za Ubalozi wa Mareani nchini Libya katika mji wa Benghazi zilichomwa moto na kupelekea vifo vya watu 4 akiwemo balozi wa Marekani nchini Libya, Christopher Stevens
KUZALIWA
1700 - Mshairi wa Scotland, James Thomson.
1877 - Mwanasayansi James Jeans.
1862 - Mwandishi wa Marekani O. Henry (William Sydney Porter) alizaliwa.
1939 - Charles M. Chuck Geschke muanzilishi wa Adobe System Inc.
1965 - Rais wa Syria Bashal al-Assad. Yupo madarakani tangu mwaka 2000.
VIFO
1971 - Nikita Khrushchev moja kati ya viongozi wa kisoshalist alifariki akiwa na miaka 77 katika kipindi cha vita baridi.
NUKUU
"Kama mtu ameishi katika vita, umaskini na upendo, ameishi maisha kamili" - O. Henry.
KWA MSAADA WA MTANDAO.
MAPIGANO YAPAMBA MOTO SYRIA KUELEKEA SULUHU YA MGOGORO
Saa chache baada ya Marekani na Urusi kutangaza makubaliano ya kumaliza mgogoro wa kivita uliyodumu kwa miaka mitano nchini Syria, mapigano yemepamba moto upya. Karibu raia 100 wameuawa katika mashambulizi ya angani.
Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London,Uingereza, limeripoti siku ya Jumamosi kwamba raia wasiopungua 58 wameuawa katika mkoa unaodhibitiwa na waasi wa Idlib baada ya ndege za kivita kuliripua kwa mabomu soko kaskazini-magahribi mwa mji huo, saa kadhaa baada ya kutangazwa kwa masharti ya makubaliano ya kusitishwa mapigano nchini kote.
Mjini Aleppo, jeshi la Syria lilifanya mashambulizi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi katika jitihada za kuimarisha nafasi yake kuelekea usitishaji wa uhasama, unaoanza siku ya Jumatatu wakati wa siku kuu ya Eid al-Adha. "Mapigano yamepamba moto katika maeneo yote ya Aleppo," alisema kapteni Abdul Salam Abdul Razak, msemaji wa kundi la waasi la Brigedi za Nour al-Dine al Zinki , ambalo ni sehemu ya jeshi Huru la Syria (FSA). Watu wasiopungua 30 wameuawa katika mashambulizi hayo, kulingana na shirika la uangalizi wa haki za binaadamu.
Ongezeko hilo la machafuko linafuatia tangazo lililotolewa mapema Jumamosi juu ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na Urusi baada ya mazungumzo marefu mjini Geneva, Uswisi. Chini ya makubaliano hayo. Moscow itaushinikiza utawala wa Assad kukomesha kampeni yake ya kijeshi dhidi ya waasi wanaoungwa mkono na Marekani.
Kwa Urusi kufanya hivyo, Marekani itaanzisha mashambulizi ya pamoja na Urusi dhidi ya kundi lililobadili jina la Jabhat Fatah al-Sham, zamani likijulikana kama Jabhatu Nusra wakati likiwa na mafungamano na mtandao wa Al-Qaeda, ikiwa makubaliano hayo yataheshiwa kwa muda usiyopungua siku saba.
"Hili linahitaji kusitisha mashambulizi, yakiwemo ya angani, na majaribio yoyote ya kutwaa ardhi zaidi kwa gharama ya pande zilizomo kwenye makubaliano ya usitishaji uhama. Inahitaji ufikishaji wa misaada usiyo na vikwazo vyovyote katika maeneo yote yaliozingirwa, ikiwemo Aleppo," alisema waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry.
Serikali ya rais Bashar al-Assad haijatoa tamko rasmi kuhusu makubaliano hayo. Badala yake, shirika la habari la serikali SANA limesema serikali inayakubali mapatano hayo, na kuongeza kuwa uhasama utaanza kusita katika mji wa kaskazini wa Aleppo kwa sababu za kibinaadamu. Halikusema ni lini vurugu zitamalizika, na kuongeza kuwa makubaliano hayo kati ya Marekani na Urusi yalifikiwa kwa idhini na taarifa ya serikali.
Basma Kodmani, kutoka muungano wa upinzani unaoungwa mkono na Saudi Arabia wa Kamati Kuu ya Majadiliano (HNC) alisema kundi linachukuwa tahadhari kwa makubaliano hayo, na kuongeza kuwa kunahitaji kuwepo na mifumo ya kuhakikisha utekelezaji wake.
Vurugu za Jumamosi zinaonyesha kuwa huenda ikawa vigumu kuyatekeleza makubaliano kati ya Marekani na Urusi kwa sabau mataifa hayo mawili yana ushawishi wenye mipaka kwa serikali na makundi ya waasi kuhusu kusitisha mashambulizi.
Makubaliano ya kusitisha uhasama yaliofikiwa na mataifa hayo mawili makubwa duniani mapema mwaka huu na kuanza kutekelezwa mwishoni mwa mwezi Februari yalishindwa muda mfupi baadae na yalifuatiwa na miezi miwili ya vurugu zilizouwa maelfu.
Urusi ndiyo muungaji mkono mkuu wa utawala wa Assad huku Marekani ikiyaunga mkono makundi ya waasi wanaotaka kum'ngoa madarakani. Vita vya Syria vilivyoigia mwaka wake wa tano, vimeendelea licha ya duru kadhaa za mazungumzo ya amani na majaribio ya jumuiya ya kimataifa kukomesha vurugu nchini humo. Watu wasiopungua robo milioni wameuwawa,na nusu ya wakazi wa nchi hiyo kabla ya vita wamekoseshwa makaazi.
Mashambulizi ya angani ya Jumamosi yalifanyika hasa katika miji ya Aleppo na Idlib. Aleppo imekuwa kituo cha vurugu nchini Syria katika miezi ya karibuni, ambapo watu karibu 2,200 wakiwemo raia 700 wameuwawa tangu mwezi Julai mwaka huu kwa mujibu wa shirika la uangalizi w ahaki za binaadamu, linalofuatilia vurugu hizon kupitia mtandao wa wanaharakati walioko ndani ya Syria.
Mgogoro wa Syria ulianza mnamo mwaka 2011, wakativikosi vya serikali vilipoanzisha ukandamizaji wa vurugu dhidi ya waandamanaji waliokuwa wanadai demokrasia, wakimtolea mwito Assad kuachia ngazi. Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 250,000 wameuawa, na zaidi ya nusu ya wakaazi jumla wamekosa makaazi.
Chanzo: DW
Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London,Uingereza, limeripoti siku ya Jumamosi kwamba raia wasiopungua 58 wameuawa katika mkoa unaodhibitiwa na waasi wa Idlib baada ya ndege za kivita kuliripua kwa mabomu soko kaskazini-magahribi mwa mji huo, saa kadhaa baada ya kutangazwa kwa masharti ya makubaliano ya kusitishwa mapigano nchini kote.
Mjini Aleppo, jeshi la Syria lilifanya mashambulizi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi katika jitihada za kuimarisha nafasi yake kuelekea usitishaji wa uhasama, unaoanza siku ya Jumatatu wakati wa siku kuu ya Eid al-Adha. "Mapigano yamepamba moto katika maeneo yote ya Aleppo," alisema kapteni Abdul Salam Abdul Razak, msemaji wa kundi la waasi la Brigedi za Nour al-Dine al Zinki , ambalo ni sehemu ya jeshi Huru la Syria (FSA). Watu wasiopungua 30 wameuawa katika mashambulizi hayo, kulingana na shirika la uangalizi wa haki za binaadamu.
Makubaliano kati ya Marekani na Urusi
Ongezeko hilo la machafuko linafuatia tangazo lililotolewa mapema Jumamosi juu ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na Urusi baada ya mazungumzo marefu mjini Geneva, Uswisi. Chini ya makubaliano hayo. Moscow itaushinikiza utawala wa Assad kukomesha kampeni yake ya kijeshi dhidi ya waasi wanaoungwa mkono na Marekani.
![]() |
Mawaziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry, na wa Urusi Sergei Lavrov wakitangaza makubaliano ya kusitisha mapigano Syria. |
Kwa Urusi kufanya hivyo, Marekani itaanzisha mashambulizi ya pamoja na Urusi dhidi ya kundi lililobadili jina la Jabhat Fatah al-Sham, zamani likijulikana kama Jabhatu Nusra wakati likiwa na mafungamano na mtandao wa Al-Qaeda, ikiwa makubaliano hayo yataheshiwa kwa muda usiyopungua siku saba.
"Hili linahitaji kusitisha mashambulizi, yakiwemo ya angani, na majaribio yoyote ya kutwaa ardhi zaidi kwa gharama ya pande zilizomo kwenye makubaliano ya usitishaji uhama. Inahitaji ufikishaji wa misaada usiyo na vikwazo vyovyote katika maeneo yote yaliozingirwa, ikiwemo Aleppo," alisema waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry.
Uidhinishwaji usiyo rasmi kutoka serikali ya Syria
Serikali ya rais Bashar al-Assad haijatoa tamko rasmi kuhusu makubaliano hayo. Badala yake, shirika la habari la serikali SANA limesema serikali inayakubali mapatano hayo, na kuongeza kuwa uhasama utaanza kusita katika mji wa kaskazini wa Aleppo kwa sababu za kibinaadamu. Halikusema ni lini vurugu zitamalizika, na kuongeza kuwa makubaliano hayo kati ya Marekani na Urusi yalifikiwa kwa idhini na taarifa ya serikali.
Basma Kodmani, kutoka muungano wa upinzani unaoungwa mkono na Saudi Arabia wa Kamati Kuu ya Majadiliano (HNC) alisema kundi linachukuwa tahadhari kwa makubaliano hayo, na kuongeza kuwa kunahitaji kuwepo na mifumo ya kuhakikisha utekelezaji wake.
Vurugu za Jumamosi zinaonyesha kuwa huenda ikawa vigumu kuyatekeleza makubaliano kati ya Marekani na Urusi kwa sabau mataifa hayo mawili yana ushawishi wenye mipaka kwa serikali na makundi ya waasi kuhusu kusitisha mashambulizi.
Makubaliano ya kusitisha uhasama yaliofikiwa na mataifa hayo mawili makubwa duniani mapema mwaka huu na kuanza kutekelezwa mwishoni mwa mwezi Februari yalishindwa muda mfupi baadae na yalifuatiwa na miezi miwili ya vurugu zilizouwa maelfu.
![]() |
Waokozi wakitafuta maiti na manusura katika vifusi baada ya shambulizi la angani mkoani Idlib siku ya Jumamosi. |
Muungaji mkono mkuu wa Assad
Urusi ndiyo muungaji mkono mkuu wa utawala wa Assad huku Marekani ikiyaunga mkono makundi ya waasi wanaotaka kum'ngoa madarakani. Vita vya Syria vilivyoigia mwaka wake wa tano, vimeendelea licha ya duru kadhaa za mazungumzo ya amani na majaribio ya jumuiya ya kimataifa kukomesha vurugu nchini humo. Watu wasiopungua robo milioni wameuwawa,na nusu ya wakazi wa nchi hiyo kabla ya vita wamekoseshwa makaazi.
Mashambulizi ya angani ya Jumamosi yalifanyika hasa katika miji ya Aleppo na Idlib. Aleppo imekuwa kituo cha vurugu nchini Syria katika miezi ya karibuni, ambapo watu karibu 2,200 wakiwemo raia 700 wameuwawa tangu mwezi Julai mwaka huu kwa mujibu wa shirika la uangalizi w ahaki za binaadamu, linalofuatilia vurugu hizon kupitia mtandao wa wanaharakati walioko ndani ya Syria.
Mgogoro wa Syria ulianza mnamo mwaka 2011, wakativikosi vya serikali vilipoanzisha ukandamizaji wa vurugu dhidi ya waandamanaji waliokuwa wanadai demokrasia, wakimtolea mwito Assad kuachia ngazi. Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 250,000 wameuawa, na zaidi ya nusu ya wakaazi jumla wamekosa makaazi.
Chanzo: DW
TETEMEKO LA ARDHI LIMEPITA MIKOA YA MWANZA NA KAGERA NA KUFANYA UHARIBIFU
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.7 limetikisa mkoa wa Mwanza likitokea mkoa wa Kagera umbali wa kilomita 44 karibu na ukingo wa magharibi wa Ziwa Victoria huku likijirudia kwa ukubwa zaidi ya ule wa awali. Tetemeko hilo lilipita umbali wa kilomita 10 kwenda chini limefanya uharibifu mkoani Kagera kama picha zinavyoonesha hapa chini. Pia kumeripotiwa vifo vya watu.
PICHA KWA HISANI YA JAMII FORUMS.
PICHA KWA HISANI YA JAMII FORUMS.
MOVIE MPYA KATI YA SEPTEMBA 15 HADI 19
Hii ni orodha ya muvi mpya zitakazooneshwa kwenye Cinema kuanzia Septemba 15 hadi Septemba 19 na baadae kuanza kuuzwa na kusambazwa kwingineko duniani. Nimekusogezea movie mpya 9 ambazo kama wewe ni mfuatiliajia, mpenzi na muangaliaji unaweza kununua pindi zitakapotoka.
Hii inatwa BLAIR WITCH itaoneshwa kwenye Cinema Septemba 15 na baadae kusambazwa duniani. Ndani wapo James Allen McCune, Callie Hernandez na Corbin Reid.
Hiii inaitwa BRIDGET JONES' BABY. Hii itakuwa tayari kuoneshwa kwenye Cinema Septemba 16. Ndani wapo Renèe Zellweger, Colin Firth na Patrick Dempsey.
Hii inaitwa SNOWDEN. Itaoneshwa kwenye Cinema Septemba 16. Ndani yake kuna Joseph Gordon-Levitt, Shailene Woodley na Merissa Leo.
Hii inaitwa MR. CHURCH. Itaoneshwa kwenye Cinema Septemba 16. Ndani wapo Edson Murphy, Britt Robertson na Madison Wolfe.
Hii inaitwa THE GOOD NEIGHBOR. Itaoneshwa kwenye Cinema Septemba 16. Ndani wapo James Caan, Logan Miller na Keir Gilrchrist.
Hii inaitwa THE BEATLE: EIGHT DAYS OF WEEK - THE TOURING YEARS. Itakuwa kwenye Cinema Septemba 16. Ndani wapo Paul McCartney, Rigo Starr na John Lennon.
Hii inaitwa WILD OATS. Itaoneshwa kwenye Cinema Septemba 16. Imeigizwa na Jesca Lange, Demi Moore na Shirley MacLane.
Hii inaitwa SISTER CITIES. Itaoneshwa kwenye Cinema Septemba 17. Ndani wapo Troin Bellisario, Stana Katic na Michelle Trachtenberg.
Hii inaitwa MY BLIND BROTHER. Itakuwa kwenye Cinema Septemba 19. Mastaa waliomo ni Jane Slate, Zoe Kazan na Adam Scott.
UNAWEZA KUANGALIA TRELA ZA MUVI ZOTE HIZI KWA KUPAKUWA NA KUSAKINISHA KITUMIZI CHA IMDb KWENYE SIMU YAKO YA MKONONI AMA KUTEMBELEA TOVOUTI YA IMDb
Chanzo: IMDb
MAREKANI NA URUSI ZAKUBALIANA KUSITISHA MAPIGANO SYRIA
Marekani na Urusi zimefikia makubalinao kuhusu mchakato wa kupatikana amani nchini Syria ikiwemo kusitishwa kwa mapigano kote nchini Syria kuanzia Jumatatu wiki ijayo.
Makubaliano hayo yaliyofikiwa mapema Jumamosi (10.09.2016) kati ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov yanafuatia mazungumzo ya kina yaliyokuwa yakifanyika mjini Geneva, Uswisi.
Lavrov amesema licha ya kuendelea kutoaminiana kati ya pande hizo mbili, wamefanikiwa kuafikiana kuhusu jinsi ya kushirikiana kupambana dhidi ya ugaidi na kuyafufua mazungumzo ya kisiasa ya kupatikana amani nchini Syria kwa njia bora zaidi.
Je mzozo wa Syria utakoma sasa?
Kerry ambaye alichelewesha kwa siku moja safari yake kutoka Geneva na kurejea Marekani ili kuhakikisha wamefikia makubaliano na mwenzake wa Urusi amesema utawala wa Rais wa Marekani Barack Obama unajituma zaidi katika kuutatua mzozo wa Syria kwasababu wanaamini Urusi ina uwezo wa kuushinikiza utawala wa Rais wa Syria Bashar al Assad kusitisha vita na kuja katika meza ya mazungumzo ili kupatikane amani nchini humo.
![]() |
Kerry na Lavrov walikutana na maafisa wengine Geneva kuhusu Syria |
Kerry ameongeza kusema kuwa msingi wa mazungumzo hayo ya Geneva ilikuwa ni makubaliano kuwa serikali ya Syria haitafanya mashambulizi ya angani kwa kisingizio cha kuwasaka wapiganaji wa kundi la wanamgambo wenye itikadi kali wa al Nusra Front, linalofungamanishwa na mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda.
Waziri huyo wa mambo ya nje wa Marekani amesema kusitishwa huko kwa mashambulizi ya angani katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi kutafikisha kikomo matumizi ya mabomu ya mapipa na mashambulizi ya kiholela na ina uwezo wa kubadili mkondo wa mzozo wa Syria.
Marekani na Urusi zimekubaliana iwapo mapigano yatapungua, nchi hizo mbili zitashirikiana kufanya operesheni za kijeshi kwa pamoja dhidi ya Al Nusra na kundi la wanamgambo wenye itikadi kali la Dola la Kiislamu IS.
Chini ya makubaliano hayo pande zote zinazohusika zinapaswa kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano kote nchini Syria, kusitisha mashambulizi yote yakiwemo ya angani, kutojaribu kuyadhibiti maeneo mapya wakati wa kusitishwa kwa mapigano, kuruhusiwa kwa misaada ya kibinadamu kufika katika maeneo yaliyozingirwa ikiwemo katika mji unaodhibitiwa na waasi wa Aleppo.
Umoja wa Mataifa siku ya Ijumma ulisema serikali ya Syria imezuia misafara ya magari ya kutoa misaada ya kibiandamu mwezi huu kuingia katika mji wa Aleppo na mji huo unakumbwa na hatari ya kuishiwa mafuta katika kipindi cha wiki moja ijayo na hivyo kuyafanya mazungumzo kuhusu Syria kushughulikiwa kwa dharura zaidi.
Marekani na Urusi kushirikiana kijeshi
Iwapo hayo yatazingatiwa kuanzia Jumatatu wiki ijayo, Urusi na Marekani zitaanza siku saba za kazi za maandalizi ya kuunda kituo cha pamoja cha kuteleza shughuli zao za kijeshi Syria ikiwemo kubadilishana taarifa kuhusu maeneo yanayodhibitiwa na wanamgambo na kuhusu makundi ya upinzani.
![]() |
Mwanamke akitathmini uharibifu mjini Aleppo
|
Marekani na Urusi zimekuwa kila moja ikiunga mkono upande tofauti katika vita vya wenyewe kwa wenyewe Syria ambavyo havionyeshi dalili ya kukoma hivi karibuni hata baada ya miaka mitano ya mzozo ambao umesababisha nusu ya idadi ya Wasyria kuyahama makaazi yao, maelfu kuuawa na mamilioni ya wengine kuwa wakimbizi.
Katika mzozo huo, Urusi inamuunga mkono Rais Bashar al Assad huku Marekani ikiunga mkono upinzani unaotaka kumng'oa madarakani Rais Assad. Pendekezo la Kerry la ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi yake na Urusi limekumbwa na upinzani kutoka kwa maafisa wa Marekani wa ulinzi na wa kijasusi wanaodai Urusi haiwezi kuaminiwa.
Chanzo: DW
LEO SEPTEMBA 10 KATIKA HISTORIA
![]() |
George Washington, Rais wa Kwanza wa Marekani |
TUANGALIE MATUKIO MUHIMU YALIYOTOKEA TAREHE KAMA YA LEO
210 K.K - Mtawala wa kwanza wa Dola ya Qin (Qin Dynasty) ya nchini China alifariki.
1776 - George Washington aliomba mpelelezi wa siri wa kujitolea, Nathan Hale akajitolea.
1993 - Israel ilisaini mkataba wa utambuzi na PLO.
1919 - Jiji la New York lilimkaribisha nyumbani Jenerali John J. Peshing na wanajeshi wengine 25,000 waliolitumikia jeshi la Marekanj katika vita ya kwanza ya Dunia katika divisheni ya kwanza.
1939 - Canada ilitangaza vita dhidi ya Ujerumani.
1945 - Vidkun Quisling alihukumiwa kifo kwa kushirikiana na jeshi la Ujerumani Nazi nchini Norway. Aliuawa kwa kupigwa risasi Oktoba 1945.
1963 - Wanafunzi weusi 20 (negro) waliruhusiwa kusoma katika shule za serikali za Alabama kufuatia makubaliano kati ya Serikali kuu na Gavana George C. Wallace.
1974 - Guinea-Bissau ilipata uhuru wake kamili kutoka kwa Ureno.
1979 - Wanaharakati wanne wa Puerto Rico walihukumiwa kwenda jela kwa kosa la kufanya shambulizi katika Bunge la Wawakilishi nchini Marekani mwaka 1953 na jaribio la kutaka kumuua Rais wa Marekani, Harry S. Truman mwaka 1950. Waliachiwa baadae kwa msaha kutoka kwa Rais Jimmy Carter.
2008 - Jaribio lililoitwa Hadron Collider ambalo ni jaribio kunwa kiwahi kufanyika katika historia ya binadamu lilifanywa huko Geneva, Uswisi.
KUZALIWA
1638 - Malikia Maria Theresa akiwa mke wa Mfalme Lous XIV wa Hispania maarufu kama "Maria Theresa wa Hispania" alizaliwa huko El Escorial nchini Hispania.
1928 - Mwanafalsafa wa Canada, Jean Vanier alizaliwa.
1931 - Muigizaji wa Matekani Philip Baker Hall alizaliwa.
1940 - Mwanamuziki wa Marekani Roy Ayers alizaliwa.
1953 - Muigizaji wa kike wa Marekani Amy Irving alizaliwa.
1957 - Mwanamuziki wa Uingereza Siobhan Fahey alizaliwa.
1958 - First lady wa Canada Margaret Trudeau alizaliwa.
1960 - Muigizaji wa Uingereza Colin Firth alizaliwa.
1968 - Muongozajj wa filamu wa Uingereza Guy Ritchie alizaliwa.
1974 - Muigizaji wa Marekani Ryan Phillippe alizaliwa.
1979 - Muigizaji wa Marekani Jacob Young alizaliwa.
1928 - Mwanafalsafa wa Canada, Jean Vanier alizaliwa.
1931 - Muigizaji wa Matekani Philip Baker Hall alizaliwa.
1940 - Mwanamuziki wa Marekani Roy Ayers alizaliwa.
1953 - Muigizaji wa kike wa Marekani Amy Irving alizaliwa.
1957 - Mwanamuziki wa Uingereza Siobhan Fahey alizaliwa.
1958 - First lady wa Canada Margaret Trudeau alizaliwa.
1960 - Muigizaji wa Uingereza Colin Firth alizaliwa.
1968 - Muongozajj wa filamu wa Uingereza Guy Ritchie alizaliwa.
1974 - Muigizaji wa Marekani Ryan Phillippe alizaliwa.
1979 - Muigizaji wa Marekani Jacob Young alizaliwa.
KWA MSAADA WA MTANDAO
WATU 10 WAMEKUFA KATIKA AJALI YA MOTO KIWANDANI HUKO BANGLADESH
Takribani watu 10 wamekufa katika mlipuko mkubwa wa moto huko Bangladesh kufuatia kulipuka kwa kontena la kuchemshia maji ya moto.
Polisi wamesema kuwa takribani watu 100 walikuwa ndani ya kiwanda hicho chenye jengo la ghorofa 4 ambapo mlipuko ulisikika katika mji wa Tongi.
Takribani watu 30 wamejeruhiwa kutokana na moto huo kusambaa kwa haraka katika jengo hilo.
Huduma za dharura zinadai kuwa moto bado unaendelea kuwaka na inasemekana idadi ya watu kufariki katika ajali hiyo inaweza kuongezeka.
"Mpaka sasa tumepata uhakika wa watu 10 kufariki. Lakini bado idadi inaweza kuongezeka kwa sababu moto bado ni mkali kushindwa kuzimwa." Inspekta wa Polisi Sirajul Islam aliiambia AFP.
Kumekuwa na majanga mengi ya moto viwandani nchini Bangladesh kufuatia kutokuwa na usalama wa kuzuia majanga hayo katika nchi hiyo.
Canzo: BBC
Polisi wamesema kuwa takribani watu 100 walikuwa ndani ya kiwanda hicho chenye jengo la ghorofa 4 ambapo mlipuko ulisikika katika mji wa Tongi.
Takribani watu 30 wamejeruhiwa kutokana na moto huo kusambaa kwa haraka katika jengo hilo.
Huduma za dharura zinadai kuwa moto bado unaendelea kuwaka na inasemekana idadi ya watu kufariki katika ajali hiyo inaweza kuongezeka.
"Mpaka sasa tumepata uhakika wa watu 10 kufariki. Lakini bado idadi inaweza kuongezeka kwa sababu moto bado ni mkali kushindwa kuzimwa." Inspekta wa Polisi Sirajul Islam aliiambia AFP.
Kumekuwa na majanga mengi ya moto viwandani nchini Bangladesh kufuatia kutokuwa na usalama wa kuzuia majanga hayo katika nchi hiyo.
Canzo: BBC
KANSELA ANGELA MERKEL ASEMA UJERUMANI YA SASA NI BORA ZAIDI
![]() |
Kansela Angela Merkel akihutubia bungeni siku ya Jumatano (7 Septemba 2016). |
Vichwa vya habari katika magazeti na ripoti za televisheni na redio mara tu baada ya CDU kushindwa uchaguzi huo wa Jumapili, zilitazamiwa kumrejesha Kansela Merkel nyuma, na hotuba ya leo ilidhaniwa kuwa ingekuwa nyepesi na laini. Lakini hivyo sivyo ilivyokuwa, kwani kwenye hotuba ya bungeni ya leo Jumatano (7 Septemba 2016), ambapo alionekana kusimama imara.
"Hali yetu leo ni bora zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka mmoja uliopita kwetu sote. Hapana shaka, bado kuna mambo ya kufanywa. Changamoto kubwa ikiwa kuwarejesha nyumbani wahamiaji ambao hawawezi kubakia hapa na sisi. Na kwa uadilifu kuwahudumia raia wetu, huku tukiwafahamisha kuwa tunapaswa kuwasiaidia wale wenye haki ya kusaidiwa," aliwaambia wabunge.
Katika hotuba hii, ambayo tayari imeshaonesha kuzua mjadala mkali, Kansela Merkel amesema si kweli kuwa mmiminiko wa mamia kwa maelfu ya wakimbizi nchini Ujerumani utapunguza mafao wanayopata raia wazawa wa Ujerumani, hoja ambayo imekuwa ikitumiwa na wapinzani wake wa kisiasa.
Chama chake, CDU, kiliangushwa kwenye uchaguzi wa mwishoni mwa wiki na chama kinachopinga wahamiaji nchini Ujerumani, AfD, katika jimbo la Mecklenburg-Vorpommern, kwa hoja hiyo hiyo dhidi ya wakimbizi.
Wapigakura kwenye jimbo hilo walitumia nafasi hiyo kumuonesha kutokubaliana na sera yake ya kufungua milango kwa wakimbizi na wahamiaji kutoka mataifa yenye Waislamu wengi, hasa baada ya matukio kadhaa ya mashambulizi kwenye miji ya kusini mwa Ujerumani, lakini kwenye hotuba yake ya leo bungeni, Kansela Merkel amesema ugaidi si jambo linalohusiana moja kwa moja na wakimbizi.
Kansela Angela Merkel wa Ujerumani na Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki wakiwa kwenye mkutano wa kilele wa mataifa ya G20, mjini Hangzhou, China.
![]() |
Makubaliano na Uturuki ni sahihi
Sambamba na hilo, alitetea pia namna anavyoliendea suala la mahusiano kati ya nchi yake na Uturuki, akiwakosoa wale wanaomwambia ameshinda kulaani hatua kali za ukandamizaji zinazochukuliwa na utawala wa Rais Tayyip Erdogan baada ya jaribio la mapinduzi yaliyoshindwa mwezi Julai.
Merkel amesema makubaliano kati ya Umoja wa Ulaya na serikali ya Uturuki yaliyolenga kuzuia mmimiko wa wahamiaji yalikuwa hatua muhimu na inayoweza baadaye kuigizwa kama msingi wa makubaliano na mataifa mengine.
Mdahalo wa jioni ya leo kuhusiana na hotuba hii iliyoshadidia msimamo na muelekeo wa Kansela Merkel kwa masuala ya wakimbizi, usalama, na sera yake ya nje unatazamiwa kuwa mkali sana.
Tayari msuguano ndani ya serikali yake ya muungano umeshadhihirika, huku mshirika wake mkuu, chama cha SPD kikionekana kujipanga kumpiku.
Upinzani mkali pia umo ndani ya chake mwenyewe cha CDU, huku chama ndugu cha CSU kikiwa tangu mwanzoni mbali sana na sera ya wakimbizi ya Kansela Merkel.
Chanzo: DW
TCU IMEFUNGUA DIRISHA LA UDAHILI KWA AWAMU YA PILI
Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imefungua tena dirisha la udahiri kwa Wanafunzi wanaoomba kuchaguliwa katika kozi mbalimbali za Shahada ya Kwanza mwaka huu wa masomo 2016/2017. Linasomeka hivi:
TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA (TCU)
TAARIFA KWA UMMA
Tunapenda kuutangazia Umma kuwa tulifunga mfumo wa pamoja wa udahili tarehe
31/08/2016 saa sita usiku ili kuchakata maombi ya waombaji waliofanikiwa kuomba
udahili kwa mwaka wa masomo 2016/2017.
Hata hivyo kutokana na wengine kushindwa kufanikiwa kutokana na sababu mbali
mbali, Tume inatangaza kuwa itafungua maombi kwa awamu ya pili kuanzia tarehe
12 hadi 23 Septemba 2016 ili kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili.
• Waombaji watakaokuwa wamekosa nafasi kwenye awamu ya kwanza
• Waombaji wa kidato cha Sita walioshindwa kuomba katika awamu ya kwanza
• Waombaji wenye vigezo vya Stashahada ambao walishindwa kuomba kutokana
na matokeo yao kuchelewa kufika NACTE kwa wakati,
• Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya “Cambridge” mwaka 2016 na
matokeo yao yameshatoka,
• Waombaji waliofaulu mitihani ya RPL,
• Waliokuwa wanafunzi wa vyuo vikuu watakao kuwa na uthibitisho toka vyuo
vyao vya awali.
Baada ya hapo Tume haitaruhusu tena maombi ili kuruhusu taratibu zingine za
kiudahili kuendelea kwa ngazi ya Bodi ya Mikopo na vyuoni.
Asanteni
Imetolewa na
Prof. Eleuther Mwageni
Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
02 Septemba 2016.
Unaweza kusoma zaidi kwa KUBOFYA HAPA
RAIS WA UZBEKISTAN AZIKWA KWA HESHIMA YA DINI YA KIISLAMU
Karimov, mwenye umri wa miaka 78 na ambaye ameiongoza Uzbekistan kwa muda mrefu, alifariki dunia jana Ijumaa baada ya kuugua kiharusi mwishoni mwa wiki iliyopita. Waziri Mkuu wa Urusi, Dmitry Medvedev anatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo yatakayofanyika kwa heshima ya dini ya Kiislamu.
Mazishi hayo pia yatahudhuriwa na viongozi wengine wa mataifa ya iliyokuwa Umoja wa Kisovieti, akiwemo Rais wa Tajikistan, Emmomali Rakhmon, Rais wa Turkmenistan, Gurbanguly Berdymukhamedov na Waziri Mkuu wa Kyrgyzstan, Belarus na Kazakhstan. Rais wa Marekani, Barack Obama ameelezea kusikitishwa na kifo hicho na amethibitisha kwamba nchi yake iko tayari kuwasaidia wananchi wa Uzbekistan katika kipindi hiki.
Waombolezaji wajipanga barabarani
Uvumi ulianza kuzagaa siku chache zilizopita kuwa kiongozi huyo amefariki dunia, lakini kifo chake kilithibitishwa rasmi hapo jana. Maelfu ya wananchi wa Uzbekistan wameanza kujipanga tangu mapema asubuhi ya leo, huku waombolezaji wengi wakiwa wamebeba maua waridi, ambayo wamekuwa wakiyaweka kwenye barabara. Waziri Mkuu wa Uzbekistan, Shavkat Mirziyoyev, ameteuliwa kuwa kiongozi wa kusimamia mazishi ya Karimov, hatua inayoonyesha kuwa huenda akawa rais ajaye wa nchi hiyo.
Mapema jana, serikali ya Uturuki ilitoa salamu za rambirambi kutokana na msiba huo. Akizungumza katika mkutano na baraza la mawaziri, Waziri Mkuu wa Uturuki, Binali Yildirim amesema wanaungana na watu wa Uzbekistan katika kipindi hiki cha majonzi. Aidha, katika taarifa yake aliyoitoa jana Rais wa Urusi, Vladmir Putin amekielezea kifo cha Karimov kama pigo kubwa kwa watu wa Uzbekistan.
Karimov ameitawala nchi hiyo ya Asia ya Kati tangu mwaka 1989 akiwa kama mwenyekiti wa chama cha Kikomunisti na mwaka 1991 alikuwa rais wa Uzbekistan wakati nchi hiyo ilipokuwa huru kutokana na kuvunjika kwa uliokuwa Umoja wa Kisovieti. Karibu ya nusu ya raia milioni 32 wa Uzbekistan, walizaliwa wakati wa utawala wake.
Wengi wanamchukulia Karimov kama kiongozi dikteta kutokana na maamuzi ya kikatili aliyoyafanya wakati wa utawala wake na serikali yake imekuwa ikishutumiwa kwa kukiuka haki za binaadamu. Steve Swerdlow mtaalamu kutoka Shirika la kimataifa la haki za binaadamu, Human Rights Watch Asia ya Kati, anasema kuwa Karimov alikuwa na utawala wa kimabavu, kwani aliwafunga gerezani na kuwatesa wapinzani na mahasimu wake kisiasa. Kwa mujibu wa Swerdlow, kiongozi huyo aliamuru jeshi kuwapiga risasi waandamanaji katika mji wa mashariki wa Andijan mnamo mwaka 2005, mauaji mabaya kabisa kuwahi kushuhudiwa nchini humo.
Hadi sasa kiongozi huyo wa kimabavu hana mrithi kamili, hali inayozusha wasiwasi kwamba kifo chake kinaweza kusababisha kukosekana kwa hali ya utulivu. Mtoto mkubwa wa kike wa Karimov, ambaye alionekana kama anaandaliwa kuchukua nafasi ya baba yake, hajaonekana hadharani tangu mwaka 2014, huku kukiwa na uvumi kwamba yuko katika kizuizi cha nyumbani. Amekuwa akishutumiwa na waendesha mashtaka wa nchini Marekani na Ulaya, kwa kuhusika na rushwa.
Mtoto wa pili wa kike wa Karimov, Lola Karimov-Tillyaeva, ni balozi wa Uzbekistan katika shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Elimu, Sayansi na Utamaduni-UNESCO. Nchi ya Uzbekistan ina utajiri mkubwa wa madini ya dhahabu, gesi asilia na pia ni msafirishaji mkubwa wa pamba.
Chanzo: Deutsche Welle (DW)
NEW VIDEO: ANGALIA VIDEO YA RAYMOND-NATAFUTA KIKI HAPA
Hatimaye Raymond a.k.a. RayVanny wa WCB Wasafi Classic ameachia video ya wimbo wake Natafuta kiki. Production ya video imefanyika Kwetu studios ya hapa hapa Tz. Pata nafasi ya kuangalia video hiyo hapa.